The road towards 2010 Elections

The road towards 2010 Elections

Kati ya hawa nani atafaa kutuongoza 2010-2015?

  • Edward Lowassa

    Votes: 0 0.0%
  • Dr. Slaa

    Votes: 7 38.9%
  • Prof. Lipumba

    Votes: 0 0.0%
  • Mizengo Pinda

    Votes: 5 27.8%
  • Samwel Sitta

    Votes: 0 0.0%
  • Jakaya Kikwete

    Votes: 2 11.1%
  • Mark Mwandosya

    Votes: 2 11.1%
  • Harisson Mwakyembe

    Votes: 2 11.1%
  • None of The above

    Votes: 0 0.0%

  • Total voters
    18
  • Poll closed .
- Mkuu ukisoma tena post yangu, utaona haina uhusiano wowote na ya kwako, hebu soma vizuri post yangu hapo juu.

William.

Nami sikusema kwamba ina uhusiano hebu isome tena, bali nimeongezea sababu za wao kutoa vitisho badala ya kuishia pale ambapo wewe ulitaka waishie.
 
Naomba kuuliza BAK, Je, hivyo vitisho ilivyotolewa na hao wastaafu wa CCM ni vya kuganga njaa au? Spati picha katika ulimwengu wa kidemokrasia watu kusimama na kutoa hoja zisizo na makanyagio.

Hata mimi sielewi ndugu yangu, inasikitisha kwa kweli halafu Kikwete mwenyewe pamoja na vitisho hivi yeye kakaa kimya kabisa kama kawaida yake!!!!
 
Hata mimi sielewi ndugu yangu, inasikitisha kwa kweli halafu Kikwete mwenyewe pamoja na vitisho hivi yeye kakaa kimya kabisa kama kawaida yake!!!!


Njaa zao zitawaua, yani wako radhi kuuza hutu na haki zao kisa kuseek audience na favors kutoka kwa JMK.
Kazi kweli kweli!
 
1.
Bubu Ataka Kusema;

Huyu ni mmoja wa kambi ya "Ni Mwenzetu huyu" hivyo kazi yake hapa ni kutaka kuonyesha kinachoandikwa na yeyote yule ambacho yeye hakiafiki kina kasoro.

- Usiogope kivuli chako mkuu, maana hizi name calling ni dalili za uoga na kukosa hoja, mimi ni mwananchi wa Tanzania kama wewe na mwenye haki kama zako za kuwa na mawazo huru na kuyasema bila kuogopa, hayo ya mwenzetu ni yako, naomba usinitishe au kuniogopesha kutoa maoni yangu mkuu, wewe toa yako na mimi niweke yangu, tulisaidie taifa tusibaguane kwa sababu tu ya nyimbo tofauti.

2.
Tunajua fika kutokana na dalili za wazi kabisa kwamba upinzani hauna dalili ya kuchukua Urais 2010, lakini pamoja na hayo haina haja ya kumpa tena Kikwete. Katiba ya CCM inaruhusu wagombea wengine wanaotaka kufanya hivyo kuchukua form, sasa hivi vitisho dhidi yao vya nini tena? Na lini katiba ya CCM ilibadilishswa na kuruhusu vitisho kwa wale ambao wanataka kumpinga Rais!? Haya mambo ya unafiki ndiyo yanaifikisha nchi yetu pabaya. Rais kama kuna mazuri aliyoyafanya yawekwe hadharani, lakini hakuna hivyo Watanzania tunastahili kabisa kupata Rais mpya ambaye ataweka maslahi ya nchi mbele kwa manufaa ya Watanzania.

- Haya ni mawazo yako, na pia wananchi wengine wanatakiwa kuwa na mawazo tofauti au sawa na yako, ndio demokrasia at work.


William.
 
Ndugu WJM, nini msimamo wako katika hili suala la hao wastaafu wa CCM kumpigia debe JMK? May be itatusaidia na kumsaidia BAK pia katika kufanya tafakuri?
 
Ndugu WJM, nini msimamo wako katika hili suala la hao wastaafu wa CCM kumpigia debe JMK? May be itatusaidia na kumsaidia BAK pia katika kufanya tafakuri?

- Wastaafu wanne wa CCM, wanawezaje kuwaamulia wananchi Millioni 40, nani awe rais wao? I mean kama kweli wanaweza basi hili taifa tuna tatizo kubwa sana, otherwise ninaamini kwamba kila mwamnanchi wa Tanzania ana haki ya kusema maoni yake kuhusu nani awe next rais,

- Na ni haki ya kila mwananchi kupingana na mwingine kwa hoja, lakini tunahitaji kuepuka kejeli na matusi kwa sababu zinaishia kuigawa jamii na kuharibu mshikamano wetu wa taifa, binafsi sijaamua nani anafaa kuwa next rais, au kutoka chama gani.

William.
 
Shadow naona sasa nchi inaelekea kwenye udikteta, maana hata failure kubwa ya uongozi wa Kikwete ambayo ni kupambana na ufisadi wale wanaotaka kuitumia kupambana naye wameshatishwa kwamba wasitumie ufisadi dhidi ya Kikwete!!! Wao wako tayari kutumia 'utamaduni wao' wa kumuachia Rais akae madarakni kwa awamu mbili, lakini wale wanaotaka kumpinga na kuleta vigezo vya kuonyesha kwamba Rais hastahili kuendelea kuwa madarakani kwa sababu kadhaa wa kadha wanatishwa!!!!
 
- Wastaafu wanne wa CCM, wanawezaje kuwaamulia wananchi Millioni 40, nani awe rais wao? I mean kama kweli wanaweza basi hili taifa tuna tatizo kubwa sana, otherwise ninaamini kwamba kila mwamnanchi wa Tanzania ana haki ya kusema maoni yake kuhusu nani awe next rais,

- Na ni haki ya kila mwananchi kupingana na mwingine kwa hoja, lakini tunahitaji kuepuka kejeli na matusi kwa sababu zinaishia kuigawa jamii na kuharibu mshikamano wetu wa taifa, binafsi sijaamua nani anafaa kuwa next rais, au kutoka chama gani.

William.

Hakuna tusi wala kejeli hilo la huyu ni Mwenzetu ni neno lenye umaarufu mkubwa ndani ya CCM na si kejeli wala tusi.
 
1.

- Usiogope kivuli chako mkuu, maana hizi name calling ni dalili za uoga na kukosa hoja, mimi ni mwananchi wa Tanzania kama wewe na mwenye haki kama zako za kuwa na mawazo huru na kuyasema bila kuogopa, hayo ya mwenzetu ni yako, naomba usinitishe au kuniogopesha kutoa maoni yangu mkuu, wewe toa yako na mimi niweke yangu, tulisaidie taifa tusibaguane kwa sababu tu ya nyimbo tofauti.

2.

- Haya ni mawazo yako, na pia wananchi wengine wanatakiwa kuwa na mawazo tofauti au sawa na yako, ndio demokrasia at work.


William.

Hakuna demokrasi kama watu wanatishwa kuchukua form ili kumpinga Rais aliye madarakani na pia kutotumia udhaifu wake katika kumpinga huko. Huo ni udikteta.
 
Hakuna tusi wala kejeli hilo la huyu ni Mwenzetu ni neno lenye umaarufu mkubwa ndani ya CCM na si kejeli wala tusi.

- Ahsante mkuu, lakini sijawahi kusema mimi ni mwachama wa chama gani, na sijui wewe ni mwanachama wa chama gani, na sidhani kama ni muhimu sana, au? Lakini nimekuelewa.

William.
 
Njaa zao zitawaua, yani wako radhi kuuza hutu na haki zao kisa kuseek audience na favors kutoka kwa JMK.
Kazi kweli kweli!

Bora njaa hizo zingekuwa zinawau wao tu, lakini yupumbavu wanaofanya unalirudisha nyuma Taifa letu kwa kukosa viongozi jasiri na watakaoweka mbele maslahi ya Taifa. Maana yake hata kama uongozi umekushinda watasimama wastaafu wa CCM, Wazee wa CCM, akina Chiligati, Msekwa, Malecela, na maandamano hapa na pale basi mchezo umekwisha na unarudi madarakani. Hakuna debate yoyote kwanini huyu anastahili kurudi madarakani au kwanini hastahili kurudi madarakani. Tunakuwa tunaburuzwa tu kama gari bovu!!!!
 
- Ahsante mkuu, lakini sijawahi kusema mimi ni mwachama wa chama gani, na sijui wewe ni mwanachama wa chama gani, na sidhani kama ni muhimu sana, au? Lakini nimekuelewa.

William.

Ndg WJC, unajua kuna kitu kinaitwa'presumption' kutokana na uhusiano na ubini wako na matendo yako yanamfanya kila mtu afikie hitimisho hilo. Hii presumption ni 'rebuttable' na wakuikanusha na kuonyesha sivyo ndivyo ni wewe pekee uliyebeba hiyo dhamana ya kukanusha hiyo 'presumption'
 
Mimi sioni Tatizo kwa a kina ndbeji kuanza talalila ya kumkweza muungwana. Tatizo langu ni kwa UMMA wa Watanzania ambao watameza uozo huo na kuamini kuwa JK ni rais bora na aendelee. Kama ni mu endorse ndani ya Thithiem let it be. Lakini sio lazima achaguliwe na watanzania. na hapo ndiyo njia rahisi ya kuitema CCM maana watanzania wanamjaua Muungwana mazingaombwe mengi, Hivyo upinzania ni wakati muafaka wa kuhakiki anasimama mtu anaeuzika na mahiri mwenye mang'amuzi na anakubalika! Hapo ndiyo kitendawili. Who? iwapo kila mtu anataka mayai ya Ikulu?
 
Kila nikijaribu kujiuliza nini maana ya democracy sipati jibu, nimejaribu kurudi kwenye definitions zote nilizowahi kusoma na kujibia mitihani enzi hizo lakini naona hazifanani na reality ya Chama kinachotangaza kila siku kuwa kina fuata misingi ya haki na democracy!!!!! Au nimepitwa na wakati huenda definitions za kisasa za democracy zimebadilika?? Kwa wale waliopo madarasani leo wanasoma General Study, enzi hizo tunaita Siasa wanisaidie.
 
- Wakuu ufike wakati tujadili alternative, otherwise politically tunakuwa tunakubali kwamba ni CCM, au hakuna,

- Tutoe mapendekezo ya kuelekeza wananchi kwenye mabadiliko, na pia tuseme mchango wetu utakua ni nini hasa katika njia hiyo ya kuwabadilisha mawazo wananchi wapiga kura, au tujiunge na vyama vya siasa now.

Respect.

FMES!


Vipaumbele vipaumbele hatuna .... yaani wazee wastaafu kuitisha wanahabari na kuongea mambo yao imeshakuwa udikteita, sijui nini ... nani anajali!! Hivi kwani ni lazima Rais wa Tanzania atoke CCM? Inavyoelekea JK ni kikwazo cha upinzani kuchukua nchi 2010 ... Ama kweli "Rais Bora atatoka CCM", NYERERE KAMBARAGE (1995).
 
Ndg WJC, unajua kuna kitu kinaitwa'presumption' kutokana na uhusiano na ubini wako na matendo yako yanamfanya kila mtu afikie hitimisho hilo. Hii presumption ni 'rebuttable' na wakuikanusha na kuonyesha sivyo ndivyo ni wewe pekee uliyebeba hiyo dhamana ya kukanusha hiyo 'presumption'

- Sasa mkuu si niliambiwa siku za mwanzo kwamba hapa hatujali jina wala nini na hatuwekezi kwenye watu, sasa hii vipi tena imekaa sawa kweli?

- Anyway, ahsante mkuu kwa a decent debate.

William.
 
Back
Top Bottom