Chenge, Chenge, Chenge,......
Mkuu
Naona ukupata cha kuandika lakini ukisikia mtu anasema vijisenti hujue ana maana yake.
Lakini anakingiwa kifua. Ajue atatembe a na miguu kwa kuw3adhalilisha watanzania.
Wafadhili wa nchi wote wameisha pata hizi message je kesho tutapata msaada wowote?
Mkuu, Wafadhili wameshastuka na sasa hivi wamekuwa wasomaji wazuri sana wa magazeti ya Tanzania hasa THIS DAY ili kufuatilia habari za ufisadi. Kama sikosei Mkullo au Meghji walishazungumza kwamba ikifika mwezi wa kwanza au wa pili nchi wafadhili huwa zimeshasema zitachangia kiasi gani ili kuziba pengo la 60% (hivi ni 60% au 40% inayotolewa na wafadhili?) katika bajeti yetu. Sasa kama watakula ngumu na kutotoa chochote basi kutakuwa na kazi nzito ya kupanga bajeti. Kodi zitaongezwa kila kona ili kufidia pengo hilo. Hapo ndio tutaona maisha bora kwa kila Mtanzania kama alivyoahidi jamaa wakati wa kampeni zake.
Huu mkakati wa kumzuia nadhani haujaandaliwa vizuri. Watakaa mlangoni kwa siku ngapi? Je Jumatatu Chenge akikacha kikao cha bunge halafu akitokea jumanne, jumatano...ijumaa?
Chenge, Chenge, Chenge,......
Chenge, Chenge, Chenge,......
hongereni ndugu zetu wa Dodoma, sisi sote tuko pamoja nanyi...huu ni mwanzo wa mwisho wa MAFISADI wote