The Radar Scandal: Investigation & Progress


Unaturusha roho mkuu! umri umekwena haya mambo yanahitaji kukaa juu ya stuli ndefu ndo uyapokee! This stuff is too old tupeni current issues naona tume msahau kabisa vijisenti
 
Kuna umuhimu wa kuwa na word censor ambayo itatambua mtu anaweka kitu gani kama kipo inamwambia moja kwa moja kabla ya kupost inakuwa na dk 1 kukagua
 
Du!!!! Hhahaaaaaaaa Piem pole sana Naona Confo limerudi mpaka Minus unajiona mdogooo ila ndiyo kukua next time utakuwa makini kabla ya kupost zedataz. JF usikurupuke na ze datas, soma kwanza zilizopo na kujiridhisha kuwa hazipo ndiyo umwage unazodhani ni mpya. Na hiyo haitoshi uwe tayari kuzidefend yaani umezipata wapi?. Ila hongera umewapata Sober na Edo.
 
Aliipata katika mailing list inaonyesha

Na hizo 'Dataz' za toka May mwaka huu hazijazaa chochote miezi saba baadaye na Mzee wa vijisenti bado anapeta tu uraiani!!! 'Dataz' nyingine si za kuaminika kabisa.
 
Chenge yumo njiani kwenda kwenye sheria kama kina Mgonja, na order ya kuwataka wote waliohusika kuondolewa CCM ipo mezani kwa mwenyekiti wa CCM, mara ya mwisho ilipigiwa kelele na Msuya kwenye NEC, kwamba waondolewe,

Chenge alisachiwa na kukutwa na billioni moja ndani ya nyumba, otherwise Lowassa na Karamagi nao pia walipelekwa London kwenye huu uchunguzi,

Kwa hiyo hizi dataz ziko current, ila naona kuna anyejaribu kunichafua, asiwe na wasi wasi maana na mimi nikiamua kumchafua hapa asilie. Maana this is a cheap shot naomba atafute real ishus kama antaka vita na mimi za kihoja.

mkuu bubu among all the people hapa nilifikiri tunaheshimiana sana lakini karibu sana mkuu!
 
ila naona kuna anyejaribu kunichafua, asiwe na wasi wasi maana na mimi nikiamua kumchafua hapa asilie
Ha ha ha ha mkuu kwa mkwala tu siku wezi!
Lakini huu mjadala umepoa uliuleta wewe toka mwezi May ndo hivyo tena tunasubili sheria ifuate mkondo wake au sio mkuu?Ngoja twendelee kusubili...lakini anaye taka kukuchafua lazima atakuwa anakujua weakness na strongest point zako.
 

Mkuu FM ES, waambie haraka haraka haina baraka. Subira yavuta heri. Na pia utafiti yakinifu unachukua muda. Everything will be exposed soon. Hakuna haja ya kukurupuka kuleata taarifa nusunusu. Ngojeni FM ES afanye utafiti wake. Namuamini sana mimi, asilimia kubwa ya taarifa zake ni sahihi (confidence interval 95%).
 
Niliiona mapema nikaonelea ni vyema niziunganishe ili mwenyewe ajue hii kitu imeongeleka hapa siku nyingi tu

Invisible,

Hivi JF ina sheria za copyright? Huyu Piemu Esquire inatakiwa amlipe FMES kwa kutumia makala yake bila hata kubadili neno.
 
Invisible,

Hivi JF ina sheria za copyright? Huyu Piemu Esquire inatakiwa amlipe FMES kwa kutumia makala yake bila hata kubadili neno.

LOL! amlipe kiasi gani!? na kwa Currency ipi T shiling, U$ or Streling Pound? Just thinking aloud 🙂
 
Duh sasa Tina unatutisha sasa unataka umpe raha gani FISADI huyo??unataka mle wote za RICHMOND?mmh wabongo bwana unakimelea cha ufisadi nini??mfatilie anaweza kukukonyeza.
Tina usibabaishwe mbona Yanga wanakula hela za manji .Endelea mwana pengine atakuonyesha mali zake nyingine utuarifuJF
 

Bado nakuheshimu lakini hii habari siyo tena current na Kikwete asingekubali kumuweka Mzee wa Vijisenti katika kamati ya kuchunguza mkataba wa jengo la UVCCM. Hivyo 'dataz' hizi inawezekana kabisa hazijakaa sawa sawa maana ni miezi saba sasa na njemba bado inapeta tu uraiani. Labda vile alivyonyunyiza pale bungeni Dodoma vimewaziba macho hata wazungu waliokuwa wanachunguza kashfa ya vijisenti 😉. Tusubiri labda tutapata update karibuni. Kwa kumalizia watu wanapohoji 'dataz' siyo kwamba wanataka kukuchafua au hawakuheshimu kumbuka hapa ni JF where we dare to talk openly...Have a great day 🙂
 
 

Mhuum hii kali du kazi kweli kweli kwa mkwala tu!Wrong is Wrong no matter who says it!
 
FMES, waswahili ndio tulivyo!!!!!!!!!!!!!!

Wakikuwa wataelewa!!!!
 

Mkuu, huna haja ya kuchukia. Si lazima kila mtu akakubaliana na hoja zako kama vile wewe pia si lazima ukubaliane na hoja za kila mtu.
Huyu jamaa anayekutia hasira asikunyime raha mpaka ukaacha kutupa dataz muhimu hapa JF. Mchango wako ni muhimu sana hapa JF kwani ni mara nyingi umekuwa ukimwaga nondo za kweli, na unatoa hoja za uhakika pia huna mabishano ya kijinga.

Elimisha umma kwani wengi wetu watanzania hatujui kwamba hatujui, na hatukubali kwamba hatujui.
 
Kelele za mlango huwa hazisumbui mtu kulala ndani ya nyumba, wakuu niko busy maana nina ugeni mkubwa sana wa viongozi wa taifa, kwa hiyo samahani wakuu sina muda wa kujadili pua, maana niko busy ninakula darasa la siasa ya taifa letu. Andikeni points muhimu kusudi niwaonyeshe hawa wakuu wa taifa, maana siwezi kuwaonyesha hizi pumba!

See you later and have a nice day!

FMES!
 
Ha ha ha Wakuu hao wa Taifa kama kweli huwa wanakusikia unachowaambia ni bora uwaambie kazi imewashinda wajiuzulu kazi ili tufanye uchaguzi mwingine hatuna haja ya kusubiri 2010. Tunataka viongozi wenye kujali na kuweka mbele maslahi ya Taifa siyo hawa walioweka mbele maslahi yao, usanii na vitisho kila kukicha.
 

- Wajiuzulu kwa sababu wewe uliyewachagua huwataki? Mkuu sikujua kua una nguvu kiasi hiki hongera sana bro!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…