The road towards 2010 Elections

The road towards 2010 Elections

Kati ya hawa nani atafaa kutuongoza 2010-2015?

  • Edward Lowassa

    Votes: 0 0.0%
  • Dr. Slaa

    Votes: 7 38.9%
  • Prof. Lipumba

    Votes: 0 0.0%
  • Mizengo Pinda

    Votes: 5 27.8%
  • Samwel Sitta

    Votes: 0 0.0%
  • Jakaya Kikwete

    Votes: 2 11.1%
  • Mark Mwandosya

    Votes: 2 11.1%
  • Harisson Mwakyembe

    Votes: 2 11.1%
  • None of The above

    Votes: 0 0.0%

  • Total voters
    18
  • Poll closed .
NOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO! msekwa he is right kikwete amefanya mambo mazuri sana sana bila yeye nchi hii pangekuwa hapakaliki hebu fikiria angeruhusu Mkapa ashitakiwe au angesema mifisadi yote iende mahakamani na isipewe hata dhamana kwa sababu wameihujumu nchi unafikiri ni nini kingeendelea???????????????????
Amefanya mazuri kwa watu matajiri wenye pesa zao na kwasababu nchi hii inamilikiwa na wenye fweza msekwa yuko right....., naamini mimi na wewe hatujaona mazuri yake kwa sababu sio makada wa CCM, sio majambazi, sio wauza madawa ya kulevya, sio mafisadi hata tukifa kikwete hata kuja kwenye msiba wetu.. yani tupotupo tuuu.

Nchi isingekarika kivipi?
Unataka uniambie hawa mapapa pamoja na Ben ndo wenye wafuasi wengi wanao waunga mkono?
 
Alivyosema CCM inakusudia kumpitisha Kikwete alitaja ni kikao gani kilifanyika na uamuzi huo ulifikiwaje?

Ikiwa chama kinaruhusu watu kuwania uarais, chama kitakusudiaje kumpitisha mgombea mmoja bila ya kuwasikiliza wagombea wengine? Hawawezi hata kufanya a sham process? Sasa ukifika muda wa kuwasilisha majina na Shibuda akisema alipigwa vita na viongozi wa juu wakiwamo kina Msekwa wataweza kujitetea kwamba walikuwa neutral na objective katika process?

Tunaendesha mambo kienyeji kweli!

Lazydog,
Kama unavyojua wanamtandao wao huwa na vikao miaka 5 kabla ya uchaguzi.

Hivi ndivyo walivyofanya kabla ya 2005 na usishangae kusikia kuwa wamekaa na kuamua kuwa JK agombee tena 2010.

Vikao hivi si formal bali informal lakini vina nguvu nyingi sana ndani ya sisiemu. Na ndivyo vina maamuzi ya mwisho. Hivi vikao unavyoona Jakaya anaitisha kila leo ni geresha tu maana sisiemu wameshapigwa bao na wanamtandao.
 
--------------------------------------------------------------------------------

Quote:
Originally Posted by Kigogo
mi najisikia kichefuchefu tupu...Msekwa kazeeka sasa jamani

NOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO! msekwa he is right kikwete amefanya mambo mazuri sana sana bila yeye nchi hii pangekuwa hapakaliki hebu fikiria angeruhusu Mkapa ashitakiwe au angesema mifisadi yote iende mahakamani na isipewe hata dhamana kwa sababu wameihujumu nchi unafikiri ni nini kingeendelea?

Amefanya mazuri kwa watu matajiri wenye pesa zao na kwasababu nchi hii inamilikiwa na wenye fweza msekwa yuko right....., naamini mimi na wewe hatujaona mazuri yake kwa sababu sio makada wa CCM, sio majambazi, sio wauza madawa ya kulevya, sio mafisadi hata tukifa kikwete hata kuja kwenye msiba wetu.. yani tupotupo tuuu.


loooooooooooooooooooh!!!!!

hata wewe lorah
 
Baada ya kutamka wewe mwenyewe kwamba humuogopi mtu ndani ya CCM na kwamba mwaka 2010 lazima upambane na JK mimi leo niko hapa kukuhimiza ufanye kweli tafadhali na tuweze kuona ushindani wa kweli ndani ya CCM na hatimaye pelekea CCM kufa.
 
Ushindani wa kweli kutoka kwa Shibuda?!

Yes kwa kuwa ndiye mtu pekee kaamua kusema wazi nia yake na amekuwa akisakamwa wazi wazi a akina Makamba .Akifanya kweli atakuwa kaleta jambo zito na anaweza kumlaza JK maana watu wamechoka wanangoja filimbi tu .
 
Kama mmnavyojua kuwa JK kazi imemshinda..tunahitaji kufanya grass root campeni kama aliyofanya Barack Obama...
Muelekeo wa vita kupinga ufisadi unaendelea vyema...Nnawaomba wanabodi wote tuandae mtu ambaye tutampa nchi iwapo JK hatafanya tunalomtata afanye....
Hii thread is not a joke...tunahitaji mchango usio na masihara...

Naipenda nchi yangu..tusaidiane kuijenga.
 
Sijui hapa tutapendekezanaje na majina yetu haya.
Kuna watu wana mwelekeo mzuri lakini ndo hivo hawajitokezi.
Wanaojitokeza wazi wazi hapa jamvini wengi umri hauwaruhusu kugombea Urais.
Kama mimi hapo juu si unaona bado nanuka ziwa la mama!! siunona!
 
Lyatonga!!!!!!!!

Waziri wa mambo ya ndani=Mahita
Waziri wa michezo=Ndolanga
Waziri wa Fedha=Mramba
Waziri wa Uchumi=Yona
Waziri wa Habari=Mengi
Waziri wa kupiga vita ufisadi=RA
Waziri wa Nishati na Madini=Karamagi
Waziri, Ushirika na masoko=Cheyo
Mambo ya Nje=Nkapa
Viwanda na Biashara=Manji
Sheria=Chenge

..................... endelea mpaka

Waziri Mkuu=EL
 
Chaguo langu ni Dr Slaa kwa kuwa huyu mtu ni makini sana, ana mapenzi ya kweli na nchi yetu hana chuki na kiongozi yeyote yule ndani ya CHADEMA au chama kingine chochote kile, ni msomi hana makundi na anaelekea ni mchapa kazi hodari.

Si mwoga maana vitisho alivyovipata alipoanza kutangaza mafisadi ndani ya serikali na CCM angeweza kabisa kusalimu amri na kuamua kunyamaza kimya lakini akaendelea kutupasha habari mbali mbali za Mafisadi na ufisadi waliofanya dhidi ya nchi yetu hadi pale ukweli ulipodhihiri na uwongo kujitenga. Wale wote waliomtishia kumfikisha mahakamani kwa kuwatuhumu kama mafisadi hatukumuona hata mmoja aliyetimiza ahadi yake ya kumfungulia mashtaka Dr Slaa.

Hili mimi ndiyo chaguo langu la Rais wetu atakayefuata baada ya Kikwete kumaliza awamu yake moja hapo 2010.
 
Ni wazo zuri sasa ndugu kujipanga mapema na kuwa na mikakati ya ushingi mapema.
Ila,
Uoni tutakeye mwandaa atapigwa zengwe na kupakwa matope ya kutoshwa na wataalam wa siasa mpaka itapofika iyo pindi ya kampeni atakuwa anaonekana hafai.

Grass roots wanatokea baada ya mtu kutokea na inahitaji strong driving force ya kutuunganisha wote sisi ktk local level (grass roots)

Sasa tutajuaje kuwa you wanna work undercover !?

Ok wewe ktk mawazo yako umeona nani anafaa kumpendekeza kugombea uraisi 2010 na tum support?
 
Sitashangaa kusikia kuwa CCM wamempendekeza LOWASA kugombea kiti cha uraisi, na Mheshimiwa Kikwete ameamua kustaafu kwa sababu za kiafya.
 
Majina tunayo lakini si busara kuyataja sababu ya usalama wao. Nadhani lililo la busara kwa wakati huu ni kuweka wazi mbele ya Watanzania kuwa mpangaji wetu wa sasa pale ikulu HATUFAI na hivyo tusimpatie miaka mingine mitano.

Amechafua kuta za nyumba yetu kwa kupikia ndani ya nyumba kutumia kuni za miti mibichi. Yaani kuni (mawaziri) wa kupikia chakula watoto wake (Watanzania) ni wabichi (washikaji). Mpangaji mwenyewe (Rais) haoni hilo (uwezo mdogo). Nyumba yetu (Tanzania) inazidi kuharibika rangi (umaskini) kwa moshi (ubadhirifu/ufisadi).

Nadhani tuthibitishe hayo kwanza. Watanzania wajue muungwana hatatufikisha kwenye kauli mbiu yake ya maisha bora kwa kila Mtanzania ili mwaka 2010 tutafute mpangaji mwingine. Let's be serious. Yes, we can.
 
Mimi nampendekeza Salim Ahmed Salim,Makamo Asha Rose Migiro na Waziri mkuu awe John Pombe Magufuli.
 
Majina tunayo lakini si busara kuyataja sababu ya usalama wao. Nadhani lililo la busara kwa wakati huu ni kuweka wazi mbele ya Watanzania kuwa mpangaji wetu wa sasa pale ikulu HATUFAI na hivyo tusimpatie miaka mingine mitano. Amechafua kuta za nyumba yetu kwa kupikia ndani ya nyumba kutumia kuni za miti mibichi. Yaani kuni (mawaziri) wa kupikia chakula watoto wake (Watanzania) ni wabichi (washikaji). Mpangaji mwenyewe (Rais) haoni hilo (uwezo mdogo). Nyumba yetu (Tanzania) inazidi kuharibika rangi (umaskini) kwa moshi (ubadhirifu/ufisadi).

Nadhani tuthibitishe hayo kwanza. Watanzania wajue muungwana hatatufikisha kwenye kauli mbiu yake ya maisha bora kwa kila Mtanzania ili mwaka 2010 tutafute mpangaji mwingine. Let's be serious. Yes, we can.

ehe, urais tena usalama?? atafanya kampeni kuzimu?
 
yaani wewe jamaa, kama ulikuwa mawazoni mwangu, nilitaka kuanzisha thread kama hii,nadhani wakati umefika wa kuwaza nani anafaa ka urais mwaka 2010. tuwe serious na maada iwe endelevu yenye michango ya kujenga ...no jokes please

by doing that

1. Tutajua udhaifu na uimara wa kila mmoja.
2.kuna watu tunawaona wanafaa machoni lakini kumbe wengine wana data zaidi, hapa pawe mahali pake pa kusemea na kuweka vithibitisho.
3. tutakuwa tunajiweka katika nafasi nzuri ya kujiona wana JF ni waona mbali!!


tuwe serious, kwanza nipeleleze nani anafaa na kwa nini??

sio lazima watoke katika hawa tunaowafahamu kuna wengine hatuwajui mnawajua wasemeni.hata kama hawatakuwa marais wengine watajifunza ili uonwe inabidi uwe kama nani na ufanye nini!!!

waberoya
 
Mimi nampendekeza Salim Ahmed Salim,Makamo Asha Rose Migiro na Waziri mkuu awe John Pombe Magufuli.

Piga ua!! CUF, Chadema, NCCR, UDP, etc.... hawakubali ng'o?

Wana JF pendekezeni mpaka liyamba, humu ndani wenyewe hatutakubaliana. Si kwa sababu ya uwezo wa hao watu, bali kwa ujinga uleule ulio katika siasa za mitaani kuwa chama kwanza!!!!!

Mara ngapi tumeshuhudia CCM na Chadema wakiraruana humu hata kwa mambo yaliyo dhahiri?

Bado siamini kama wana JF tuna_share common vision/mission/objectives! Kwa mantiki hiyo pengine watu wange propose names of parts candidates!
 
Uamuzi wa nani awe rais after Kikwete haliko mikononi mwa wananchi bali chama na wenye vyama vyao. usidhani ni rahisi sana kupita vipingamizi vya kichama hadi kufika pale juu kwenye kupigiwa kura. Hapa JF mtasema sana lakini wenye vyama vyao wakikataa huna la kufanya. Labda kwanza tupigie debe kwa nguvu sheria ya Mgombea binafsi pengine hivyo itasaidia maana mtu hatokuwa na vipingamizi vingi kufikia azma hiyo ya kugombea hicho kiti muhimu nchini.

Leo hii mtamtaka Dr Slaa Chadema wakasema no biashara inaishia hapo hapo. the same to CCM na Salim A Salim. Lakini wakiamua kwenda front line kama wagombea binafsi basi itakuwa ni rahisi kuwaunga mkono na kuwapa nguvu ya kuendelea mbele.

Sisi tusubiri wateue then tujue ni yupi mwenye CV njema then tutamsapot kwa nguvu zote
 
Back
Top Bottom