Kweli Tumerogwa. Badala ya kujadili namna ya Kuendelea Kwanza Tumtafute Mchawi Wetu. Seriously Nimekubali kuwa Watanzania Tumerogwa. Seriously , Seriously , Seriously !!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Sasa Mnadhani atasema nini wakati yeye nd' anayepigiwa debe na kukingiwa kifua kama hivyo hata ningekuwa mimi nisingesema kitu! mi natamani siku nijitoe mhanga nife na FISADI mmoja wapo tena mzizi mkuu!
Sikusema popote kwamba nadhani, bali nimesema naamini kwamba ndani ya CCM anaweza kupatikana kiongozi bora mara 1,000 zaidi ya huyu Kikwete ambaye tangu aingie madarakani nchi imekuwa ikiyumba kuliko wakati wowote ule tangu tupate uhuru.
Ndugu WJM, BAK kaweka wazi kwamba kuna watu walio bora kuliko JMK ambao CCM inaweza kuwasimamisha and that is very very clear statement kwa hiyo sijaona mkanganyiko hapo. May be let me slow down: anasema ukipanga mstari wa viongozi kwa ubora katika viwango vya Ki-CCM JMK hawezi kusimama natumai sasa umeipata picha na ujumbe kamili!
Huyu ni mmoja wa kambi ya "Ni Mwenzetu huyu" hivyo kazi yake hapa ni kutaka kuonyesha kinachoandikwa na yeyote yule ambacho yeye hakiafiki kina kasoro. Tunajua fika kutokana na dalili za wazi kabisa kwamba upinzani hauna dalili ya kuchukua Urais 2010, lakini pamoja na hayo haina haja ya kumpa tena Kikwete. Katiba ya CCM inaruhusu wagombea wengine wanaotaka kufanya hivyo kuchukua form, sasa hivi vitisho dhidi yao vya nini tena? Na lini katiba ya CCM ilibadilishswa na kuruhusu vitisho kwa wale ambao wanataka kumpinga Rais!? Haya mambo ya unafiki ndiyo yanaifikisha nchi yetu pabaya. Rais kama kuna mazuri aliyoyafanya yawekwe hadharani, lakini hakuna hivyo Watanzania tunastahili kabisa kupata Rais mpya ambaye ataweka maslahi ya nchi mbele kwa manufaa ya Watanzania.
Msekwa: Enzi za kulindana,kubebana CCM zimekwisha
Basil Msongo
HabariLeo; Sunday, November 18, 2007 @00:03
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Pius Msekwa amesema enzi za kulindana, ‘mwenzetu' na kubebana katika chama hicho zimekwisha.
Jamani njaa ni kitu kibaya sana........dah
Wazee hao pia walieleza kukerwa na tabia ya baadhi ya wanachama wa CCM, walioamua kujitokeza hadharani na kulumbana kwani kufanya hivyo, kunakidhoofisha chama, huku kikijenga mgawanyiko miongoni mwa wananchi na kuendeleza chuki na uhasama.
"Suala la kukosoa, kujikosoa na kukosoana katika chama ni njia ya kukijenga na kukiimarisha chama chetu. Lakini ni kweli pia kuwa hatujajenga tabia hii ipasavyo. Mara nyingi tumependelea kuteteana na kufichiana makosa, awamu hii itaondokana nayo," alisema Msekwa.
...Sambamba na kukiri kulindana, Msekwa pia alikiri kuwa rushwa imetawala katika uchaguzi ndani ya chama hicho na kubainisha kwamba CCM haikumbatii rushwa ila utekelezaji na usimamizi wa sera ya chama hicho kupambana na rushwa umekwama.
Shadow naona sasa nchi inaelekea kwenye udikteta, maana hata failure kubwa ya uongozi wa Kikwete ambayo ni kupambana na ufisadi wale wanaotaka kuitumia kupambana naye wameshatishwa kwamba wasitumie ufisadi dhidi ya Kikwete!!! Wao wako tayari kutumia 'utamaduni wao' wa kumuachia Rais akae madarakni kwa awamu mbili, lakini wale wanaotaka kumpinga na kuleta vigezo vya kuonyesha kwamba Rais hastahili kuendelea kuwa madarakani kwa sababu kadhaa wa kadha wanatishwa!!!!
Mr 0, hakuna aliyerogwa labda wewe mwenyewe. Watu wako kazini. Unategemea nini baada ya madudu yote haya! Lazima kwanza mtu apime upepo na mikwara kibao ili aone ni kiasi gani amekalia kuti kavu. Sina hakika, ila naamini walikuwa na mkutano na mzee kabla ya kuja kuwachefua wananchi kupitia kwa waandishi wa habari! Kazi inaendelea na katika hii miezi kama 12 iliyobaki tutaona mengi sana.
Bubu bado hatujafika huko unakosema kwani hili si geni hapa kwetu. Nilitowa mfano wa Karume/Bilali na huu ulitendwa na wana CCM wote(mafisadi na mashujaa) na sikumbuki kama yupo hapa aliesimama na kuuzungumza huo upotevu wa Demokrasia. Ni CCM hii hii kwa kupitia Wazee hao hao waliosimama na kusema hawataki kutawaliwa na 'Mwarabu" na vyombo vya habari vikashajiisha ubaguzi huo. Wakati huo Demokrasia ilikuwa na maana.?
Nafikiri Wazee walichosema si cha uongo kuwa ni desturi yao CCM kuwaweka viongozi wao kwa vipindi viwili, na wazee hao hawakusema kuwa watamfukuza mtu kwenye chama, walichosema ni jambo la kawaida kuwa watamtetea wanaemuona anafaa. Tusilazimishe yule tunaemuona hafai kwa nadharia yetu kuwa hafai bali kama tuna hoja za kuuza kwa wananchi wenzetu na tufanye hivyo ili tuwafanye wakubali msimamo wetu.
Kulitangazia Taifa kuwa liko katika udikteta si sahihi kwani Si hivi tunajadili kwa uwazi bila oga na kumnanga kiongozi wa juu kabisa sasa demokrasia gani tunaihitaji. Tumuangushe JK kwa kura na kama kura ni demokrasia hili la kungangania nje ya kura lina maana gani?
...maandamano bila sababu za msingi ni uthibitisho tosha wa uvivu wetu wa kufikiri. Kama tunataka demokrasia ya kweli, ugombea pekee maana yake nini?
__________________
Mbu,
Mkuu uvivu wa kufikiri unaanza na sisi hapa JF.. Mimi nashindwa kabisa kuelewa kinachogomba hapa kwani hawa wazee ni wanachama walezi wa chama CCM ambao wana kila sababu kulingana na mtazamo wao kuwa Kikwete ndiye mgombea pekee wanayemtaka kwa tiketi ya CCM..Wana kila sababu ya kufanya kampeni hizo kwa sababu wanajua kinachoendelea ndani ya chama.. Wewe na mimi hatufahamu kitu. Hayo madogo aliyoyafanya Kikwete wameridhika nayo na pengine wanaelewa zaidi kinafuatia baada ya misafara na umaarufu...
Sisi hapa tumeanza kupinga hoja hiyo na kuita ni Udikteta kama vile ndio kwanza tunakuwa na mgombea urais kwa vipindi viwili..Halafu kinachonishinda kabisa kuelewa ni mtu kama Bubu ambaye siku zote analia na CCM waondolewe madarakani kama vile ni mpinzani lakini inapofikia swala la Kikwete kusimama tena inamwasha sana lakini pia ameshindwa kutupa mgombea ambaye anaweza kufikisha salamu za hayo maombi yake,,
Kikwete ameshindwa kufuta Ufisadi na ikiwa kweli Ufisadi ndiye adui yetu mkubwa kwa nini bado mnafikiria CCM?.. kwa nini bado watu wanafikiri kiongozi bora atatoka CCM kama huu sii uvivu wa kufikiri kitu gani?..
Binafsi sioni big deal kabisa chaguo la wazee hao na kusema kweli sioni kiongozi bora ndani ya CCM ambaye ataweza kutimiza yale nayoyataka..Wengi ambao ningefikiria pengine wanaweza kuleta mabadiliko wameondoka ktk kurupushani za siasa..Waliobakia wote wanaogopa Mtandao kama anavyoogopa Kikwete mwenyewe!
Tuna watu kama Dr. Slaa akienda sambamba na Mafisadi, akichukua kila kitu hatua kwa hatua lakini ameshindwa kwenda mbele kwa sababu hana ubavu..Now, just imagine mtu huyu anakuwa Rais au Waziri Mkuu wa Tanzania!..
Matatizo yetu yote yamekwisha!