The road towards 2010 Elections

The road towards 2010 Elections

Kati ya hawa nani atafaa kutuongoza 2010-2015?

  • Edward Lowassa

    Votes: 0 0.0%
  • Dr. Slaa

    Votes: 7 38.9%
  • Prof. Lipumba

    Votes: 0 0.0%
  • Mizengo Pinda

    Votes: 5 27.8%
  • Samwel Sitta

    Votes: 0 0.0%
  • Jakaya Kikwete

    Votes: 2 11.1%
  • Mark Mwandosya

    Votes: 2 11.1%
  • Harisson Mwakyembe

    Votes: 2 11.1%
  • None of The above

    Votes: 0 0.0%

  • Total voters
    18
  • Poll closed .
Bokassa umenena, beba tano mzee. Hatutakubaliana hapa nani anafaa kuwa rais wetu ajaye. Tutajaza pages za thread tu. Kumbuka hatuna itikadi moja. Tutaishia kupondana, kukashifiana na hata kuchafua majina ya watu bure.

Ndiyo maana nilisema awali "kwa usalama wao"si vyema kuwataja majina wakati huu. Kipindi cha kampeni hakijafika, na hata kikifika muhusika anayo nafasi ya kukubali au kukataa. Akikubali ndiyo hapo jamii inaweza kumchambua nje na ndani kama anafaa.

Sasa muhusika mtakayempendekeza hajasema wala kukubali kuwa atawania hiyo nafasi, halafu sisi tuanze kumchambua hadharani hatuoni kuwa hatumtendei haki mtu? Obama, Maccain walichambuliwa kila kona kwa sababu wenyewe walikuwa wako katika kinyangányiro kwa hiari yao, hivyo wamarekani walikuwa na haki ya kuweka mambo hadharani ili wawe katika hali nzuri ya kumpata rais wao atakayefaa.

Sisi kipindi hicho hakijafika. Tukianza kubandika majina ya watu bila hata uhiari wao wakati we don't share the same vision, objectives,missions nk kama alivyosema Bokassa tutaishia kukashifiana humu ndani. "usalama" hauna maana ya kuuawa tu bali ni heshima ya majina yao waliyojijengea kwa jamii.

Ndiyo maana nilipendekeza tuijadili kwa kina serikali iliyopo madarakani. Hapo tunayo haki ya kufanya hivyo maana huyu muungwana kwa hiari yake aliomba kazi kwetu na sisi tukamuajiri. Tunayo haki ya kumchambua kama anastahiili au hastahili kupata kazi kwetu tena 2010. Muungwana anajadiliwa sambasamba na serikali yake inayoundwa na mawaziri na watendaji kadhaa wanaoteuliwa na huyu muungwana tuliyempa ajira ya kutuundia serikali hiyo.
 
CCM: Asha Rose Migiro\Salim Ahmed Salim
CHADEMA: Slaa\Zitto
 
Sitashangaa kusikia kuwa CCM wamempendekeza LOWASA kugombea kiti cha uraisi, na Mheshimiwa Kikwete ameamua kustaafu kwa sababu za kiafya.

Ikiwa hivyo wafanye kama urusi. Lowassa awe Raisi afu JK awe waziri mkuu.Then wabadilishe katiba Waziri mkuu awe powerful kuliko raisi
 
Piga ua!! CUF, Chadema, NCCR, UDP, etc.... hawakubali ng'o??????

Wana JF pendekezeni mpaka liyamba, humu ndani wenyewe hatutakubaliana. Si kwa sababu ya uwezo wa hao watu, bali kwa ujinga uleule ulio katika siasa za mitaani kuwa chama kwanza!!!!!

Mara ngapi tumeshuhudia CCM na Chadema wakiraruana humu hata kwa mambo yaliyo dhahiri??????

Bado siamini kama wana JF tuna_share common vision/mission/objectives!!!!!!!! Kwa mantiki hiyo pengine watu wange propose names of parts candidates!!!!!

Mkuu upo sawa. lakini katika hali ya kawaida haiwezekani tukafanana! Wengine ni memba humu kwa sababu maalumu wanazoaijua wao.Unategemea tutafanana vipi!Cha msingi yule mwenye wazo atoe na anaepinga apinga.Hoja yenye nguvu itasimama na hoja ya mfa maji itakufa 'natural death'
 
Chaguo la mtu anayefaa KUONGOZA na yule Atakayeongoza 2010 ni vitu viwili tofauti... mapendekezo ya watu yatabakia mapendekezo na pengine kutufumbua wengine maamuma tusiofahamu viongozi wa Bongo wanaofaa.

Uchaguzi wa mwaka 2005 tulibishana weee na mada ile ilikuwa ndefu kichizi hadi zikafunguliwa site zinazohusu uchaguzi tu.. hatukukubalina hadi mwisho na Kikwete akachukua nchi.
Mbali na huko tuendako huko nyuma tu tukirudi tunaweza kukesha ikiwa swalio litakuwa nani alikuwa kiongozi mzuri Tanzania au nani alifaa kuwa kiongozi.

Kifupi ni kwamba hatujui tunataka nini ktk maisha yetu...pia yawezekana hatuna experience ya kiongozi bora..
 
Jamani wanaukumbi, legislative process ya kupata independent candidates katika chaguzi zetu imefika wapi!! Keshokutwa tunaanza 2009 na uchaguzi wa serikali za mitaa ,lakini hakuna kinachozungumzwa kuhusu wagombea wa kujitegemea ingawa mahakam kuu ya Rufaa iliisha amua kuwa kuwe na independent candidates!! Mhe. Zitto nadhani atakuwa in a position kutuhabarisha juu ya hili huko aliko kwenye operesheni Sangara.
 
Uamuzi wa nani awe rais after Kikwete haliko mikononi mwa wananchi bali chama na wenye vyama vyao. usidhani ni rahisi sana kupita vipingamizi vya kichama hadi kufika pale juu kwenye kupigiwa kura. Hapa JF mtasema sana lakini wenye vyama vyao wakikataa huna la kufanya. Labda kwanza tupigie debe kwa nguvu sheria ya Mgombea binafsi pengine hivyo itasaidia maana mtu hatokuwa na vipingamizi vingi kufikia azma hiyo ya kugombea hicho kiti muhimu nchini.

Leo hii mtamtaka Dr Slaa Chadema wakasema no biashara inaishia hapo hapo. the same to CCM na Salim A Salim. Lakini wakiamua kwenda front line kama wagombea binafsi basi itakuwa ni rahisi kuwaunga mkono na kuwapa nguvu ya kuendelea mbele.

Sisi tusubiri wateue then tujue ni yupi mwenye CV njema then tutamsapot kwa nguvu zote

Labda kinachoweza kufanyika kabla ya uteuzi ndani ya vyama, ni kutoa wito kwa mhusika (aliyeko katika chama fulani), kumtaka agombee kupitia chama chake, inshallah chama nacho kikimpitisha tutakuwa tumefanikiwa kwa kiasi hicho.
 
Mtu anaweza kusema JF haina nafasi ya aina yeyote katika kuathiri uchaguzi au maamuzi makubwa ya kisiasa Tz, sawa hayo ni mawazo yake maana wengine tunaweza fikiri kuwa wana JF ni kundi tu dogo sana la watu ambao wengi wao wako ughaibuni na hawana nafasi yeyote nyeti Serikalini au Vyamani au kwamba hawana kabisa ushawishi wowote wa nguvu katika vyama vinavyoteua hayo majina na hata kwa Wananchi-wapiga kura ingawa ni kweli kuwa Wananchi wengi hawana uwezo wa kuwa mtandaoni hapa kama sisi.

Binafsi ninakubali kuwa JF kama vilivyo vyombo vyovyote vya habari ina nafasi nzuri tu ya kuathiri kama si fikra basi matendo (au vyote) ya Watanzania wengi wakiwamo walio katika uongozi wa juu wa hivyo vyama vya sisasa. Na si lazima waje hapa kwa majina yao na kusema mimi fulani nawashukuru sana kwa mchango wenu ambao nimeufanyia kazi katika mada au jambo fulani ili kuthibitisha hili.

Wengine wanafikiri kuwa hapa JF kuna watu wapo kwa kutumwa kupata news na au kupima joto la 'reactions' za wananchi siwezi kulipinga hilo wala hata siwezi kupinga kuwa huenda JF imeanzishwa ili kukusanya habari na mikakati ya kulisaidia Taifa letu ili liweze kustawi na kumuendeleza Mtanzania.
Hakika, sijali kujua chanzo au kiini cha mwanzilishi au waanzilishi wa JF wala kutaka kuona eti watu wote hapa tunakubaliana na kuwa na mwelekeo mmoja katika kila jambo hasa suala nyeti kama nani anafaa (au nani achaguliwe) kuwa Rais.
Cha msingi kwangu ni kuwa watu wanapata nafsi ya kutoa maoni yao ambayo ni ya busara (au hata ya kuchekesha tu) yenye uelekeo wa kumuendeleza Mtanzania na tupo tunaofaidika na michango ya hapa iwe ni kupinga, kuunga mkono au kurekebisha au kutoa tetesi juu ya jambo fulani lenye maslahi ya Taifa.

Back to the topic:

Binafsi nadhani kuwa pengine ni vyema kuunda mkakati kwanza hata kabla ya kufikiria kuwa ni nani tunaona anafaa kutuongoza . Kwani ni kupitia njia ya mkakati wenye ufanisi ambapo hata nafasi ya kidemokrasia itapatikana katika kumchambua mtu yeyote kwa makini na katika wigo mkubwa hata nje ya JF.

Kuna thread humu zilikuwa zinagusia uwekaji huo wa mikakati mfano aliyoianzisha Mwanakijiji yenye jina:
CCM kumeguka ni muhimu kwa Taifa!- Bofya hapa
(https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/20430-ccm-kumeguka-ni-muhimu-kwa-taifa.html) na hata ile yangu yenye kichwa cha habari:-
2009 kisiasa- Bofya hapa
(https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/19251-2009-kisiasa.html)

Watu wamechangia juu ya mkakati ambayo kupitia njia hizo kweli Wananchi wanaweza kuanza kusema nani anawafaa. Na pia tujue kuwa hata hao viongozi wa vyama msifikiri kuwa huwa wanakurupuka tu na kuweka jina la mtu huwa wanapima uelekeo wa Wajumbe wa Mikutano yao na Wananchi kwa ujumla!
 
Umebaki almost mwaka mmoja tuingine tena kwenye heka heka za uchaguzi wetu(waTZ), ni muhimu kwa vyama husika kufanya tadhimini since 2005 mpaka sasa vimefanya nini.
Chadema wao wana operation sangara,CUF nao?

Je hi kamata kamata ya kina mramba,yona sio danganya toto kwamba ionekane serilikali chini ya utawala wa CCM iko makini so inajisafisha ili 2010 ishinde tena kwa kishindo, kama sababu ni matumizi mabaya ya madaraka mbona wale walio ridhia nyumba za serikali ziuze tena kwa bei chee then jamaa wamezigeuza mahekalu huku wakipata faida ya kufa mtu hatujasikia kufikishwa mahakani,au wako kwenye Queue
 
Kama kosa la Mgonja ni kutumia madaraka vibaya na kulisababishia Taifa hasara, basi Lumbanga arudishwe na yeye apandishwe kizimbani kwa kosa kama hilo hilo kwa ununuzi wa ndege ya Rais kwa bei ya kupaa dalali akiwa yule yule wa Radar!!

John Rubambe aliyekuwa mwenyekiti wa PSRC apandishwe pia kwa kuhujumu uchumi kwani aliidhinisha uuzwaji wa mali nyingi kinyume na utaratibu wa sheria ukiwemo mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira.i.
 
Hizi kesi za akina Yona, Mramba, Mgnja na wale mafisadi wa EPA ni kiini macho tu wakati tunaelekea katika uchaguzi 2010. Hizi kesi zote zitavutwa na kutokamilika kabla ya uchaguzi wa 2010 au kutakuwa hakuna ushahidi wa kutosha na hatimaye watuhumiwa wote kuachiwa huru.

Sirikali ilibidi kuwafikisha wahusika mahakamani maana iliona maji yanazidi kuwafika shingoni katika vita dhidi ya ufisadi, hivyo ikabidi watuonyeshe wananchi kwamba na wao wana nia ya kweli ya kupambana na mafisadi.

Lakini mafisadi wengi bado wanapeta uraiani akiwamo fisadi Mkapa, Chenge, Rostam Azizi, Mwanyika, Hosea, Mkono, Majiyatanga Mzindakaya na wengine wengi. Tusubiri tuone lakini kwa maoni yangu hii ni danganya toto tu na hizo 69 billioni zilizorudishwa na mafisad wa EPA mbona kuna usiri wa hali juu zimewekwa wapi na majina ya mafisadi wote waliorudisha mbona bado yanafanywa siri kubwa!?

Je, chama cha mafisadi kinataka kuzitumia pesa hizo katika uchaguzi wa 2010!? au hakuna hata senti tano iliyorudishwa!?
 
Heshima zenu wanaJF. Tukiwa tumebakiza mwaka mmoja tuingie katika uchaguzi wa Rais na wabunge nimeona tujikumbushe jambo moja. Mtakumbuka suala la mgombea binafsi wa urais limekuwa likizungumzwa sana na hata kufikishwa mahakamani. Pia mtakumbuka kuwa mahakama ilisha ruleout kuwa kumzuia mtu kusimama kama mgombea binafsi is unconstitutional.

Aidha mpaka sasa hakuna sheria yoyote inayohalalisha mgombea binafsi kufuatiwa mahakama kudhihirisha kuwa kuzuia mgombea binafsi ni kumnyima mtu haki za kikatiba. Kwa sababu 2010 inakuja kwa kasi wanJF naomba msaada na ushauri kwaajiri ya utekelezaji kwa wahusika. Je, baada ya mahakama kurule out kuwa kuzuia mgombea binafsi is unconstitution ni nani alie/ane takiwa kupeleka mswaada bungeni ili sheria iundwe kuhalalisha jambo hili? Je, kwakuwa haikufanyika hivyo ni namna gani mtu huyu anaweza kuwajibishwa kisheria?

Nini kifanyike ndani ya muda huu mfupi uliobaki kuitafuta 2010 ili kujihakikishia kuwa swala la mgombea binafsi linapata baraka za bunge na tunakuwa na wagombea binafsi 2010?. Naomba kuwakilisha.
 
Mwaka huu kutakuwa na uchaguzi wa serikali za mitaa kwa hiyo ni vema legislation inayoruhusu private candidates ikapitishwa mapema ama sivyo tusijetukajikuta mahakamani tena tukiahirisha uchaguzi kwa sababau kuna watu hawakutimiza wajibu wao!!

Mgombea binafsi anaweza kusimama katika chaguzi toka ngazi ya kijiji mpaka upangaji magogoni!! Wabunge wetu wanaweza kutusaidia kwa kupeleka private motion ili jambo hili lishuhulikiwe.
 
Baada ya uamuzi wa mahakama serikali ilipaswa kuandaa muswada wa kwenda bungeni ili sheria ya kuruhusu mgombea binafsi ipitishwe.

Pamoja na hii kuwa mara ya pili kwa mahakama kutoa uamuzi huo serikali (soma CCM) ilitangaza kuwa itakata rufaa kupinga uamuzi huo. Nijuavyo mimi mpaka sasa hilo halijafanyika. Hii inaonekana kuwa ni delaying tactics za CCM ili 2010 ipite hali ikiwa kama ilivyo. Mimi navilaumu vyama vya upinzani ambavyo kwa ujumla wao vinabweka bila kung'ata.

Swala hili wangelivalia njunga na kurudi mahakamani ikibidi ili hukumu ya mahakama itekelezwe. Vile vile swala la kuwa na katiba mpya ya nchi. Nalo linazungumzwa kwenye majukwaa bila hatua zozote kuchukuliwa. Siyo lazima serikali ndiyo i-initiate kila kitu. Napendekeza muungano wa vyama vya upinzani (kama upo) uitishe kongamano la wadau wote (wakiwemo wawakilishi wa wafadhili, asasi za haki za binadamu, n.k) ambao utapitisha maazimio ya kuishinikiza serikali kuanza mchakato wa kutunga sheria/kubadili katiba kuruhusu wagombea binafsi. (Wanasheria tupeni ushauri wa kisheria).
 
Mgombea binafsi wa uRais? Yaani mtu atoke huko na hisia zake binafsi na aongoze nchi? Yaani tuongozwe na hisia binafsi? Kwa kisa gani hasa?

Siamini kuwa kuna tija yoyote zaidi ya madhara kama tukiwa na Rais atakaechaguliwa bila kutoka kwenye chama au taasisi yenye mfumo thabiti wa uongozi. Kuwa na mgombea wa kuteuliwa na chama chake, inatuhakikishia kuwa anafuata sera zinazoaminika, zinazokubalika, zinazoweza kudumu na zenye tija kwa Taifa. Mtu binafsi akichaguliwa kuwa Rais anaweza kuji-control hasa katika masuala ya ethics, policies na kutekeleza mambo sustainably? I doubt.
 
Jamani katika haka ka list kangu haka mnaona Nani anaweza kuliongoza taifa letu angalau tukawa na imani na serikali yetu ?

Bernard Membe

Edward Lowasa

Dr.Wilbard Slaa

Ibrahim Lipumba

Samwel Sitta

Mizengo Pinda

Mark Mwandosya

Jakaya kikwete
 
Jamani katika haka ka list kangu haka mnaona Nani anaweza kuliongoza taifa letu angalau tukawa na imani na serikali yetu ?

Bernard Membe

Edward Lowasa

Dr.Wilbard Slaa

Ibrahim Lipumba

Samwel Sitta

Mizengo Pinda

Mark Mwandosya

Jakaya kikwete
 
Last edited:
Six!!! Lakini ... Mkuu mbona kalist kako umekalimiti sana!!
..... Mbatia je?
 
Back
Top Bottom