The Radar Scandal: Investigation & Progress



Haleluya. Kwa hiyo unatishia kuua watu au. Hata wakifa watakuwa hawajaziba lako na wewe siku moja utakufa kifo ni cha kila mtu. Pole kwa hilo lakini hakuna anayeogopa kufa labda wewe. Na wala usinitishie maisha mimi kwani pia hunijui. Lakini siogopi kufa kamwe nakuhakikishia Kama wewe ndio utakuwa sababu ya kifo changu basi mapenzi ya bwana yatimizwe Upo
 
najaribu kuangalia ni wapi mtu katishia kuua mtu? vinginevyo naamini mjadala huu ni mzuri na kila mtu anahaki ya kuchagua upande...
 

Ee bana naona hujamaliza tu kumtetea Msukuma mwenzako hadi umeamua kurudi tena na leo?! Sasa leo wacha kubwatabwata kama jana na juzi nataka utuambie huo upande mzuri wa shilingi kuhusu Chenge unaodai. Ni sifa zipi au matendo gani ya kuvutia kuhusu Chenge yanayokufanya udamkie humu kila siku kumtetea kila kukicha?
 
Afadhali Mkuu umeingilia kati!
Atuambie sasa bana maana naona mlolongo wa mabishano ni mrefu na maana halisi ya mjadala huu kuelekea kupindika ama kupindishwa.
Matiksa anaweza akawa Chenge mwenyewe/wife ama mtu wa karibu sana!
He/she is very passionate! But so am i!
I believe in a war against ufisadi where as he/she doesn't!
I believe Ufisadi upo na ni Hatari kama UKIMWI lakini mwenzangu yeye anaona tuko peponi!
Ndugu yangu huyu anaonyesha ana akili sana lakini za kizamani! Lugha inaonyesha!
Sasa ushauri wangu ni kuwa a check na reality!
Kwa nia na makusudi kabisa anajaribu kutwist issue kudai kuwa nimemtisha kummua!
Hainishangazi! Lakini wa kuogopa na kutishika ni mimi na sio wale wanaolindwa na dola!
Hebu sasa mwaga something and then we'll see!
 

Inawezekana ni Mkuu mwenyewe unazungumza hapa!
As a noble member of JF niko hapa wazi na identity yangu sijaficha!
Hii haina maana kuwa sikubaliani na wale wanao amua kuficha identity zao!
Ndio JF hii na we love it with all its uniqueness!
Hivyo basi nachukua nafasi hii kukufahamisha kuwa tuko hapa kwa mijadala yenye kujenga na sio propaganda ama application of defensive mechanism where your ego uses these protective methods in order to reduce anxiety by unconsciously distorting reality!
You're a victim..Pole sana!
 

Kama kawaida desparate and meaningfull distortion of the actual meaning and reality!
And then kwa akili yako ya kizamani bado una ni intimidate ili kuniogopesha kisaikolojia!
Mkuu sijatisha kukuua mahali popote!
Hata Afande Mwema anaweza kuja na kusoma hapa ili kukueleza wewe unayejua sheria kuwa hujatishwa na wewe uko salama kuliko asilimia 90 ya wabongo!
Sikuchukii wewe binafsi bali matendo yako!
Ukitubu na kuwajibika kwa watanzania utapata msamaha wao na wa Mungu!
Inawezekana kuwa naogopa kufa! Lakini si all the time for we all gonna die!
Ila kufa for what i beleieve for is what i never fear!
Remeber this: "Courage is not the absence of fear..But the strenght to speak the truth on the face of it!"
Siwezi kuwa sababu ya kifo chako labda wewe ndio uwe sababu ya kifo changu kwani sina maslahi yoyote ya kulinda!
Kwa maana nyingine wewe ndio unanitisha kisaikolojia..Na ndio maana nasema hivi..Mkitaka kuniua hamtashindwa! Ila itafahamika kwasababu i am not stupid!
Kama nimekuelewa vibaya basi ni mimi na watanzania wenzangu tunaweza kukusababishia ugonjwa wa moyo kwa vilio vyetu kuhusu vijisenti vyetu!
Najua unajaribu kusema kuwa hatuwezi kuwalalumu nyie kwa umasikini wa kila mtanzania..Hili hata MKJJ anakubaliana na wewe ila mimi sikubaliani na wewe kwasababu hivyo vijisenti ni vya wananchi na hivyo usianze kutisha watu ama kuwaogopesha wasiviulizie!
Wataachaje kuviulizia na sasa wanajua nchi yetu ni tajiri na nyie ni wa viwango vya juu kwa kupitia migongo yao na utajiri huo?
Jichanganye kidogo na watu wa kawaida ili ujue reality na sio kukaa na watu wanaosema ndio mzee all the time!
 

matiksa naona kafyata mkia na kutokomea mitini. jmushi1 endelea kumwagia vidonge vyake huyu Msukuma. Nyambafu kabisa!!
 
Serikali imelala usingizi wakati huyu fisadi anaachwa ile asambaze uwongo wake. Lowassa naye alifanya hivyo. Angekuwa amewekwa rumande huu usanii usingetokea

Chenge aanza kujisafisha

* Aenda kujieleza kwa wapigakura wake
* Wapambe wamwandalia mapokezi makubwa
* Wasema ataeleza sababu za kujiuzulu
* Safari kuanzia mkoani Mwanza

Na Mwandishi Wetu, Mwanza
Mwananchi

BAADA ya kukumbwa na tuhuma nzito za ufisadi, Andrew Chenge, sasa ameamua kwenda jimboni kwake Bariadi Magharibi, kujisafisha kwa wapigakura wake.

Mtindo kama huo ulitumiwa pia na aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, ambaye baada ya kujiuzulu katika mkutano wa 10 wa Bunge la Februari alikwenda jimboni kwake Monduli ambapo alipokewa na watu na magari mengi, kitendo ambacho kilitafsiriwa kuwa alikuwa anajisafisha kutokana na kashfa ya Richmond.

Ziara hiyo ya Chenge kwenda jimboni ni ya kwanza tangu aanze kuchunguzwa na makachero wa Taasisi ya Kuchunguza Makosa Makubwa ya Jinai ya Uingereza ya Serious Fraud Office (SFO).

Uamuzi huo wa Chenge pia kufanya ziara jimboni kwake umekuja ikiwa ni wiki moja baada ya kuzushiwa kifo.

Habari zilizopatikana kutoka jijini hapa zilisema Chenge alitarajiwa kuwasili Bariadi jana usiku akitokea Mwanza.

Taarifa hizo ziliongeza kwamba, Chenge ambaye alijiuzulu wadhifa wa Waziri wa Miundombinu baada ya kukutwa na Sh1.2 bilioni katika akaunti yake katika kisiwani Jersey, zinazohusishwa na biashara ya kifisadi ya rada, pia atawaeleza wananchi wake sababu za kujiuzulu kwake.

Tumemwandalia mapokezi makubwa, kwanza ni kwa ajili ya kuja kuwathibitishia wapigakura wake kuwa yuko hai, kutokana na uzushi kuwa amefariki dunia," kilisema chanzo hicho na kuongeza:

"Lakini pia kuwaeleza wapigakura wake watapenda kujua sababu ya yeye kujiuzulu kwake, maana yamekuwa yakisemwa mambo mengi,? alieleza msemaji mmoja kutoka Bariadi ambaye hakutaka kutaja jina lake.

Habari zaidi zilieleza kwamba, Chenge atakwenda katika jimbo hilo ambako baadhi ya watu wanaojiita wafuasi wake wamemwandalia mapokezi makubwa ya kumsafisha na tuhuma za ufisadi zinazomkabili.

Hata hivyo, pamoja na kuandaliwa maandamano hayo, huenda yakageuka mwiba mchungu kwake kwa kuzomewa kwani eneo hilo ni ngome ya chama cha upinzani cha United Democratic (UDP).

Mara baada ya Chenge kujiuzulu, wananchi wa jimbo hilo waliandaa maandamano ya kumpongeza kuachia ngazi kwake. Hata hivyo, wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanaamini kuwa, Chenge bado anakabiliwa na wakati mgumu kuweza kujisafisha, kutokana na tuhuma za ufisadi zinazomkabili kuwa kubwa.

Chenge mbali ya kukabiliwa na tuhuma za kujipatia mabilioni hayo ya pesa kwa njia ya rada, pia anatuhumiwa kuiingiza nchi katika mikataba mibovu.

Miongoni mwa mikataba mibovu inayohujumu uchumi wa nchi hadi leo, ambayo Chenge alishiriki ama kutia saini au kushauri akiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) ni pamoja na Kampuni ya Uzalishaji Umeme ya IPTL, mabilioni ya Kampuni ya Tangold na mengineyo.

Chenge pia katika ziara hiyo atakabiliwa na wakati mgumu kutokana na uamuzi wake wa kuziita Sh bilioni 1.2 alizoficha Jersey kuwa ni 'vijisenti', wakati jimboni kwake, baadhi ya wapigakura hawana huduma za maji safi na salama, uhaba wa huduma bora za kijamii kama afya na elimu.

Hadi sasa uchunguzi dhidi ya tuhuma za Chenge kuhusiana na Sh1.2 bilioni zinazohusishwa na rada, umebaki wiki mbili kukamilika.

Lengo la makachero wa SFO ni kuona kama fedha hizo zinahusiana na kutoa kashfa ya ununuzi wa rada inayodaiwa kununuliwa kwa bei kubwa zaidi ya uwezo na ubora wake.
 
Bongooo weee bongo darisalaam utalialialiaaaa bongo darisalaaam.....

Napiga mluzi taratiiibu hapa.
 
Watu washajua kuna "vijisenti" vinakuja hawataki kukaa mbali tena.
 
wameandaliwa baasha ili wampokee kwa shangwe, kama mwenzake alivyofanya arusha...atapokelewa kama shujaa
 
Serikali imelala usingizi wakati huyu fisadi anaachwa ile asambaze uwongo wake. Lowassa naye alifanya hivyo. Angekuwa amewekwa rumande huu usanii usingetokea

Nilijua anaanza spin pale alipoanza kuwahusisha Wasukuma na ufisadi wake!

Ni wazi anataka kuanza kututenganisha na kutafuta sympathy!
Anakwenda kuanzisha ngome yake badala ya kuwajibika na kurudisha mali za wananchi!

Ushauri wangu kwa ndugu zetu wasukuma ni kuwa wasikubali kuingia Mkenge!

Jamaa ni yeye na usukuma badala ya utanzania!

Nani kasema yeye ni fisadi kwasababu ni msukuma?

Si anataka tuamini kauli yake ilikuwa ni ya kisukuma na wala si ya kifisadi na kijeuri?

Anataka aanzie kanda ya ziwa ili umati wa watu masikini watakaojitokeza walete impression kuwa na yeye ana support miongoni mwa wananchi na wala sio watanzania wote wenye kufikiri yeye ni fisadi!

Tuwe tayari kwa mpambano!

Si mnakumbuka kwenye ile thread ya Klh News ya kutoka Ahera? Matiksa alipokuwa akibishana na mimi kuwa sio watanzania wote wanaodhani kuwa yeye ni fisadi?

Kazi ipo!
 
Nyani ngabu are sure CCM hoyee?? Nadhani ni kakichaka ka kuficha majambawazi mnatakiwa kujisafisha kwanza then mshangilie!!
 
Acha CCM itawale bana...
Nyani sio swala la nani atawale ama chama gani kitawale nchi right at this time and moment!
Hapa swala ni uwajibikaji and then kutawala ni 2010!
Nyani hautabiriki kabisa na sometimes very unstable!
Nani kataja vyama hapa?
 
Nyani sio swala la nani atawale hapa at this time and moment!
Hapa swala ni uwajibikaji and then kutawala ni 2010!
Nyani hautabiriki kabisa na sometimes very unstable!
Nani kataja vyama hapa?

Ni vizuri kutokutabilika kwa sababu ukiwa unatabilika kiurahisi watu wanakuzoea hovyo hovyo....Lakini kama hutabiriki mtu atajiuliza mara mbili mbili kabla hajasema au kufanya kitu kwa vile hajui utachukuliaje...

Halafu Chenge si mwana CCM..? Kwa hiyo CCM hoyee...CCM milele
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…