Tujadili: Pre-ndoa... Plan B aka 'BIMA'

Tujadili: Pre-ndoa... Plan B aka 'BIMA'

Mie mtu akinambia kuwa ana Plan A pekee ila pia anaiba mara moja moja nitamwelewa. Ila yule ambaye anasema kwamaba anamaitain A, B, C...etc na kutoa huduma zote basi nitamwogopa sana...

Anyway...ngoja niishie hapa kwani akina Dena Amsi wanaweza kunambia nimepitwa na wakati...lol!

Babu DC!!
wakati mwingine ni vizuri kupitwa na wakati babu......
kuna sehemu nimesikia eti kuna dawa ya hospitali inayoweza kufanya mtu awe na feelings nawe.........
na aliyesema ni daktari siyo layman kama mimi
nikaona kweli duniani tunaendelea......
sasa masangoma sijui watatapeli wapi tena?
 
Nakumbuka sana mafundisho ya dini nikiwa secondary kuhusu Urafiki, Uchumba na Ndoa; tuliambiwa (na kweli ina make sense) kuwa ni vizuri kuwa na marafiki wengi, lakini mchumba ni mmoja na kipindi cha uchumba maana yake unakuwa umefungwa (huwezi kuruhusu mchumba mwingine in case umemkubali wa kwanza); hiki ni kipindi cha kuchunguzana tabia kabla ya kujifunga moja kwa moja kwenye ndoa.

Lakini kwa sasa idadi kubwa ya watu (hasa wadada) walioko kwenye uchumba wana kuwa na bima au plan B au mpango wa kando. Hali hii ikija kugundulika mara nyingi hupelekea muhusika kukosa yote hata kama alikuwa anapenda kuolewa.

Sasa wana jamvi naomba tujadili kuhusu:-

  • ulazima au umuhimu wa plan B
  • Kiini cha tatizo hasa ni nini?
  • Nini kifanyike ili hii hali isiendelee?

tatizo inakuwaje awe mchumba wakati hata hujamchunguza? Akesha kuwa mchumba hapo umechelewa sana maana ukiachana naye ujue ni kizaazaa kingine na kinakuongezea shinikizo la kumkubali ajaye hata kama unaona ana hitilafu kibao na baadaye hizo hitilafu kuja kukuletea maumivu makali. Peer pressure hujitokeza maana utasikia minong'ono ambayo huwezi kuipuulizia mbali hata siku moja wapambe wakidai huyu naye hakai na mchumba hata siku moja pengine ana mikosi au hana tabia nzuri n.k

Nionavyo katika marafiki ulionao wachunguze na unaposema ni huyu basi awe kweli ni yeye. Mpango wa kando kabla na hata baada ya ndoa ni dalili za ulafi na kutokujiamini na wakati ni ukuta kweli kwani mwishowe huwa ni kilio kwa wahusika kwani kamwe mpango huo hauwezi kukidhi mahitaji yako. tukumbukle hakuna mkamilifu kweye lolote ila kuvumiliana ndiyo chemuchemu ya maelewano na mafanikio kwenye mahusiano.
 
quote_icon.png
By Dark City

Mie mtu akinambia kuwa ana Plan A pekee ila pia anaiba mara moja moja nitamwelewa. Ila yule ambaye anasema kwamaba anamaitain A, B, C...etc na kutoa huduma zote basi nitamwogopa sana...

Anyway...ngoja niishie hapa kwani akina Dena Amsi wanaweza kunambia nimepitwa na wakati...lol!

Babu DC!!

mwizi ni mwizi hakuna uwizi mdogo. Kwahiyo hakuna kisingizio kuwa huyu kala kidogo na huyu ni mlafi ukishachepuka wewe ni mlafi ule tonge moja au umeze mengi wewe ni mlafi tu tena umevimbiwa ila hujui ya kuwa umevimbiwa. Kwani ulafi wako umekupumbaza na kukufanya kuwa mpumbavu na utatafuta vijisababu vya kuhalalisha upumbavu wako lakini haitasaidia utabakia papo hapo hadi za mwizi ni arobaini na ndipo utajuta na kujisemea moyoni hivi nilitoka wapi na huyu?
 
wakati mwingine ni vizuri kupitwa na wakati babu......
kuna sehemu nimesikia eti kuna dawa ya hospitali inayoweza kufanya mtu awe na feelings nawe.........
na aliyesema ni daktari siyo layman kama mimi
nikaona kweli duniani tunaendelea......
sasa masangoma sijui watatapeli wapi tena?

ukiamini huu utapeli basi umekwisha. Kumpenda mtu siyo suala la kimwili ni la kiroho lazima umkubali na hakuna dawa ya hilo ila zipo dawa za kishirikina za kumpumbaza ili akuone tofauti na ulivyo lakini siyo za kumbadilisha misimamo yake dhidi yako na ndiyo maana zinapofubaa basi naye huzinduka na kibanio chake atakachokuweka nacho huwa ni mwendo mdundo hakomi mpaka ahakikishe umelipa siku zote ulimzomkamatia chini nazo na hakuna tiba pale!

Jisomee Mathew 5:26
"Assuredly I say to you, you shall not leave there till you have paid the last penny."
 
duh nimepitwa leo,kama ni maiti imefikishwa makaburini,imeingizwa hadi shimoni,imeanza kufukiwa mie ndo nafika msibani,hata sina cha kuongezea yote yamesemwa.
 
Well ambacho ninakumbuka au kwa uzoefu ni kwamba wengi wameoana-na wachumba ambao sio wale wa mwanzo, au waliotarajiwa, bali na wengine waliojitokeza kwa muda muafaka, mazingira muafaka, na kuwa na maono muafaka. Mara nyingi wachumba 'wa zamani' inabidi kuwaaacha...ustaarabu gani unatumika, ni juu ya mtu mwenyewe lakini wengi wameendelea kuwa marafiki wa familia mpya..na hata kushiriki kwenye sherehe za ndoa za wenzi wao wa zamani.

na labda niseme tu kwamba hapa sio ile mtu unakuwa na plan B intentionally au kama insurance kama ilivo 'siku hizi' hapana....inatokea tu kutokana na mizunguko ya dunia hii na hali halisi ya maisha....kuwa na wachumba wawili at the same time na wote umeahidi kuwaoa/kuolewa nao ni uhuni uliopitiliza....

CC: Dark City retired major general, FP snowhite, Kaunga, SnowBall, cacico, Mtambuzi, AshaDii, gfsonwin, Asprin, Kongosho, BADILI TABIA.

BCC: Nicas Mtei, kwa mafunzo zaidi. sosoliso, saudari, Erickb52.
 
Last edited by a moderator:
duh nimepitwa leo,kama ni maiti imefikishwa makaburini,imeingizwa hadi shimoni,imeanza kufukiwa mie ndo nafika msibani,hata sina cha kuongezea yote yamesemwa.

ulipotea wapi mtoto Asnam?
 
Last edited by a moderator:
inawezekana pia wakawa na ndoa ya amani/raha tele kwani plan B huwa zinatofauti kidunchu sana na plan A, vimeo vinaanzia plan D kuendelea.

Haha ila kweli lakin plan A akikatiaa tu roho lazi,a i undergo vibration
 
wakati mwingine ni vizuri kupitwa na wakati babu......
kuna sehemu nimesikia eti kuna dawa ya hospitali inayoweza kufanya mtu awe na feelings nawe.........
na aliyesema ni daktari siyo layman kama mimi
nikaona kweli duniani tunaendelea......
sasa masangoma sijui watatapeli wapi tena?

Hakuna kitu kama hicho mkubwa mwenzangu, ni utapeli tu kama utapeli mwingine.....

Kama kweli hiyo dawa ipo, basi naomba anipatie mimi.....

Babu DC!!
 
na huu ndio ukweli mtamu/mchungu wenyewe, maisha ndio kama hivi, nina mdogo wangu mtoto wa mama mdogo nadhani yeye anaenda mpaka Z na kurudia A-Z tena, kuna siku nikamuuliza hivi unawezaje kuwa handle hawa binadamu jamani na kwanini unafanya haya, aliniambia" sister acha unafiki, ina maana kuna ugumu gani hapa, kwani kuna alieweka pete kidoleni? basi na nitakaemwambia leo siwezi kukuona na anitii".....

Haha daah kashindikana huyo sasa ebu chukulia alivyo na hadi z halafu kati ya hao alio nao nao wanazo plan mpaka d, hapo ndo tuko wangapi inapo take nafasi.
Lakini utafanyaje plans za ziada muhimu
 
Pengine zombie angekuwa staring ninge hinunua
Na wakaka je? Hawana changamoto hizo?

Mfano elmagnifico tumeshuhudi hapa hapa, kama haikuwa muvi.

Mie nadhani wote tumechachamalishana nywele kwa kweli.
 
Last edited by a moderator:
Aiseeeeeee!
what i believe is smtms watu huwa wna date wrong choice na baadae Mungu huwa analeta the correct choice kwao.

kwan nasema hivi??? nilipokuwa na mhaya nilijua niko na hubby to be ila nafsini mwangu moyo haukuwah kufunga sana kivilee sijui kwann, hatukuwah kugombana wala nini na tulikuwa tunacope vyema but, siku alipokuja hubby ndipo nilijisemea sasa hili ndilo chaguo langu.hakuwa na cha ziada ila kuna kule moyo kufunguka hadi ukajiskia nafsini na akilini mwako.
 
The coastal Theory ya Mafiga matatu

Swali, yanaleta uhakika wa ndoa??Au ni vibuzi tu vya kununua unga kilo moja na dagaa?

Theory ya Mafiga matatu sio kwa ajili ya kuleta uhakika wa ndoa, havihusiani kabisa. Mafiga matatu huwa yanakuwepo kabla ya ndoa na pia yanaendelea kuwepo baada ya ndoa(ndani ya ndoa).

Ishu ni kwamba always kunakuwa na wanaume watatu:


Wa kwanza ni yule ambaye anamiliki jumla kiunyumba/kigharama, huyu mara nyingi ndiye anakuwa ndiye mtunzaji mkuu.

Wa pili ni yule ambaye ni chaguo la moyoni la mwanamke, ni yule ambaye mwanamke anampenda tu kwa jinsi alivyo.

Wa tatu ni yule ambaye ni fundi mzuri wa kupiga ile mashine.

Wenyewe(wanawake wenye theory hiyo) wanakwambia ni mara chache kumpata mwanaume mmoja mwenye sifa zote tatu.
 
Unajua concept ya ndoa nayo katika dunia ya utandawazi hii imekuwa ngumu sana kuijadili.

Kwanza waliowafundisha mafunzo hayo ya uchumba ni watawa au watu wenye ndoa zao?? Nataka kupima uzoefu wao wa hali halisi. Mtu anayekufundisha theory ya kuogelea wakati si mwogeleaji ni ngumu sana kujua changamoto za swimming pool, bahari, mto na ziwani. Mengine ana-assume tu kumbe ndivyo sivyo. Hakuna kitu kilichokuwa naona muujiza kama 'alteration in rocks' lakini kiuhalisia ize tu, anyway. Changamoto ya kwanza.

Lakini pia, unapokuwa na Plan B, wakati Plan A iko active, una uhakika kiasi gani Plan B itakuoa pale A mambo yanapokwenda mrama? Je Plan B nayo ikiingia mitini? Kutakuwa na haja ya kuwa na Plan C and D labda??

Aisee, ndoa na mapenzi hayana mahakama wala insurance kwa mtizamo wangu. Noana hapa Plan B inataka kutumika kama insurance hivi.

Pale Msimbazi Center wanafundisha kwa maadili ya dini,(padri au mchungaji) kiafya (daktari) na maadili ya ndoa (wazazi wawili M na F waliodumu kwenye ndoa muda mrefu) kwahiyo angalau unaelimika kila upande huko kwingine sijui mafundisho yao yakoje. uwalu walu wetu tu hatusikii la mkuu wala lamwazini

hii plan B,C,D.... Huko ni kujilipua bora kushika moja likiponyoka unatuliza akili unatafakari unaanza upya
 
Mmmmh!
Plan B si kitu chema hapo utakua unaishi maisha ya mashaka , maanake hata message ikiingia tu wewe moyo unaenda mbio hivi utamwambia Plan A huyo ni nani.
Mimi nafikiri Kuwa upendo wa dhati ulionao juu ya mtu fulani ndio jibu, unapokua na upendo wa kweli hauwezi kuifikiria vinginevyo. Hapa cha msingi ni vema kujitunza kipindi chote cha mahusiano ili mambo yakienda kombo basi unakua hauna doa . Pia kabla ya kukubaliana uchumba ni vizuri mkajuana kwa undani pasipo kutenda dhambi hii inasaidi kufanya maamuzi pasipo shaka.
Unapoolewa au kuoa na plan B mara nyingi sana kunakua na migogoro ktk ndoa, hivyo ni bora vijana muwe waangalifu.
Kumbuka Plan B anaweza yeye akawa amekufanya wewe kua chaguo lake na hawezi kuishi bila wewe , je huoni kuwa utakua umemuumiza mtu hapo na hatakusahau maisha yake yote.
 
Well ambacho ninakumbuka au kwa uzoefu ni kwamba wengi wameoana-na wachumba ambao sio wale wa mwanzo, au waliotarajiwa, bali na wengine waliojitokeza kwa muda muafaka, mazingira muafaka, na kuwa na maono muafaka. Mara nyingi wachumba 'wa zamani' inabidi kuwaaacha...ustaarabu gani unatumika, ni juu ya mtu mwenyewe lakini wengi wameendelea kuwa marafiki wa familia mpya..na hata kushiriki kwenye sherehe za ndoa za wenzi wao wa zamani.

na labda niseme tu kwamba hapa sio ile mtu unakuwa na plan B intentionally au kama insurance kama ilivo 'siku hizi' hapana....inatokea tu kutokana na mizunguko ya dunia hii na hali halisi ya maisha....kuwa na wachumba wawili at the same time na wote umeahidi kuwaoa/kuolewa nao ni uhuni uliopitiliza....

CC: Dark City retired major general, FP snowhite, Kaunga, SnowBall, cacico, Mtambuzi, AshaDii, gfsonwin, Asprin, Kongosho, BADILI TABIA.

BCC: Nicas Mtei, kwa mafunzo zaidi. sosoliso, saudari, Erickb52.
Kuweka kwa muhtasari ni kuwa asilimia kubwa ya wanandoa hawajaoa/olewa na wapenzi wao wa kwanza.

CC: Kaunga
 
Last edited by a moderator:
Theory ya Mafiga matatu sio kwa ajili ya kuleta uhakika wa ndoa, havihusiani kabisa. Mafiga matatu huwa yanakuwepo kabla ya ndoa na pia yanaendelea kuwepo baada ya ndoa(ndani ya ndoa).

Ishu ni kwamba always kunakuwa na wanaume watatu:


Wa kwanza ni yule ambaye anamiliki jumla kiunyumba/kigharama, huyu mara nyingi ndiye anakuwa ndiye mtunzaji mkuu.

Wa pili ni yule ambaye ni chaguo la moyoni la mwanamke, ni yule ambaye mwanamke anampenda tu kwa jinsi alivyo.

Wa tatu ni yule ambaye ni fundi mzuri wa kupiga ile mashine.

Wenyewe(wanawake wenye theory hiyo) wanakwambia ni mara chache kumpata mwanaume mmoja mwenye sifa zote tatu.

This is why naipenda JF
 
Watu wote hap at per si nikuuchosha mwili

Theory ya Mafiga matatu sio kwa ajili ya kuleta uhakika wa ndoa, havihusiani kabisa. Mafiga matatu huwa yanakuwepo kabla ya ndoa na pia yanaendelea kuwepo baada ya ndoa(ndani ya ndoa).

Ishu ni kwamba always kunakuwa na wanaume watatu:


Wa kwanza ni yule ambaye anamiliki jumla kiunyumba/kigharama, huyu mara nyingi ndiye anakuwa ndiye mtunzaji mkuu.

Wa pili ni yule ambaye ni chaguo la moyoni la mwanamke, ni yule ambaye mwanamke anampenda tu kwa jinsi alivyo.

Wa tatu ni yule ambaye ni fundi mzuri wa kupiga ile mashine.

Wenyewe(wanawake wenye theory hiyo) wanakwambia ni mara chache kumpata mwanaume mmoja mwenye sifa zote tatu.
 
na labda niseme tu kwamba hapa sio ile mtu unakuwa na plan B intentionally au kama insurance kama ilivo 'siku hizi' hapana....inatokea tu kutokana na mizunguko ya dunia hii na hali halisi ya maisha....kuwa na wachumba wawili at the same time na wote umeahidi kuwaoa/kuolewa nao ni uhuni uliopitiliza....

hapo kwenye red hapo.. ndo imekuwa fashion siku hizi.. they don't actually say kwamba ni plan B.. ila wanaita multiple choice.. ila kwa wadada wanaotafuta ndoa kwenye multiple choice mara nyingi wanakuwa wao picked up Kaizer.. unajua ni kwanini..? kwa sababu wanafuata taratibu zote za uke tarajiwa kwa kuwa wapole.. wasikivu.. wanyenyekevu.. wenye upendo.. all that in a full package (japo baadae wakishaingia ndani ya ndoa wengine wataonyesha their true colors)..
 
Back
Top Bottom