The Interview: mshana Jr.

The Interview: mshana Jr.

Dah kuwaelewesha wa Tanzania ni kazi sana. Yaani tahadhari imetolewa mapema kabisa lakini hakuna aliyeelewa. Kibaya zaidi kuna wanaouliza maswali ya kijinga kabisa.
Mimi naomba kama imeshindikana kufuata protocol mjadala interview ifungwe tu.
Nawasilisha
 
Kwako mshana, nina maswali kadhaa hapa.

1. Ni kitu gani haswa unajutia maishani.?
2. Elimu yako ya mambo ya kiroho imekusaidiaje wewe binafsi na watu wanaokuzunguka.?
3. Je ushawahi kupata woga.? Ilikuwa ni wakati gani na nini kilipelekea wewe kuogopa.?
4. Haya unayoshare nasi jukwaani, je familia yako inajua kuwa unajua.? Wanakuchukuliaje juu ya hilo.?

5. Umeshawahi kuona visivyooneka kwa macho ya kawaida.? Vipoje.?
6. Nakumbuka katika thread mojawapo inayozungumzia budhist college, ulsema kuwa ushawahi shuhudia kafara ya mtu toka kwa waabudu shetani, na ulipewa offer ya kujiunga nao. Je ulifikia nao wapi.?

Tuanze na hayo kisha nitarejea na mengine ninayohitaji kujua toka kwako.
Nitarejea naomba uvumilivu wenu
Mkuu mshana hivi uchawi una nafasi gani katika maendeleo ya mwanadamu?(Asilimia kubwa ya watu wanaamini, Mali & Utajiri unapatikana kwa njia zisizo halali,mfano utapeli,uchawai n.k) Na hata matapeli,Majambazi n.k wanatumia sana uchawi hili kutimiza Malengo yao.
Je kuna ukweli upi kuhusu hili jambo mkuu.
 
Gamboshi ipo ni kijiji cha kawaida machoni pa wengi ila kwenye dunia ya giza ni habari nyingine
Vyeo vya wachawi vipo kutegemeana na makafara lakini kuna ranks zinazotambulishwa na bangili ya shaba mkononi
Kuhusu mabangili ya shaba:kuna mtu alinambia kuwa yanazuia mapepo pia ni kinga kwa mfano kutochukuliwa pesa na wazee wa chuma ulete,hii imekaaje?
 
Asaalam, karibu katika mahojiano ya moja kwa moja hapa JF. Mhojiwa leo ni mshana jr mimi mwanzisha uzi ndiye Host.

Labda niseme tu leo mshana jr atahojiwa kila kitu, hasa kipaji chake alichojaliwa na bila kupepesa macho majibu atakayotoa angalau Yatatufungua macho tujue ulozi, uganga, uchawi umekaa vipi.

Naomba mshiriki kwa kusoma tu. Narudi tena kwa kusoma tu hadi pale muda wa kuuliza maswali utakaporuhusiwa. Karibuni.
naomba kuelewa kuhusu uhusiano wa wachawi na majini,je hawa watu ni maadui au ni marafiki sana,je binadamu anaweza kuwa mchawi halafu muda huo huo ana mapepo au majini
 
Uzi upo vizuri.
Mshana, ningependa kujua aina ya meditation unayofanya pia kama utaweza kutoa realization za ndani za hiyo meditation itakuwa vizuri
 
Mshana Jr Kwann Ww Husalimiani Na Watu Wala Kubebishana Na Watu Katika Nyuzi Je Inamaanisha Huna Ndugu Wala Mpenzi Humu Jf?!
 
Back
Top Bottom