TCRA, Tunaomba ufafanuzi

TCRA, Tunaomba ufafanuzi

Dstv naona local channel moja tu yaani TBC, zingine sioni na wala sijawahi ona hata siku moja, please anayejua namna ya kufanya hata nione Star TV tu. Msaada please

Mkuu DSTV bana haipo kwenye michakato ya TCRA, utaishia kuiona TBC tu
 
me mbona nina cha startimes na local chaneli zote tano nazipata though bado nasubiri vingine nihame.elfu kumi na nane then chaneli zenyewe za kizushi tu.kwa anayetumia zuku anaweza tupa data zake?

Elfu kumi na nane za nini? tumeambiwa local channels zitakuwa za bure.....upuuzi mtupu! najiandaa kuandamana peke yangu, wanatangaza kuwa king'amuzi kinauzwa 39,000/= ukifika pale unaambiwa ni sh. 62,000/= nimeenda kufunga kimegoma wameniambia ninunue antena yao!!!????
 
Mkuu DSTV bana haipo kwenye michakato ya TCRA, utaishia kuiona TBC tu

Kwa sheria, walitakiwa waoneshe local channels zote - free. DSVT ni scandal mwanzo mwisho.

Na hii switch-over imeenda vibaya sana, na naona ni failure ya Wizara na TCRA kutofanya maandalizi ya kutosha ili kuhakikisha local channels zinapatikana.
 
Kwa sheria, walitakiwa waoneshe local channels zote - free. DSVT ni scandal mwanzo mwisho.

Na hii switch-over imeenda vibaya sana, na naona ni failure ya Wizara na TCRA kutofanya maandalizi ya kutosha ili kuhakikisha local channels zinapatikana.

Ofkoz nakubaliana na wewe kuhusu DSTV walitakiwa kuingia kwenye mipango ya TCRA. lakini hili neno free nalo ni tata.
lakini pia unaposema hii ni failure ya wizara na TCRA inabidi utoe ufafanuzi kuntu mkuu FJM
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Awali tulielezwa kuwa tv zitakazoathirika kwa kutokuonyesha ni zile za analogy ambazo ndiyo zitahitaji visimbuzi! Sasa inaonekana kila mtu amekuwa affected na inafanywa bihashara. Hivi nchi zingine waliotutangulia nazo unahjitaji visimbuzi kuona channel ambazo si za kulipiwa? zaidi kwa nini mtu ununue visimbuzi vinavyoonyesha vituo vya ajabu usivyotaka kuangalia ilimradi tu upate TBC na Channel ten?
 
kwani ni lazima sana muangalie TV? Hamna shughuli zingine za kufanya?

umetoka baaa sio mda mrefu wewe,sio kosa lako,hata humu jamvini sio mahali panapokufaa.HABARI,MATANGAZO, NA BURUDANI UTAZIPATA WAPI?
 
Natumia Startimes; nipo mby city; naona local channel zote 5; ITV, STARTV, EATV, TBC & CHANNEL 10. Ila nitahama vikija ving'amuzi ambayo package zake zina ridhisha, coz ktk startimes kifurushi cha bei rahisi (9,000) channel za ziada nyingi hazina mvuto sana!
 
Siyo viwili ila tegemea sebule nzima, am tired!Hivi hawa jamaa TCRA si wao ndo wangeuza hivyo ving'amuzi na sisi tukawafuatehao jamaa wengine ili tulipie hizo chanel zingine za movie?Yaani ni usumufu kweli
Kwa mwendo huu wa hawa TCRA tutajikuta tuna ving'amuzi zaidi ya viwili kupata local Channels..... Gharama zaidi kwa mwananchi....
 
Natumia Startimes; nipo mby city; naona local channel zote 5; ITV, STARTV, EATV, TBC & CHANNEL 10. Ila nitahama vikija ving'amuzi ambayo package zake zina ridhisha, coz ktk startimes kifurushi cha bei rahisi (9,000) channel za ziada nyingi hazina mvuto sana!

Itv na eatv zina sauti?
 
Siyo viwili ila tegemea sebule nzima, am tired!Hivi hawa jamaa TCRA si wao ndo wangeuza hivyo ving'amuzi na sisi tukawafuatehao jamaa wengine ili tulipie hizo chanel zingine za movie?Yaani ni usumufu kweli

acha uvivu. inaonyesha hukuwa unafuatilia matangazo ya tcra. changamoto zipo lakini baadhi yetu hatupendi mabadiliko.
 
Naona usanii unaendelea kulitafuna taifa!kwa waelewa wa mambo tumeshanusa harufu chafu ya ufisadi ndani ya TCRA.nisiseme mengi bali nijikite kwenye swali langu au letu!

Ili niweze kuona local channels zote ninunue king'amuzi kipi?

This is a very serious question from the common mwananchi.
Mkuu uko nchi gani wewe?, yaani matangazo yote yale yaliyotolewa na TCRA wewe bado hujaelewa!.
King'amuzi ni kimoja tuu utaona TV zote tano za "free to air" bure!.

Mpaka sasa kuna makampuni matatu ya kurusha matangazo, Star Media, Agape Associets "ting" na kampuni ya Mengi na Dialo ambayo king'amuzi chao bado hakijaingia sokoni, ila kimeanza kutangazwa!.

Ukishanunua king'amuzi chochote, hizo TV tano za bure utaziona bila kulazimika kuzilipia na zitaonekana kwenye ving'amuzi vyote vitatu, hivyo uko huru kuchagua kununua kingamuzi chochote kati ya hivyo!.

Mfano kingamuzi cha Star media hawana chanel ya movie ya HBO, kama wewe ni mpenzi wa HBO, huna jinsi, lazima ununue king'amuzi cha Agape!. Huko pia utaziona bute zile tv tano za bure!.

By choice, kama unataka usipitwe kitu, na unapenda mambo mazuri yote, then utavinu nua ving'amuzi vyote vitatu?.

Mimi nilianza na kingamuzi cha Easy TV, nikaja cha DSTV, Sasa ninacho cha Star Media, my boys wanapenda movies za HBO hivyo soon nitanunua cha Agape!.

Wengi wa Wakazi wa Dar, tunapenda zaidi starehe kuliko kuzijali familia zetu!, mimi nakunywa Sinza, kuna bar 250 na zote zinajaa, kwa nini tushindwa kulipia king'amuzi elfu 10 kwa mwezi?!.
Heri ya Mwaka Mpya.
Pasco.
 
Wakuu dunia ya leo hakuna kitu inaitwa bure tena, huku nchi za dunia ya tatu ndio tunaona mambo haya maajabu na hii inatokana na kulemazwa na mfumo wa kizamani wa bure bure
Labda tuangalie mfumo wa urushaji matangazo kwenye mfumo huu wa dijitali ili tuelewane
Zamani mtu yeyeto anaweza kuanzisha tv station yake labda akaiita miningits tv akawa anafanya vipindi vyake na kwa mfumo wa analojia maana yake alikuwa anaweka dish lake na kurusha na wenye tv zao za analogi wanadaka na kuendelea na maisha
mfumo wa dijitali umekuja kivingine maana sasa meningits tv atahitaji mtambo mkubwa wa kurusha matangazo kwa digitali kitu ambacho ni kigumu kwake
kinachofuatia ni watatokea watu wenye uwezo wa kurusha matangazo kwa dijitali na watakuwa wanakusanya tv station kadhaa za nje na ndani na kuziweka kwenye ving'amuzi vyao kisha kivirusha kidijitali na hii hufanyika kwa makubaliano ya kibiashara zaidi, hapa inabidi meningits tv aende kwa hawa jamaa ajiunge nao wamrushie matangazo yake

Hadi sasa tuna Ting, Startimes, Zuku na Easytv kama sijakosea, hawa ndio wanarusha matangazo kidijitali kupita vingamuzi vya fta na setelaiti

sasa wenye tv stations wanayo haki ya kuchagua kufanya kazi na nani kati ya wenye ving'amuzi hawa kulingana na offer zao, lakini ikaibuka hoja inamaana mtu atalazimika kununua ving'amuzi vingapi kuona local channel mbalimbali?
hapo sasa TCRA ikaja na ubabe kwa manufaa ya mwananchi kwa kuwalazimisha wenye tv stations 5 walizoita za kitaifa kuingia mikataba na wenye ving'amuzi wote.
Wakatoa agizo kwamba lazima ITV, EAT, STARTV, TBC na CHANNEL10 ziingie mikataba na wenye ving'amuzi wote na pia ikatoa amri wenye ving'amuzi warushe chaneli hizo tano bure hata kama muda wa package ya kawaida ukiisha basi chaneli hizi ziendelee kuonekana

Hadi hivi sasa kampuni zote zinarusha chaneli hizo tano lakini bado hawajaafikiana vizuri kibiashara kwasababu ya ulazima waliopewa na TCRA
Sasa hizi tv station zingine kama DTV, clouds nk wanalazimika kutafuta kampuni moja ya kufanya nayo kazi au kama wakiweza basi wataingia mkataba hata na kampuni zaidi ya moja, kwataarifa nilizo nazo Clouds tv wameshindwana na Startimes na wamekwenda Zuku

Kama hutaki usumbufu wa kulipia kwa mwezi walau kwa muda huu wakati bado tupo ugenini kwa dijitali basi unaweza kufunga dish la free chanel na utaweza kuona baadhi ya stations zinazorusha matangazo kwa setelaiti....na hii ni kwa muda tu maana biashara ikichanganya watazitoa na utalazimika kuziangalia kupitia ving'amuzi

Kwa kuongezea tu,sio kwamba clouds wameshindwa kukubalina na star times bali star times walikuwa wanarusha matangazo ya clouds kwa mfumo wa analogia

Zuku wanalocal channesls 3 channel ten,tbc1 na clouds tv,bwana mengi kakataa kurusha matangazo yake kupitia zuku kwa sababu ambazo nasikia ni zaidi ya sababu za kibiashara japo kuna taarifa kwamba na yeye king'amuzi chake pamoja na bakresa viko kwenye pipeline kuingia sokoni.
 
Mkuu uko nchi gani wewe?, yaani matangazo yote yale yaliyotolewa na TCRA wewe bado hujaelewa!.
King'amuzi ni kimoja tuu utaona TV zote tano za "free to air" bure!.

Mpaka sasa kuna makampuni matatu ya kurusha matangazo, Star Media, Agape Associets "ting" na kampuni ya Mengi na Dialo ambayo king'amuzi chao bado hakijaingia sokoni, ila kimeanza kutangazwa!.

Ukishanunua king'amuzi chochote, hizo TV tano za bure utaziona bila kulazimika kuzilipia na zitaonekana kwenye ving'amuzi vyote vitatu, hivyo uko huru kuchagua kununua kingamuzi chochote kati ya hivyo!.

Mfano kingamuzi cha Star media hawana chanel ya movie ya HBO, kama wewe ni mpenzi wa HBO, huna jinsi, lazima ununue king'amuzi cha Agape!. Huko pia utaziona bute zile tv tano za bure!.

By choice, kama unataka usipitwe kitu, na unapenda mambo mazuri yote, then utavinu nua ving'amuzi vyote vitatu?.

Mimi nilianza na kingamuzi cha Easy TV, nikaja cha DSTV, Sasa ninacho cha Star Media, my boys wanapenda movies za HBO hivyo soon nitanunua cha Agape!.

Wengi wa Wakazi wa Dar, tunapenda zaidi starehe kuliko kuzijali familia zetu!, mimi nakunywa Sinza, kuna bar 250 na zote zinajaa, kwa nini tushindwa kulipia king'amuzi elfu 10 kwa mwezi?!.
Heri ya Mwaka Mpya.
Pasco.

Mkuu nashukuru kwa ufafanuzi,vipi kuhusu Dstv wataonyesha hizi 5 local channels?
 
Mkuu nashukuru kwa ufafanuzi,vipi kuhusu Dstv wataonyesha hizi 5 local channels?
Mkuu Namungula Jr, DSTV ni foreign channel, iko Africa ya Kusini, hii itaonyesha TBC tuu, tena hiyo TBC iliingia enzi za Tido, sijui kama itadumu!. Hizo TV tano za bure zinaweza kujiunga na DSTV ila kiukweli, kama kujiunga Star media ni issue, DSTV itakuwa ndio kabisa hawawezi kuigusa!.

Kwa mujibu wa matangazo ya ITV, king'amuzi chao kitakuwa kama cha DSTV, ni cha Digital signal, na picha ni za HD, hiki kingamuzi cha Star Media, kinapokea matangazo ya analojia na kuyarisha yakiwa hivyo hivyo analojia ila katika mfumo wa digitali.

Heri ya Mwaka Mpya!
Pasco
 
bongo mna kazi kweri kweri kudadadadeki kwa hiyo jana wengi wenu bila bila tv bwahahahaaha
 
itv na star tv unazipata?

binafsi naipata star tv kupitia king'amuzi cha startimes. Itv sijaiona, pengine pia ipo! Kwa mtizamo wangu swala hili limekaa kibiashara zaidi kuliko kuboresha huduma kama ambavyo tcra wamekuwa wakihutubia. Walisema katika mfumo wa digitali huhitaji kuzungusha zungusha antenna ili uone picha nzuri lakini kwa upande wangu bado nahitaji kuzungusha-zungusha antenna ili kupata vizur baadhi ya channels. Moreover, quality ya picha bado iko kama ilivyokuwa zamani. Kwa kifupi so far bado sijaona tofauti ya hii change (analogy-digital) zaidi ya usumbufu!
 
Awali tulielezwa kuwa tv zitakazoathirika kwa kutokuonyesha ni zile za analogy ambazo ndiyo zitahitaji visimbuzi! Sasa inaonekana kila mtu amekuwa affected na inafanywa bihashara. Hivi nchi zingine waliotutangulia nazo unahjitaji visimbuzi kuona channel ambazo si za kulipiwa? zaidi kwa nini mtu ununue visimbuzi vinavyoonyesha vituo vya ajabu usivyotaka kuangalia ilimradi tu upate TBC na Channel ten?

Du misamiati imekuwa mingi, hizo red red nayo ndiyo mdudu gani? Mnatuchanginyi!
 
Back
Top Bottom