TCRA, Tunaomba ufafanuzi

TCRA, Tunaomba ufafanuzi

Je hao TCRA wakiongeza muda ndio kila mtu atakuwa na uwezo wa kununua ving'amuzi wacha wafunga hiyo analog sababu dunia nzima itakuwa mwisho 2015 na afadhali wameanza sasa kila mtu atatkumbuka kuliko wasubiri hadi 2015 kwa sisi waaafrika hatufanyi mambo kwa hiari yetu hadi tushikiwe bakora,hata kusajiri simu ni hivyo hivyo,heri lawama lakini utekeleze kuliko kumchekea nyani shambani utakuta mabua
 
TCRA inatumia mwanya huu kuwarangua wananchi pasipo sababu kwa vile wananchi hawajaelewa vema kuhusu elimu ya DIGITAL.

Wanakumbatia biashara hii kwa wale waliowapa leseni kuuza ving'amuzi kwa masharti ya kupata faida kubwa. pasipo kutoa elimu sahihi kwa wananchi.

1. Kutotoa maelezo sahihi kuhusu wenye flat screen zilizotengenezwa kuanzia 2006 zina ving'amuzi tayari built in digital search, kwa hiyo ni kufunga cable na tv antenna aliyonayo au chadema antenna au hata home made antenna lakini wao wamenyamaza kimya ili biashara iendelee. hivyo wengi wanaamini antenna zingine haziwezi kufanya kazi.

2.Wanarangua wanachi kwa ving'amuzi vya contract Decoder. SI LAZIMA kingamuzi kiwe na decoder. kuna ving'amuzi vingi dunia USA UK SA ambako vingamuzi ni kibox kidogo chenye remote ambacho ni dola $10 hadi $20 viko madukani ni uchaguzi wako tu ukitaka contract unaenda kwa provider ukapate package pamoja na local tv. Lakin kama unataka Local unaenda maduka ya electronics na kununua king'amuzi pasipo decoder.

TCRA ruhusu watu welete vingamuzi rahisi toka nje kwa bei nafuu, mimi nina kidogo cha $10 mbona kinafanya kazi?

:wof:
 
dah sijaelewa kumbe decoda na king'amuzi ni vitu viwili tofauti? Vipi kuhusu receiver
 
Edit heading yako kwanza! Ulisoma kabla ya kupost? "Wanawatia hasa"?
 
Back
Top Bottom