The road towards 2010 Elections

The road towards 2010 Elections

Kati ya hawa nani atafaa kutuongoza 2010-2015?

  • Edward Lowassa

    Votes: 0 0.0%
  • Dr. Slaa

    Votes: 7 38.9%
  • Prof. Lipumba

    Votes: 0 0.0%
  • Mizengo Pinda

    Votes: 5 27.8%
  • Samwel Sitta

    Votes: 0 0.0%
  • Jakaya Kikwete

    Votes: 2 11.1%
  • Mark Mwandosya

    Votes: 2 11.1%
  • Harisson Mwakyembe

    Votes: 2 11.1%
  • None of The above

    Votes: 0 0.0%

  • Total voters
    18
  • Poll closed .
Hata mimi sielewi ndugu yangu, inasikitisha kwa kweli halafu Kikwete mwenyewe pamoja na vitisho hivi yeye kakaa kimya kabisa kama kawaida yake!!!!

The man is always the key actor, he organises fake deals remotely and pretend to be not part of nor know it
 
Hawa unaowasikia wanampinga Karume ,maana Karume anatayarishwa kuchukua nafasi ya Kikwete ,ikiwa Kikwete ataamua kuachia ngazi ,ila wapo katika kutoa ishara kuwa hakuna sababu ya Kikwete kuachia ngazi, kama unakumbuka Mwinyi alipomaliza kuwa Raisi wa Zanzibar alipewa wa Tanzania na ndio hivyo hivyo ,kama unavyofahamu taratibu za CCM ,ili kujificha na ile dhana kuwa Zanzibar haipewi uongozi wa Tanzania ,ndio inaonekana kuwa Karume apishwe katika kipindi hiki au hata Kikwete akimaliza miaka kumi yake kama akiipata apewe Karume.Ni utaratibu wanaosema wamejipangia au wameamua kuurudisha ili kudumisha muungano.

Mkuu, kina nani hao wanaosema wamejipangia utaratibu huo?

Frankly, itakuwa ngumu kwa KARUME kuchukua urais whether 2010 or 2015
 
Wewe Mwiba, nani kakuambia Karume anasifa za kuwa rais wa Tanzania? Unaacha kuangalia watu wenye uwezo na mtizamo? huyo sana sana labda kuwa mkuu wa mkoa tu.

Hivi sifa za kuwa Rais wa Tanzania ni zipi? Kusafiri kila siku au? Please advise..
 
Bubu Ataka Kusema,
Mkuu swali langu rahisi sana.. kama yeye hafai nani anafaa?.. ambaye wewe una hakika atayaleta yale unayoyataka.. mwenye kutimiza ahadi zake maanake nijuavyo Mimi sii Mwinyi wala Mkapa walitimiza lolote..
Ukishindwa hilo bila shaka ni kutokana na uvivu wa kufikiri..Unapinga kitu ukiwa na solution mkononi, kama huna wewe pia mvivu vile vile, ndio nachosema mimi..

Wako wengi tu ambao kwa kujua udhaifu utakaomfanya Kikwete asikae madarakani kwa awamu ya pili, wao watayafanya yale ambayo Kikwete alikuwa anayaogopa kuyafanya kwa kuwa ni Kiongozi dhaifu na hao anaowaogopa kama akina Rostam, Karamagi na wengineo wengi ambao wana tuhuma nzito za kifisadi watachukuliwa hatua za kisheria bila woga wowote. Kwanini tunyooshe mikono juu eti Kikwete aendelee tu kwa sababu hakuna mwingine? Kwenye Urais huwezi kuwa na solution maana hakuna yoyote aliyewahi kushika nafasi hiyo zaidi ya Nyerere ambaye ni marehemu, Mkapa na Mwinyi ambao wamemaliza muda wao na hawaruhusiwi tena kurudi madarakani. Nchi ya watu 40 millioni kweli tushindwe kupata Kiongozi mzuri kuliko Kikwete!!!!! 😕 Haya kwangu ya kung'ang'ania Kikwete aendelee ni maajabu ya hali ya juu. Kuwe na sababu za kiutendaji ambazo zimeturidhisha Watanzania na hivyo kumuona anastahili kuendelea na miaka mitano mingine, lakini hili la 'utamaduni wa kuachiana' eti Mwinyi tulimuachia miaka mitano mingine na Mkapa tukamuachia miaka mitano basi na Kikwete tumuachie miaka mitano mingine kamwe siafikiani nalo!!!!
 
Wako wengi tu ambao kwa kujua udhaifu utakaomfanya Kikwete asikae madarakani kwa awamu ya pili, wao watayafanya yale ambayo Kikwete alikuwa anayaogopa kuyafanya kwa kuwa ni Kiongozi dhaifu na hao anaowaogopa kama akina Rostam, Karamagi na wengineo wengi ambao wana tuhuma nzito za kifisadi watachukuliwa hatua za kisheria bila woga wowote. Kwanini tunyooshe mikono juu eti Kikwete aendelee tu kwa sababu hakuna mwingine? Kwenye Urais huwezi kuwa na solution maana hakuna yoyote aliyewahi kushika nafasi hiyo zaidi ya Nyerere ambaye ni marehemu, Mkapa na Mwinyi ambao wamemaliza muda wao na hawaruhusiwi tena kurudi madarakani. Nchi ya watu 40 millioni kweli tushindwe kupata Kiongozi mzuri kuliko Kikwete!!!!! 😕 Haya kwangu ya kung'ang'ania Kikwete aendelee ni maajabu ya hali ya juu. Kuwe na sababu za kiutendaji ambazo zimeturidhisha Watanzania na hivyo kumuona anastahili kuendelea na miaka mitano mingine, lakini hili la 'utamaduni wa kuachiana' eti Mwinyi tulimuachia miaka mitano mingine na Mkapa tukamuachia miaka mitano basi na Kikwete tumuachie miaka mitano mingine kamwe siafikiani nalo!!!!


MKUU BUBU kwanini hutaki kutusikia nasi wenzio. Tumeshakusikia kuwa JK aasirudi tena kwenye madaraka lakinimbona hutaki kulisaidia Taifa katika mchakato wa kumtafuta mbadala wa JK?
Unatwambia kuwa tusikate tamaa bali tutampata mbadala tu tena kutoka CCM hiii hii tunayoijuwa. Sijui kiasi gani wewe mwenyewe unaamini hili lakini wengi wetu tunaona kuwa mbadala huyo kutoka CCM kama hayupo.
Hoja yako ya kumuondowa Jk na kumpata mbadala wake mpaka sasa umeijenga katika ufisadi tu,tu. Tunashindwa kumpata mpiganaji halisi wa Ufisadi kutoka CCM kwani Ufisadi ndio uliowaweka madarakani Wabunge wote wa CCM. Kama walipandia ngazi hiyo wana nguvu gani kuipiga mateke?
Ufisadi si kila kitu katika maendeleo ya nchi yetu hivyo ubora wa kiongozi hautapimwa kwa ufisadi peke yake bali kuna mambo mengine chungu nzima pengine JK amewashinda wengine. Halafu uozo huu mbona ulishakuwepo toka kiongozi wa mwanzo iweje sasa kumshikia bango huyu mmoja tu ambae angalau anachukua hatuwa.
Bubu utakuwa umetusaidia kama utatowa hadharani wateule wako na wala usiogope kuwa watachambuliwa, kwani angalau tutakuwa tumepiga hatuwa moja katika kulitekeleza hili la kumzuia JK asigombee tena.
 
Bubu ataka kusema,
Wako wengi tu ambao kwa kujua udhaifu utakaomfanya Kikwete asikae madarakani kwa awamu ya pili, wao watayafanya yale ambayo Kikwete alikuwa anayaogopa kuyafanya kwa kuwa ni Kiongozi dhaifu na hao anaowaogopa kama akina Rostam, Karamagi na wengineo wengi ambao wana tuhuma nzito za kifisadi watachukuliwa hatua za kisheria bila woga wowote
Ama kweli bubu ataka kusema...duh..Nauliza tena ni kina nani hao?..
 
mwinyi katulaghai tume mmpa miaka kumi....
mkapa katulaghai tume mmpa miaka kumi...

kosa si kosa bali kosa ni kurudia kosa , mwinyi na mkapa inatosha
kikwete katulaghai sasa hivi kwa hiyo inatakiwa miaka mitano mwisho na wengine wote watakaofuata watajua atutaki mchezo.
 
Wakuu kinachowauma nini haswa.. yaani hawa wazee hawana haki ya kumteua mtu wanayempenda?.. jamani semeni nanyi chaguo lenu kisha pinganeni na usemi huo wa wazee hao na kuzipanga sababu zenu lakini mnaposema Kikwete hafai aondolewe hali hamna mtu mwingne inachekesha...
Mada hii mefikia kurasa zaidi ya nne na hakuna hata mmoja wenu amediriki kumtaja mgombea dhidi ya Kikwewe kwa tiketi ya chama..
Na nimeliweka swali hilo makusudi kwa sababu naelewa fika kwamba CCM bila Kikwete haiwezi kwenda popote. hakuna na narudia kusema hakuna kiongozi CCM anayeweza kuwa mbora kuliko Kikwete ktk kiti cha Ikulu.. chama kizima Muflisi, kimeshikwa na mafisadi.. Sii Mwandosya, magufuli wala mjomba wake anayeweza kuinua hata kidole against kundi hilo..
Wanaojiweza kidogo ni Mwakyembe, Sitta, Mama Kilango, na Malecela.. hawa wote ni watu wa Kikwete na wanampendekeza Kikwete kwa sababu hawawezi kupita hata Ubunge 2010 kama sio nguvu ya Kikwete..haya tukiondoa hawa huko CCM kabakia nani?..nani anaweza kumkemea Rostam au Lowassa! nani anaweza kusimama na hawa jamaa na kuwatazama usoni akawaambia wanakwenda lupango!..hakuna...
Hakuna rais hata mmoja anayeweza kuendesha nchi peke yake bila nguvu ya chama nyuma yake -hakuna..Sii Tanzania wala Afrika nzima!
 
MKUU BUBU kwanini hutaki kutusikia nasi wenzio. Tumeshakusikia kuwa JK aasirudi tena kwenye madaraka lakinimbona hutaki kulisaidia Taifa katika mchakato wa kumtafuta mbadala wa JK?

Wote wanaotaka kugombea toka CCM kama ni akima Mwandosya na wengineo wote waruhusiwe kuchukua form na kuwe na mjadala kati yao na atakayeonekana anafaaa kuliko mwingine basi apitishwe. Hili la kutoa jina kwamba fulani anafaa mimi siliafiki maana nakumbuka Mwalimu (RIP) alisema Mkapa ndiye aliyemuona anafaa kuwa Rais 1995 yalitokea baada ya hapo wote tunayajua.

Unatwambia kuwa tusikate tamaa bali tutampata mbadala tu tena kutoka CCM hiii hii tunayoijuwa. Sijui kiasi gani wewe mwenyewe unaamini hili lakini wengi wetu tunaona kuwa mbadala huyo kutoka CCM kama hayupo.

Vigezo gani mlivyotumia kufikia conclusion kwamba ndani ya CCM hakuna mbadala wa Kikwete? Hata wanaotaka kugombea hawajapewa nafasi ya kufanya hivyo, tayari nyie mmeshaona kwamba hakuna mwingine ila Kikwete!!! Je mmeenda kwa Sheikh Yahya au kwa Toboa tobo kuweza kufikia conclusion yenu!?

Hoja yako ya kumuondowa Jk na kumpata mbadala wake mpaka sasa umeijenga katika ufisadi tu,tu. Tunashindwa kumpata mpiganaji halisi wa Ufisadi kutoka CCM kwani Ufisadi ndio uliowaweka madarakani Wabunge wote wa CCM. Kama walipandia ngazi hiyo wana nguvu gani kuipiga mateke?

Kikwete kashindwa kupambana na mafisadi ndiyo maana wahusika wote wa ufisadi akina Chenge, Rostam, Idissa Rashid na wengine wengi bado wanapeta uraiani. Huoni Rais ambaye anashindwa kutetea sheria za nchi na kuweka maslahi ya nchi mbele kwamba hafai kuiongoza nchi hiyo maana sheria za nchi zinazidi kukiukwa kila kukicha bila athari yoyote kwa wale wanaokiuka sheria hizo? Wakati umefika wa kutafuta mtu atakayeisafisha CCM na Tanzania kwa ujumla

Ufisadi si kila kitu katika maendeleo ya nchi yetu hivyo ubora wa kiongozi hautapimwa kwa ufisadi peke yake bali kuna mambo mengine chungu nzima pengine JK amewashinda wengine. Halafu uozo huu mbona ulishakuwepo toka kiongozi wa mwanzo iweje sasa kumshikia bango huyu mmoja tu ambae angalau anachukua hatuwa.

Kwako wewe ufisadi si kila kitu katika maendeleo lakini inapotokea watu wanaifisadi nchi karibu shilingi Trilioni ($1 billion approximately)moja katika kipindi kifupi na kama ukaguzi wa EPA ungefanywa kuanzia 1995 mpaka 2006 badala ya 2005/2006 basi si ajabu pesa iliyoibwa ingefika hata shilingi Trilioni 2 ($2 billion approximately) , hili ni tatizo kubwa sana kwa nchi yoyote ile inayotaka kupata maendeleo kwa wananchi wake wote, kama wewe unaliona hili ni dogo hiyo ni juu yako. Inapotokea Rais anashindwa kuhakikisha rasilimali za nchi zinawanufaisha wageni badala ya wananchi wake pamoja na kuwa aliahidi kulishughulikia tatizo hilo hii ni dalili nyingine ya kiongozi dhaifu ambaye hastahili tena kurudi madarakani. Je ni akina nani hao uliowasema hapo juu walioshindwa na Kikwete!? Na wameshindwa katika mambo gani!? Na hiyo tathmini iliyomuonyesha Kikwete kawashinda hao ilifanyika lini na wapi!?[/B]

Bubu utakuwa umetusaidia kama utatowa hadharani wateule wako na wala usiogope kuwa watachambuliwa, kwani angalau tutakuwa tumepiga hatuwa moja katika kulitekeleza hili la kumzuia JK asigombee tena.

Narudia tena, ndani ya CCM kuna wengi ambao wanaona wana uwezo wa kuiongoza Tanzania vizuri zaidi ukilinganisha na Kikwete. Katiba ya CCM na ya nchi pia zinawaruhusu kugombea nafasi hiyo bila vitisho wala mizengwe toka kwa Malecela, Chiligati, Msekwa au Wazee wa CCM. Hakuna haja ya mimi kutamka kwamba fulani ndiye anayefaa kuwa Rais 2010. Wote wanaotaka kugombea ndani ya CCM waachwe wafanye hivyo na kama baada ya taratibu zote ndani ya CCM kufuatwa na bado ikaonekana Kikwete ndiye anayefaa kuwa mgombea wa CCM basi hapo taratibu za CCM zitakuwa zimefuatwa bila upendeleo wala vitisho dhidi ya wagombea wengine, lakini huu udikteta wa "watakaompinga Kikwete watakiona" na "Wasitumie ufisadi kutaka umaarufu wa kisiasa' Kamwe hilo mimi silikubali. Mambo ya kulinda viongozi dhaifu na mafisadi ni lazima tuyapige vita kwa nguvu zetu zote maana hawa ndiyo tatizo kubwa la nchi yetu kutokuwa na maendeleo ya kuridhisha pamoja na misaada na mikopo chungu nzima tunayopata toka nchi mbali mbali za wafadhili na mashirika ya kimataifa pamoja na rasilimali nyingi tulizojaaliwa na Mungu.
 
mwinyi katulaghai tume mmpa miaka kumi....
mkapa katulaghai tume mmpa miaka kumi...

kosa si kosa bali kosa ni kurudia kosa , mwinyi na mkapa inatosha
kikwete katulaghai sasa hivi kwa hiyo inatakiwa miaka mitano mwisho na wengine wote watakaofuata watajua atutaki mchezo.

Naam lazima tuachane na huu utamaduni wa kuachiana Rais akae madarakani kwa awamu mbili. Rais ni lazima aweze kufanya mambo mbali mbali ambayo yanawagusa wananchi kwa namna moja au nyingine katika kunyanyua viwango vya maisha yao na hivyo kuharakisha maendeleo ya nchi. Kikwete kashindwa kufanya hivyo na hiyo ni sababu tosha ya yeye kuwekwa pembeni.
 
Bubu ataka kusema,

Ama kweli bubu ataka kusema...duh..Nauliza tena ni kina nani hao?..

Wako wengi tu!!!! Unategemea mimi nitawajua majina wagombea wanaotaka kutumia haki yao ya kikatiba katika chama chenye wanachama milioni 4!!!!? 😕
 
Semilong,
mwinyi katulaghai tume mmpa miaka kumi....
mkapa katulaghai tume mmpa miaka kumi...
kosa si kosa bali kosa ni kurudia kosa , mwinyi na mkapa inatosha
kikwete katulaghai sasa hivi kwa hiyo inatakiwa miaka mitano mwisho na wengine wote watakaofuata watajua atutaki mchezo.
Mkuu wangu weee hivi kweli umeshindwa kuliona kosa bali unavumbua kosa kwa mtindo wa Vasco Dagama..
Kosa ni kuwachagua Mwinyi na Mkapa kuwa marais...hakuna hata siku moja miaka ikawa sababu ya makosa ya uchaguzi bali ni uchaguzi wa mtu wenyewe ndio una makosa..
sasa unaposema makosa Kumchagua Kikwete ni vizuri sana ukafikiria kuchagua nje ya Kikwete na wagombea watakuwepo.. That's the ONLY solution uliyokuwa nayo. Usitake kulazimisha bus linalokwenda Mbeya lisimame kwa sababu Ulitegemea kwamba hao madereva hupokeza njiani..Umeshaambiwa utaratibu wao sio hivyo bado hutaki, kama hutaki safari ya CCM shuka wewe acha wengine waendelee na safari..
 
Semilong,

Mkuu wangu weee hivi kweli umeshindwa kuliona kosa bali unavumbua kosa kwa mtindo wa Vasco Dagama..
Kosa ni kuwachagua Mwinyi na Mkapa kuwa marais...hakuna hata siku moja miaka ikawa sababu ya makosa ya uchaguzi bali ni uchaguzi wa mtu wenyewe ndio una makosa..
sasa unaposema makosa Kumchagua Kikwete ni vizuri sana ukafikiria kuchagua nje ya Kikwete na wagombea watakuwepo.. That's the ONLY solution uliyokuwa nayo. Usitake kulazimisha bus linalokwenda Mbeya lisimame kwa sababu Ulitegemea kwamba hao madereva hupokeza njiani..Umeshaambiwa utaratibu wao sio hivyo bado hutaki, kama hutaki safari ya CCM shuka wewe acha wengine waendelee na safari..

Taratibu za katiba ndani ya CCM zifuatwe bila kutumia vitisho wala upendeleo au michuzi ya kifisadi. Imagine wale akina 'Malecela', 'Chiligati', 'Msekwa' na Wazee wa Chama ndani ya Democratic party wangewatishia wagombea waliompinga Hillary katika kinyang'anyiro cha kumpata mgombea wa chama chao katika uchaguzi mkuu wa 2008 na kauli kama hizi, "Watakaompinga Hillary ndani ya Chama watakiona" Obama naye angejikunja zake kwa kuogopa vitisho na kusahau ndoto zake kwamba na yeye ana nafasi ya kuwa Rais wa Marekani pamoja na kuwa ni Mweusi, he has a funny name according to political analysts, Baba yake ni Muislamu na middle name yake ni Hussein just like the other guy in that country. Dunia isingepata bahati ya kuiona history ya miaka 252 tangu Marekani ipate uhuru. Pamoja na political pundits kudai kwamba "Hillary has no competition, This one is over baby, It is Hillary Clinton in 2008 and whoever will be the choice of the Republican party."

Akasimama mwanaume Obama akaanza kumwaga sera zake toka kona moja ya nchi hadi kona nyingine. Watu wakaanza kupay attention taratibu, hata weusi waliodai kwamba Obama does not speak of the issues such as police brutality, high unemployment rates, poor living conditions etc wakaanza na kumsikiliza na wengi wao waliokuwa kwenye kambi ya Hillary wakaanza kuhamia taratibu kwenye kambi ya Obama, mara tu ile advantage aliyokuwa nayo Hillary kwenye opinion polls ya points 24 ikapotea na Obama akawa mbele, pamoja na Clinton kuwa na very good organisation lakini kijana akawapiga chini na leo Obama ni kipenzi si tu cha Wamarekani bali dunia nzima. Kila anapoenda anapata umati wa watu ambao wako excited na yeye kuchaguliwa kama Rais wa Marekani. Ameingia wakati mgumu sana kuliko Rais yoyote yule wa Marekani hivyo kazi iliyo mbele yake ni kubwa sana lakini anaweza kabisa kufanikiwa na juhudi zake zinaonekana.

Sasa na Tanzania tunaweza kabisa kupata Obama wetu ambaye hana jina kubwa wala hajulikani ndani ya Tanzania na ni mwanachama wa CCM. Huyu si ajabu amehamasishwa na ushindi wa Obama naye akajaribu bahati yake na kuzikonga nyoyo za Watanzania kutoka kona moja ya nchi hadi nyingine kutokana na yale atakayoyazungumza kama sera zake ambayo labda yatakuwa yanagusa maisha ya Watanzania walio wengi ya kila siku na hivyo kuweza kumbwaga Kikwete maana hata wale wapiga debe wake wanaweza kabisa kumtelekeza baada ya kumsikiliza huyo mgombea asiye na jina kubwa na safari hii michuzi ya kifisadi toka Kagoda, Meremeta, Deep Green iliyotolewa na fisadi Rostam labda haitakuwepo hivyo hapo ni kumwaga sera tu na kipi alichokifanya akiwa madarakani kinachostahili apewe nafasi nyingine, hakuna rushwa au kutumia mafisadi kumbeba mtu.

Tuache tabia ya kujidumaza na kutotaka kuumiza vichwa vyetu, YES we have to think outside the box especially in this century. Naam, tunaweza kabisa kumpata Rais asiye na jina kubwa toka CCM na akafanya kazi nzuri zaidi kuliko Kikwete na kuwafurahisha Watanzania wote ndani ya CCM, Upinzani na hata wale tusio na vyama. YES WE CAN!!!!!
 
Urais CCM 2010: JK apewa mtihani mzito

Monday, 06 April 2009 16:49

Kauli za wenyeviti zazua jambo

Na Said Mwishehe

Majira

KUNDI la watu waliojitambulisha kuwa wana-CCM wa Mrengo wa kati au wana-CCM Mseto limedai litampinga Mwenyekiti wa chama hicho Rais Jakaya Kikwete kwenye mchakato wa kutafuta mgombea urais kwa tiketi ya chama hicho mwakani kama atashindwa kuwashughulikia mafisadi waliopo ndani ya chama hicho.

Wanachama hao wamedai endapo chama hicho kitazidi kukumbatia mafisadi na kuwaonea haya kuwatosa kisiasa, watakuwa tayari kuondoka CCM na kujiunga na kambi ya upinzani ili kuendeleza mapambano dhidi ya ufisadi.

Kauli ya wanachama hao imekuja siku moja baada ya wenyeviti wa mikoa wastaafu wa CCM kutoa tamko la kupambana na wenye nia ya kusisima kumpinga Rais Kikwete kwenye uchanguzi mkuu ujao mwakani.

Hata hivyo walisema hawamzuii mtu yeyote kugombea nafasi hiyo, lakini hawaoni sababu ya kuwapo upinzani wakati Rais Kikwete anatarajia kumalizia kipindi chake cha pili.

Wenyeviti hao wakiongonzwa na aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dodoma ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wa wenyeviti wa mikoa yote wa CCM, Bw. Pancras Ndejembi, walionya dhidi ya viongozi wa chama hicho wanaotaka kuyatumia mapambano ya rushwa kama mtaji wa kisiasa na kujipatia umaarufu.

Wakizungumza Dar es Salaam jana na Majira kwa masharti ya kutotajwa majina, makada hao walidai dhamira ya kweli ya Rais Kikwete kupambana na mafisadi itaonekana pale tu atakapowaengua haraka ndani ya chama watuhumiwa wote wa ufisadi.

"Uhakika wa kweli kama ameamua (Rais Kikwete) kufa na mafisadi ni pale tu tutakapoona wale waliohusika katika tuhuma za ufisadi wanashughulikiwa kikamilifu ndani ya CCM mbali ya kujiuzulu serikalini," kilisema chanzo hicho.

Wanachama hao walisema wanataka kuona mafisadi wote waliohusika na kashfa za Kagoda, Richmond, Buzwagi, Deep Green, Meremeta, Rada, IPTL na zingine wanatinga kortini au kuvuliwa uanachama kabla ya 2010 vinginevyo watakihama chama hicho.

"Umefika wakati kusema ukweli wa mwenendo mzima wa chama chetu. Haiwezekani chama kishindwe kuwachukulia hatua mafisadi na kuendelea kuwalea. Katika mazingira hayo lazima tumpinge kwa misingi ya kidemokrasia mwaka 2010. Kushindwa kuwashughulikia mafisadi ni kushindwa kusimamia utekelezaji wa Ilani ya chama," alisema kada huyo.

Kada mwingine kutoka kundi hilo alisisitiza kuwa watakuwa tayari kumuunga mkono Rais Kikwete katika uchaguzi huo endapo atafanya kazi moja tu ya kuhakikisha mafisadi waliopo ndani ya chama, wanachukulia hatua za kichama sasa ikiwa ni pamoja na kuvuliwa uanachama.


Alisema endapo Rais Kikwete ambaye ni Mwenyekiti wa chama hicho ataongoza mapambano kuwatimua wote wanaoandamwa na kashfa za ufisadi, atapita bila kupingwa.

Kada mwingine wa mrengo wa kati ambaye naye aliomba kutotajwa jina gazetini, aliwalaumu wenyeviti hao na kudai wameshindwa kutofautisha ukweli wa mambo na vita ya ufisadi inayoendelea.

"Hawa wenyeviti wanadhani mkakati wa kumpinga Rais Kikwete 2010 unaendeshwa na mafisadi, hili si kweli bali mafisadi ndio wanamponza Rais mbele ya wanachama safi kwa kushindwa kuwatosa!

"Hatuwataki mafisadi na tunataka chama kiwang'oe, hata wakiomba kura hatuwapi, ndio maana tunataka Rais Kikwete aoneshe njia kwa kuwatosa nje ya chama, vinginevyo na yeye tumpinge kidemokrasia kwenye mchakato mwakani," alisema kada huyo na kufafanua:

"Hawa wenyeviti ni kama wanatubeza sisi tunasema viongozi hususani Mwenyekiti Rais Kikwete aoneshe dhamira ya kweli kupambana na mafisadi, kama anashindwa kuwang'oa mafisadi ndani ya chama kwanini wanachama wengine watakaokuwa na ubavu wa kuwang'oa watu hao wasijitokeze tuwape nafasi?


"Kumtetea mtu aliyeshindwa kuwang'oa mafisadi ndani ya chama ni kama kushabikia ufisadi na kuwabeza waliojitolea kwa nguvu zote kupambana na ufisadi."

Kada huyo alisema baadhi ya viongozi wa ngazi za kati ndani ya chama hicho wakiwemo wabunge wamefanya kazi nzuri ya kupambana na mafisadi zaidi ya viongozi wakuu wa chama hicho, hivyo madai kwamba walio mstari wa mbele katika mapambano hayo wanajitafutia umaarufu hayana msingi.

Alitoa mfano kwa Mbunge wa Kyela (CCM), Dkt. Harrison Mwakyembe na Mbunge wa Nzega (CCM), Bw. Lucas Selelii kuwa wanapaswa kuwa mfano wa kuigwa kwa kazi nzuri waliyoifanya katika kupambana na mafisadi.

"Wanaopambana na ufisadi kama hao niliwataja lazima waungwe mkono, binafsi sioni kama Rais Kikwete anawashughulikia mafisadi waliopo ndani ya CCM. Mambo ya chama na Serikali ni tofauti, ukitimuliwa serikalini mnaanza kutafuta haki mahakamani, lakini chama ni kama dini ukishakuwa na doa ni kuondoka kama hutaki unaondolewa," alisema.

Alimtaka Rais Kikwete kufuata nyayo za Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere katika kukiongoza chama na kusema kwamba hakuvipa nafasi vitu hivyo na wote waliobainika, walitimuliwa bila kujali hali na nafasi zao.

Alikwenda mbali zaidi na kudai ana wasiwasi wenyeviti hao wasije wakawa wanatumiwa bila kujijua na baadhi ya watu ili kuwahadaa wanachama wengine na kupotosha dhana na matokeo ya vita ya ufisadi hadi sasa.

Wenyeviti walioambatana na Bw. Ndejembi ni aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Hemed Mkali, Bw. Tasir Mgoda (Iringa) na Bw. Jumanne Mangara (Pwani).


Hadi sasa miongoni mwa wana-CCM walioonesha nia ya kugombea urais kwa tiketi ya chama hicho ni pamoja na Mbunge wa Maswa, Bw. John Shibuda.

Last Updated ( Monday, 06 April 2009 17:18 )
 
Bubu ataka Kusema,
Wakizungumza Dar es Salaam jana na Majira kwa masharti ya kutotajwa majina, makada hao walidai dhamira ya kweli ya Rais Kikwete kupambana na mafisadi itaonekana pale tu atakapowaengua haraka ndani ya chama watuhumiwa wote wa ufisadi.
Mkuu, kwanza ningeomba mada hii iunganishwe na zile nyingine tunajaza ukumbi tu...
hata hivyo, haya madudu ndio nayazungumza - hakuna mtu CCM, sasa kama wewe unataka kupinga hoja kwa nini unajigubika na blanketi usionekane!.. Ndo unafiki huo, wajitokeze hadharani waseme ukweli wananchi wawasikie na wafahamu kwamba wapo watu wanaweza kusimama na Rostam/Lowassa na Mkapa ktk ufisadi..

Kumbuka mkuu wangu labda unasahau nguvu ya Mtandao, kumbuka Mzee Es alituambia nini wakati wa uchaguzi mkuu mwaka 2005 ndani ya chama CCM.. Mkapa, Kawawa na Mwinyi walifungwa midomo...Malecela alitupwa nje kama mbwa na hakuna mtu aliyesimama kutetea..salim kura hazikurudiwa kama utaratibu unavyotakiwa nahawa hawa waliunga mkono utaratibu unaovunja ilani ya chama, leo unambie ati kuna watu CCM wanataka mafisadi washughulikiwe..comeon now, watu wenyewe bila Rostam hawana kazi!

Ikiwa bungeni tu wameshindwa kunyoosha vidole vyao kupendekeza mafisadi wakidai Usalama wa nchi utapotea, leo unambie ati kuna watu wanataka JK asisimame.. Hawa wote ni Wanafiki wametumwa na Rostam/Lowassa, sio habari ya awamu mbili kwa sababu KJK kashindwa kazi.. nakwambia hakuna kati yao, hakuna hata mmoja angeweza kuwa ondoa madaraka hata watu wa usalama kina Apson au Mahita - Hakuna... that is the fact..
 
Bubu ataka Kusema,

Mkuu, kwanza ningeomba mada hii iunganishwe na zile nyingine tunajaza ukumbi tu...
hata hivyo, haya madudu ndio nayazungumza - hakuna mtu CCM, sasa kama wewe unataka kupinga hoja kwa nini unajigubika na blanketi usionekane!.. Ndo unafiki huo, wajitokeze hadharani waseme ukweli wananchi wawasikie na wafahamu kwamba wapo watu wanaweza kusimama na Rostam/Lowassa na Mkapa ktk ufisadi..

Kumbuka mkuu wangu labda unasahau nguvu ya Mtandao, kumbuka Mzee Es alituambia nini wakati wa uchaguzi mkuu mwaka 2005 ndani ya chama CCM.. Mkapa, Kawawa na Mwinyi walifungwa midomo...Malecela alitupwa nje kama mbwa na hakuna mtu aliyesimama kuettea, leo unambie ati kuna watu CCM wanataka mafisadi washughulikiwe..

Ikiwa bungeni tu wameshindwa kunyoosha vidole vyao kupendekeza mafisadi wakidai Usalama wa nchi utapotea, leo unambie ati kuna watu wanataka JK asisimame.. Hawa wote ni Wanafiki wametumwa na Rostam/Lowassa, sio habari ya awamu mbili kwa sababu KJK kashindwa kazi.. nakwambia hakuna kati yao, hakuna hata mmoja angeweza kuwa ondoa madaraka hata watu wa usalama kina Apson au Mahita - Hakuna... that is the fact..

Unataka wakolimbwe!!? Au umesahau nini kilichotokea baada ya Kolimba kutamka hadharani kwamba CCM haina mwelekeo!? Si umeona vitisho watakaompinga Kikwete kukiona!! Watu wana familia zao zinawategemea hivyo lazima wawe extra careful wakati huu wa vitisho na ubabe hadharani. Basi kama Rais anakuwa hana uwezo wa kuondoa madarakani watu aliwaoteua basi nchi ina matatizo makubwa sana, kama alivyosema aliyekuwa mshauri wa Commandoo kwamba nchi imeoza.
 
Bubu ataka kusema,
Mkuu hata sikuelewi kwani katiba ya chama Demokratik cha US na CCM zii sawa?.. Unazungumza kitu gani lakini hivi kwani kulikuwepo na watu waliompinga Bush au Clinton kutorudia kupindi cha pili hadi kufikia watoe kauli ile..Huyo Hillary anaingia vipi ktk mada hiii kimfano!

Mkuu labda hufahamu kinachoendelea na pengine unaifanya kazi ya watu kwa malipo yasiyokupa hifadhi yoyote... Mbinu za Rostam na watu wake nitazipinga hadi kesho na kama Kikwete hafai wewe nambie nani anafaa hizi habari za katiba hivi katiba vile hazina uhusiano kabisa na taratibu zinazokubalika ndani ya chama kimoja...Ni katiba hiyo hiyo mlilia na Lowassa abakie madarakani kama Waziri mkuu..
Kikwete hajasema anataka kuwa rais wa Tanzania nzima wala kubadilisha taratibu za awamu mbili isipokuwa kutokana na nguvu zinazotumika kuhakikisha anaondoka mwaka 2010 kama Mzee ES alivyotufahamisha wala sii muda mrefu hivyo wa kusahau..
Mkuu wangu mimi nakumbuka kila kitu kinachotokea humu na husubiri wakati kama huu kuwakumbusha kwani sisi Wadanganyika wepesi sana kusahau na bongo zetu zipo kizani kama miji yetu..Ni asilimia 14 tu yenye mwanga kichwani kama asilimia yenye umeme nchini..
Mtanisamehe lakini..
 
Bubu ataka kusema,
Wakolimbiwe na nani?.. sii wamesimama kupinga, sasa kazi yote ya nini kama wanaogopa kukolimbiwa.. Mtapinga vipi au mtawakilisha vipi hoja yenu kama sio Unafiki..haya ni magazeti ya Rostam tu hakuna mtu wala kiongozi ambaye yuko tayari kuhakikisha JK harudi mwaka 2010 na kwamba yeye atashughulikia kina Rostam. kama unaogopa kusema leo kweli huyo mtu atadiriki kusimama dhidi ya Mafia ya Rostam/Lowassa! acheni msifanye mzaha nyie..
Chagua Chadema mkuu wangu kwa nini unapata taabu hizi zote..
Mkandara nitaomba nafasi ya Hosea kisha tutazungumza - Haaa haaa haaa!
 
Unafiki ni huo wa kumtetea mtu ambaye hajafanya lolote katika awamu yake ya kwanza na kuna ushahidi chungu nzima wa kuthibitisha hilo na kutumia vitisho na ubabe kutaka kumpitisha, huo ndiyo unafiki ambao hauweki mbele maslahi ya nchi bali ya Kikwete na wapiga debe wake ambao si ajabu hawafikii hata Watanzania millioni moja. Taratibu za chama zinajulikana ni kipi kinachowafanya wapindishe taratibu hizo na kuanza kutumia vitisho!!!? Naona si ajabu wakipata nguvu kwamba wamewanyamazisha wapinzani wa Kikwete basi wanaweza kuja na kauli, "Atakayepinga kununuliwa mitambo ya Dowans ndani ya CCM kukiona."

Ama kweli Tanzania tumejidumaza mno na ni wavivu wa kufikiri, maana kuna juhudi kubwa sana za kuwanyamazisha wale wote ambao wanataka Kikwete asigombee tena 2010 na sasa wameanza kutumia hata vitisho na ubabe. Ukiwaambia waorodhoshe mazuri yaliyofanywa na Kikwete hawana hata moja watatoa blanket statement kwamba amefanya mazuri hivyo ni yeye tu!!! Maskini Tanzania!!! 🙁 Ni miaka 5 mingine na si ajabu zaidi ya mafisadi kuendelea kupeta uraiani huku Watanzania walio wengi kutoona chochote cha ahadi za Maisha bora kwa kila Mtanzania yanawezekana, Ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya na nitaipitia mikataba yote ya uchimbaji madini yetu ambayo wananchi wanailalamikia mwaka wa nne huu hakuna ahadi hata moja iliyotimizwa lakini wapiga debe hawalioni hilo!!!! wamekuwa vipofu!!!! 🙁.
 
Back
Top Bottom