Tujikumbushe vitabu vya zamani

Tujikumbushe vitabu vya zamani

machimbo ya mfalme suleiman and ALLAN QUATERMAN by H RIDDER HAGGARD ni zaidi ya burudani

Nimetafuta Sana Kitabu Hiki Lakini Sijakipata. Mwenye Kujua Namna Ya Kukipata Tafadhali Tuwasiliane 0767320599
 
Dah ni siku nyingi nlisoma pengine 97 lkn ladha yake bado naihisi.

Solais bibi wa usiku alikuwa anapendwa sana na Sir Good wakati Henry alimpenda sana Nyleptha,.Unamkumbuka Mtoto Flosie pale mji wa mission?Vipi pale mtumbwi wao ulivyochukuliwa na mto wa chini ya ardhi?Unakumbuka kisa cha wale viboko?
 
1.oparesheni vipusa
2.Nteko vano mapato
3.Titi la mkwe
4.Yai jeupe
5.Watanitambua
6.Amekufa anacheka
7 . pili pilipili
8 . Dunia hadaa,ulimwengu shujaa
9.Unyama wa mafia
10.Sikunyongwa
11.Johari ndogo
1.Sifi mara mbili.
2.akuanzae mmalize.
3.buriani.
4.kabwe makanika,jitu kumbuka.
5.kamlete akibisha mlipue.
6.sanda ya jambazi.
7.uwike usiwike kutakucha.
8.salamu toka kuzimu.
9.lazima ufe joram.
10.adili na nduguze.
 
Pia yalikuwepo majarida yenye hadithi tamu sana kama sani na ambha sijui kama yapo duniani. Nakumbuka love story tanganyika and zanzibar ilivyonivutia naa baadae nikaona video yake. Akina vuai. Pia kulikuwa na msako wa mr x. Kwenye ambha nakumbuka hadithi iliyokuwa inatoka kwa mtindo wa tenzi ilikuwa inaitwa ushauri wa mwendawazimu. Jamaa kamfumania mkewe akaua. akiwa jela kaja mwehu akamshauri ushauri uliomnusuru na kifo asema mwenye:
Mwehu huyo mashuhuri
Aitwa kindorindori
Akaja kanishauri
.......
 
Nahisi utakuwa hujasoma riwaya nyingine za Musiba. Sidhani kama HOFU inashinda KIKOSI CHA KISASI!
Walivumisha kuwa musiba alitunga kitabu kinaitwa HUJUMA,eti kikapigwa marufuku kuwa ukikisoma unapata maujuzi ya kupindua hata nchi,sidhani kama ilikuwa kweli lakini.
 
Pia yalikuwepo majarida yenye hadithi tamu sana kama sani na ambha sijui kama yapo duniani. Nakumbuka love story tanganyika and zanzibar ilivyonivutia naa baadae nikaona video yake. Akina vuai. Pia kulikuwa na msako wa mr x. Kwenye ambha nakumbuka hadithi iliyokuwa inatoka kwa mtindo wa tenzi ilikuwa inaitwa ushauri wa mwendawazimu. Jamaa kamfumania mkewe akaua. akiwa jela kaja mwehu akamshauri ushauri uliomnusuru na kifo asema mwenye:
Mwehu huyo mashuhuri
Aitwa kindorindori
Akaja kanishauri
.......
Umenikumbusha mzee ole,zumo,obi,ilikua balaa.
 
Kwa Mdomo wa Bastola kinamhusu Stoni Puto. Full ujasusi.
 
Mtaalamu Joram Kiango wa Je tutarudi na roho zetu?
 
Mambo ya ajabu yaliyompata Allan Quterman na wenzake,,kuiendea nchi ya watu weupe.Bonge la kitabu japo kwa kiwango fulani kinamdhalilisha mwafrika

Mfalme Twala, Kigagula, Umsolopagaz na Inkosi kazi, Bwana Gud,?


Long long way back with a natural setting feelings
 
Ah mkuu! baba! makumazahn! mzee mwindaji! akeshae! hodari mwepesi! ambae risasi zake hazikosi shabaha! muuwaji wa simba mla tembo! rafiki muaninifu!ile methali ya kikwetu isemayo milima haikutani ni ya kweli kabisa na tena yenye busara. tazama alikuja tarishi kutoka natal akalia na kusema makumazahn amefariki! na nchi haitamuona tena! lakini tazama leo baba yangu katika nchi ngeni tena yenye harufu mbaya kama hii namuona tena makumazahn! hakika ndie yeye bila shaka! manyoya ya mzee mbweha yamekwisha ingia mvi lakini meno na macho yake bado ni makali vilevile kama zamani! mkuu baba unakumbuka namna ulivyopitisha risasi kwenye jicho la nyati aliekuwa anashambulia?
 
dah nakumbuka darasa la la nne kitabu cha kiswahili enzi zile kuna stori moja tamu ya MANGASINI na MFALME, darasa la 3 kuna MUWA ULIOZAMISHA MELI, SAFARI YA MINJINGU, dah tumetoka mbali, la pili kulikua na PAMELA NA KIPINI, TOLA ALIA GIZANI

hawafu mwenye nguvu
sikulamba sukari
mkutano wa wanyama
la la laaaa
Utanikumbuka
Safari ya kigoma
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom