TTCL Corporation: Support thread (Maswali, ushauri na malalamiko)

TTCL Corporation: Support thread (Maswali, ushauri na malalamiko)

Ni dhahiri kabisa TTCL inahujumiwa meneja masoko TTCL achunguzwe ikibidi afukuzwe kazi!

Hili shirika ni dhahiri linahujumiwa kwa maksudi, ni aibu kwa shirika kama hili ambalo linatumia mabilioni ya walipa kodi kusimika mitambo nchi nzima halafu kuwepo kwa mambo ya ajabu hivi

Hivi mnajua kuwa TTCL ndo mtandao ghali zaidi Tanzania kwa sasa? Wakati wenzao wanauza gb kwa 1200 hadi 1300 wao wanauza gb kwa 1600

Vifurushi vyao ni ghali sana, sio dakika sio sms, hawa walitakiwa wawe na unafuu kidogo ili watu watumie kwa wingi then mapato yapatikane.

Nasema haya kwasababu, serikali imetumia mabilioni ya pesa kulilifua hili shirika lakini wayafanyayo hayastahili kabisa

Halafu pamoja na kuenea karibu nchi nzima, meneja masoko hana mpango wowote wa kufanya promo kama yafanyavyo makampuni mengine,

Yeye yupo kwa maslah ya wengine nadhani, pale ttcl kulikua na mchezo wa meneja kupokea mishahara miwili, mmoja analipwa na ttcl/serikali mwingine anaingiziwa na hizi kampuni shindani

Kifurushi cha bufee kiliwafanya hawa jamaa kujizolea mamia ya watu sasa hivi wamekiharibu kiukweli huyu meneja wa masoko hafai kabisa kuendelea kuwepo pale, anatumika kuua shirika.

Tukiendelea kuchekea huu upuuzi tutajuta siku moja tunapoteza mabilioni ya pesa kufufua mashirika kama haya halafu kikundi cha watu wachache kinaua shirika kwa mgongo wa nyuma kupitia hawa makanjanja wanaofanya kazi shirikani

Meneja masoko ttcl asimamishwe kazi, mkurugenzi naye abadilishwe, hili shirika bila hivyo linaenda kufa tena!
 
Ndugu mteja,

Una tatizo lolote unapotumia mtandao wetu? Una ushauri wowote ili tuiboreshe huduma yetu?

Tafadhali itumie mada (thread) hii ili tukusaidie kwa urahisi.

Unapokuwa na tatizo, ili tukusaidie kirahisi zingatia haya:

- Ni tatizo gani? (T-PESA, SMS, Calls, Internet, usajili, kukatika kwa mawasiliano n.k)

- Maeneo gani? (Tukifahamu maana ulipo, inakuwa rahisi kukuelekeza wapi uende ili upate msaada toka kwa wakala wetu aliye karibu nawe)

- Tatizo limeanza lini na limejirudia au kuendelea kuwa kero kwako kwa muda gani?

- Kama ni ushauri, zingatia ya juu lakini tutafurahi tukijua kwanini unapendekeza unachopendekeza.

- Kama ni pongezi, zingatia ya juu na tungependa pia upendekeze lipi tufanye kuzidi kuiboresha huduma kwako.


Zifuatazo ni ofisi zetu za huduma kwa wateja ndani ya jiji la Dar es Salaam.


1. POSTA
Mtaa wa Samora, jengo la Extelecom ghorofa la Chini.


2. KARIAKOO
Mtaa wa Makamba/Msimbazi, jengo la Akamba Bus Service.

3. UPANGA
Mtaa wa Magole/Maliki, karibu na Diamond Jubilee.


4. MAGOMENI
Mtaa wa Minaki/Fundiki, karibu na Manispaa ya Kinondoni.


5. KIJITONYAMA
Kijitonyama Sayansi, barabara ya Ali Hassan Mwinyi/ Rose Garden.


6. OYSTERBAY
Barabara ya Haile Selassie.


7. UBUNGO
Jengo la Ubungo Plaza/ Ghorofa la chini.


8. MBEZI BEACH
Mbezi Makonde/ Jengo la Shamo Tower.


9. TABATA
Tabata Bima, barabara ya Segerea karibu na kanisa la Romani Katoliki.


10. CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM.
Jirani na tawi la benki ya NBC, jirani na kilipo kituo cha polisi cha UDSM.


11. BARABARA YA PUGU
Barabara ya Mwalimu Nyerere, karibu na Sigara.


12. WAGENI
Uwanja wa ndege.


13. PUGU
Jengo la Quality Centre, ghorofa la chini.


14. KISUTU
Mtaa wa Mchafukoge/Libya jengo la Haad Plaza.


15. TEGETA SHOP
Jengo la Kibo Complex, ghorofa la chini.


16. MWANANYAMALA SHOP
Mwananyamala A, barabara ya Mwinjuma yalipo makutano ya Mwananyamala A.


17. KURASINI
Kurasini Exchange Area, jirani na Chuo cha Diplomasia.


Wasiliana nasi:
022 210 0100
0738 151 511
www.ttcl.co.tz


#RudiNyumbaniKumenoga
View attachment 1529645


Karibu.

Rudi Nyumbani Kumenoga
Ni dhahiri kabisa TTCL inahujumiwa meneja masoko TTCL achunguzwe ikibidi afukuzwe kazi!

Hili shirika ni dhahiri linahujumiwa kwa maksudi, ni aibu kwa shirika kama hili ambalo linatumia mabilioni ya walipa kodi kusimika mitambo nchi nzima halafu kuwepo kwa mambo ya ajabu hivi

Hivi mnajua kuwa TTCL ndo mtandao ghali zaidi Tanzania kwa sasa? Wakati wenzao wanauza gb kwa 1200 hadi 1300 wao wanauza gb kwa 1600

Vifurushi vyao ni ghali sana, sio dakika sio sms, hawa walitakiwa wawe na unafuu kidogo ili watu watumie kwa wingi then mapato yapatikane.

Nasema haya kwasababu, serikali imetumia mabilioni ya pesa kulilifua hili shirika lakini wayafanyayo hayastahili kabisa

Halafu pamoja na kuenea karibu nchi nzima, meneja masoko hana mpango wowote wa kufanya promo kama yafanyavyo makampuni mengine,

Yeye yupo kwa maslah ya wengine nadhani, pale ttcl kulikua na mchezo wa meneja kupokea mishahara miwili, mmoja analipwa na ttcl/serikali mwingine anaingiziwa na hizi kampuni shindani

Kifurushi cha bufee kiliwafanya hawa jamaa kujizolea mamia ya watu sasa hivi wamekiharibu kiukweli huyu meneja wa masoko hafai kabisa kuendelea kuwepo pale, anatumika kuua shirika.

Tukiendelea kuchekea huu upuuzi tutajuta siku moja tunapoteza mabilioni ya pesa kufufua mashirika kama haya halafu kikundi cha watu wachache kinaua shirika kwa mgongo wa nyuma kupitia hawa makanjanja wanaofanya kazi shirikani

Meneja masoko ttcl asimamishwe kazi, mkurugenzi naye abadilishwe, hili shirika bila hivyo linaenda kufa tena!
 
Siku hz ukinunua vocha ukiweka salio linakatwa.Mfano ukinunua vocha ya elfu 3 salio litasoma 2974 na points kadhaa.
Acheni wizi
 
Jaribuni kupunguza gharama za vifurushi maana havikamatiki katika mtandao wenu, ile kauli ya nyumbani kumenoga imekua haina maana tena mmetumia nguvu na gharama kuvuna wateja msishangae kuwa rahisi sisi wateja kurudu tulipotoka mboreshe gharama za vifurushi zishuke au muongeze ujazo wa vifurushi kwa gharama hizo hizo.

Sent from my SM-N960U using JamiiForums mobile app
 
Jaribuni kupunguza gharama za vifurushi maana havikamatiki katika mtandao wenu, ile kauli ya nyumbani kumenoga imekua haina maana tena mmetumia nguvu na gharama kuvuna wateja msishangae kuwa rahisi sisi wateja kurudu tulipotoka mboreshe gharama za vifurushi zishuke au muongeze ujazo wa vifurushi kwa gharama hizo hizo.

Sent from my SM-N960U using JamiiForums mobile app
Asante sana kwa ujumbe wako.
#RudiNyumbaniKumenoga
 
Bufee mmezingua 1mb kwa 2.5 tsh mmeenda mbali sana bora hata ingekuwa 2tsh kwa mb.
 
Inakuwaje njie ndio mnauzia wengine Internet kupitia mkongo wa Taifa lakini ndio muwe na mtandao usio aminika kuliko hao mnao wauzia?
Napendekeza; mtoe huduma ya kufungiwa internet mkianza na mjini, kwa kasi ya juu na sio kufunga nyumba sijui 100 kwa mwaka. Mnaweza kujumlisha na gharama zote za kufungiwa halafu mtu akatwe hadi atakapomaliza deni ndio aanze kulipia; Mkisubiri mdundulize hadi mpate hela ndio mfungie watu bure inafika karne ya 22 watu wengine hawajafikiwa
 
Back
Top Bottom