The road towards 2010 Elections

The road towards 2010 Elections

Kati ya hawa nani atafaa kutuongoza 2010-2015?

  • Edward Lowassa

    Votes: 0 0.0%
  • Dr. Slaa

    Votes: 7 38.9%
  • Prof. Lipumba

    Votes: 0 0.0%
  • Mizengo Pinda

    Votes: 5 27.8%
  • Samwel Sitta

    Votes: 0 0.0%
  • Jakaya Kikwete

    Votes: 2 11.1%
  • Mark Mwandosya

    Votes: 2 11.1%
  • Harisson Mwakyembe

    Votes: 2 11.1%
  • None of The above

    Votes: 0 0.0%

  • Total voters
    18
  • Poll closed .
CCM Again, Hell NO!. Semilong, hebu tuwekee ya CHADEMA:

-Profesa Mwesiga Baregu
-Mfanyabiashara Freeman Mbowe
-Dr Wilbroad Slaa
-Dr Kitila Mkumbo
-Wakili Tundu Lissu

Nani kati yao anafaa kuwa Rais? Nani mwingine anafaa kuwemo kwenye hiyo orodha?

Halafu tutengenezee nyingine ya watanzania walio nje ya vyama. Wakina Issa Shivji, Reginald Mengi nk!

Asha
 
du

kuna mtu humu kasema jamaa akipewa kipindi cha pili ataharibu zaid. atakomba mpaka tutakoma. na mafisad watakuwa free kuanza upya. ebanaeeeeeeeeeee
 
Waboreya,
hii kitu haipo kabisa, una maneno mengi mkuu, lakini hapa wadanganye hao hao, kumbe na wewe ni wa aina ya mhariri wa mwanahalisi!
Haya maneno mazito sana na bahati mbaya ni kwamba staki kudaganya mtu haitanisaidia kitu zaidi ya kudhoofika..
Weka sababu zote unazotaka against Kikwete lakini huwezi kutoa sababu hata moja inayohusiana na Rostam au Lowass. nimewazoea sana watu kama nyie.. Mimi nafahamu fika kwamba Kikwete hana ubavu, hafai kuongoza nchi na kweli hana sifa ya Uongozi lakini kibaya zaidi ni kwamba hakuna mtu CCM mwenye uwezo huo.. that is the case!.
kama alivyosema Jasusi -None of the Above, hili ni neno zito sana..
Mimi nachofahamu Kikwete ni sawa na mwanamke ambaye mume wake ni malaya wa kutpa.. lakini mume huyo huyo ndiye anayemweka mjini..
Uamuzi wa Kikwete kuwashughulikia Mafisadi ni mdogo na pengine hakuna kabisa kwani Kikwete kama mwanamke yule pia ana historia yake..Ukielewa haya hasa kama ulikuwa ukifuatia mada zote za nyuma hapa JF bila shaka utaiona picha nzima..
 
JMK inafaa asigombee bali aombwe na vyama vyote apite bila kupingwa. Maendeleo anayotuletea sasa yalibidi yaletwe miaka 40 iliyopita .

huyu nae bwana. kila mara mi niko kinyume nyume naye. is there something wrong with me? or there is something wrong with him/her?
 
huyu nae bwana. kila mara mi niko kinyume nyume naye. is there something wrong with me? or there is something wrong with him/her?

Mwakatojofu,

Yaani aliyekupa hilo jina aliudharau kweli kweli, kule kwetu hakuna mwakatojofu yaani huwezi kuwa kajinga miongoni mwa wajinga. Kuna Mwaitojofu, yaani lile lililokubuhu miongoni mwa wajinga (Mwaitojofu) kwi kwi kwi!!!!

Easter njema wakuu!
 
Waboreya,

Mimi nafahamu fika kwamba Kikwete hana ubavu, hafai kuongoza nchi na kweli hana sifa ya Uongozi lakini kibaya zaidi ni kwamba hakuna mtu CCM mwenye uwezo huo.. that is the case!.
kama alivyosema Jasusi -None of the Above, hili ni neno zito sana..
Mimi nachofahamu Kikwete ni sawa na mwanamke ambaye mume wake ni malaya wa kutpa.. lakini mume huyo huyo ndiye anayemweka mjini..
Uamuzi wa Kikwete kuwashughulikia Mafisadi ni mdogo na pengine hakuna ..

Kama unajua hayo mkuu what makes you to say afadhali JK aendelee kuliko wengine!

Pia nijuvye habari gani au kitu gani kinamtofautisha JK na EL na RA, are they not friends?
 
Waboreya,
Kama unajua hayo mkuu what makes you to say afadhali JK aendelee kuliko wengine!

Pia nijuvye habari gani au kitu gani kinamtofautisha JK na EL na RA, are they not friends?
He is the President..na bado tunapumua ni uafadhali huo ndio unamfanya tofauti na wengine..
Friends? - No, Used to be!
 
Waboreya,

He is the President..na bado tunapumua ni uafadhali huo ndio unamfanya tofauti na wengine..
Friends? - No, Used to be!

Asipokuwa Rais tutaacha kupumua... ni kitu alichokifanya kinachowafanya Watanzania wapumue....Yeye amekuwa Mungu!? 😕 😕 😕
 
Mh.Lyatonga Mrema alipokuwa akizungumza na TBC taifa jana alisema kwake yeye Urais si dili 2010 bali atagombea Ubunge.Maana ya dili ni namna fulana ya kufanya ili kunufaika kiuchumi,sijui kama Mheshimiwa alikuwa na maana hiyo lakini ni wazi kuwa amegundua kuwa mbio za Urais haziwezi.Kinachosikitisha zaidi ni ubakaji wa demokrasia anaofanya wa kuwafukuza uanachama kila anayepingana naye.Kwa mtindo huu hakuna upinzani wa hoja bali wa maslahi.Kupitia JF Mh.Mrema ashauriwe njia sahihi anayopaswa kufuata ili astaafu siasa vizuri kama wanasiasa wenzake kama akina Mtei,Makani na wengine.
 
...Something is Definitely Cooking! Kwenye taarifa ya habari ya ITV ya saa mbili usiku kuna habari tatu zilizotokea maeneo tofauti nchini lakini zenye muelekeo mmoja:

1. Vijana CCM Dodoma wameandamana kuunga mkono maneno ya Mzee Cigwiyemisi ya kutaka Mheshimiwa Kikwete apewe nafasi nyingine tena ili kumaliza kazi alizoanza e.g kupiga vita Ufisadi, wauaji wa Albino.

2. Akina mama wa Wilaya moja ya Moshi nao wametoa tamko kama hilo hilo la kutaka Kikwete kuwa mgombea pekee wa Urais kutoka CCM

3. Kuna wazee kutoka Wilaya nyingine nchini ambayo bahati mbaya sikusikia jina lake nao wametaka Mheshimiwa Kikwete kupewa nafasi ya kumaliza kazi alizoanza!

Nafahamu kwamba hakuna tatizo lolote kwa taarifa moja ya Habari kuwa na matukio matatu kutoka maeneo matatu tofauti nchini TZ yote yakihusu Mheshimiwa Kiwete kuwa mgombea pekee wa Uraisi kutoka CCM, but it just makes one raise an eyebrow....!

wasiwasi wangu mimi ni mmoja: kama wanamkubali kikwete wanahofia nini kumpambanisha na wanachama wengine CCM..haingii akilini kuona mgombea anakubalika afu watu wanapata hofu kibao ooh mara hatumtambui yule mara tunaandamana saa mnafanya hivyo kumwambia nani? Sisi watanzania hatubabaishwi na propaganda zenu zilizopitwa na wakati...wacheni demokrasia iamue si kuleta ujanja ujanja tu.
 
toleola35_phixr.jpg


Makala motomoto: "wameuza haki yetu ya mzaliwa wa kwanza!" pamoja na Habari nyingine ambazo huwezi kuzipata mahali popote kwa kulipia!
 

Attachments

Last edited by a moderator:
Wanaodharau watanzania hawajui wanachokisema na hawajui dalili za mabadiko ya kweli. Ukitazama, ukisoma au ukisikiliza maoni mbalimbali ya watu utaona kuwa zama za kuamini kuwa watu wachache au kundi fulani la watu linaweza kuongoza Tanzania zimepitwa na wakati.Kuna vuguvugu kubwa la chini chini. Niwape mifano miwili tu juu ya hili: moja, wapo wananchi wengi vijijini wanaosema waliopewa vocha za mbolea yenye ruzuku ndio watakaoichagua CCM mwakani na wapo waliobadilisha vocha hizo kwa crate za bia. Ukienda Ruvuma, ukitaka Bia ya safari au Serengeti we sema nataka minjingu. Pili wapo watu wanaoona kuwa kundi fulani la watu limekuwa likiendeleza uhalifu na halichukuliwi hatua kwasababu tu wanajiita ni wana CCM. Hebu angalia ule mfano wa Diwani aliyeharibu miundo mbinu ya umwagiliaji kule Pawaga Iringa ambako ni eneo la ukame na mwaka huu hakuna possibility ya watu kupata chakula halafu PM anasema Diwani huyo afutiwe kesi kwakuwa kumshitaki ni kuharibu sifa za Chama. Haieleweki tunasimamia nini siku hizi kwasababu sidhani kama magereza yalijengwa kwa ajili ya wanyonge wasio wana CCM. Ukiitazama sana Serikali na hsa wanasisa waliopewa dhamana ya kuisimamia utaona karibu wote, wana lengo moja kupata sifa na kuwaacha wananchi wakiwa maskini.
 
Nimefurahia makala ya Da'Jessy.

Matatizo makubwa (kama ufisadi wa jumla etc) huanza na vitu ambavyo pengine tutaviona vidogo (maadili ya nyumbani na malezi)

Kama lile tangazo la dawa ya kichwa linavyosema "Maumivu ya kichwa huanza pooole pole..."

Au methali ya Kiswahili inavyosema "Usipoziba ufa, utajenga ukuta"

Kudos kwa ku-observe hili swala la maadili katika malezi.
 
Tatizo kwanini hawakati kamba na kuelekea kwengine ,Mwalimu Nyerere alikwishawambia kuwa huwezi kupinga wakati umo ndani ya CCM ni lazima utafute uwe nje ya Chama ndio upinge,kubakia CCM ni kuendeleza makundi yao,kila siku ninapiga makelele kama unaamini unawatumikia wananchi na wewe umo ndani ya CCM ,basi ukiona uchafu na hakuna linalotokea toka kwenye CCM ,kuna vyama tele vya upinzani na wananchi watakujua kwamba ulisimama kidete na umefanya kweli katika kuzikataa na kupinga hila za Chama cha mafisadi ,kwa msimamo wa Nyerere huwezi kuwemo ndani na ukawa mkweli kwa unayoyasema ,zaidi itaonekana ni majungu ,toka CCM na watu wasikie kuwa umetoka kwa sababu unazozipigia makelele kwa ufupi hakuna utawala wa sheria ndani ya CCM ,au sheria ni kwa walala hoi tu ,vibosile.
Ondoka huko CCM ,sasa kama kuna kundi linaona utawala uliopo ni wawachache kwanini halimeguki na kuongezea nguvu zao kwa upinzani ,wanabakia humo humo kuzozana ,zaidi itakuwa mmezidiana kete hamna ukweli wa kuwatendendea kuwaletea wananchi kile wanachokitafuta na kukisaka ,ugonvi wa matatizo yenu na machozi yenu ya mamba unatafuta huruma za wananchi ,lakini mnapiga makelele kwa sababu mmepigwa buti na kuzidiwa na wajanja miongoni mwenu.

Zaidi wananchi waelewe hawa wanaopigia makelele ndani ya CCM dhidi ya wenzao nao pia ni mafisadi ,dawa yao ikiwa mtu atabakia ndani ya CCM basi apigwe buti la nguvu katika uchaguzi ,aidha wapewe uhuru wa kujiengua ikiwa imebaki siku moja kupiga kura ili kuonyesha kupinga kwao , ila wanaubavu wa kufanya hivyo inataka mtu ambae amejitolea kupambana na CCM mpaka dakika ya mwisho. Kubaki na makelele yao ni hila za kuwadanganya wananchi.
 
wazazi kunahaja ya kuliangalia hiliswala la kuwaacha watoto kwenye kumbi za starehe mpaka usiku wa manane hata kama ni mara moja kwa mwaka
 
Wazazi hawawezi kuhusishwa na jambo hili kwani Serikali iliyopo madarakani ndio ,yenye uwezo wa kuzuia na kupiga marufuku na kuwapangia muda wa watoto kuwepo kwenye luninga za TV na hata huko kwenye kumbi za kuserebuka ,ni serikali na si mwingine yeyote.

Zanzibar walikuwa na muamko huo ,watoto walikuwa hawaruhusiwi kuwepo kwenye TV baada ya saa mbili za usiku na wakipita watu maalum kutazama kama sheria hiyo inafuatwa na kweli ilikuwa inafuatwa na mwisho watoto walizoea kuwa muda wao umekwisha na hutafuta kitanda kulala ,na wazee nao walipata nguvu kuwahimiza watoto wao kuondoka kwenye TV kwani kulikuwa na adhabu ya viboko kwa watoto na mzazi nae analipishwa au TV inachukuliwa na hivyo hivyo wahusika wa kumbi za disco japo kwa wakati huo zilikuwa zinahesabika hawakuruhusu watoto kuwepo na kuonekana sehemu hizo baada ya magharibi na hivyo kuleta muelekeo wa kizazi bora hapo baadae ,lakini ila kwa sasa mambo yote yameharibiwa na serikali ya Muungano.
 
Back
Top Bottom