The road towards 2010 Elections

The road towards 2010 Elections

Kati ya hawa nani atafaa kutuongoza 2010-2015?

  • Edward Lowassa

    Votes: 0 0.0%
  • Dr. Slaa

    Votes: 7 38.9%
  • Prof. Lipumba

    Votes: 0 0.0%
  • Mizengo Pinda

    Votes: 5 27.8%
  • Samwel Sitta

    Votes: 0 0.0%
  • Jakaya Kikwete

    Votes: 2 11.1%
  • Mark Mwandosya

    Votes: 2 11.1%
  • Harisson Mwakyembe

    Votes: 2 11.1%
  • None of The above

    Votes: 0 0.0%

  • Total voters
    18
  • Poll closed .
Sambamba na kukiri kulindana, Msekwa pia alikiri kuwa rushwa imetawala katika uchaguzi ndani ya chama hicho na kubainisha kwamba CCM haikumbatii rushwa ila utekelezaji na usimamizi wa sera ya chama hicho kupambana na rushwa umekwama.
Sasa chukulieni gari hili la CCM limekwama, nanyi mnataka kubadilisha dereva kwa sababu gari limekwama... hii kweli inaingia akilini jamani..Shukeni, tatizo sio dereva kuna gari jingine pembeni linasubiri abiria tena bureee hakuna gharama zaidi...
Jamani mweee, muambiwe vipi ikiwa makamu mwenyekiti wa chama CCM mwenyewe amekiri kwamba UTEKELEZAJI na USIMAMIZI wa sera za chama kupambana na Rushwa Umekwama!..
Utekelezaji na Usimamizi wa sera ndio sifa kubwa ya UTAWALA wowote ule, sasa kama hawa wamekwama bado mna tumaini lipi..
 
kusema kweli sioni kiongozi bora ndani ya CCM ambaye ataweza kutimiza yale nayoyataka..Wengi ambao ningefikiria pengine wanaweza kuleta mabadiliko wameondoka ktk kurupushani za siasa..Waliobakia wote wanaogopa Mtandao kama anavyoogopa Kikwete mwenyewe!

...Mkuu Mkandara, bado na imani ndani ya CCM anaweza kutokea kiongozi (nje ya huo mtandao) ambaye ataweza kuleta mabadiliko ya kweli. Wanaposimama wazalendo kama kina Mh.Selelii, Mh. Mwakyembe nk naendelea kupata imani ipo siku!!!

Tuna watu kama Dr. Slaa akienda sambamba na Mafisadi, akichukua kila kitu hatua kwa hatua lakini ameshindwa kwenda mbele kwa sababu hana ubavu..Now, just imagine mtu huyu anakuwa Rais au Waziri Mkuu wa Tanzania!..Matatizo yetu yote yamekwisha!
Kwa nini bado mnafikiria CCM!

...Naam, naaam, naam! Uwezo, busara na uzoefu wa Dr. Slaa (CHADEMA), au Mh. Hamad Rashid Hamad (CUF), ni miongoni mwa viongozi ninaowa admire sana kwenye ulingo wa siasa. kwanini wanakosa ubavu wa kusimama kiti cha uraisi?

Nilipojiunga kwenye mtandao huu miaka miwili iliyopita, CHADEMA ilikuwa na nguvu sana JF katika kunadi sera zake. Imagine; ni miaka miwili imeshamalizika tangu Mh. Mbowe alipotuletea waraka wa nne kwa watanzania (soma); Blogu ya Freeman Mbowe

Kusubiri nyakati za kampeni na ruzuku, hakuwatendei haki viongozi wa vyama vya upinzani. Iwapo kama Mh. Slaa na Zitto Kabwe, John Mnyika na Freeman Mbowe wangendeleza mapambano ya fikra humu ndani, kwa kweli 2010 tungekuwa na hadithi nyingine badala ya kuzungumzia mgombea toka CCM.

Hayo maoni yangu tu.
 
Kweli jamani njaa kitu kibaya sana hao wastaafu wameona hapo ndio pa kutokea sasa maana pesa zatoka tuu haziingii na wanaona kama wamesahaulika.....single hiyo ndio nitoke vipi......kila mwanachama ana haki ile ilikuwa ni mazoeaa na kuoneana haya tuu sasa watu wamechoka maana JK wenu hana uwezoo nchi inaangamia...hawezii aachie ngazi aone wenzake wenye uwezo....yeye hawezii.,
 
Mbu,
Mkuu wangu nakusikia sasa hoja yangu inaambatana na matakwa yako..
Wewe na wengineo mnasema Kikwete ameshindwa ku deliver.. kitu gani mlichotaka?..
Je, ni kukomesha Ufisadi?... huyo Selelli na Mwakyembe wataweza vipi? hawa hata kukemea tu wameshindwa tena basi Mtu kama Mwakyembe ali vote against kuwajibisha viongozi..Ni wapi amesimama kuhusiana na swala lolote na Ufisadi toka Mkapa/Lowassa na Rostam..hana hata ubavu wa kuzungumza na Rostam uso kwa uso..
Ni type ya viongozi ambao kwa uzalendo wao hata akipigwa kofi hujibu namwachia Mungu atalipa..Mwinyi kind of..
He is too soft for CCM chairman acha mbali President wa nchi..
 
hawaitendei haki tanzania yetu kama wanatumia ushawishi wao na pengine madaraka yao na nafasi zao kutuburuza.

kilichotakiwa kwa wao ni kutufafanulia kwanin jmk anafaa kuendelea. na hilo lisifanywe kijuu juu. kwamba ccm wana kawaida ya kuachiana miaka kumi kumi si hoja

na kama wana ujasiri watuambie mapungufu yake pia. katka ccm kuna watu wengi na tukumbuke wakat nyerere anakaribia kuachia nchi watu wangeulizwa kama aendelee au la wengi wangesema aendelee. lakin mambo kadhaa yalikuwa yanaenda sivyo. hata kipind cha mwinyi wengi wangesema aendelee na urais japo kulikuwa na mapungufu mengi tu ya msingi. hata mkapa kama si kupakwa pakwa matope sana na 'mtandao' wengi wangetaka aendelee. na hao wengi ni pamoja na viongoz wa ccm kama kina ndejembi. lakin leo tunajua kama kuna kipind watz walishiriki kwenye rushwa kubwa kubwa basi ni kipind cha cha che mkapa

kina ndejembi wakae tena na watutangazie mafanikio ambayo huyu jamaa kayafanikisha. wasikwepe kuongelea uchumi wetu, vita dhidi ya mafisad na nk. hapo watakuwa wametutendea haki na kweli watakuwa wanaipenda nchi yao. lasivyo itakuwa kuangalia maslah yao binafs

mwakatojofu
 
Mwakatojofu,
kilichotakiwa kwa wao ni kutufafanulia kwanin jmk anafaa kuendelea. na hilo lisifanywe kijuu juu. kwamba ccm wana kawaida ya kuachiana miaka kumi kumi si hoja
Mkuu wangu wakuambie mara ngapi?.. wamesema sifa zote za Kikwete sasa kama wewe hukubaliani na sifa hizo, sii kura yako unayo mkononi?.. Unachotaka wewe wafanye kipi..wao ndio chaguo lao au wataka wamruhusu Rostam agombee na kwa sifa zipi?
Iweje rahisi kwenu kumkataa Kikwete lakini huna mtu wa kum replace zaidi ya kutegemea atakayekuja poa tu lakini sio Kikwete hivi kweli ndio kuutolea uvivu kufikiri jamani!
 
tukishakuwa na raisi tunaona hakuna tena kama yeye. na mara ingine akifanya mambo mawili matatu mazuri tunafurah na kuridhika na kuona kazi imeisha. lakin kimsingi anaweza kufanya mengi mazuri kuliko aliyoyafanya

watu sampuli ya kina ndejembi ndio kikwazo cha tanzania mara nyingi. taarifa waliyotoa kwa gazeti lililonukuliwa hapo juu wangeifanya kwa namna ya kumchochea jmk kuwajibika ipasavyo katka kuongoza kaya yetu. miaka 5 haijaisha. mengi mazur kwa tz anaweza kufanya kabla ya mwez wa uchaguz 2010

lakin badala yake wanambwetesha. wanakuja na misifa kibao na kuongea mambo kijuujuu. na jmk ataona amefika. kaz keshamaliza. kumbe ndo kwanza kunapambazuka
 
Eti miaka na miezi hii kuna wanasiasa toka CCM na Upinzani wanajipanga foleni kwa Burushi maarufu nchini kupokea mikopo ya riba nafuu au misaada?

Na wengine ni Mawaziri na wakuu wa vyama vyao. Je, wenye vyama vya siasa mnafahamu hili?
 
.............. kwa Rais Kikwete, haoni kitakachowafanya wampinge kutokana na uwajibikaji wake kwa taifa na mapambano dhidi ya rushwa.

...............Utamaduni wetu ndani ya chama unafahamika, Mwinyi tulimpa miaka kumi, Mkapa naye vile vile

...............amekuwa mvumilivu wa kukosolewa, msikivu na ni mtu anayeipenda nchi yake kwa moyo wote na si kiongozi wa visasi.

...............tunaamini kwamba usalama na amani ya nchi yetu upo salama leo na kesho chini ya uongozi wake.

Kwa maana hiyo, nasi tunaungana na wale wengine kumuunga mkono kwa kipindi cha pili cha urais," alisema.


hizo ndizo sababu za watz kumpa jmk miaka mingine 5. hii ni kwa mujibu wa mabosi wazaman wa ccm. nikiiangalia tz yetu nina waswas sana na sababu hizo
 
Mwakatojofu,
Sasa unachopinga kitu gani? hkaweza au hakuweza!.. maanake ndio sifa hizo hupendi chagua mtu mwingine, hizo ndizo sifa za kiongozi wa CCM leo na sidhani kama wazee hao wamekosea kitu...Sera ni za chama na huyu ni kiongozi ambaye wamemkubali, yaani vipaumbele vya chama chake kavitimiza.. wewe hutaki!..
Sema nani mbora kuliko Kikwete! aaaaaahhh huna jamani nitarudia mara ngapi?. Mie sioni kosa kabisa ikiwa Kura yangu nitampa Kikwete kwa sifa hizo mbovu na upofu wangu, maadam wewe una uhuru wa kumchagua mtu mwingine - kura yako unayo mkononi hakuzuii mtu...Wee ulimtaka nani?
 
Kikwete na wanamtandao wake fake wapo kazini hapo. Wewe unadhani hao wazee wamejiamulia tu kusafiri kutoka Morogoro, Dodoma, Iringa na kwingineko!? Kweli njaa inaplay part kubwa hapo lakini ni kwamba wameshawishiwa kufanya walichofanya

JMK yupo anapima joto na hii ni dalili ya kupanic.

Na tusubiri vimbwanga zaidi kadri tunavyosogelea 2010!
 
Mwaka jana kwenye kampeni za uchaguzi wa Raisi Marekani tulishuhudia mchango wa kizazi kipya katika kuchochea mabadiliko katika siasa ya nchi. Tulishuhudia vijana wakitofautiana wazi wazi na wazazi wao katika misimamo yao mpaka kutishia kukata mawasiliano nao. Vijana wa Marekani walidhihirisha kuwa kweli wao ni taifa la leo na siyo kesho kama vijana wetu hapa wanavyodanganyika kirahisi siku zote.

Nikiangalia hapa nyumbani Tanzania nashuhudia vijana wanavyopigana vikumbo kufuata nyayo za wazazi wao ambao ni wazi wamepitwa na wakati. Baada ya tamko la wazee wastaafu wa CCM, nilitegemea vijana wa CCM kujitokeza na kupinga kwa nguvu kauli zao. Lakini kinyume chake nasikitika kusema vijana hawa kama kawaida yao wanafanya maandamano kuunga mkono hizi kauli mfu - ama yawezekana nilikuwa naota tu !

Wako wapi akina Nape, Januari, Ridhwani, Masauni, Beno n.k. au tayari mmejipanga kurithi na hamtaki kutia mchanga vitumbua vyenu ? Je, mnakubaliana na kauli kama hizi zisizoendana na wakati na zinazoturudisha kwenye zile tawala za kiimla ? Hamuoni kuwa hapa hamuwi tena tegemeo la taifa bali sasa mnabakia tu kama mafisadi-in-waiting mkisubiri muda wenu muafaka muendeleze yale yale ya baba zenu ?
 
Mwaka jana kwenye kampeni za uchaguzi wa Raisi Marekani tulishuhudia mchango wa kizazi kipya katika kuchochea mabadiliko katika siasa ya nchi. Tulishuhudia vijana wakitofautiana wazi wazi na wazazi wao katika misimamo yao mpaka kutishia kukata mawasiliano nao. Vijana wa Marekani walidhihirisha kuwa kweli wao ni taifa la leo na siyo kesho kama vijana wetu hapa wanavyodanganyika kirahisi siku zote.

Nikiangalia hapa nyumbani Tanzania nashuhudia vijana wanavyopigana vikumbo kufuata nyayo za wazazi wao ambao ni wazi wamepitwa na wakati. Baada ya tamko la wazee wastaafu wa CCM, nilitegemea vijana wa CCM kujitokeza na kupinga kwa nguvu kauli zao. Lakini kinyume chake nasikitika kusema vijana hawa kama kawaida yao wanafanya maandamano kuunga mkono hizi kauli mfu - ama yawezekana nilikuwa naota tu !

Wako wapi akina Nape, Januari, Ridhwani, Masauni, Beno n.k. au tayari mmejipanga kurithi na hamtaki kutia mchanga vitumbua vyenu ? Je, mnakubaliana na kauli kama hizi zisizoendana na wakati na zinazoturudisha kwenye zile tawala za kiimla ? Hamuoni kuwa hapa hamuwi tena tegemeo la taifa bali sasa mnabakia tu kama mafisadi-in-waiting mkisubiri muda wenu muafaka muendeleze yale yale ya baba zenu ?
Pilipili usioila inakuwashia nini? Sikujua kama CCM imekukaa namna hiyo!
 
Pilipili usioila inakuwashia nini? Sikujua kama CCM imekukaa namna hiyo!

Duh!!! Hili siyo swala la CCM tu, kama mnataka kutumia utamaduni wenu wa kuachiana ndani ya chama chenu hakuna atakayewaingilia, lakini inapokuja kwenye uongozi wa Taifa hilo ni swala la Watanzania wote.

Kwa hiyo kwa akili yako Watanzania hatuna haki ya kujadili jambo hili ambalo linatuathiri Watanzania wote with exception ya mafisadi, huku ni kuendekeza udikteta!!!!? Kazi kweli kweli!!!!
 
Mbu,
Mkuu wangu nakusikia sasa hoja yangu inaambatana na matakwa yako..
Wewe na wengineo mnasema Kikwete ameshindwa ku deliver.. kitu gani mlichotaka?..
Je, ni kukomesha Ufisadi?... huyo Selelli na Mwakyembe wataweza vipi? hawa hata kukemea tu wameshindwa tena basi Mtu kama Mwakyembe ali vote against kuwajibisha viongozi..Ni wapi amesimama kuhusiana na swala lolote na Ufisadi toka Mkapa/Lowassa na Rostam..hana hata ubavu wa kuzungumza na Rostam uso kwa uso..
Ni type ya viongozi ambao kwa uzalendo wao hata akipigwa kofi hujibu namwachia Mungu atalipa..Mwinyi kind of..
He is too soft for CCM chairman acha mbali President wa nchi..

Yaani huelewi ni kitu gani Kikwete ameshindwa kudeliver!!!!? 😕
 
Duh!!! Hili siyo swala la CCM tu, kama mnataka kutumia utamaduni wenu wa kuachiana ndani ya chama chenu hakuna atakayewaingilia, lakini inapokuja kwenye uongozi wa Taifa hilo ni swala la Watanzania wote.

Kwa hiyo kwa akili yako Watanzania hatuna haki ya kujadili jambo hili ambalo linatuathiri Watanzania wote with exception ya mafisadi, huku ni kuendekeza udikteta!!!!? Kazi kweli kweli!!!!
Hakuna Mtanzania yoyote aliyekatazwa na CCM kugombea urais. Bandiko hili umelibandika mwenyewe lakini naona hujalifahamu.

Kwani kuna vyama vingapi hapo TZ, mpaka mfanye issue kubwa kwa mambo ya ndani ya CCM?

Kwa ufupi wengi humu ni visebu sebu na viroho vi papo!
 
Hakuna Mtanzania yoyote aliyekatazwa na CCM kugombea urais. Bandiko hili umelibandika mwenyewe lakini naona hujalifahamu.

Kwani kuna vyama vingapi hapo TZ, mpaka mfanye issue kubwa kwa mambo ya ndani ya CCM?

Kwa ufupi wengi humu ni visebu sebu na viroho vi papo!

Mimi nimekatazwa na CCM kupitia katiba kwa sababu ya kijinga kuwa sina chama - sasa sielewi kama chama ndicho kinakuwa Raisi ama mtu binafsi. Kwa kuatamia katiba hii CCM ndio serikali, bunge na mahakama - hivyo kwangu yeyote hata mwehu akiongea kwa niaba ya CCM, anaongelea taifa.
 
"Kwa kifupi ni kwamba hatuna wazee!! Hao ndio washauri? Haishangazi tupo hapa tulipo."

*************************

Mpigafilimbi: Correct kabisa, hatuna wazee, waliishia enzi yaJKN. Nakumbuka mapema miaka ya 90 wakati Mwinyi ananadi sera ya kuchangia eklimu ya juu, ktk mkutanio mmoja wa ndani na wazee wa Mbeya, alikuwa anakatizwa kwa kupigiwa makofi na vigelegele ktk hotuba yake ya kuwataka wazazi wachangie.

Hivi sasa wazee hao wanajisikia vipi watoto wao wanatimuliwa hovyo Vyuo Vikuu kwa kukosa hela za kuchangia ada! Wazee wetu siku hizi hawana maana yoyote, hawa wa CCM waliotoa tamko juzi wanaganga njaa tu, na bila shaka utakuta wamehongwa na mafisadi ili kusema.

Kwa mtindo huu tutasikia mengi siku zijazo na wengi kujitokeza ktk kampeni ya kunadi "JK TENA": Viongiozi wa walemavu, vijana, wanawake wanawake, machinga, vijana, wanafunzi etc watapewa hela na mafisadi ili waende ukumbi wa maelezo kutoa matamko ya kiajabuajabu!

Hadi sasa sijamsikia mzee yoyote wa CCM akisimama jukwaani na bila kigugumizi kuwashambulia mafisadi. Hakuna! labda Warioba na Butiku, lakini angalia jinsi mafisadi wanavyojaribu kuwageuzia vibao!

Ni kweli kabisa!! Ndio maana siku zote nasisitiza tujaribu kuwanyamazisha hawa wazee wanaojidai wao ndiyo nchi.Hao ndio wametufikisha hapa tulipo kwa kuwa wavivu wa kufikiri. Wamebakia kutumia matumbo kwa ajili ya kufikiria badala ya vichwa kwa sababu walishawakabidhi mafisadi vichwa vyao, kazi yao ni kucheza ngoma ya mafisadi. Wazee wetu sijui ni mambumbu au wamekuwa brainwashed au sijui ni nini? Kauli zao zinaonyesha siku zote kuwa ni mental retards, tukianzia na Kingunge na hao wengine wote. Ilitakiwa tuanze kuwachapa viboko, kwa sababu tupo hapa tulipo kwa ujinga wao. Mtu kama Malecela anapoteza muda wake kuongea mambo yasiyo na maana, waandishi wetu sasa wawe wazalendo kwa kutowapa coverage hawa retards na waache kupokea fedha kwa ajili ya kuwasafisha mafisadi.
Hawa wastaafu wamegeuka ombaomba kwa mafisadi, matokeo yake watatokea hadharani kusema lolote hata kama litachafua hadhi yao.
 
Hakuna Mtanzania yoyote aliyekatazwa na CCM kugombea urais. Bandiko hili umelibandika mwenyewe lakini naona hujalifahamu.

Kwani kuna vyama vingapi hapo TZ, mpaka mfanye issue kubwa kwa mambo ya ndani ya CCM?

Kwa ufupi wengi humu ni visebu sebu na viroho vi papo!

Wewe ndio kisebu sebu na kiroho papo namba moja. Una hakika utawala wa nchi ukiendeshwa kwa mujibu wa sheria na taratibu zinazokidhi wakati tulionao hutakuwa na nafasi si wewe tu na ukoo wako wote wa kifisadi. CCM ni nini hata hivyo, kwa nini wewe unadhani una uchungu sana na CCM? get brains and think for the future of this country!! Watu kama ninyi mpo radhi hata kuua wengine ili muendelee kufaidika na mfumo wa kidhalimu. Jifunze kuheshimu pia mawazo ya wengine, huna haki miliki ya mawazo.
 
Back
Top Bottom