TCRA, Tunaomba ufafanuzi

TCRA, Tunaomba ufafanuzi

Mkuu Pasco,

Nashukuru saana kwa ufafanuzi wako, ingawa umetumia a lot of technical terminologies zinazotoa picha kuwa kuwa jambo hilo ni gumu sana na haiwezekani kwa hawa jamaa kuingiza hizo 5 local channels kwenye ving’amuzi vyao vya DSTV.

Mimi bado naamini kuwa haijarishi hayo matangazo ya DSTV yanarushwa kutoka wapi, eidha ni South Africa, au Bongo – kikubwa hawa jamaa wanafanya biashara hapa kwetu na and they’re making a lot of money, umeifka wakati sasa Serikali isimamie mchakato (ikibid kuwalazimisha) wa hizo local channels kuonekana na kwenye DSTV Decoder, ambapo kwa sasa zaidi ya 99% ni channel za nje (hii kitu utaikuta Tanzania tu)


Hapo kwenye Red: Je pale ambapo wanaporusha hayo matangazo ya TBC kwa kutumia hiyo uliyoiita 'Service licence only', huwa wanakiuka masharti ya leseni yao?!! Anyway, if that the case, TCRA ilitakiwa iwapatie licence (technically sijui inaitwaje ) ambayo itawawezesha kupokea local contents na kuzingiiza kwenye Decoder zao kwa manufaa ya mlaji ambaye ni mtanzania, na hizo local channel ziendelee kuonekana bure hata kama account ya mteja haina hela.

Wakati mwingine kwenye hii biashara huria, Serikali inatakiwa iwe na mkono wake kuweza ku-regulate mambo, kama ambayo Serikali mefanya ubabe wa kulazimisha hizo hizo 5 local channels ziwe za free, kumbe inawezakana kukaa nao meza moja na ku-harmonize hii kitu, kama haiwezekana ni kuwalazimisha na wakishindwa wachape mwendo (japo hii opotion ya mwisho, naamini itakuwa ngumu saana kwani kuna baadhi ya wakubwa wana 10% zao)
Nakubaliana na wewe, serikali kilifanya kuwa ni mandatory kwa kila anarusha matangazo ya Tanzania, lazima anazirushe zile TV 5 bure!. Hata kama wanarushia matangazo Afrika Kusini, wana jinsi ya ku beam Tanzania ili decoder yoyote utakayonunua, iwe Zuku, DSTV au yoyote zile 5 channels ziwe mandatory!.
Kwa mfano kule Afrika Kusini, wazo baadhi ya lugha kuu ikiwezo Kizulu, Xhosa, Twasa na Sotho, sasa kila TV imelazimishwa kwa eneo la Wazulu, matangazo yote ya local, lazima yawe na tafsiri ya Kizulu for the locals japo wite wanazungumza lugha yao ya taifa ni Afrikaans na Kiingereza!.
Tungewalazimisha hata Isidingo itafsiriwe Kiswahi ndipo waruhusiwe kuirusha humu nchini!.

Pasco.
 
Wale wasio na uwezo wa kununua satelite dish unawashauri nini?

Btw, mimi kwa upande wangu tbc na channel ten ziko poa lakini itv, eatv na startv ndio mzozo. Matangazo yake yalikuwa yanastuck mara kwa mara lakini baadae yakakata kabisa (no service). Nimejaribu kupiga customer care hakuna msaada wowote.
mkuu hapo issue ni antena tu... mimi TBC 1 na 2 ndo zina stack balaa ila hizo nyingine shwari kabisa.
 
Mkuu uko nchi gani wewe?, yaani matangazo yote yale yaliyotolewa na TCRA wewe bado hujaelewa!.
King'amuzi ni kimoja tuu utaona TV zote tano za "free to air" bure!.

Mpaka sasa kuna makampuni matatu ya kurusha matangazo, Star Media, Agape Associets "ting" na kampuni ya Mengi na Dialo ambayo king'amuzi chao bado hakijaingia sokoni, ila kimeanza kutangazwa!.

Ukishanunua king'amuzi chochote, hizo TV tano za bure utaziona bila kulazimika kuzilipia na zitaonekana kwenye ving'amuzi vyote vitatu, hivyo uko huru kuchagua kununua kingamuzi chochote kati ya hivyo!.

Mfano kingamuzi cha Star media hawana chanel ya movie ya HBO, kama wewe ni mpenzi wa HBO, huna jinsi, lazima ununue king'amuzi cha Agape!. Huko pia utaziona bute zile tv tano za bure!.

By choice, kama unataka usipitwe kitu, na unapenda mambo mazuri yote, then utavinu nua ving'amuzi vyote vitatu?.

Mimi nilianza na kingamuzi cha Easy TV, nikaja cha DSTV, Sasa ninacho cha Star Media, my boys wanapenda movies za HBO hivyo soon nitanunua cha Agape!.

Wengi wa Wakazi wa Dar, tunapenda zaidi starehe kuliko kuzijali familia zetu!, mimi nakunywa Sinza, kuna bar 250 na zote zinajaa, kwa nini tushindwa kulipia king'amuzi elfu 10 kwa mwezi?!.
Heri ya Mwaka Mpya.
Pasco.
kweli shibe mwana malevya!
Sina hakika kama uliwaelewa TCRA au unafanya makusudi kwa kuwa umelamba kibahasha.
Imagine mimi nitanunua ving'amuzi vitatu halafu kuna babu yangu pale kisarawe,kuna baba mdogo,wajomba n.k

hili zigo la gharama litanirudia mimi tu na bado uhuru wa habari utakuwa umeminywa!

Pasco fikra zako ni za ki TCRA au kimasaki masaki hivi!
 
Ni aibu kwa TCRA. Nchi hii bora liende! Local channels hazipatikani kwenye ving'amuzi, na hata zikipatikana baadhi zinakuwa hazina sauti. Shame on you!
 
kaka unaponiambia 'dish' nakumbuka nilivyokuwa naogeshwa na mama enzi hizo.fafanua kama wewe ni mtumishi wa TCRA.
Dish lipi?mbona mlituambia king'amuzi ?tuwe serious katika hili!

Uwe serious bwana acha u.se.nge!
 
Mimi nazipata zoote zinazorushwa kwa sattelite tena vizuri bila chenga. Nunua sattelite dish utapata channel mpaka utakimbia halafu asilimia kubwa kama sio zote za sattelite ni Digital. Mimi nnakauelewa ka kuyarekebisha hayo madish kwa msaada tuwasiliane kwa namba 0767-387560

Hili tangazo lako unatakiwa ulipie.
 
ITV na Star tv unazipata?

TBC1, STAR TV, ITV, EATV, CHANEL 10 chanel hizi zinapatikana bure kwenye kingambuzi cha star times nina zaidi ya mwezi sijalipia na nazipata
 
Ni aibu kwa TCRA. Nchi hii bora liende! Local channels hazipatikani kwenye ving'amuzi, na hata zikipatikana baadhi zinakuwa hazina sauti. Shame on you!

hivi TCRA wakufundishe mpaka namna ya kutune sauti kwenye kingambuzi? Kwenye rimoti kuna batani imeandikwa track hapo utamaliza tatizo la sauti,
 
kweli shibe mwana malevya!
Sina hakika kama uliwaelewa TCRA au unafanya makusudi kwa kuwa umelamba kibahasha.
Imagine mimi nitanunua ving'amuzi vitatu halafu kuna babu yangu pale kisarawe,kuna baba mdogo,wajomba n.k

hili zigo la gharama litanirudia mimi tu na bado uhuru wa habari utakuwa umeminywa!

Pasco fikra zako ni za ki TCRA au kimasaki masaki hivi!
Mkuu Meni', hivi si nimekujibu hivi?!,
Mkuu uko nchi gani wewe?, yaani matangazo yote yale yaliyotolewa na TCRA wewe bado hujaelewa!.
King'amuzi ni kimoja tuu utaona TV zote tano za "free to air" bure!.

Ukishanunua king'amuzi chochote, hizo TV tano za bure utaziona bila kulazimika kuzilipia na zitaonekana kwenye ving'amuzi vyote vitatu, hivyo uko huru kuchagua kununua kingamuzi chochote kati ya hivyo!.
Pasco.

Hii inamaanisha Kinga'amuzi kimoja tuu kinatosha!, na kwa ajili ya zile stesheni 5 basic ni bure!, zaidi ya hapo ni starehe!, starehe gharama!. Hivyo ving'amuzi vyako vitatu vya nini?, mimi nilijua hilo lalo ni jina tuu, kumbe ni kweli wewe una ...!. Tukija hili suala la bahasha, hii ndio kazi yangu inaendana na pakee ya bahasha, kama chef anavyoonjea jikoni, au mbuzi anayekula kwa urefu wa kamba yake!.

P.
 
Naangalia ITV na EATV zooote hazina sauti SHAME ON THEM sijui ni hujuma kwa IPPMEDIA kutoka kwa hawa TBC??? Maana Startime ni wadau wao?

Mkuu hii inarekebishika,kwenye remote ya Startimes juu karibia na kiwashio kuna button imeandikwa track ukishabonyeza nenda option ya pili(sikumbuki inaitwaje) chagua stereo alafu enter uone,ikikataa rudi tena jaribu right ikigoma jaribu center kama sikosei itatoa sauti tu.
 
TBC1, STAR TV, ITV, EATV, CHANEL 10 chanel hizi zinapatikana bure kwenye kingambuzi cha star times nina zaidi ya mwezi sijalipia na nazipata

kwa hiyo king'amuzi cha kununua ni star times!
Kwa hiyo lile dudu linaloitwa king'amuzi =star times?nielimisheni jamani!
 
Poleni sana wadau wenye tv...mi radio yangu mkulima aaah sina shida nasikiliza tu habari nimerudi enzi za mwalimu
 
Du misamiati imekuwa mingi, hizo red red nayo ndiyo mdudu gani? Mnatuchanginyi!

Kwa mujibu wa Baraza la Kiswahjili la Taifa (BAKITA) kisimbuzi ndiyo kiswahili sahihi kwa 'Decorder'. King'amuzi ni kiswahili sahihi kwa 'detector'
 
Pasco ,
heri ya mwaka mpya na HEKO sana kwa kutoa darsa kwenye hii mada........
Kama Serikali imeamua/imetamka kuwa local channel ziko tano (in my opinion huu ni ubabe kwa zile private TV Stations)....basi upatikanaji wa hizo local channels uwe across the board kupitia ving'amuzi vyote kwa wanaotoa service ya Television nchini kwetu.....with no exception........period
 
Last edited by a moderator:
Kwa TCRA

Kwanini gharama za simu Tanzania ziko juu sana kulinganisha na majirani zetu e.g Kenya

kwa mfano nikitaka kupiga simu nyumbani inanigharimu dola senti 18 hadi 40 kwa dakika......wakati nikipiga simu kenya inanigharimu dola senti 6 mpaka 10 kwa dakika.......
 
Haya yote tulipaswa kuyajadili kabla analogy haijazimwa.

mkuu yalijadiliwa hadi bungeni !sio mageni haya!
Nilivyowaelewa TCRA ni kwamba ifikapo jana kila mwenye TV apaswa kuwa na king'amuzi ili aweze kupata matangazo ya runingani.tena wakatufariji kuwa hakuna haja ya kutupa tv zetu na matangazo kutoka channel za nyumbani yatakuwa bure!na ving'amuzu vikaanza kushushwa bei!

Hivi kwa nini mnapenda kuwafanya watanzania ni mbumbumbu?

Message ya TCRA ilikuwa nunua king'amuzi utaziona hizo channel za nyumbani bure,kamwe sikusikia kuwa nunua 'dish' au 'king'amuzi cha star times' ili upate hizi local channels !

Juzi tulisikia ITV na Star Tv wanakuja na vinga'amuzi vyao....

Hapa nilipo nina Kinga'muzi cha zuku hakina ITV na star tv...ina maana ni suppliment kwa star times.

Mjadala ni mmoja tu ambao mpaka sasa sijaona aliyejibu....je mtanzania wa kisarawe anunue kinga'muzi gani aweze kujipatia habari 'bure' tena kutoka kwenye hizi local channels?

Kama hili 'dili' ni la star times tuwekane wazi.

Hivi ofisi za serikali zitatumia kinga'muzi gani....labda nirahisishe swali kwa namna hii.
 
Back
Top Bottom