The Radar Scandal: Investigation & Progress

The Radar Scandal: Investigation & Progress

- By the way umepata dataz kuwa waziri wa OIC ndiye aliyem-recordia Mengi tepu ya waziri aliyeshauri aonewe na kodi?
 
- Wajiuzulu kwa sababu wewe uliyewachagua huwataki? Mkuu sikujua kua una nguvu kiasi hiki hongera sana bro!

Duh! unajua kweli kupinduapindua maneno ili kukidhi kile unachokitaka. Nimeandika "wajiuzulu ili tufanye uchaguzi mwingine" lakini umeamua kubadilisha...ili ionekane kama mimi nina nguvu saaaaaana ya chochote ninachoktaka lazima kiwe!!!! Ningekuwa na nguvu kiasi hicho ya nini tena kukwambia wewe mzee wa 'dataz' ambaye unategema "ugeni mkubwa sana wa Viongozi wa Taifa" ufikishe ujumbe!!!!? Si ningeyamaliza mwenyewe tu!!!!

By the way wape salaam hao wataokuwemo kwenye ugeni huo mkubwa. Vipi wamekuja kuchukua 'Dataz' zaidi wakazifanyie kazi? just thinking aloud 🙂
 
Haa haa haa haa!

Ufisadi wote uliofanywa Tanzania umefanywa kwa makusudi kabisa na kundi la wasomi waliobobea ili kujenga tabaka la wenye fedha na walio juu ya sheria kwa nia ya kukuza nguvu katika duru za siasa na utawla ndani ya serikali na ukiritimba katika masuala yote ya kiuchumi.

Ushauri: Kwa sababu dawa ya moto ni moto, sioni kwa nini dawa ya fedha isiwe fedha.
Fedha wanayoihusudu na kuisujudu kwa heshima zao zote ili wakae katika enzi kuu ndiyo hiyohiyo itakayo itakayowaondolea heshima na utukufu wao na kuwapoka enzi yote.

Katika muda mfupi ujao wataendelea kutawala kwa nguvu ya fedha na katika muda mupi ujao utawala wao na mamlaka yao yatakoma na mahali pao litakuwa jivu.

Waambie wana bahati sana kwamba hatuna eneo la kuzika watu Mashuhuri Tanzania.
Lingekuwepo eneo la kuwazika watu mashuhuri nina uhakika siku ingefika sisi au wajukuu zetu wangefukua makaburi yao yote na kuchoma mabaki ya miili yao na kuzika jivu lao kwenye kaburi moja lilomiminwa kwa zenge na nondo na kuzibwa vizuri ili uovu uliomo ndani ya jivu lao usisambae.

Wana bahati sana kwamba kila mtu mashuri atazikwa huko kwao madongo kuinama kusiko fikika kirahisi nyakati zote na ambako tutakuwa hatuna nidhamu kwenda kugusa makaburi yao kwa nia yeyote ya kutaka kuyadhuru.

Zaidi tunawaombea kwa Mungu ili waishi na kukutana na uovu wao wenyewe ana kwa ana.

Mapambano bado hajaanza.
 
- By the way umepata dataz kuwa waziri wa OIC ndiye aliyem-recordia Mengi tepu ya waziri aliyeshauri aonewe na kodi?

Hakuna Waziri wa OIC katika baraza la Mawaziri, wewe kama unajua ni waziri wa wizara gani aliyerekodi maongezi na kuyafikisha kwa Mengi basi ni bora umwage dataz tu.
 
Hayo maneno hayana maana yoyote, viongozi wezi wamefikishwa kwenye sheria na wengine wako njiani, hao ndio wanahusika na maneno yako, lakini hayawahusu viongozi wote na hasa walio wasafii, ingawa maneno yako ni mazito sana na I am down pia!
 
- By the way umepata dataz kuwa waziri wa OIC ndiye aliyem-recordia Mengi tepu ya waziri aliyeshauri aonewe na kodi?

Mzee,pamoja na maneno yote yanayojitokeza hapa na pale kuhusu data zako (hayo ni ya kawaida kwenye baraza kama hizi),mie naendelea kuku-rate kama the most reliable source wa dataza hapa JF.Simlazimishi mtu kukubaliana nami lakini ukweli ndio huo.

Na mfano mzuri ni hiyo data mpya na ya moto kuhusu waziri wa OIC kuwa source wa Mengi.Na japo umei-present kama habari ya kawaida tu lakini ni ushahidi mwingine tosha kuwa vyanzo vyako ni exceedingly reliable maana muda mfupi tu nami nimenong'onezwa na mtu flani wa mahala nyeti kuhusu suala hilo.

Endelea kutumwagia dataza Mzee....
 
Ha ha ha Wakuu hao wa Taifa kama kweli huwa wanakusikia unachowaambia ni bora uwaambie kazi imewashinda wajiuzulu kazi

1. Duh! unajua kweli kupinduapindua maneno ili kukidhi kile unachokitaka. Nimeandika "wajiuzulu ili tufanye uchaguzi mwingine" lakini umeamua kubadilisha...ili ionekane kama mimi nina nguvu saaaaaana ya chochote ninachoktaka lazima kiwe!!!!

- Yote hayo juu ni maneno yako mwenyewe sijaongeza wala kupunguza.

Ningekuwa na nguvu kiasi hicho ya nini tena kukwambia wewe mzee wa 'dataz' ambaye unategema "ugeni mkubwa sana wa Viongozi wa Taifa" ufikishe ujumbe!!!!? Si ningeyamaliza mwenyewe tu!!!!

- Hapana wapo mjini tayari wengine wanakuja weekend, otherwise ni darasa tu so far!

By the way wape salaam hao wataokuwemo kwenye ugeni huo mkubwa. Vipi wamekuja kuchukua 'Dataz' zaidi wakazifanyie kazi? just thinking aloud

- Mimi sio kiongozi sina dataz wao ndio wanakwua nazo, anyways saa ya kulala mkuu, heshima mbele sana usiku mwema mkuu!
 
Hayo maneno hayana maana yoyote, viongozi wezi wamefikishwa kwenye sheria na wengine wako njiani, hao ndio wanahusika na maneno yako, lakini hayawahusu viongozi wote na hasa walio wasafii, ingawa maneno yako ni mazito sana na I am down pia!

Bado kabisa shughuli ndiyo kwanza zinaanza bado kuna mafisadi wengi tu ndani ya chama na serikali. Nasikia safari za kwa waganga zimeongezeka ili wajikinge wasiibuliwe kwa ufisadi waliofanya dhidi ya Watanzania. Wote hawa wamekuwa matajiri wakubwa sana katika kipindi kifupi mno na utajiri wao wanatafuta kila njia kuuficha ili Watanzania tusiujue kwa kuandikisha mali zai zao kwa majina ya watoto wao, ndugu na jamaa. Tunasubiri kusikia kama katika lile daftari la mali za viongozi fisadi Daniel Yona aliorodhesha kama ana mali zinazofikia billioni 3, kama hakufanya hivyo basi lile daftari ni usanii mtupu.
 
Hakuna Waziri wa OIC katika baraza la Mawaziri, wewe kama unajua ni waziri wa wizara gani aliyerekodi maongezi na kuyafikisha kwa Mengi basi ni bora umwage dataz tu.

- Alirekodi kwa kutumia peni maalum iliyonunuliwa Eastern Europe, ambayo ina uwezo wa kurekodi maneno na picha, kwa hiyo Mengi ana tepu na video.
 
Hayo maneno hayana maana yoyote, viongozi wezi wamefikishwa kwenye sheria na wengine wako njiani, hao ndio wanahusika na maneno yako, lakini hayawahusu viongozi wote na hasa walio wasafii, ingawa maneno yako ni mazito sana na I am down pia!

Ni kweli, hata hivyo ni asubuhi mno kudhani kwamba kuna wasafi wa kujaa walau kibaba kimoja.
 
Tunasubiri kusikia kama katika lile daftari la mali za viongozi fisadi Daniel Yona aliorodhesha kama ana mali zinazofikia billioni 3, kama hakufanya hivyo basi lile daftari ni usanii mtupu.

- Mkuu wiki moja kabla ya kushikwa Yona alikwua akijaribu kupata mkopo wa shillingi Billioni 5 toka Stanbic, benki ikadai aonyeshe source ya jinsi atakavyolilipa, ndugu yangu nasikia mbingu zilitaka kushuka Yona liapoamua kuleta usahidi wa sources zake.

- Kesho yake ule mkono mzito, ukapiga simu kule stanbic na kuamuru wasitishe mkopo mara moja, kesho yake mkulu akachukuliwa.

Thanxs!
 
- Yote hayo juu ni maneno yako mwenyewe sijaongeza wala kupunguza.

Ngumbaru ndiye anayeweza kusema kwamba hukupindua maneno ya yale niliyoyaandika mimi ili kukidhi haja yako, lakini mtu ambaye ameenda shule na ana uwezo wa kuchanganua mambo anajua ukweli umelalia wapi.

- Hapana wapo mjini tayari wengine wanakuja weekend, otherwise ni darasa tu so far!

- Mimi sio kiongozi sina dataz wao ndio wanakwua nazo, anyways saa ya kulala mkuu, heshima mbele sana usiku mwema mkuu!

Ok, best dreams of your choice see you tomorrow I hope with more 'dataz' from members of 'ugeni mkubwa wa viongozi wa Taifa' 🙂
 
Kwani aliposema waziri wa OIC wewe hujaelewa nini?? gubu hilo, kha!!

Kwa mara nyingine tena hapa ni JF where we dare to talk openly sasa ni kipi cha kuficha!? au tumebadilisha JF's motto tunaongea chini ya uvungu tena kwa kunong'ona!!!? 😕
 
Kwa mara nyingine tena hapa ni JF where we dare to talk openly sasa ni kipi cha kuficha!? au tumebadilisha JF's motto tunaongea chini ya uvungu tena kwa kunong'ona!!!?

- Pole pole mkuu, tunaelekea kwenyewe yaani Ikulu kwenye yote, soon wakuu kesho naomba kulala, maana unajua tena kesho kibarua kama kawa.
 
Mie sina mamlaka hayo tena ni JF's public enemy number one lol!! Issue sio kubadili motto, ipo wazi ni nani waziri wa OIC....

Mbona story ya "waziri kijana" hukubeba bango kuambiwa wazi ni nani, au kwasababu hii kaleta FMES??

Nilikuwa nimeshapewa 'dataz' kwamba ni nani lakini mimi si mtu wa kumwaga dataz zinapotoka jikoni maana si rahisi kuzithibisha na zikiwa si za kweli basi unaangusha credibility ya JF.
 
Woooow...hivi upo sawa ndugu yangu!?? ndio umeandika nini sasa hapo? Kwahiyo unasemaje, tubadili motto wa JF au ubaki ule ule? Naomba usome ulichoandika, fikiria, halafu utaona jinsi ulivyojichanganya...LOL😀, kaazi kweli.

Labda wewe ndiye unajichanganya pamoja na kuwa JF is 'Where dare to talk openly' huwezi kusikia habari ambao huna uthibitisho wowote na kuziweka hapa, kama huna uthibitisho basi ni bora usiweke hapa. Hapa siyo mahali pakuweka 'dataz' ambazo ni robo robo thibitisha 'dataz' zako halafu zimwage hapa na siyo kuleta hear say ukiulizwa source ni ipi unaanza kung'aa macho.
 
Usi-panic braza, eazy...90% ya habari hapa ni uzushi isipokuwa zile za copy and paste (wewe ndio King Copy bin Paste wa JF)!! Zaidi ya hapo unataka kumwonea tu FMES...halafu inaonekana "mmepania" kichizi kummaliza JF style..🙁

Ha ha ha kwani kuna ubaya wa copy na kupaste kitu ambacho kinaweza kuthibitishwa kimetoka wapi? Mbona wamiliki wa JF hawajasema lolote kuhusu hilo? Na magazeti ambayo nachukua habari hizo juzi baadhi yao yamepata zawadi kwa kuwa mstari wa mbele katika kupambana na mafisadi. Sasa kuna ubaya gani wa kushare habari hizo na Watanzania wenzangu kwa kuziweka hapa jamvini!?

Hakuna yeyote ambaye anataka kummaliza FMES kwanza siijui hiyo style unayodai inatumika kummaliza FMES. Watanzania tunahoji hata 'Dataz' za JK kama zile za pesa za EPA 69 billioni anazodai zilirudishwa ambazo hazijulikani zimewekwa bank ipi, itakuwa za FMES!!! Kama analeta 'dataz' zake basi WanaJF wana haki ya kuzihoji na kufanya hivyo haina maana ya kutaka kummaliza JF's style, kumchafua au kumdharau bali ni kutaka kuthibitisha ukweli wa 'dataz' hizo.
 
Waziri wa IOC ndio nani ?Ni Membe nini maana ndiye waziri wa mambo ya nje anahusika na Tz Kuingia kwenye IOC.Hey mnaojua tupeni kinaga ubaga

Halafu kuna mtu anasema mbona waziri kijana hakutajwa wazi kwani Mengi ni member wa JF?Smart Talented Unique Person In Demand(STUPID)!.
 
Back
Top Bottom