The Watchman
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 2,186
- 4,940
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akizindua Hoteli ya Jaz Elite Aurora iliyopo Michamvi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, leo tarehe 09 Januari, 2026 amesema ametahadharisha akiwaita wanaochokonolewa kuharibu amani ya nchi kuacha mara moja akikumbusha yaliyojiri Dar es Salaam na kwamba vijana hawatamani hata kuingia njiani.
"Kwa wale wanaochokolewa masikio kuvunja amani ya nchi hii niwasihi acheni mara moja. Amani ikichafuka haichagui na tuulizeni sisi wa upande wa pili ilipochafuka amani Dar es Salaam tu pale nenda kaulize leo vijana kama wanataka kuingia njiani, hakuna anaetamani, amani ikivunjika haichagui."
Vilevile amekiri uwepo wa tofauti za mawazo akisisitiza zisitumike kuleta migawanyo ya kisiasa na kuharibu utulivu wa kisiasa nchini.
"Maendeleo yetu, kunawiri kwetu kupendeza kwetu, kulala na kuamka salama tutunze amani ya nchi yetu tofauti za mawazo zipo lakini zisitugawe wala zisiharibu utulivu wa kisiasa na amani ya nchi yetu"
"Kwa wale wanaochokolewa masikio kuvunja amani ya nchi hii niwasihi acheni mara moja. Amani ikichafuka haichagui na tuulizeni sisi wa upande wa pili ilipochafuka amani Dar es Salaam tu pale nenda kaulize leo vijana kama wanataka kuingia njiani, hakuna anaetamani, amani ikivunjika haichagui."
Vilevile amekiri uwepo wa tofauti za mawazo akisisitiza zisitumike kuleta migawanyo ya kisiasa na kuharibu utulivu wa kisiasa nchini.
"Maendeleo yetu, kunawiri kwetu kupendeza kwetu, kulala na kuamka salama tutunze amani ya nchi yetu tofauti za mawazo zipo lakini zisitugawe wala zisiharibu utulivu wa kisiasa na amani ya nchi yetu"