The Radar Scandal: Investigation & Progress


The hypocricy!!
 

Moelex23,

Kwa yanayomkabili Chenge sitegemei UK wampe visa ya kuja kutembea UK. Kuna maagizo ya kutosha kuhusu viongozi ambao wanahusika na corruption third world kutokupewa visa ya kuingia UK. Suala la Chenge liko wazi, naamini hana sifa tena za kupewa visa ya UK labda kama serikali ya UK wana nia naye.

Nitashangaa kweli kweli kama Chenge kapewa visa kuja kwa masuala ya kifamilia.

Ukiniuliza mimi kwa uzoefu wangu, nitasema hapa kuna jambo kubwa zaidi ya masuala ya kifamilia.
 

When you read this and reflect to the close relationship between Mkapa and Tony Blair, it makes you wonder if Tanzania was used a s a conduit on this contract to make some British officials (including Blair) rich by over charging and bribing military stuff from BAE!

May be Kikwete was right in some way kuwa we need British Government and BAE to reimburse Tanzania the difference!
 

Moe,

You nailed it well better than everyone here. Where is our government to ask Chenge and all other Mafisadi to show us how they got rich. There is no need to find from somewhere else, tumiulize hii mijamaa, pesa hizi umezipata wapi? wakishasema walipozipata, tuwaulize vielelezo vya kuzipata fedha hizo na memngine mengi.

Si mnakumbuka vita vya Uhujumu na ile sheria ya 1984, ulikuwa unaulizwa je umepata wapi Colgate na si kwa nini una Colgate!
 

Nimemtetea wapi Chenge hapa? Tumesema kuna taratibu za kubadilishana wahalifu na masuala ya Jurisdiction baina ya nchi, vitu ambavyo vinaonekana vimepinda katika hii stori ya wachunguzi Waingereza ku execute search warrant iliyo sainiwa na Kikwete (huoni ni kichekesho?). Usipindishe mambo ndugu. Na pointi ya Chenge kusema anachunguzwa pia hukuielewa. Chenge ndie alianzisha uzushi wa kusema anachunguzwa wakati sio kweli. Hukunielewa au unasema namtetea Chenge ili u ride a wave of popular opinion kwa sababu Chenge tunajua ni pariah?
 
mmmmmh,chenge cannot be persecuted in uk.watamchunguza for while then ataendelea kudunda mtaani
 
Kundi la mafisadi limekusanywa pamoja na linaonekana ni kubwa na bado lina nguvu za kufurukuta na kujikomboa kutoka hapo lilipo. Kitakachotokea TZ kwa kipindi cha miezi michache sana ijayo ni JK kupata ajali ya ndege na kututoka ghafla kama Sokoine.

Ni utabiri tu lakini!
 

Yakhe hiyo ni Kufuru bin balaa. Pamoja na kutokukukbaliana nami na Kikwete na kutokufurahia Uongozi wake, kumuombea dua baya kama hilo ni kufuru kwa Mwenyezi Mungu na Taifa letu!
 
..sidhani kama Raisi anasaini-saini tu kila kibali na search warrant.

..nilitegemea IGP, AG, au PS ofisi ya Raisi, ndiyo wenye mamlaka na wajibu wa kutoa kibali hicho.

..halafu inakuwaje raia wa Tanzania achukuliwe na maofisa usalama wa UK na kuondoka naye nchini. hii inakuwa kama kuvuka mipaka na sheria za nchi vile.

..ningependa sana Chenge akamalize masuala yake mahakamani, lakini hii habari inatuacha na maswali mengi kuliko majibu.
 
Imagine nchi kuongozwa na Shein!Mzito toka mdomo mpaka......halafu PM pinda ...mamaah .....naisi kama mchi sasa basi....woooh
 

Uko sahihi. Rais wa Tanzania hana nguvu ya ku sign Search Warrant. Ni Mkuu wa Kituo, deputy wake, au kama wote hawapo, basi Waziri wa mambo ya ndani anateu Polisi wa ku sign Search Warrant.

CRIMINAL PROCEDURE ACT 1985-9
Procudure Relating to Criminal Investigation


Power to issue Search Warrant


38.-(1) If a police officer in charge of a police station is satisfied that there is reasonable ground for suspecting that there is in any building, vessel, carriage, box, receptacle or place:
(i) anything with respect to which any offence has been committed;
(ii) anything in respect of which there are reasonable grounds to believe that it will afford evidence as to the commission of any offence;
(iii) anything in respect of which there are reasonable grounds to believe that it is intended to be used for the purpose of committing any offence, and the officer is satisfied that any delay would result in the removal or destruction of that thing, or would endanger life or property,

he may search or issue a written authority to any police officer under him to search the building, vessel, carriage, box, receptacle or place as the case may be.
 
I thought aliyeidhinisha kusachiwa kwa Chenge alikuwa mwanasheria mkuu..? well at least ndivyo nilivyosikia/ambiwa...as always wengine tunakaa pembeni tunaangalia
 
Yeyote aliyekuwa, hakuwa Rais. Rais hana mamlaka ya ku sign Search Warrant.
 
Chenge amepekuliwa na wazungu kuanzia ofisini kwake mpaka nyumbani kwake, na amekutwa na shillingi billioni moja cash, safari ya UK ilikuwa siri je imatangazwa anywhere zaidi ya hapa JF?

Je Chenge yupo UK au hayupo, Chenge alionyeshwa kibali kilichosainiwa na rais kabla hajaenda India, na alipotaka uthibitisho akapewa kuwa kimetoka kwa rais, akasachiwa baada ya kuachiwa akakimbilia Kwa Mkono, Butiama ndio kwa mara ya kwanza mkono anawafahamisha wakulu wengine kuwa Chenge, amesachiwa na anauhitaji msaada wake lakini hawezi kumsaidia, I can go on and on ila siwezi kwa sababu ya kumridhisha mtu mmoja mwenye majina mia humu, wewe huna dataz na utaendela kusubiri za wengine tu hapa JF na kubaki na logic zako za chooni,

sisi tunasonga mbele, na tutakapozipata zaidi tutaziomwaga, mkuu tumekuambia kuwa umaarufu hapa huletwa na hoja na dataz, sio logic maana kila member anazo hapa, ila hoja na dataz sio kila mtu anazo hapa, kuna wengi hapa kama Lunyungu wameenda kuzitafuta zaidi sisi tumewapa lead tu, ila kuna the zero wa logic ndio kazi kujifanya kujua kumbe hujui nothing, ila ni ujuha tu anytime write, ni pure nonesense!

I stand for kila nilichosema, unless useme ukweli tofauti, logic hata mtoto wangu anazo, ila hoja na dataz hana, kama na wewe ulivyo huna, dawa ni kukaa pembeni upewe dataz hapa tunazo all the time, from day one tulipoingia hapa na tunaendele, hazikusaidiii wewe lakini kuna wengi zinawasaidia, sasa kaaa pembeni!
 
Chenge akifungwa UK ni poa tu sio kama Jela za Bongo vile vile ni bora Chenge atokomee UK kama Balali alivyotokomea USA kwa sababu kubwa moja ushahidi kwa waliobaki Bongo unakuwa rahisi zaidi hivyo kumuacha JK na serikali yake kwenye unafuu wa migogogoro ambayo wanakabiliwa nayo.

Bunge butu ambalo linachechemea linatakiwa kupewa Tiba na kumuuliza maswali magumu waziri mkuu Pinda ili hawa Nguchiro ambao tunao hapa nyumbani wasitokomelee huko ughaibuni bali wasimamishwe kizimbani na kujibu maswali magumu ya kulihujumu taifa.


Nchi imekuwa kama Kichuguu ambako nguchiro wanaingia kama wanavyotaka na kuwapekuwa raia kama vile hatuna jeshi la polisi wetu kufanya kazi hizo. Well wameuza migodi yote pamoja na rasilimali zake sasa wamehamia kuuza raia. Who's next?
 

Kumbe kunaushindani humu? Kumbe ukipata info mtu kasafiri ni data jf? Dont you think Mkono would would be the obvious choice since he runs the most successful international firm in bongo?? and why atakataa kwakuwa yeye ni mwanasheria wa british embassy??? Usilete siasa na maneno meeengi about how long u been at jf...LOGIC is way greater than hisia and vihoja (naona imekugusa sana hadi comparison to your kid?? wow!!! was that necessary mr JF Senior Premium Expert Member??)... Someone is bitter about being criticised?? its a new day at JF...dont matter how long u been a member here..

Kamavipi wekeni rules stating kwamba kuna members info zao can't be disputed...(Weka clear cut evidence and we shall give you your earned thanks)
 

Mkuu,

Hapa unaongea utafikiri kwa TZ sheria ni msumeno? Kwa Tanzania polisi hawawezi kumsearch waziri bila rais wa nchi kukubali.

Hata kama hakuna sheria ilipoandikwa, usitegemee hata siku moja polisi waende kumsearch waziri wa Tanzania bila rais kuwa na habari.

Ingelikuwa hivyo basi kufikia leo hii mawaziri kibao wangisha chunguzwa maana kuna ushahidi tosha kwamba ni mafisadi.

Kama Chenge alikuwa searched basi rais JK alihusika full stop.
 
Kapinga

Tuambie Chenge yuko wapi hivi sasa kama unazo nyeti? Kuhusu Premium members vipi una beef nalo hilo? Mbona wewe ni Expert member? Rules zipo kwa JF members wote ingefaa utuwekee info za Chenge na tumsute FMES na ukweli maana habari zote nyingi huanza kwa tetesi kama hizi labda uwe GT ndio mashaka hutokea. Kwa hii info FMES anasema ni za uhakika sasa wewe weka za kwako ku-prove otherwise.

BTW kila member anafahamu SFO wanafanya kazi kwa maslahi ya walipa kodi wa UK na si kwa walalahoi wa Bongo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…