Katika mapenzi ya kileo wadada walio wengi hupenda kuwa na "Plan B", nadhani hufanya hivyo kutokana na kupenda ubwerere wa mambo. Unamkuta mdada anakuwa na wapennzi wengi kiasi kwamba kawapangia kila mmoja position yake bila wenyewe kujijua, unakuta kuna mpenzi wakumlipia kodi ya nyumba, kuna wakumvisha, kuna wakumlisha na kuna wa kumpatia burudani. Hii yote inatokana na wadada kutotaka kuzitumia pesa zao.
Ukija upande wa pili, wakaka nao pia huwa hawatabiriki bhana unamkuta leo
sosoliso yuko na
Paloma ila ukimkuta kesho unamkuta yuko na
Blue G ,hii pia inapelekea wadada wetu kuwa na "Plan B" ili pakiharibika huku wanako pakuegeshea mgongo huku wakitafuta wapi penye mapenzi ya kweli.
BTW hii tabia ya kuwa na "Plan B" haina umuhimu wowote chamsingi ni kila mmoja kuwa mwaminifu katika mapenzi yake na kujua ni nini alichofata katika mahusiano hayo. Wadada acheni kutegemea sana wakaka katika kuyaendesha maisha yenu kwani hata nyinyi mnaweza bila kuwezeshwa. Pia wakaka acheni tabia za kuwabadilisha dada zetu kama nguo.
Kila mtu amcague ampendae kwa dhati na amchunguze kwa kadri awezavyo ndipo afanye maamuzi stahiki.