The road towards 2010 Elections

The road towards 2010 Elections

Kati ya hawa nani atafaa kutuongoza 2010-2015?

  • Edward Lowassa

    Votes: 0 0.0%
  • Dr. Slaa

    Votes: 7 38.9%
  • Prof. Lipumba

    Votes: 0 0.0%
  • Mizengo Pinda

    Votes: 5 27.8%
  • Samwel Sitta

    Votes: 0 0.0%
  • Jakaya Kikwete

    Votes: 2 11.1%
  • Mark Mwandosya

    Votes: 2 11.1%
  • Harisson Mwakyembe

    Votes: 2 11.1%
  • None of The above

    Votes: 0 0.0%

  • Total voters
    18
  • Poll closed .
Asha,
mkuu wangu naona umeamua,Angalau kwa mwaka 2010 tuwe na vijana makini 50.I mean walio na umri wa chini ya miaka 35
 
Jmani si tuna Raisi kijana, mwenyekiti wa uVCCM, el, and the list goes on.............??????

Hawa si walijinadi na kunadiwa hivyo just 3 yrs ago.
 
Jmani si tuna Raisi kijana, mwenyekiti wa uVCCM, el, and the list goes on.............??????

Hawa si walijinadi na kunadiwa hivyo just 3 yrs ago.

Kama vijana tunaowataka ndio wa design hii. NI afadhari tutawaliwe na kina babu, sasa hivi nchi ni kama inatawaliwa na vijana wa shule. Kila kitu kinaenda ovyo ni kama nchi inapiga hatua nyuma kutoka pale alipotuacha Mkapa.

Kama unazungumzia vijana design ya hao waliojinadi miaka mitatu iliyopita kwa ujana NO THANKS, unless tuna vijana wengine!
 
Kama vijana tunaowataka ndio wa design hii. NI afadhari tutawaliwe na kina babu, sasa hivi nchi ni kama inatawaliwa na vijana wa shule. Kila kitu kinaenda ovyo ni kama nchi inapiga hatua nyuma kutoka pale alipotuacha Mkapa. Kama unazungumzia vijana design ya hao waliojinadi miaka mitatu iliyopita kwa ujana NO THANKS, unless tuna vijana wengine!

Wale walikuwa wanatoka Chama Cha Matapeli jamani, ndio maana Mzee Kikwete na umri wake wa kustaafu kwa hiyari wa miaka 55 wao wakamuita kijana. Sasa kama Kikwete alikuwa kijana basi Mbowe na umri wake wa miaka 40 ya mwanzoni wakati huo alikuwa nani? Na Zitto chini ya 30 alikuwa mtoto kabisaaaaa!.

Tutafute vijana wa kweli sio vijana wa kupigwa cream!

Unajua ujana huwa unasifa zake, nguvu, ubunifu nk- si unaona mtu kama Zitto alivyo huku na kule? Unadhani Kingunge na umri wake anaweza hizo?


Asha
 
Dada Asha,

Unaposema vijana, una maana ya kundi gani la umri (age group)?

Je ni vijana kutoka kila vyama au unachofanya ni yale ya mwamba ngoma kuvutia kwake kutaka Chadema kiwe chama pekee?

Je nafasi ya vijana wa CUF, CCM, TLP, NCCR, UDP iko wapi katika mchakato mzima na msukumo unaouleta?

Je vijana ni suluhisho la matatizo ya Tanzania au ni vipi kuwe na umuhimu mkubwa wa kuongeza marudufu vijana katika Bunge, vijana ambao bado hawana upeo wa maisha au kazi?
 
Mimi sijui kuhusu nani kati a vijana ama na wazee kuwa ndio watupe dira ya wapi tuelekee.

Ninachofahamu michango kutoka kwa wote inahitajika...Na hviyo basi kupelekea umuhimu wa kambi zote hizo za kijamii.

Pengine nigusie jambo moja...Kuwa mawazo ya vijana yapewe kipaumbele na pia yanakshiwe na busara za wazee credible.

Si wazee ni wazee tu....Hata wakati wa mwalimu nadhani kila mzee alikuwa ni babu yako na kila baba ni baba yako...Majukumu ya ulezi wa watoto yalikuwa ni ya jamii husika kwa mfano kijiji nk.

Dunia ya sasa imebadilika....Na hivyo na sisi hatuna budi kufanya hivyo.

Vijana wapewe nafasi na wazee wabaki kuwa washauri kwani mawazo yao ni MGANDO!

Kuwa na mawazo mgando na wakati hata Lady jay D keshatufahamisha kuwa siku hazigandi...Ni sawa na kitendo cha kucheza peku kama aliyodai Isaya Mwita.

Nchi wameshaifikisha hapa ilipo na hatuwezi kuifumbia hali hii iliyopo mbele yetu macho hata kidogo!

Kufanya hivyo ni kukisaliti kizazi kijacho.

Nakubaliana kwenye vijana pia kuna wenye fikra za kimapinduzi na za kimaendeleo.

Kuna wale wasiokuwa hivyo...Just kama wazee wasiokuwa na busara.

Tusisahahu pia kuwa kila mwanadamu ana kipaji chake.
Tatizo letu espicially sisi waafrika ni kuwa "Square peg in a round hole"

Ni vitu visivyoingiliana...Unakuta mtu ana kipaji cha biashara na yeye anakwenda anasome kitu kingine....Ama mtu anakipaji kingine na yeye anakwenda kusomea biashara..Mtu kama huyo..Tena wengi wao wenye degees feki...Ndio hao wenye kutuingiza kwenye huu mtenenge wa madai ya UHURU.
Issue hii nitaianzishia thread yake tofauti kwani ndio mambo ya kina Mkullo na Makamba.

Kila mtu atapewa nafasi ya kulijenga Taifa kutegemeana na kipaji chake na kiongozi mkuu wa nchi ni lazima awe na conceptual skills.

Hivyo basi nakubaliana na pointi kuwa vijana wapewe nafasi ya kujaribu kuleta mapinduzi amabayo ni LAZIMA!

Hapa tusisahau kuwa mabadiliko ni lazima na hivyo hoja ama mjadala huu ni wa muhimu sana.
 
Nafikiri Tanzania sasa inachokosa siyo wabunge vijana, kinachokosekana ni watu wenye mapenzi ya dhati/ Vision katika kuliongoza taifa na kufuata misingi ya kukomboa nchi yetu kutoka katika janga la umasikini na fedhea zinazolikabiri Taifa.

Tukiangalia changamoto iliyopo, tunagundua kuna watu wazuri sana ambao wangeweza kututoa tulipo kutufikisha pengine lakini kwa sababu tunaongozwa na kundi la watu waliokumbatia wafanya biashara, watu makini wanapata taabu sana kushiriki siasa zetu badala yake taifa limeishia kupoteza maana na sifa tulizokuwa tumejipatia katika kipindi cha mwalimu Julius K. Nyerere.

Tunapoelekea 2010, suala lisiwe kuwasaidia vijana ambao wanaanza maisha hili wawe wabunge labda tuwasaidie vijana hao waweze kuwa makada wa vyama na kuweza kuwa vingozi wetu katika siku za usoni.

Hili nafikiri hata Chama Cha Mapinduzi kabla ya kupoteza mwelekeo na kukumbatia mafisadi walio either marafiki wakaribu sana na viongozi wa chama au wanaowafadhiri viongozi hao, kilikuwa kikifanya maandalizi ya vijana na ndipo kiliweza kuwapata akina Jakaya M. Kikwete, Edward Lowassa, Benjamini W. Mkapa, Jenerali Twaha Ulimwengu, Marehemu Ukiwaona Ditopile M(DITO), nk. Hawa hawakuingia siasa za juu(kugombea ubunge) mara tu ya kumaliza vyuo vikuu.

Suala la kusaidia watu kuingia bungeni lisiwe kama lilivyo ndani ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) ambao wao hawako katika kutafuta watu safi wenye uwezo wa kuliokoa taifa kama ilivyo kuwa Zamani. Wao kwa sasa wanatafuta watu wenye sifa sifa nzuri(kwao) za KIFISADI, KIFISADI, hili waweze kupata ubunge, na ukiwa msafi inakuwa taabu kuukwaa ubunge, au unaingizwa kwenye UFISADI bila kujua.

Anyway bado pamoja na hayo tunaowachache ambao wanashindwa kuwaingiza katika marashi haya mapya katika ulimwengu wa siasa za Tanzania. Mnakumbuka hata wakati baraza la mawaziri la mwanzo lilipo kuwa likitangazwa walisema wanachagua wale tu waonaowajua. Wale wanaowajua baadaye tulikuja kuambiwa ni MAFISADI wa kutupwa tangu zamani. Sijui ndizo sifa zilizotakiwa?!

Sasa swala la kuangalia watu wa 2010 lisifanywe kwa haraka sana na wapinzani kwa kupendelea makundi Fulani Fulani either yawe ya wazee au yawe ya vijana, au wanawake nk.

Hili suala lijikite katika kuangalia watu wenye uwezo wa kusaidia taifa letu na kuweza kuangalia njia mbadala ya kuwasaidia/kuwashawishi kuweza kugombea ubunge. Hili linaweza kusaidia watanzania wote ambao tayari wako na mwelekeo wa kuweza kuongoza taifa letu wapewe ama nguvu au wapewe ujasiri hili kuweza kugombea ubunge kupitia majimbo mbali mbali ya uchaguzi.

Hata kuna ambao wako Chama tawala lakini wana ethics za kusaidia nchi yetu na inawezekana wasipate nafasi katika itikadi na ahadi mpya za uongozi ndani ya CCM.

Kwa hiyo hata watanzania kila kona ya dunia wawe na wajibu wa kutambua na kumuona mtu anayefaa wamwezesha hata waaangalie chama either iwe CHADEMA, TLP nk kulingana na wapi wataona ataweza kuingilia na kumshawishi agombee.

Nimekuwa nikiangalia michango inayotolewa JF, mara nyingi nashindwa kuelewa taifa la Tanzania tuna matatizo gani, michango iko juu sana lakini mambo yanayofanyika katika Taifa la Tanzania naweza kusema hayako kabisa katika kiwango cha watu wanaokata issue hapa.

2010 wazee jitoseni tuache longo longo za kuruka angani tu, tukanyage chini tupambane na wafanya biashara za kifisadi. Tusiogope wanaotumia pesa tuwashawishi watanzania siyo tu wasichukue pesa hila wachukue na wasitoe kura kwa kufuata pesa wachague mtu mwenye uwezo.

Na pia kuna haja ya kuweka mkakati tupate tume ya uchaguzi yenye mwelekeo wa kitaifa katika mazingira ya vyama vingi vya kisiasa. Tusiachie tume ya uchaguzi yenye makada wa CCM.

Kataeni dhana ya mafiga matatu ipige vita, nafikiri hoja haitakuwa na nguvu kabisa.

Watanzania wa sasa wamebadilika kidogo tunaweza kuona mageuzi na mapinduzi katika bunge letu.
 
Age matters.
Hilo halina ubishi.
Tatizo si ku discriminate...NO!
Tatizo ni kuwapanga watu kwenye position kutokana na qualifications,mawazo mapya na ofcourse dedication.

BONGO...UMENEJA NI LESS RESPONSIBILITIES BADALA YA MORE RESPONSIBILITIES!
Hapo ndio UPUUZI WETU ULIPO.

Meneja anatakiwa kufanya kazi zaidi ya wale walioko chini yake!

Ubosi kwetu ni kupata supu ya asubuhi kusubiri lunch na kupanga miadi ya kinyaji cha jioni na kubwata mi amri na huku ukiwa huna mawazo mapya ya kuendeleza kazi unayofanya!

Na ndio maana hata hao wanaopata elimu hawaendi vijijini na wamerundikana mijini na hivyo kupelekea jamii mbovu tu.

Na serikali yenye haiwapi wananchi wa vijijini kipaumbele na hapo ndio shida!

Ona hapo Dar wasomi wamegeuka matapeli na wameivamia serikali kwa style ya siasa!

Ebu niambie kama hao wasomi wangekuwa DISPATCHED KWENYE KILA KIJIJI NA WAKAWA DEDICATED NA FUNDED KULETA MABADILIKO YA KILA NYANJA!

Niltembelea hapo bongo na niliona maajabu ya Musa!
IMEOZA!
 
Ukiwa na Bunge ambalo chini ya watu 10 ndio wako chini ya miaka 35, na juu ya watu 200 wako zaidi ya miaka 50, kati yao zaidi ya 100 wako zaidi ya miaka 60 lazima hilo bunge liwe linafikiria nyuma badala ya kufikiri mbele.

Je, bunge kama hilo litakuwa na standard and speed au litakuwa bunge goi goi? Saikolojia na bailojia zinaonyesha kuwa kuna uhusiano kati ya umri na tabia, ingawa kunaweza kuwa na exceptional chache yaani Dr Slaa akawa more progressive kuliko Peter Serukamba. Lakini ni aghalabu kukuta mtu kama Kingunge kufikiri kama Zitto Kabwe.

Though it is said age aint nothing but a number! Leo Kapuya kasema mengi kujenga hoja yake kuwa mzee wa miaka 50 bado ni kijana tu na amekumbushia jibu la Kenyatta kwa waliosema amechoka! Alikuwa akifanya majumuisho ya hotuba ya wizara ya vijana

Asha

Orodha ya Wabunge waliochini ya miaka 35:

1. Zitto Kabwe(CHADEMA)
2. Halima Mdee(CHADEMA)
3. Mhonga Saidi(CHADEMA)
4. Lucy Mayenga(CCM)

Haya endelea kama watafika 10 kati ya wabunge 324, tungekuwa kwenye aging society kama ulaya ambapo wazee ni wengi kuliko vijana hapo kungekuwa na hoja lakini katika taifa Tanzania ambapo vijana ni 35% ya taifa na 60% ya nguvu kazi. Watanzania 60% kwa ujumla wako chini ya miaka 35 halafu wawakilishi wao bungeni ndio hao tu. Wallah tunahitaji kuongeza jamani.

Niliwahi kusoma uchambuzi wa Zitto na Mnyika kuhusu generational politics, na haja ya generation change katika uongozi wa Taifa letu. Uchambuzi wao ndio msingi wa hoja yangu kwa kweli, na baadhi ya takwimu nimezichukua toka kwao

Asha
 
Ndungu wanajamii.....

Tangia kufanikiwa kwa kile kilichoitwa kama mapinduzi ya kirika kule Chimwaga mwaka 2005 na kuhakikisha kuwa waliojitwisha umiliki wa taifa hili enzi zile wanakubali kuachia nafasi ya ugombea urais kwa "bwana mdogo" Kikwete na "wanamtandao", kumekuwa na muamko mkubwa wa ushiriki katika siasa kwa vijana wengi nchini.

Kuanzia wakati huo nimekuwa nikisikia vijana wenzangu wengi wakiongelea nia yao ya ama kuingia katika siasa ama kugombea nafasi kadhaa zikiwemo za ubunge na urais. Kwa kuangalia juu juu unaweza ukasema kuwa hili ni jambo bora linalopaswa kuungwa mkono kwa hali na mali.

Hata hivyo, kuna kitu kimekuwa kikinitatiza na nia ya vijana wenzangu katika hili. La kwanza ni hili la kudhani kuwa kufanya siasa maana yake kuwa na nafasi fulani ama kwa lugha nyingingine kuu-kwaa UHESHIMIWA. Wapo vijana wengi wenye fikira za ama kugombea Ubunge ama URAIS. Hili la ubunge wengi wanafikiria kuingia katika uchaguzi wa mwaka 2010. La urais wengi wanafikiria kuanzia mwaka 2015 na kuendelea.......

Kitendo hiki kinaniumiza kichwa kutokana na uzoefu wangu kuonyesha jinsi gani siasa si nafasi uliyonayo bali mchango unaotoa kuboresha nchi kwa hali yoyote na katika nafasi yoyote uliyonayo....wengi wao wanasubiri kupata nafasi ndio watoe mchango wao. Wanatoa mchango kwa sasa mradi tu utakuwa ni moja ya hatua za kuwawezesha kupata nafsi hapo baadae.....

Lingine ni lile la mikakati wanayoitumia ana wanafikiria kuitumia kufanikisha mipango yao. Wapo walioamua kutumikia na hata kukuwadia asasi za kifisadi na MAFISADI wa sasa ili kujijenge mazingira ya kukubalika. Wapo wafanyao hayo na mengine mengi ya kifisadi ili kujijenga kiuchumi kwa fikira kuwa bila ya nguvu za kiuchumi nafasi ni ndogo zana "kushinda" nafasi waziwindazo. Wapo ambao tayari waliacha kugombea nafasi hizo hapo mwanzoni kwa ama kuhongwa ama kukubaliana na waheshimiwa wa sasa ambao wengi ni walewale tuwajuao kwa ufisadi wa kisiasa, kijamii na kijamii, wakitegemea kuachiwa nafasi hizo hapo 2010. Yaani ni vijifisadi in waiting.....

Lingine ambalo ningependa tulijadili kwa mapana zaidi ni haiba, nasaba na uwezo wa vijana hawa wenzangu. Naamini kosa moja kubwa tulifanyalo watanzania na watawaliwa wengi duniani ni kudanganyika na maneno ya jukwaani, viambazani na mabarazani kuhusu uwezo wa wale tuwachaguao kutuongoza..

Ni muhimu tukawajua waHESHIMIWA watarajiwa muda mrefu kabla haujafika wakati wa kutulaghai kuwapa kura. Na wakati wenyewe ni sasa. Wakati tukiongelea suala kuu ambalo ni mfumo tulionao sasa.....ni vilevile muhimu kutumia muda uliobakia kuelekea 2010 kuwajadili wagombea watarajiwa wa makundi yote ya kisiasa na haswa hao vijana wenzetu. Vijana tunaoamini wanahitajika kubadili hali iliyopo sasa. Ni wazi kuwa ili mabadiliko tunayoyatarajia yawe mabadiliko ya heri na fanaka kwetu na sio BORA MABADILIKO ambayo yatatupeleka kwenye majanga mapya na makubwa zaidi, tunahitaji kutambuana na kuwasaidia wenzetu kujitambua kabla kuingia kinyang'anyironi hapo mbeleni.

Ni muhimu na ni wajibu wetu kujichambua na kuwachambua wagombea watarajiwa kuanzia sasa.

Kwa yeyote anayejua kuwa fulani na fulani, ama rafiki, ndugu, mfanyakazi mwenzie ama mtu mwengine ana nia ya kugombea nafasi ama UDIWANI ama UBUNGE ama UWAKILISHI nashauri amtaje hapa ili tuchambuane....wapo watakaotukana, kudhihaki na hata kugombana....lakini mwisho wa siku tutakuwa tumelisaida taifa letu kuepuka anguko kuu linalotunyatia.......

Tusiendelee kurudia makosa....kama kizazi cha sasa tuna wajibu kwa taifa letu.....

Tanzanianjema
 
Ningekuwa ndo mimi JMK ningeachia madaraka ya nchi 2010.

Sababu kuu ni hizi;

Mambo mengi ya ufisadi yametokea katika kipindi kifupi tu cha utawala wake, Richmond, Buzwagi, Tume ya mawasiliano nk.

Kushindwa kuushughulikia ufisadi wa EPA

Kushindwa kuushughulikia ufisadi wa Richmond na Buzwagi

Kusainiwa mikataba tata ya Richmond na Buzwagi

Hali ya maisha ya wananchi imeendelea kuwa duni na mbovu kuliko wakati wote.

Ikulu kupoteza kauli na kila mtu kuwa na kauli zake ambazo hufuatwa na watendaji.

Kuwa na maswahiba wenye nguvu zaidi kiasi kwamba kauli zao ndio kauli za Ikulu

Kuporomoka kwa uchumi wa nchi

Dalili za kukosa uvumilivu kati ya makundi mbalimbali katika Jamii

Mpasuko mkubwa ndani ya chama kufuatia mtandao ulioanzishwa na maswahiba wake walomweka Ikulu

Hatari ya kuvunjika kwa Muungano uliodumu kwa zaidi ya miaka 44 sasa kufuatia rais kokosa ushawishi na ahadi ya kuupatia ufumbuzi wa mgogoro wa ZNZ ambayo haijatimizwa.

Yote kabisa ni hili la nchi kukosa Dira, Kiuchumi na kisiasa. Bora liende.

Ningekuwa JMK, mzalendo, ninayeipenda nchi yangu, nikiwa na akili timamu, bila kushawishiwa na mtu yeyote, ningekiomba chama changu cha SISI EM kisiniteue kwenye nafasi nyeti kama hiyo kwa maslahi ya kizazi kijacho na pia kulinda heshima yangu na kuwatosa Mafisadi ambao wengi ni maswahiba wangu

Je ingekuwa wewe ndo JMK ungechukua uamuzi gani 2010?
 
Ningekuwa ndo mimi JMK ningeachia madaraka ya nchi 2010.

Sababu kuu ni hizi;

Mambo mengi ya ufisadi yametokea katika kipindi kifupi tu cha utawala wake, Richmond, Buzwagi, Tume ya mawasiliano nk.

Kushindwa kuushughulikia ufisadi wa EPA

Kushindwa kuushughulikia ufisadi wa Richmond na Buzwagi

Kusainiwa mikataba tata ya Richmond na Buzwagi

Hali ya maisha ya wananchi imeendelea kuwa duni na mbovu kuliko wakati wote.

Ikulu kupoteza kauli na kila mtu kuwa na kauli zake ambazo hufuatwa na watendaji.

Kuwa na maswahiba wenye nguvu zaidi kiasi kwamba kauli zao ndio kauli za Ikulu

Kuporomoka kwa uchumi wa nchi

Dalili za kukosa uvumilivu kati ya makundi mbalimbali katika Jamii

Mpasuko mkubwa ndani ya chama kufuatia mtandao ulioanzishwa na maswahiba wake walomweka Ikulu

Hatari ya kuvunjika kwa Muungano uliodumu kwa zaidi ya miaka 44 sasa kufuatia rais kokosa ushawishi na ahadi ya kuupatia ufumbuzi wa mgogoro wa ZNZ ambayo haijatimizwa.

Yote kabisa ni hili la nchi kukosa Dira, Kiuchumi na kisiasa. Bora liende.

Ningekuwa JMK, mzalendo, ninayeipenda nchi yangu, nikiwa na akili timamu, bila kushawishiwa na mtu yeyote, ningekiomba chama changu cha SISI EM kisiniteue kwenye nafasi nyeti kama hiyo kwa maslahi ya kizazi kijacho na pia kulinda heshima yangu na kuwatosa Mafisadi ambao wengi ni maswahiba wangu

Je ingekuwa wewe ndo JMK ungechukua uamuzi gani 2010?

Swali lako ni ni trivial kwa vile kama wewe ndiye ungekuwa Kikwete, basi ungekuwa na akili ya Kikwete na hivyo usingeyaona yote hayo. Labda ungeuliza kama wewe ndiwe ungekuwa katika position aliyonayo Kikwete lakini ukiwa na akili zako timamu, siyo za kwake.
 
Ukiwa na akili timamu na una mapenzi ya kweli na nchi yako, wala hutangoja 2010 utaachia ngazi sasa ili kuinusuru nchi katika maangamizi ya kuogopa kuwashughulikia mafisadi na kumpisha mwenye ujasiri wa kupambana na mafisadi bil kujali ni matajiri wakubwa kiasi gani au wana nyadhifa zipi.
 
Wengi wetu tuna TOFAUTI gani na JMK kama tutapewa nafasi aliyopo sasa? Au ni yale ya kwenye viwanja vya michezo ambako "WACHEZAJI WAZURI" ni wale wanaoutazama mchezo wenyewe?
 
Wengi wetu tuna TOFAUTI gani na JMK kama tutapewa nafasi aliyopo sasa? Au ni yale ya kwenye viwanja vya michezo ambako "WACHEZAJI WAZURI" ni wale wanaoutazama mchezo wenyewe?
...Acha utani kwamba ukiingia uwanjani goli hulioni??? Watu tuna machungu nchi inafilisiwa kila kona kweli usilione goli??
 
Acheni kumdhihaki JMK.Amekwishafanya mengi tangu aingie madarakani isipokuwa wanaombeza hawaoni.

Mkapa alipoingia tu akaunda tume ya Warioba, kaanza kuuza NBC,NMB n.k hakuna aliyethubutu kumsema wakati huo kwa sababu alikuwa mbogo.
Leo mna uhuru wa kutosha wa kubwatabwata na kila kukicha mnamsema na kumdharau.Rais gani katika wale waliomtangulia aliyepambanana ufisadi? Mbona wote kuanzia Mchonga mpaka huyu wako level moja tu?

Unadhani kuna mtu ataingia kichwakichwa na kuanza kamatakamata ,ua weka ndani bila mpangilio ati napambana na mafisadi..
Tatizo si JMK wala Rais ye yote atakayekuwa madarakani.Tatizoni utawala mkongwe wa CCM ambao umekusanya kila aina ya watu.

Kama Watanzania wanataka kubadili si kubadili Rais bali ni kubadili mfumo mzima wa utawala na hili ndiyo tatizo.Wako wapi Watanzania wanaoweza kuindoa madarakani CCM ili tupate Rais atakayekuwa na mfumo tofauti wa kiutawala?Hii ndiyo problem na wala si JMK.

Na nikiangalia kwa undani bado naona hakuna chama kinachoweza kuwaweka Watanzania na kuwaondolea kasumba ya miaka nenda rudi.Kasumba ambayo ilisimikwa na Mchonga,ambaye baada ya kuboronga vibaya kwenye utawala wake lakini anaonekana na vijana wa leo kama mkombozi na malaika, amliambukiza taifa maradhi ya woga,unafiki na ubinafsi ambao hadi hii leo ni vigumu kutoka ndani ya mioyo ya Watanzania.

kwa hiyo hakuna haja ya kuuliza kama ningekuwa JMK ningeamua nini.Niamue nini na mimi nina CCM na nina Watanzania!
 
Mwalimu na Kikwete ni level moja!!!!!? 😕
Sidhani kama unamjua Mwalimu na mengi aliyoifanyia Tanzania na Afrika kwa ujumla. Kikwete hana hata 1/1000 level ya Mwalimu!! Kama binadamu, Mwalimu hakuwa perfect na yeye mwenyewe mara nyingi alisema hivyo, lakini kafanya mengi mno.

Hayo mengi aliyoyafanya Kikwete ni yepi? Yaweke hapa ili tuyajadili kwa urefu na mapana. Kikwete mwenyewe hata siku moja hawezi kujiweka level moja na Nyerere, kamwe hatafanya hivyo hata level ya kichuguu haifikii.
 
Jamani mbona tunajaribu kufananisha vitu ambavyo havilandani, JMK na Mwalimu! Wapi na wapi jamani,m.

Wakati Mchonga aliwaita na kukemea na hata kulambwa bakora (kama hamna taarifa Waziri mmoja liwahi kuchapwa na Mchonga enzi hizo) Jamaa yetu yeye kimya tu! Na bado wanatamba tu bila kufanyiwa chochote.

Mimi wala nisingejisumbua 2010 kamwe!
 
Back
Top Bottom