jmushi1
Platinum Member
- Nov 2, 2007
- 26,381
- 25,476
TLP chasambaratika mkoani Kilimanjaro
Na Victor Kwayu, PST Moshi
Zaidi ya viongozi na wanachama 100 wa Tanzania Labour Party (TLP) mkoani Kilimanjaro wakiongozwa na Mwenyekiti wao mkoani hapa, Rose Masuruali wamekihama chama hicho na kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Akizungumza na viongozi wa kata mbalimbali za Kirua Vunjo, Masuruali alisema amefikia uamuzi wa kuihama TLP baada ya kubaini mapungufu kadhaa ya uongozi ndani yake.
Alisema TLP pamoja na viongozi wake wa ngazi za juu akiwemo Mwenyekiti wake, Augustine Mrema, wamekosa mwelekeo ikiwa ni pamoja na kutokuwa na sera mbadala za kumkomboa Mtanzania.
`` hama chetu (TLP) kimekosa mwelekeo, viongozi wa ngazi za juu wamekosa dira na ndio maana hatuna hata mbunge wala diwani, chama kimefilisika kisiasa na badala yake yamebakia majungu yanayosababisha kukigawa, sasa tumeamka,`` alisema Mwenyekiti huyo ambaye kabla ya kuukwa Uenyekiti wa mkoa alikuwa Mwenyekiti wa Wanawake Kata ya Kirua Vunjo.
Wanachama na viongozi wa kata waliokihama chama hicho na kujiunga na Chadema ni waliotoka katika vijiji vya Nganjoni, Mrumeni, Kireuwo pamoja na kijiji cha Mero ambao kwa pamoja walipitisha azimio la kukihama cha hicho.
Naye Mwenyekiti wa TLP Kata ya Kirua Vunjo, Joseph Assey alisema kutokana na Mwenyekiti wa chama hicho, Augustine Mrema kuonekana kukosa sera mbadala, wameamua kukihama chama hicho na kujiungana na Chadema katika kupambana na vita vya mafisadi sanjari na zoezi la kuwasakama mafisadi la Operesheni Sangara linaondelea Kanda ya Ziwa.
Alisema kimsingi Chadema imeonyesha nia ya dhati ya kupambana na viongozi wasio waadilifu na kwa msingi huo wameona chama pekee kinachoweza kuing`oa CCM madarakani ni Chadema pekee.
``Operesheni Sangara imeitikisa nchi, viongozi na mafisadi ndani ya serikali matumbo joto...kuingia kwetu Chadema kutasaidia kuonyesha nia ya dhati ya kuendelea na mapambano dhidi ya mafisadi na viongozi wasio makini, lengo ni kumkomboa mwananchi na lindi la umasikini,`` alisema Assey.
Naye Katibu Mwenezi wa Chadema Manispaa ya Moshi, Augustine Makelele alisema kundi la wanachama hao pamoja na viongozi wa TLP kuamua kujiunga na chama hicho, limedhihirisha ni namna gani chama hicho kinavyokubalika hivi sasa.
Alisema kwa msingi huo, chama hicho kimeazimia kuhakikisha kinahamishia zoezi la Operesheni Sangara katika Mkoa wa Kilimanjaro ikiwa ni pamoja na kuhamasisha wananchi kuhakikisha wanajiunga na chama hicho ambacho alikiita kama chama chenye mwelekeo wa kumtetea mnyonge dhidi ya vita ya umasikini wa kipato.
Alisema kutokana na TLP kuonyesha udhaifu kiutendaji ikiwa ni pamoja na kukosa sera ya kweli, wanachama kadhaa wa vyama kadhaa vya siasa mkoani Kilimanjaro wamekuwa wakituma maombi kadhaa ya kujiunga na chama hicho.
``Tumekuwa tukipokea maombi mengi kutoka kwa wanachama wa vyama vya siasa kikiwemo chama tawala cha CCM...kutaka kujiunga na chama chetu, sera na mwelekeo wa Chadema umekuwa ukikubalika na kuwa na mvuto mkubwa, hivyo tunawakaribisha kwa mikono miwili,`` alisema Makelele.
Aidha, alisema viongozi na wanachama hao waliojiunga na chama hicho wakitokea TLP, watakabidhiwa kadi rasmi na Mwenyekiti wa chama hicho kitaifa, Freemani Mbowe hivi karibuni mjini hapa.
SOURCE: Nipashe
Kule Iringa ilikuwa ni CUF na sasa Kilimanjaro ni TLP...Kaazi kweli kweli.
Masuruali anasema hivi Makelele naye anasema vile...Wakati wa furaha hiyo ya kukabidhiwa kwa kadi ikiendelea...Makelele yeye anadai kuna maombi ya CCM kutaka kujiunga na CHADEMA....Ila hajataja vichwa zaidi ya furaha ya wanachama hao wapya wa kutoka TLP huko Vunjo.
Mbona sisikii kabisa kuhusu hao wa CCM?
Ama wananchi wote ni upinzani tu?
Hiyo Sangara si ianzie huko CCM? Ama macho yangu?
Hao kina Assey nao wanakuja wanadai Mrema hana sera mbadala...Ni TLP hakina sera mbadala ama ni individual this time mwenyekiti? Sababu walizozitaja za kuhama hazina nguvu...Lakini dhambi ile ile ya CCM isijekuwa ndiyo dhambi inayowatafuna wapinzani.
Ama na wao wanajiposition tu...Cha muhimu muungane.