The Interview: mshana Jr.

The Interview: mshana Jr.

Asante mshana jr

Nakupongeza kwa kutuonesha picha yako halisi.
Wengi tulidhani kwa mambo unayoyajua basi utakuwa mzee au mbabu fulani.

Kumbe ndo kwanza unatafuta mchumba.
Safi sana mheshimiwa
Mshana Jr
Kwa kututhamini

Naposti
Asante sana japo umri umesonga
 
Mshana
1.Kuna uhusiano gani kati ya maisha ya mtu na nyota?
2.mtu anaweza kumuibia mwazake nyota?
3.Zipi ni dalili au njia za kujua kama nyota yako ipo au vibaka walisha ikwapua?
4.Je nyota iliyo ibwa yaweza kurudishwa kwa mhusika? how?
Haya mambo kwa sehemu ni imani na mtazamo na mitazamo huleta uhalisia....nafsiroho zetu ndio engine ya maisha yetu
Ila kuna elimu ya nyota na maisha yetu kwenye muktadha huo
 
Mipaka yake ni ip? Ni sehemu gani uchawi au ulozi unafikia kikomo cha kushindwa kufanya kazi? Kwanini inakuwa hivyo. Funguka vya kutosha
Kila kitu kina ukomo wake hata Bomu la nyuklia kutokana na uasili wale
Uchawi haupatani na ugwadu maji ya baraka nk
 
Kwenye Bible na Quruan uchawi umepigwa vita. Na wewe inaonekana unauamini. Je, imani na msimamo wako ni upi?
Huko walikoukataza ndio asili yake..imani yangu kwenye uchawi imejikita hapo ila siuamini kama kinga ama solution ya changamoto zangu....siamini katika waganga wa kienyeji naamini uchawi na ushirikina vipo
 
Huko walikoukataza ndio asili yake..imani yangu kwenye uchawi imejikita hapo ila siuamini kama kinga ama solution ya changamoto zangu....siamini katika waganga wa kienyeji naamini uchawi na ushirikina vipo
Kipi kinachowafanya wachawi wasiutumie uchawi kwa faida ya wengi? Shughuli zao nyingi ni za siri na za kafara za kuteketeza?
 
Back
Top Bottom