The road towards 2010 Elections

The road towards 2010 Elections

Kati ya hawa nani atafaa kutuongoza 2010-2015?

  • Edward Lowassa

    Votes: 0 0.0%
  • Dr. Slaa

    Votes: 7 38.9%
  • Prof. Lipumba

    Votes: 0 0.0%
  • Mizengo Pinda

    Votes: 5 27.8%
  • Samwel Sitta

    Votes: 0 0.0%
  • Jakaya Kikwete

    Votes: 2 11.1%
  • Mark Mwandosya

    Votes: 2 11.1%
  • Harisson Mwakyembe

    Votes: 2 11.1%
  • None of The above

    Votes: 0 0.0%

  • Total voters
    18
  • Poll closed .
Man, if this goes thru watanzania tutaendelea kuwa watu wa ajabu. Is it that we want bigger parliament or effective parliament. Our parliamnet has for a long time been lame, is it because of size or something else.

Hii inaweza kuwa ni "EPA" ya kujtakia, na sijui ni nani mwenye uamuzi wa mwisho juu ya hili. Kama ni bunge ndio linaamua basi tunastahili kuwa na sauti juu ya bunge. If that is true, is so sad.
 
you can fool some people sometime but you cannot fool all the people all the time. Bob Marley the great

Thanx mkuu for this. Its just yesterday I had a call from fella in Moshi, eti Tanrod wameenda kuwapa wananchi wa moshi vijijini taarifa ya kujenga barabara ya kibosho umbwe kwa kiwango cha lami!

Barabara mbovu kuliko zote wilaya hii. Mwanakijiji wa kawaida kabisa akawauliza wale warembo waliotumwa na Tanrod, hii barabara itaanza kujengwa lini? Wakawaambia mwishoni mwa mwaka 2010! hapo ndo ?

zikaanza. Mheshimiwa alikuwa amepiga kambi huko kwa kipindi akihamasisha watu kuhusu chama. Ndipo wakaibuka na hii hongo ya sasa. Niliwahi siku moja kumuuliza kada wa sisiem ni kwa nini barabara hii haijengwi, alichonijibu kiliniacha hoi! Ati " ULISHAONA CHAKULA CHA WATOTO WANAPEWA MBWA?"
 
Lakini kwa tunaomjua John Magale Shibuda, hatushangai kwa hayo maneno anayotamka hivi.

Kwa taarifa fupi tu ni kwamba huyu jamaa, kuanzia shule yake hadi asset alizonazo vinatokana na ujanjaujanja ambapo yeye huwa yuko radhi kumfanyia mtu kazi yoyote alimradi anapata ujira. Ukifuatilia CV yake hutashindwa kubaini kuwa hajawahi kuwa mkulima, mfanyabiashara wala mfanyakazi.

Mnamo mwaka 2002, alikuwa ni miongoni mwa waliolipwa fedha nyingi ili kuchafua hali ya hewa kwenye mkutano mkuu hali ilivilazimu vyombo vya usalama kumshusha kwenye treni iliyobeba wajumbe wa mkutano mkuu na kumzuia kuhudhuria mkutano huo.

Na hata mwaka 2005, pia alipokea fedha ili agombee urais kwa lengo la kupunguza idadi ya kura za Kanda ya Ziwa kwa mgombea mmojawapo.

Hata ukifuatilia maelezo yake wakati akijinadi, utabaini kuwa hana shule bali alikuwa ni mahiri katika matumizi ya ISTILAHI za kiswahili bila ya kuzingatia kanuni za Lugha.

Na taarifa zilizopo ni kwamba, yeye kujitangaza mapema kuwa anakusudia kugombea urais mwaka 2010, ni mkakati wa kumjengea UHALALI wa kugombea urais mshikaji wake aliyemfadhili mwaka 2005 ambaye pia vyanzo vya uhakika vinaeleza kuwa anautaka urahisi.
 
Ruksa mwana-CCM kutangaza kuwania Urais...

2008-11-17 10:26:42
Na Muhibu Said

Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimesema mwanachama wake yeyote anaruhusiwa kutangaza nia ya kugombea Urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 kabla ya muda wa kufanya hivyo haujafika, kwa vile suala hilo ni katika upanuzi wa demokrasia katika chama hicho.

Kauli hiyo ilitolewa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi na Uenezi, Kapteni John Chiligati, alipozungumza na waandishi wa habari, katika Ofisi Ndogo za chama hicho, Barabara ya Lumumba, jijini Dar es Salaam jana.

Chiligati, ambaye pia ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, alisema kutokana na demokrasia kupanuka ndani ya CCM, mwanachama yeyote wa chama hicho anaruhusiwa kutangaza nia ya kuwania Urais katika hali yoyote awayo na kwamba, kitu pekee kinachokatazwa na chama, ni kufanya kampeni kabla ya muda wa kufanya hivyo haujafika.

Alisema hayo baada ya kutakiwa na mmoja wa waandishi wa habari aeleze msimamo wa CCM kutokana na Mbunge wa Maswa, John Shibuda (CCM) kutangaza hivi karibuni kuhusu nia yake ya kukusudia kuchukua fomu ili akiombe chama hicho kimsimamishe mwaka 2010 agombee Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kama Shibuda amesema atagombea Urais mwaka 2010, ni kupanua demokrasia, ni vizuri, watasema mengi. Hata wewe unaweza ukanywa pombe zako ukasema nitagombea. Hajavunja sheria wala Katiba. Ila kama tutasikia anazunguka sehemu mbalimbali nchini, anafanya kampeni hivi sasa, hapo tutamchukulia hatua, alisema Chiligati.

Alisema CCM ina utaratibu wake wa kuteua wagombea wa nafasi zote za uchaguzi, hivyo vikao vya chama ndivyo vitakavyoamua nani agombee na nani asigombee.

Wiki iliyopita, baadhi ya vyombo vya habari, vilimkariri Shibuda akitangaza nia ya kuchukua fomu mwaka 2010 kwa lengo la kukiomba chama kimteue agombee Urais katika Uchaguzi Mkuu, unaotarajiwa kufanyika mwaka huo.

Hatua hiyo ya Shibuda, ambaye alikuwa mmoja wa wanachama waliochukua fomu kuomba wateuliwe kugombea urais mwaka 2005, iliwashtua wengi kutokana na kuonekana kuwa inalenga kuleta upinzani dhidi ya Rais Jakaya Kikwete, ambaye anatarajiwa kuteuliwa tena na CCM kuwania kiti hicho katika Uchaguzi Mkuu huo wa mwaka 2010.

Hali hiyo, inatokana na utaratibu uliozoeleka ndani ya CCM wa kumwachia rais aliye madarakani amalize vipindi viwili vya uongozi katika nafasi hiyo.

SOURCE: Nipashe
 
"Hata wewe unaweza ukanywa pombe zako ukasema nitagombea. Huvunji katiba wala sheria" Huyu Chiligati vipi? yaani bila mtu kunywa pombe huwezi kusema nitagombea? Yaani kufanya jambo ambalo si uvunjifu wa katiba wala sheria lazima unywe pombe!!!!
Hizo ni kauli zilizo jaa unafiki mkubwa, yaani unaunga mkono jambo ambalo hulipendi! alitakiwa kuwa wazi tu kuwa hapendi watu wagombee 2010 japokuwa sheria inawaruhusu!
 
Kaka nimekuelewa vizuri kwenye mahitimisho yako. Pia utakubaliana na mimi kuwa we as Tanzanian pindi mtu anapokusaidia popote pale unakuwa mtumwa kwa namna moja hata nyingine.

Ni nadra sana kuona mtu amemsadia mtu then yule aliesaidiwa akawa na confidence ya kutofautiana na mfadhili. Go back to JK and his team.

Kwa hiyo Mwalimu alipokuwa akipewa misaada na wazungu tuligeuka watumwa wa wazungu, au?

Kama binadam ni mtumwa ni mtumwa tu msaada hauongezi wala kubadili anything kwenye tabia ya mtu yule ambaye amezoea utumwa!
 
Kwa hiyo Mwalimu alipokuwa akipewa misaada na wazungu tuligeuka watumwa wa wazungu, au?

Kama binadam ni mtumwa ni mtumwa tu msaada hauongezi wala kubadili anything kwenye tabia ya mtu yule ambaye amezoea utumwa!


...naona issue ya john magale shibuda inawaumiza ccm ..hadi wamemtuma naibu katibu mkuu wa chama ..capt mkuchika kufanya ziara ya siku 8 shinyanga ..ambako anahimiza wanachama kufuata utaratibu wa kupeleka malalamiko ndani ya chama na kuacha tabia ya kulalamikia maamuzi ya chama vichochoroni....amekaririwa na TBC1 Asubuhi hii..
 
Shibuda aitikisa CCM




na Edward Kinabo

Source: Tanzania daima


CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimesema kinakusudia kumpitisha Rais Jakaya Kikwete, kuwa mgombea wake wa urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, licha ya katiba na kanuni za chama hicho kutoa uhuru kwa mwanachama yeyote, mwenye sifa zinazostahili kuwania kiti hicho.

Hayo yalibainishwa mwishoni mwa wiki na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, John Chiligati, katika mahojiano maalumu na Tanzania Daima yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Msekwa akihojiwa katika ofisi ndogo ya makao makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, alitoa msimamo huo wa chama chake baada ya kuombwa kutoa maoni yake kuhusiana na hatua ya Mbunge wa CCM, Jimbo la Maswa, John Shibuda, kutangaza nia yake ya kugombea kiti cha urais katika uchaguzi mkuu wa 2010, kupitia chama hicho.

Akizungumza kwa tahadhari kubwa na kuchagua maneno ya kutumia, Msekwa alisema katiba, kanuni na taratibu za CCM zinaruhusu mtu kutangaza nia yake ya kutaka kugombea nafasi yoyote ya uongozi serikalini.

Alisema Shibuda hajakosea kutangaza nia yake mapema kwa sababu katiba ya CCM haikuweka muda ni lini mhusika atangaze nia yake ya kugombea, ila kinachokatazwa ni kuanza kampeni mapema.

"Katiba yetu haikatazi mtu kutangaza nia yake ya kutaka kugombea na haikuweka muda wa kutangaza nia hiyo. Kwa hiyo yeye ametangaza nia yake … ni sawa. Ila kinachokatazwa ni kuanza kampeni mapema …hiyo ni sawa na sheria ya uchaguzi. Hairuhusu kufanya kampeni kabla ya wakati. Kusema kwamba mimi nitagombea ubunge, udiwani au urais, kanuni hazikatazi," alisema.

Msekwa aliendelea kusema kuwa, pamoja na katiba ya CCM kuruhusu mwanachama kutumia haki na uhuru wake wa kutaka kugombea nafasi yoyote, ikiwemo urais, chama hicho kina utaratibu wake wa ndani uliozoeleka lakini ulio nje ya kanuni, wa kumwachia rais aliye madarakani agombee na kumalizia kipindi chake cha pili, kwa kuwa muda wa ukomo wa urais ni vipindi viwili.

Alisema CCM inakusudia kumpitisha tena Rais Kikwete awanie kiti hicho kwa awamu ya pili, kwa kuwa hadi sasa amefanya kazi nzuri sana ya kuboresha maisha ya wananchi, kwa hiyo itampa nafasi nyingine ya kuomba ridhaa ya wananchi, kama ilivyofanya kwa Rais aliyepita, Benjamin Mkapa.

"Lakini tukiachana na hilo la katiba na kanuni za chama chetu, sisi tuna utaratibu wetu wa ndani ya chama…hii si kanuni, ni utaratibu wetu, ni mazoea. Kwamba kwa kuwa kikomo cha urais ni miaka 10, basi sisi huwa tunamwacha rais aliye madarakani, hasa rais mwenyewe anapokuwa amefanya kazi nzuri, kama Rais Kikwete alivyoboresha maisha ya wananchi, …huwa tunamchagua rais huyo aliye madarakani, agombee urais mara ya pili. Na hivyo ndivyo tunavyokusudia kufanya kwa Rais Kikwete…amefanya kazi nzuri sana," alisema.

Kwa hiyo kama kuna mwenye nia ya kugombea urais kupitia CCM, hakatazwi…lakini kwa kuzingatia mazoea yetu, tunakusudia kumchagua Rais Kikwete. Na haya si maoni yangu binafsi kama ulivyoniuliza…huu ni utaratibu wetu, ndiyo mazoea yetu katika chama," alisema Msekwa.

Naye, Chiligati akizungumza kwa njia ya simu kuhusu suala hilo, alisema Katiba ya CCM haikatazi mwanachama mwenye sifa, kuwania uongozi au kutangaza nia yake ya kutaka kufanya hivyo, isipokuwa inakataza watu kuanza kampeni mapema.

Hata hivyo, kama alivyosema Msekwa, Chiligati pia alisema japo Katiba ya CCM inasema hivyo, bado chama hicho kina utaratibu wake wa kumpa rais aliye madarakani vipindi viwili vya uongozi, kama hajafanya kosa lolote kubwa.

"Kwa hiyo katiba yetu inasema hivyo, japo ndani ya chama chetu tuna utaratibu wetu wa kumwachia rais aliye madarakani apitishwe kugombea urais mara ya pili ili amalizie vipindi vyake vyote viwili. Lakini huo ni utaratibu wetu wa ndani tu…lakini Bwana Kinabo (Mwandishi wetu), wanachopaswa kufahamu walio nje ni kwamba Katiba ya CCM inatoa uhuru kwa mwanachama yeyote yule kugombea wadhifa wowote ule anaotaka," alisema Chiligati.

Katika hatua nyingine, Chiligati alijibu shutuma zilizoelekezwa kwake na kwa Yusufu Makamba, kuhusu kulimbikiziwa vyeo vingi na Rais Kikwete, hata kuelemewa na kukosa ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao.

Chiligati alisema, habari hizo amezisoma katika magazeti tu, lakini shutuma za wabunge hao, watazijadili ndani ya vikao vyao vya chama.

Hata hivyo Chiligati, aliwataka wabunge hao wanaomwona kuwa hana ufanisi kuelewa kuwa yeye (Chiligati), kama walivyo binadamu wote, hajakamilika.

"Hayo nimeyasoma kwenye gazeti tu, tutalizungumza hilo kwenye vikao vyetu vya chama. Sina lolote la kusema…ee wanasema sina ufanisi, nilikuwa China wakati wa kampeni za Tarime. Lakini hakuna binadamu aliyekamilika," alisema Chiligati.

Awali katika mahojiano na Msekwa kuhusu shutuma zilizotolewa na wabunge hao ambazo pia zinamgusa Rais Kikwete, Msekwa alisema Rais Kikwete hakufanya kosa lolote katika uteuzi huo kwani alizingatia Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Katiba ya CCM, ambazo zote, moja kama Rais na nyingine kama Mwenyekiti wa CCM, zinampa mamlaka ya kuteua viongozi anawaona wanafaa.

Alisema tofauti iliyopo ni kwamba, kwa mujibu wa katiba ya nchi, rais anapaswa kuteua waziri kutoka miongoni mwa wabunge, na kwa mujibu wa Katiba ya CCM, rais huku akiwa ni Mwenyekiti wa CCM, ana mamlaka ya kuteua Katibu Mkuu wa chama lakini uteuzi huo lazima uthibitishwe na Halmashauri Kuu ya chama hicho (NEC).

Alisisitiza kuwa Rais Kikwete kumteua Makamba kuwa Katibu Mkuu wa CCM na wakati huo huo kuwa Mbunge wa Kuteuliwa na Rais, hakufanya kosa wala hajakosa busara kufanya hivyo.

Alisema hata Rais wa kwanza, Baba wa Taifa, hayati, Julius Kambarage Nyerere, aliwahi kumteua Oscar Kambona kuwa Waziri wa Tawala za Mikoa na wakati huo huo alikuwa ndiye Katibu Mkuu wa kwanza wa Chama cha TANU, kabla ya kuzaliwa CCM, mwaka 1977.

Hata hivyo alisema, Mwalimu alitumia busara kumteua Kambona kushikilia nyadhifa zote hizo kwa sababu majukumu ya uwaziri wa Tawala za Mikoa kwa wakati huo, yalikuwa yakiendana sana na majukumu ya Katibu Mkuu wa TANU.

Msekwa aliwataka, Zambi na Mpesya, kujenga hoja za kutaka kuwe na sera ya Rais au Mwenyekiti wa CCM, kuwekewa mpaka katika uteuzi wake ili awe anateua mtu mmoja kushikilia wadhifa mmoja tu, badala ya wabunge hao kuendelea kulalamika tu kupitia vyombo vya habari.

"Wao wasilalamike tu kwenu …kwenye vyombo vya habari. Haitawasaidia…wajenge hoja kwenye vikao halali vya chama kwamba sisi tunapendekeza kuwe na policy (sera) inayomshinikiza Rais au Mwenyekiti wa chama (CCM) kuteua mtu mmoja kushikilia cheo kimoja tu, kwamba mtu mmoja asilimbikiziwe vyeo vingi kama wanavyosema, iwe ni ‘one man, one position policy' (iwe ni sera mtu mmoja cheo kimoja). Kwa hiyo wajenge hoja ya kutaka kubadilisha taratibu. Nasisitiza tena, hizi ndizo taratibu zetu," alisema Msekwa.

Tangu kumalizika kwa uchaguzi mdogo wa ubunge na udiwani katika Jimbo la Tarime na Kata ya Tarime Mjini, ambapo Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kilishinda, kumekuwa na mjadala mzito ndani ya chama hicho, ambapo baadhi ya wabunge wa chama hicho wameripotiwa mara kadhaa wakimtaka Katibu Mkuu wao, Yusufu Makamba, ajiuzulu.

Aidha, katika hali inayoonyesha kutoridhishwa na uongozi wa Rais Kikwete, mmoja wa wabunge wa chama hicho wa Jimbo la Maswa, John Shibuda, wiki iliyopita alitangaza nia yake ya kugombea urais katika uchaguzi mkuu wa 2010, kupitia chama hicho.

source tanzania daima

My take;

Jamani hawa watu wanatuona madanganyika mazuzu eh?? Nashindwa hata kufikiria kama huyu mzee anajua anachokiongea.

Hebu mwenye data tunaomba atuorodheshee kazi nzuri sana alizozifanya huyu anayetajwa hapa jamani jamvini
 
Mzee,

Kusema hakuna mazuri aliyofanya ni UONGO wa kutupa! Sema mengi mabaya yamemeza mazuri.
 
Mzee,

Kusema hakuna mazuri aliyofanya ni UONGO wa kutupa! Sema mengi mabaya yamemeza mazuri.

FP sijasema hakuna mazuri aliyofanya ila kwa msisitizo wa mzee wetu nimeomba tuyalist mazuri aliyofanya hadi sasa tuweze kuqualify statement ya mzee msekwa. Amerudia JK kafanya kazi nzuri sana sasa tunajaribu kupata ushahidi ili tumpe haki yake

Kila apandaye atavuna alichopanda, tupo pamoja mkuu
 
shibuda aitikisa ccm


]

“lakini tukiachana na hilo la katiba na kanuni za chama chetu, sisi tuna utaratibu wetu wa ndani ya chama…hii si kanuni, ni utaratibu wetu, ni mazoea. Kwamba kwa kuwa kikomo cha urais ni miaka 10, basi sisi huwa tunamwacha rais aliye madarakani, hasa rais mwenyewe anapokuwa amefanya kazi nzuri, kama rais kikwete alivyoboresha maisha ya wananchi, …huwa tunamchagua rais huyo aliye madarakani, agombee urais mara ya pili. na hivyo ndivyo tunavyokusudia kufanya kwa rais kikwete…amefanya kazi nzuri sana,” alisema.

[/b]


......nausea ....disgusting....somebody help me .....naomba mfuko wa kutapikia please!!!!!!!....hawa wanafikiri watanzania...mabwege?
 
FP sijasema hakuna mazuri aliyofanya ila kwa msisitizo wa mzee wetu nimeomba tuyalist mazuri aliyofanya hadi sasa tuweze kuqualify statement ya mzee msekwa. Amerudia JK kafanya kazi nzuri sana sasa tunajaribu kupata ushahidi ili tumpe haki yake

Kila apandaye atavuna alichopanda, tupo pamoja mkuu

1. Misafari mingi ya nje ya nchi
2. Kubadili baraza la mawaziri hovyo
3. Kushindwa kuwashughulikia wazungu wa Unga
4. Kushindwa Kuwashughulikia mapapa wa EPA, Richmond, Kiwira Coal Mining, IPTL, Buzwagi etc
5. Kushindwa kutimiza ahadi alizotoa wakati akiomba kura ili aweze kula 2005
6. Kushindwa kudhibiti sera mbovu za serikali yake zinazowakandamiza na kuwanyima haki walimu, Madaktari, wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu,wastaafu wa EAC etc...........weka na wewe zako unazoona ni kazi nzuri za JK!!!!!!!
 
Mzee,

Kusema hakuna mazuri aliyofanya ni UONGO wa kutupa! Sema mengi mabaya yamemeza mazuri.

Fairplayer be fairler kwa kuorodhesha hayo mazuri ambayo unasema yamefunikwa na mabaya, unajua kama ukisema kuna mazuri utakuwa unamsaidia sana rais ukiyataja kuliko kusema tu yapo wakati wengine hawayaoni.

Unajua kauli ya Msekwa inaweza kukubaliwa na mjinga, naweza kukubaliana naye kuwa JK awe mgombea wa CCM 2010, lakini akisema awe mgombea kutokana na kazi nzuri aliyoifanya kwa Chama na serikali, hapo sijui kama ni kweli.

Ndio tunarudi kulekule kwenye siasa za kudanganyana. Mkubwa akikosea unamlinda ili uendelee kuwepo kwenye utukufu wake.
 
Alivyosema CCM inakusudia kumpitisha Kikwete alitaja ni kikao gani kilifanyika na uamuzi huo ulifikiwaje?

Ikiwa chama kinaruhusu watu kuwania uarais, chama kitakusudiaje kumpitisha mgombea mmoja bila ya kuwasikiliza wagombea wengine? Hawawezi hata kufanya a sham process? Sasa ukifika muda wa kuwasilisha majina na Shibuda akisema alipigwa vita na viongozi wa juu wakiwamo kina Msekwa wataweza kujitetea kwamba walikuwa neutral na objective katika process?

Tunaendesha mambo kienyeji kweli!
 
mi najisikia kichefuchefu tupu...Msekwa kazeeka sasa jamani
 
mi najisikia kichefuchefu tupu...Msekwa kazeeka sasa jamani

NOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOOO! msekwa he is right kikwete amefanya mambo mazuri sana sana bila yeye nchi hii pangekuwa hapakaliki hebu fikiria angeruhusu Mkapa ashitakiwe au angesema mifisadi yote iende mahakamani na isipewe hata dhamana kwa sababu wameihujumu nchi unafikiri ni nini kingeendelea?

Amefanya mazuri kwa watu matajiri wenye pesa zao na kwasababu nchi hii inamilikiwa na wenye fweza msekwa yuko right....., naamini mimi na wewe hatujaona mazuri yake kwa sababu sio makada wa CCM, sio majambazi, sio wauza madawa ya kulevya, sio mafisadi hata tukifa kikwete hata kuja kwenye msiba wetu.. yani tupotupo tuuu.
 
Mnyonge Mnyongeni Haki yake mpeni......Hebu tutafakari na tuangalie mazuri aliyofanya huyu bwana mkubwa ( white) ..tusimsilibe tu, haya mimi natoa haya wewe utaongezea.:

1. Amejenga barabara ya Kwenda Kilwa,
2. Amekamata Wezi Wa EPA bila Woga
3. Ameweza kushawishi Marekani/wahisani wakatupa fedha nyingi kwa ajili ya shughuli za maendeleo.
4. Amejenga shule nyingi za msingi na sekondari nchini kote...at least kila kata.
5. Amekua Menyekiti wa AU.
6. Tunategemea safari zake zitatuletea wawekezaji wengi siku za usoni.
7. Utalii umeogezeka ...hii ni kutokana na taarifa ya wizara.
8. Amani kama kawaida.
9. Ameweza kukemea mimba mashuleni.
10.Ameweza pia kukemea mauaji ya maalbino na kushauri pia masuala ya ufugaji bora wa ngombe.


aaah..! wakuu naona naishiwa mazuri..nikiendelea zaidi ya hapo ni uongo..maana nimejitahidi sana mpaka kufika hapo kwenye point ya kumi. Endeleeni na nyie...!
 
Mnyonge Mnyongeni Haki yake mpeni......Hebu tutafakari na tuangalie mazuri aliyofanya huyu bwana mkubwa ( white) ..tusimsilibe tu, haya mimi natoa haya wewe utaongezea.:

1. Amejenga barabara ya Kwenda Kilwa,
2. Amekamata Wezi Wa EPA bila Woga
3. Ameweza kushawishi Marekani/wahisani wakatupa fedha nyingi kwa ajili ya shughuli za maendeleo.
4. Amejenga shule nyingi za msingi na sekondari nchini kote...at least kila kata.
5. Amekua Menyekiti wa AU.
6. Tunategemea safari zake zitatuletea wawekezaji wengi siku za usoni.
7. Utalii umeogezeka ...hii ni kutokana na taarifa ya wizara.
8. Amani kama kawaida.
9. Ameweza kukemea mimba mashuleni.
10.Ameweza pia kukemea mauaji ya maalbino na kushauri pia masuala ya ufugaji bora wa ngombe.


aaah..! wakuu naona naishiwa mazuri..nikiendelea zaidi ya hapo ni uongo..maana nimejitahidi sana mpaka kufika hapo kwenye point ya kumi. Endeleeni na nyie...!

La 11. Ameongoza kwenye kampeni ya kupima ukimwi.
.......angeongoza pia kwenye kutoa majibu hadharani.
 
Kwa hiyo katiba ya sisiemu haifatwi ila utatatibu ambao hauko katika katiba. Thus why hata katiba ya nchi haifatwi ila ni matakwa ya mafisadi ambayo ni utaratibu wa watu wachache waliojiwekea kulinda maslahi yao. Jamani tukiondoe chama hiki madarakani wapinzani andaeni watu wakutukomboa kutoka mikononi mwa jinamizi hili ccm linatumaliza. wakulima, wafanyakazi na wananchi kiujumla tufumbue macho tu mpige nyani huyu bila kumuangalia usoni tusijemwonea huruma.

I dont see good things from this guy even if there is one he should have done more. Cheki ktk mtandao wa chama hiki viongozi ni walewale tunaowastukia kwa sana.

Tanzania yote inalia
 
Back
Top Bottom