The Radar Scandal: Investigation & Progress

The Radar Scandal: Investigation & Progress

Jamani kama chege huyu huyu ndiye aliyeshiriki kwenye mikataba mibovu tangu enzi za BM, sasa ianluwaje tena ndugu zangu wanasisiem wenzangu ateuliwe kuwa kwenye kamati ya kuchunguza udhalihu wa EL, kama ndio hivyo kwanini mkuu wao RA hakuteuliwa, hawaoni kwa kufanya huvyo ni kumbagua? Nape usife vijana wote upinzani na ccm tupo pamoja nawe.

Makamba `mzee wa kupopoka` kuwa mwangalifu sana na mdomo wako jasije kukuta kama yale ya jamaa wa mchinga.
cha kushangaza CHENGE bado ni mwenyekiti wa kamati ya maadili ya CCM. inatisha
 
Si wamejipanga kama timu ya mpira au unafikiri watajipanga vipi. Ndege wanaofanana huruka pamoja au sio. Sasa tusingetegemea kuwa wamejipanga shaghala baghala etiii!
 
Duhh! Hii ndiyo wanasema "heaping insult upon injury". Yaani jambakazi Chenge nalo limepewa tume yake mwenyewe? Ama kweli sasa nimeelewa maana ya "kusafisha", "kumsafisha", "kusafishwa" nk yaliyokuwa yakisemwa kuhusu Lowassa.
 
Yaani Mkataba wa Kifisadi anapewa Fisadi auchunguze duh kweli nimechoka na hawa CCM. Chenge ni Fisadi mwenye kutumia elimu yake kutoka Harvard kuendeleza UFISADI, Chama Cha MAFISADI (CCM) kinazidi kujionyesha kwa jamii kwamba sera na itikadi yao ni Chukua Chako Mapema na chama kitakulinda kwa gharama zote.
 
Kuna mtu aliwahi kusema: CCM ina wenyewe. Ndio hao sasa akina Chenge. Pamoja na kutapakaa kinyesi cha ufisadi mwili mzima, bado anaonekana kwa baadhi ya watu kuwa ananukia marashi.
 
Tume ya Mwisho Tutaiunda sisi.

Itakuwa ni Tume ya kuwanywesha ghadhabu ya maovu yao kwa kipimo kilicho mara mbili ya kile watupimiacho.

Mafisadi wote wanadhani watabaki madarakani, kisha wakizeeka waendelee kulishwa kwa jasho letu.

Mafisadi na hayawani wote wa kisiasa Jiandaeni tunakuja Ground Level muda si mwingi.
Si Dodoma si Dar patakuwa hapatoshi.

Kimbembe tutakachozua,
ughaibuni itakuwa karibu kuliko vijijini kwenu kwa wajomba na shangazi zenu wanukao umasikini kama sisi na kutembea makalio nusu wazi.

Jiandaeni kuja kuzeekea huku ughaibuni asikopendwa mtu wala pochi ila misuli yake na tija yake tu.

Kwani kamwe hatutakaa tunyamaze,tubweteke tuwaachie nchi, ni mpaka wa mwisho katika uzao wenu atakapobuishwa tamu ya chungu.

Kumbukeni kila siku" MTAJI WETU MKUU NI UDHAIFU WENU"

RUSHWA- Mkipewa Rushwa hamuinui vichwa vyenu juu kutazama ni nani awapae Rushwa.

KUTAMANI FEDHA KULIKO NAFSI ZENU- Mbele ya Fedha mko radhi kupanga bei na kuuza Nafsi zenu na nafsi za Wake na watoto wenu, zaidi za Mama na baba zenu kwa yeyote mwenye mshiko.

TAMAA ZA MWILI- Mnakesha hamlali mpaka mkidhi tamaa chafu za miili yenu.

Ole wenu!!
 
japo unauma lakini huu ndio ukweli wenyewe

"uongozi ccm haujali mwanachama wake wa kawaida, mwananchi
wala jf wanasema nini, la muhimu ni maslahi yao tu" hali hii itakujabadilika
pale ambapo ccm itapata mtikisiko kupitia sanduku la kura kwa
kupoteza viti vingi hata kama watabaki madarakani.

inabidi kila mwana jf aweke nadhiri kwamba 2010 atapiga kura,
kama upo nje ya nchi anza kujiandaa sasa kwa ajili ya upigaji
wa kura na kama upo nchini usikate tamaa balili hakikisha
unapiga kura.
 
Last edited:
Ha ha ha ha ha!tume tumechoka.........
Tukisema hawa CCM ni wajinga mnasema tunawatukana haya sasa mnaaona kwenye hiyo tume tumechoka wanao unda tume duhhhh! kweli Wadanganyika tunawakumbatia viongozi wababaishaji walio vamia fani ya uongozi wakati hawauwezi.....
 
jamani mm naona hafai hata kidogo ila ndio kulindana huku. hwa jamaa bwana waache tu wanajuana kwa vilemba.
 
Nilikuwa namuheshimu JK sana na baada ya kuchaguliwa kuwa rais...nilikuwa na mategemeo makubwa hasa kwa maisha ya waTanzania kuinuliwa....kufuatana na hotuba na sera alizopigia kampeni yake....na pia ahadi km ya "nafasi za kazi milioni moja"......lakini sasa hivi namuona kama ni mlinda mafisadi na kutwa anajichekesha chekesha tu ....hasa akipigwa picha, na kama kukiwa na akina mama karibu basi anawaangalia na "eyes of desire".......
 
Mi nawashangaa nyie mnaoshangaa Mzee wa 'coins' kuwa kwenye kamati hii, hi system ilikua inatumika Soviet Union zamani mtu akiharibu anawekwa pembeni kwa muda alafu anaibuliwa sehemu ingine ili asiwe mpinzani na watu wakipigia kelele jambo inaundwa tume wakishasahau ndio IMESHATOKA HIYO! Na walijua watu wana 'attention span' fupi na lazima litatokea lingine lakuwasahaulisha hili la sasa.
 
Hatima ya Chenge wiki hii

*Serikali ya Jersey yajiandaa kutoa tamko
*Ni linalohusu kashfa ya rada,'vijisenti'

Na Mwandishi Wetu

WAKATI wiki hii limeingia kumi la mwisho kabla ya kujulikana hatma ya watuhumiwa wa wizi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) iliyokuwa Benki Kuu, tarifa ya uchunguzi wa kashfa nyingine nzito inayomkabili aliyekuwa Waziri wa Miundombinu, Bw. Andrew Chenge, inatarajiwa kuanikwa muda wowote kuanzia sasa.

Bw. Chenge amekuwa akichunguzwa na makachero wa Kitengo cha Kupambana na Makosa ya Ufisadi nchini Uingereza (SFO) kwa miezi kadhaa sasa, kuona iwapo alinufaika kwa namna yoyote na kamisheni iliyotolewa isivyo halali na kampuni ya uuzaji vifaa vya kijeshi na anga ya BAE Systems ya Uingereza iliyoiuzia rada Tanzania.

Mfanyabiashara wa kitanzania, Bw. Shaileshi Vithlani alikiri kupokea sh. bilioni 12 kama ada ya uwakala na pia 'hongo' kwa ajili ya vigogo kadhaa wa Tanzania alipobanwa na makachero wa SFO.

Uchunguzi zaidi wa SFO kuhusu maofisa wa Tanzania wanaoweza kuwa walinufaika na sehemu ya kamisheni hiyo, ulianza huku vigogo kadhaa wa Serikali akiwamo Bw. Chenge waliohusika kwa namna moja au nyingine katika mchakato wa ununuzi wa rada, wakichunguzwa. Wakati mkataba wa ununuzi huo ukisainiwa Bw. Chenge alikuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Taarifa za uchunguzi zinaonesha kuwa maofisa hao wa Tanzania walihojiwa na kupekuliwa nyumba na mali zao jijini Dar es Salaam na baadaye kuitwa Uingereza ambako walibanwa zaidi katika mahojiano na makachero.

Kachero Helen Garlick, ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi (Upelelezi) katika SFO, Majira imebaini kuwa alifika Dar es Salaam, akiwa na timu ya makachero wengine kuendesha sehemu ya uchunguzi huo.

Tangu SFO ilipoanza 'kumchimba' Bw. Chenge na kubaini kumiliki akaunti kwenye visiwa hivyo, Serikali ya visiwa vya Jersey ambako ndiko Chenge ilikobainika kuweka takribani pauni 500,000 (zaidi ya sh. bilioni moja), nayo ilianza uchunguzi wake mbali na ule wa SFO.

Katika mawasiliano yake na Majira kwa njia ya baruapepe juzi, Msemaji wa Waziri Mkuu wa Jersey, Bibi Cathy Keir alithibitisha kuwa kwa kipindi chote hicho, maofisa wa Serikali hiyo walikuwa wamepewa kazi ya kufuatilia uhalali wa akaunti ya Bw. Chenge.

"Suala hilo limekuwa likishughulikiwa na maofisa wetu wa sheria kwa muda sasa. Nitatoa tamko muda wowote wiki ijayo," alisema Bibi Keir katika baruapepe yake hiyo kutoka Jersey.

Awali katika mahojiano na Majira Jumapili, miezi kadhaa iliyopita, Serikali ya Jersey ilitangaza rasmi kuwa itachukua hatua kali dhidi ya Bw. Chenge ikiwamo kutaifisha fedha zote za akaunti hiyo ambayo kwa sasa imezuiwa, iwapo itabainika hakuzipata kihalali.

Katika taarifa hiyo, ilisema kwa mujibu wa sheria za visiwa hivyo, wana uwezo wa kufanya hivyo kama walivyowahi kutaifisha fedha za kiongozi wa zamani wa Nijeria, hayati Jenerali Sani Abacha.

Bw. Chenge mwenyewe amekuwa akisisitiza kuwa hana hatia katika tuhuma hizo na kuzitaja fedha zilizoko Jersey kuwa ni 'vijisenti' tu.

Walipoulizwa kuhusu tuhuma hizo na hatua zilizofikia, maofisa wa kampuni ya BAE Systems waliendelea kusisistiza kuwa kwa sasa wanatoa ushirikiano kwa makachero wa SFO.

"BAE Systems inaendelea kutoa ushirikiano unaopaswa kwa wachunguzi kuhusu kashfa mbalimbali likiwamo suala la Tanzania. Kwa sasa hatuwezi kusema lolote zaidi," ilisema taarifa yao kwa gazeti hili.


source: majira
 
mimi na nawaamini sana hawa SFO, kama hakutakuwepo na unafiki wa vyombo vyetu vya habari na viongozi wetu kumlinda fisadi chenge, nina uhakika ukweli utajulikana kwa kuwa waingereza huwa hawangwi kirahisi, ingekuwa ni wachina wanachunguza ningekuwa na mashaka
 
Jambo jipya hapo ni kwamba Waingerea watasoma repoti yao bila kuficha chochote. Wataiachia Serikali ya Tanzania kushughulikia mapendekezo yao lukuki. Kuanzia hapo hatutakuwa na jambo jipya tena kwani Chenge na wahusika wenzake ni wenzetu na hakuna hatua yoyote itachukuliwa!!!!!!!! Ukweli ndo huo!!!!

Nawaonea huruma Waingereza wa watu wanapoteza muda wao kufuatilia wizi katika manunuzi ya Rada wakati wanajua fika kuwa Tanzania huwa hakuna desturi ya kufanyia kazi ripoti lukuki za tume. Kila kitu undaa tume!!! Basi sitashangaa kuona hata mapendekezo ya SIFO yatatakiwa kuundiwa tume maalum Tanzania ili kuyachunguza upya mapendekezo hayo na ripoti haitatoka kwa kisingizio kuwa Ripoti za Rushwa huchukua muda kupata uhakika na kufunguliwa kesi. Period, hakuna jipya hapo wakuu.
 
Pamoja na report nyingi kutofanyiwa kazi ila hili la rada limekaa vibaya na kama report yake itapatika ndani ya majuma kama mawili wakatati wana sisiem bado wana machungu ya tarime.... na hisi kuna uwezekano mkubwa sana wa mtu kutolewa kafara.

mambo mengi ya aibu yametendekeka na serikali kwa sasa inahitaji kujiosha ili angalau mheshimiwa akijimuvusisha awe na speech.

Ila kama anataka kuwa speech less It is up to him.

Mimi binafsi ningemshauri aachane na mafisadi awajibike na awawajibishe. Haya mambo ya mshiko yapo tu na anaweza akajitwalia mshiko wenye adabu bila shida kutoka kwa mabilionea kama kina Ibrahim.

Mkuu jenga Jina na Jiteteee

Huu ni wakati wako wa pekee kubadili mtizamo wa watanzania Juu yako. Unless ukitaka kuendele kujishauri kama kawaida yako, Unachukua miaka miwili unagundua Picha inayotumika kwenye maofisi hukua kwenye pozi ITAKULA KWAKO MKUU
 
Inategemea siku hiyo muungwana ameamka vipi!

Daah, Mkulu hili jiwe kubwa ati. Ukilichambua kidogo unakutana na vitu viwili vitatu vya haraka haraka:

---Ameamka vipi- inatanguliwa na amelala vipi
---Amelala vipi- inatanguliwa na amelala wapi
---Amelala wapi- inatanguliwa na amelala na nani
---Amelala na nani-........nakadhalika.....
 
Ni vyema ikakumbukwa kuwa uchunguzi unaofanywa na SFO siyo kwa ajili ya Tanzania bali ni kwa ajili yao wenyewe na kampuni yao ya British aeroscope. hivyo Serikali itakachosema ni kwamba Uchunguzi wa SFO ilikuwa ni kwa ajili ya waingereza wenyewe na Kampuni yao. Hivyo Serikali baada ya kupata report ya uchunguzi watajidai kuwa wanaitisha uchunguzi mwingine sasa. Uchunguzi utaendelea weeeeeee mpaka mtasahau. Kama ilivyotokea kwa Richmond etc
 
Naamini katika kile ambacho 'chama' chetu kitafanya. Kulinda na kutetea wanachama wake watiifu na kuwapa madaraka makubwa ya kuimarisha uhai wa chama.

Chenge pamoja na ubaya wake kama mtu wa kawaida, tutamtetea ili kulinda 'chama chetu' na maslahi yake kwa maendeleo ya taifa.


KAMA SIO LEO, BASI KESHO. BUBU WATASEMA
 
Back
Top Bottom