1.
Sawa sawa nimekusikia mkuu, naomba kuweka sawa kama ifuatavyo:-
1. Suala la Somaiya kutoa sh. Mill 400, kwangu sijaliona kua ni tatizo kwa sababu so far Tanzania hatuna sheria ya kukataza misaada ya wananchi kwa vyama vyetu vya siasa, nijuavyo mimi ni kwamba vyama vyetu vyote kuanzia upinzani mpaka CCM hupokea misaada mbali mbali toka nje na ndani ya nchi yetu, Mrema for the record alipewa hela nyingi sana na Scandnavians, pamoja na chama kimoja cha South Africa, hakukuwa na ubaya wowote, nitakuwa na tatizo kama tungekua na sheria, lakini ya kupewa misaada inafanyika kila siku na tunajua sana ila haisemwi tu hadharani na hatusemi kwa sababu haivunjwi sheria ya jamhuri na hiyo misaada.
- Mimi sikumtetea mtoaji wa msaada, siwezi kumtetea mtu ambaye sifahamu vizuri habari zake, sidhani kama kuna asiyeelewa hilo lakini siwezi kukataa msaaada wa mwananchi bila sababu ya msingi kama sheria inaruhusu, sasa labda wewe uniambie kosa la huyu mwananchi aliyetoa msaada ni lipi kwa sababu siamini kwamba kuwa Mhindi ukatoa msaada kwa chama cha siasa ni kosa.
2.
- Kupokea msaada kwangu sio kuwa mtumwa, tatizo ni kama ni mtumwa siku zote, maana msaada wa siku moja hauwezi kukugeuza ukawa mtumwa mwananchi ambaye hujawahi kuwa mtumwa. Obama ameshinda kwa kusaidiwa sana na misaaada sasa unasema kwamba atakuwa mtumwa kwa waliompa misaaada? Unafikiri FBI itamuacha? Hapana bro hapa tatizo hakuna kabisa ila tunajaribu kulazimisha kwa sababu hatuaminiani, na tatizo ni kwamba hatuna sheria na hata kama ingekuwepo haifuatwi, sasa hilo lisiwazuie wananchi kutoa misaada kwa sekta muhimu za taifa zinazohitaji misaada. Mimi siwezi kukataa msaada kama nina shida, ila sitakubali masharti ya msaada maana ni afadhali nikachukue mkopo if that is the case, lakini mifano ya njaaa za binafsi haiwezi kuhusishwa na siasa za taifa.
- Mimi ningeelewa kwamba huyu Mhindi ni proven fisadi, au ana kesi tayari, lakini the man is clean as mwananchi, sasa what is the beef? Unless kuna something hamukisemi!
- Ndugu yangu Mkwawa has nothing to do na this, hivi unajua kuwa akifufuka leo atajiua tena kukuta wananchi weusi wameoa wazungu, licha ya hayo unayoyasema?
3.
- Hapa sijakuelewa kabisa, una maana watu wanaotoa michango mikubwa kwenye harusi za wengine basi ni haki yao kuwaomba wake wa harusi? Is that so? Hivi unajua Mengi hutoa hela nyingi sana kusaidia harusi za wananchi, sasa unasema nini exactly?
- Pinda na Hosea wanaweza kusema anything they want, sisi tutawahukumu kwa matendo yao, kwenye ufisadi Hosea hana credibility kabisa, angalau kidogo Pinda hatujamsikia, lakini na yeye ni muoga, anawaogopa mafisadi, sasa what this has to do na Somaiya kutoa msaada kwa CCM?
4.
- Hii point ingekua na nguvu sana kama Somaiya ni proven mwizi au jambazi, lakini huyu amehojiwa na wazungu hawakumshitaki lakini wamemshitaki patner wake, I mean ninaelewa kwamba kuna some hisia, sasa in absence of sheria ya kubana hii misaada as a nation tunafanya nini? Hatuwezi kushambulia chama cha siasa kwa kupokea msaada legally na pia hatuwezi kumshambulia mtoa msaada eti kwa sababu ni Mhindi!
- I mean with all due respect na mifano ya binafsi, lakini haina uhusiano wowote na national politics zetu, ni kwamba kuna ishu moja wengi hamtaki kuiona hapa ni kwamba Tanzania hatuna sheria inayokataza wananchi kutoa misaada kwa vyama vyetu vya siasa, na hakuna sheria inayokataza vyama kupokea msaada, na hii misaada inapokewa na vyama vyote nchini,
Kwa hiyo kwangu tatizo ni sheria, kwa sababu sio siri kwamba Mtandao walipewa hela na Iran za kampeni, lakini still bado hawakuvunja sheria zetu kwa kupokea misaada hiyo, katiba mbovu ndiyo inayotuletea matatizo, maana in the absence of respect kwa rule of law ndio hivi sasa tunashitukiana, na hatuaminiani sasa badala ya kugusa panapotakiwa tunalaumu kila mtu bila sababu, tatizo mkuu wangu ni kwamba hatuna sheria ya kubana misaada!
Kumtetea fisadi hata siku moja, lakini pia siwezi kumchukia mwananchi bila ya sababu, au kwa sababu ana hela nyingi za kutoa msaaada hapana, lakini pia ninakuelewa sana, ingawa sikubaliani na mawazo yako ambayo ninayaona ni model ya kuhisi na kuhukumu, bila sababu ya msingi.