The Radar Scandal: Investigation & Progress

Chenge, Chenge, Chenge,......

programming.gif


Mwanamalundi u mwanafunzi wa PhD? Pole na matatizo
 
Hi akijiuzulu itakuwa ni mpaka kwenye U-CC na U-NEC wa CCM hatimaye ubunge? au ni uwaziri tu kwanza kabla ya kuishia keko na kupoteza hizo nyadhifa nyingine?
 
Ooh Load... Wish I cud be a sniper... Nimeishi katika jamii ya kitanzania iso kuwa na uwezo wa kupata mlo mmoja tu kwa siku...siku si nyingi ... just the matter of TIME n SPACE!
 
Mkuu

Naona ukupata cha kuandika lakini ukisikia mtu anasema vijisenti hujue ana maana yake.

Lakini anakingiwa kifua. Ajue atatembe a na miguu kwa kuw3adhalilisha watanzania.

Wafadhili wa nchi wote wameisha pata hizi message je kesho tutapata msaada wowote?

Mkuu, Wafadhili wameshastuka na sasa hivi wamekuwa wasomaji wazuri sana wa magazeti ya Tanzania hasa THIS DAY ili kufuatilia habari za ufisadi. Kama sikosei Mkullo au Meghji walishazungumza kwamba ikifika mwezi wa kwanza au wa pili nchi wafadhili huwa zimeshasema zitachangia kiasi gani ili kuziba pengo la 60% (hivi ni 60% au 40% inayotolewa na wafadhili?) katika bajeti yetu. Sasa kama watakula ngumu na kutotoa chochote basi kutakuwa na kazi nzito ya kupanga bajeti. Kodi zitaongezwa kila kona ili kufidia pengo hilo. Hapo ndio tutaona maisha bora kwa kila Mtanzania kama alivyoahidi jamaa wakati wa kampeni zake.
 
Mkuu, Wafadhili wameshastuka na sasa hivi wamekuwa wasomaji wazuri sana wa magazeti ya Tanzania hasa THIS DAY ili kufuatilia habari za ufisadi. Kama sikosei Mkullo au Meghji walishazungumza kwamba ikifika mwezi wa kwanza au wa pili nchi wafadhili huwa zimeshasema zitachangia kiasi gani ili kuziba pengo la 60% (hivi ni 60% au 40% inayotolewa na wafadhili?) katika bajeti yetu. Sasa kama watakula ngumu na kutotoa chochote basi kutakuwa na kazi nzito ya kupanga bajeti. Kodi zitaongezwa kila kona ili kufidia pengo hilo. Hapo ndio tutaona maisha bora kwa kila Mtanzania kama alivyoahidi jamaa wakati wa kampeni zake.

Huu naona kama mwanzo wa kuanguka kwa ROMAN EMPiRE. ukisikia kufuru hata siamini macho yangu.
 
Wezi wa kuku huwa wanapigwa hadi kufa kabla polisi hawajafika kuchukua maiti, kwa nini wezi wa uhujumu wa uchumi kama hawa hawashughulikiwi namna ile ile? Will it be first for Tanzania?
 
Huu mkakati wa kumzuia nadhani haujaandaliwa vizuri. Watakaa mlangoni kwa siku ngapi? Je Jumatatu Chenge akikacha kikao cha bunge halafu akitokea jumanne, jumatano...ijumaa?


Maandamano ni demostration kwa dunia nzima kuwa mnalaani kitendo hicho sasa ni juu ya serikali kukaa na aibu hizo hata yakiwa siku moja inatosha sana.
 
Kwa wale ambao hamkusoma vizuri, please soma tena hii hizi points muhimu, wana-JF tusilaze damu jamani tunahitaji kwauajua hao waliotajwa kupewa mgawo ni kina nani? Waandishi waliomegewa ni kina nani? Halafu tizama wakurugenzi wa hiyo kampuni waliokuwa na idhini ya kuidhinisha malipo ya kampuni, wazee kazi ndio kwanza imeanza mpaka kileweke hapo:-

In the meantime, ni vyema Waziri Chenge, akajiuzulu badala ya kuendelea kumpa mzigo mzito rais wa jamhuri wa kujibu maswali yake kila kona, ili pia atupe nafasi taifa turudi kwenye kujadili mambo muhimu kwa taifa letu!


1. WAZIRI wa Miundombinu, Andrew Chenge anaogelea katika utajiri wa zaidi ya Sh. 25 bilioni zenye utata huku Rais Jakaya Kikwete akiendelea kumkumbatia,

2. Chenge amekuwa mfanyakazi serikalini kwa karibu miaka 30 na hafahamiki kuwa mfanyabiashara. Kiwango kinachotajwa ni pamoja na fedha zilizogunduliwa na makachero wa Uingereza katika akaunti zake za nchi za nje.

3. Fedha zilizoko kwenye akaunti yake ya nchini, Na. 011101006950 katika benki ya NBC Limited, ni Sh. 25,794,805.89 za Tanzania hadi Ijumaa iliyopita, tarehe 11 Aprili 2008.

4. Katika akaunti yake ya Uswisi, ambako ana akaunti ya fedha za kigeni, Chenge amehamishia dola za Marekani 467,000, sawa na zaidi ya nusu bilioni kwa fedha za Tanzania.

5. Chenge ni Mkurugenzi wa kampuni ya TANGOLD Limited ambayo ina dola 12,997,950.84 sawa na Sh. 15 bilioni za Tanzania katika NBC Limited tawi la Makao Makuu.

6. makachero wa Uingereza wanafuatilia uhalali wa Euro 3 milioni (sawa na zaidi ya Sh. 8 bilioni za Tanzania) Chenge alizipeleka kwenye akaunti zake nje ya nchi.

7. Chenge alihamisha kwa mkupuo dola 600,000 za Marekani kwenda kwenye akaunti ya ofisa mwandamizi mmoja aliyekuwa Benki Kuu miaka kadhaa iliyopita, na ambaye kwa sasa anaongoza shirika la umma nchini.

8. Wakurugenzi na waidhinishaji malipo wengine wa kampuni hiyo ni, Daudi Ballali, Gray Mgonja, Vincent Mrisho na Patrick Rutabanzibwa.

9. Kutoka kwenye akaunti ya binafsi ya Chenge, mamilioni ya shilingi yamelipwa kwa watu mbalimbali wakiwa ni pamoja na Janet Mashale, Mary Nchimbi, Mary Chitanda na Livingstone Ruhere. Wengine ni Getrude Mtiga, Hawa Kiama, Leocardia Kalumuna, Athumani Sheha na David Sanga.

10. Miongoni mwa waliolipwa ni viongozi wa CCM, waandishi wa habari na wengine. Muhimu ni kwamba karibu fedha hizo zote zililipwa wakati uchaguzi wa CCM mwaka jana ambapo Chenge aliwania ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC). Alishinda kwa kura nyingi.
 
viongozi wa Tanzania wanakatisha tamaa kwa kweli. Huyu ndiye chanzo hali ngumu ya maisha kwa watanzania pia ni chanzo cha vifo vya wananchi wengi kwa kukosa matibabu, ni sababu ya vifo vya akina mama na watoto, ni sababu ya tatizo la usafiri, ni sababu ya vifo vya ajali kutokana na ubovu wa bara bara zetu pamoja na uzembe wa madereva pale wanapoendesha magari huku wakiwaza ugumu wa maisha unaowakabili, ni sababu ya mambo yote mabaya yanayoikumba nchi yetu........

Sasa kama hali ndiyo hii, ana umuhimu gani basi wa kuwa mtu Hai? Watanzania tunahaja gani kujivunia amani tunayotangaziwa wakati nafsi zetu hazina amani?

Najuta kuzaliwa Mtanzania ila Ni lazima huu upumbavu uishe hata kwa damu kumwagika.

Chenge and all Fisadi's must not only return our money but they must also GO TO HELL!
 
Wanabodi CD za bongo fleva naweza kuzipata wapi ....Kwani nishaona kuendelea kufuatilia haya mambo ni kutafuta ukichaa. Nchi imeoza kuanzia juu mpaka chini .... Hivi vitu haviingii akilini . Chenge ana kila haki ya kuita dola millioni moja " vijisenti"
 
Tupo pamoja wenzetu wa dodoma, hii kitu ikifanikiwa then it will be a message kwa waliobaki 10. lets wait
 
Back
Top Bottom