The Interview: mshana Jr.

The Interview: mshana Jr.

Mkuu mshana hivi uchawi una nafasi gani katika maendeleo ya mwanadamu?(Asilimia kubwa ya watu wanaamini, Mali & Utajiri unapatikana kwa njia zisizo halali,mfano utapeli,uchawai n.k) Na hata matapeli,Majambazi n.k wanatumia sana uchawi hili kutimiza Malengo yao.
Je kuna ukweli upi kuhusu hili jambo mkuu.
Uchawi ni dunia ya kiza na dunia ina usiku na mchana! Kila kinachotokea upande mmoja ni replica ya upande wa pili
Dhana ya uchawi na mambo yake yote vinatumiwa na kada zote katika maisha kuanzia viongozi wa dini wanasiasa mpaka vibaka
 
Asante mshana jr

Nakupongeza kwa kutuonesha picha yako halisi.
Wengi tulidhani kwa mambo unayoyajua basi utakuwa mzee au mbabu fulani.

Kumbe ndo kwanza unatafuta mchumba.
Safi sana mheshimiwa
Mshana Jr
Kwa kututhamini

Naposti
 
Asaalam, karibu katika mahojiano ya moja kwa moja hapa JF. Mhojiwa leo ni mshana jr mimi mwanzisha uzi ndiye Host.

Labda niseme tu leo mshana jr atahojiwa kila kitu, hasa kipaji chake alichojaliwa na bila kupepesa macho majibu atakayotoa angalau Yatatufungua macho tujue ulozi, uganga, uchawi umekaa vipi.

Naomba mshiriki kwa kusoma tu. Narudi tena kwa kusoma tu hadi pale muda wa kuuliza maswali utakaporuhusiwa. Karibuni.
Kabla ya yote mkuu vipi una hirizi la kujikinga?maana hayo makombora yatakayokuja hata yale ya korea kaskazini hayaoni
 
Kwako mshana, nina maswali kadhaa hapa.

1. Ni kitu gani haswa unajutia maishani.? Kwakweli sina majuto
2. Elimu yako ya mambo ya kiroho imekusaidiaje wewe binafsi na watu wanaokuzunguka.? Imenisaidia kujitambua zaidi imani yangu na maisha yangu...kupitia hii nimewasaidia wengi pia kwa njia anuwai
3. Je ushawahi kupata woga.? Ilikuwa ni wakati gani na nini kilipelekea wewe kuogopa.? Ndio maranyingi nawaogopa binadamu kuliko wanyama
4. Haya unayoshare nasi jukwaani, je familia yako inajua kuwa unajua.? Wanakuchukuliaje juu ya hilo.? Dah wapo ndugu humu jukwaani wanajua...hawana tatizo kabisa

5. Umeshawahi kuona visivyooneka kwa macho ya kawaida.? Vipoje.? Maranyingi ..viko kwenye vague images
6. Nakumbuka katika thread mojawapo inayozungumzia budhist college, ulsema kuwa ushawahi shuhudia kafara ya mtu toka kwa waabudu shetani, na ulipewa offer ya kujiunga nao. Je ulifikia nao wapi.? Sikuweza kujiunga kama unakumbuka nilitoroka

Tuanze na hayo kisha nitarejea na mengine ninayohitaji kujua toka kwako.
OK asante sorry nimejibu kwa ufupi
 
jr mi swali ni hili?je kama huamini kuna uchawi tena ikatokea ukamtukana mchawi je anaweza kukuloga na ukadhurika kwa manuizo yake?pili, je kama uchawi kweli unafanya kazi kwanini trump asimshushe hata busha kim jung ili dogo apate heshima?
Uchawi una miiko taratibu na masharti yake! Hawa wa kawaida unaeza kutukana na asikufanye chochote ila kuna namba hazichezewi asilani
Trump siwezi kumzungumzia kwakuwa sijui mtazamo wake kwenye uchawi
 
Mshana
1.Kuna uhusiano gani kati ya maisha ya mtu na nyota?
2.mtu anaweza kumuibia mwazake nyota?
3.Zipi ni dalili au njia za kujua kama nyota yako ipo au vibaka walisha ikwapua?
4.Je nyota iliyo ibwa yaweza kurudishwa kwa mhusika? how?
 
Kuhusu mabangili ya shaba:kuna mtu alinambia kuwa yanazuia mapepo pia ni kinga kwa mfano kutochukuliwa pesa na wazee wa chuma ulete,hii imekaaje?
Inategemea na bangili na manuizi iliyofanyiwa japo kuna baadhi zina material yanayovutia ama kupingana na dunia zote mbili
 
Back
Top Bottom