TCRA, Tunaomba ufafanuzi

TCRA, Tunaomba ufafanuzi

Siyo viwili ila tegemea sebule nzima, am tired!Hivi hawa jamaa TCRA si wao ndo wangeuza hivyo ving'amuzi na sisi tukawafuatehao jamaa wengine ili tulipie hizo chanel zingine za movie?Yaani ni usumufu kweli

Inakera sana mkuu.. Ndio maana post yangu nilisema ZAIDI ya viwili.....
 
  • Thanks
Reactions: bdo
Nunua vyote, yaani cha TBC-Start time, ITV -kama anacho, Nasikia wa Mwanzan nae anachake, na Zuku
Naona usanii unaendelea kulitafuna taifa!kwa waelewa wa mambo tumeshanusa harufu chafu ya ufisadi ndani ya TCRA.nisiseme mengi bali nijikite kwenye swali langu au letu!

Ili niweze kuona local channels zote ninunue king'amuzi kipi?

This is a very serious question from the common mwananchi.
 
ITV wameshaanza kutangaza kishumbuzi chao naona sebule zetu zitajaa vishumbuzi
 
Kwa mwendo huu wa hawa TCRA tutajikuta tuna ving'amuzi zaidi ya viwili kupata local Channels..... Gharama zaidi kwa mwananchi....

Itakuwa kama line za simu..Utatakiwa uwe anamiliki kingamuzi cha Star times kupata TBC, Basics kupta ITV, DCTV for Super Sports, TIN kupata ATN..... huu itakuwa ujinga. We need to have all Local Channels hata kwenye DSTV for free..otherwise itakuwa vurugu kwenye soko la ving'amuzi
 
Itakuwa kama line za simu..Utatakiwa uwe anamiliki kingamuzi cha Star times kupata TBC, Basics kupta ITV, DCTV for Super Sports, TIN kupata ATN..... huu itakuwa ujinga. We need to have all Local Channels hata kwenye DSTV for free..otherwise itakuwa vurugu kwenye soko la ving'amuzi

Well said Mkuu.... Ngoja tusubiri tuone hili varangati litaishia wapi.....
 
Mkuu Namungula Jr, DSTV ni foreign channel, iko Africa ya Kusini, hii itaonyesha TBC tuu, tena hiyo TBC iliingia enzi za Tido, sijui kama itadumu!. Hizo TV tano za bure zinaweza kujiunga na DSTV ila kiukweli, kama kujiunga Star media ni issue, DSTV itakuwa ndio kabisa hawawezi kuigusa!.

Kwa mujibu wa matangazo ya ITV, king'amuzi chao kitakuwa kama cha DSTV, ni cha Digital signal, na picha ni za HD, hiki kingamuzi cha Star Media, kinapokea matangazo ya analojia na kuyarisha yakiwa hivyo hivyo analojia ila katika mfumo wa digitali.

Heri ya Mwaka Mpya!
Pasco


Mkuu Pasco,

Pamoja na kwamba DStv ni kampuni ya kigeni, lakini naamini kwamba hao DSTV kwa hapa nchini wanafanya shughuli zao kwa sheria za hapa Bongo, na sio za South Africa, na pia wamepewa leseni kuendesha biashara zao na hawa hawa TCRA. Kama ilivyo kwa makampuni mengine yanayouza ving'amuzi (Startimes, Ting etc) ambayo na yenyewe yanasimamiwa na TCRA, hivyo hivyo na DSTv wanatakiwa na wenyewe waweke hizo channeli tano za kitaifa kwenye Ving'amuzi vyao. Hapa ndo wakati TCRA inatakiwa iweze kuonyesha meno yake na kuwasaidia wananchi.

Inavyoonekana hapa DSTv ni kama vile anaogopwa na Serikali yetu (TCRA), kwanza hawa jamaa bado wanachaji huduma zao kkwa kutumia US $ (japo suala hili limepigiwa sana kelele na wadau wengi, lakini hakuna utekelezaji wowote), leo hii tena tumeingia kwenye digitali wanaonyesha local channel moja TBC, ambayo na yenyewe kuiona ni mpaka ulipe - hii sio bure.

Ushauri kwa TCRA: Weka hawa wauza ving'amuzi na warusha matangazo ya dijitali (Startimes, DStv etc ) kwenye kapu moja (acheni uoga) na wote waonyeshe hizo local channels 5 za kitaifa - asiyetaka afunge virago arudi kwao - kuweni na msimamo ili muweze kuwasaidia wananchi wenu.
 
Mkuu uko nchi gani wewe?, yaani matangazo yote yale yaliyotolewa na TCRA wewe bado hujaelewa!.
King'amuzi ni kimoja tuu utaona TV zote tano za "free to air" bure!.

Mpaka sasa kuna makampuni matatu ya kurusha matangazo, Star Media, Agape Associets "ting" na kampuni ya Mengi na Dialo ambayo king'amuzi chao bado hakijaingia sokoni, ila kimeanza kutangazwa!.

Ukishanunua king'amuzi chochote, hizo TV tano za bure utaziona bila kulazimika kuzilipia na zitaonekana kwenye ving'amuzi vyote vitatu, hivyo uko huru kuchagua kununua kingamuzi chochote kati ya hivyo!.

Mfano kingamuzi cha Star media hawana chanel ya movie ya HBO, kama wewe ni mpenzi wa HBO, huna jinsi, lazima ununue king'amuzi cha Agape!. Huko pia utaziona bute zile tv tano za bure!.

By choice, kama unataka usipitwe kitu, na unapenda mambo mazuri yote, then utavinu nua ving'amuzi vyote vitatu?.

Mimi nilianza na kingamuzi cha Easy TV, nikaja cha DSTV, Sasa ninacho cha Star Media, my boys wanapenda movies za HBO hivyo soon nitanunua cha Agape!.

Wengi wa Wakazi wa Dar, tunapenda zaidi starehe kuliko kuzijali familia zetu!, mimi nakunywa Sinza, kuna bar 250 na zote zinajaa, kwa nini tushindwa kulipia king'amuzi elfu 10 kwa mwezi?!.
Heri ya Mwaka Mpya.
Pasco.

Pasco hayo makampuni uliyoyataja sio yote,mpaka sasa najua kuna hao Star-times,ting,zuku na mengine.Sio kweli kuwa hizo zote zimetimiza hiyo requirement ya five local channels.Labda star times tu ambao naona kama vile ndo wanapigiwa upatu na serikali.

Kinacholalamikiwa ni hiki,kwanini serikali haiwabani hawa warusha mtatangazo wawe na hizo free 5 local channel kwenye packages zao?Iliweka hili kama sheria mojawapo ya kupewa leseni ya usambazaji na ikapiga mkwara kuwa bila kutimiza hili takwa mpaka january mosi basi kampuni husika inanyang'anywa leseni.

Sasa mbona hili halijatekelezwa na yenyewe ipo kimya tu na badala yake imejikita tu kuwambia wananchi wasitupe tv zao za migongo kitu ambacho kilishaeleweka?(Raisi pia amelirudia hili la migongo juzi kwenye hotuba yake!)

Mi naona serikali inafanya makusudi tu ili watu wao star times waonekane wana local channels nyingi kuliko wengine na wafanye biashara wao kwanza!Lakini wakumbuke kuwa tupo wananchi ambao hatujaichagua star times nasi tunapenda tuone hizo local channel 5 huku tulipo na ni sheria hiyo ndiyo iliyotupa choice ya kuwa na king'amuzi chochote tunachopenda.Otherwise wangetangaza kuanzia mwanzo kuwa tununue star times kwani wao pekee ndo watakuwa na hizo local channels.

CC😡Selemani
 
Mkuu Pasco,

Pamoja na kwamba DStv ni kampuni ya kigeni, lakini naamini kwamba hao DSTV kwa hapa nchini wanafanya shughuli zao kwa sheria za hapa Bongo, na sio za South Africa, na pia wamepewa leseni kuendesha biashara zao na hawa hawa TCRA. Kama ilivyo kwa makampuni mengine yanayouza ving'amuzi (Startimes, Ting etc) ambayo na yenyewe yanasimamiwa na TCRA, hivyo hivyo na DSTv wanatakiwa na wenyewe waweke hizo channeli tano za kitaifa kwenye Ving'amuzi vyao. Hapa ndo wakati TCRA inatakiwa iweze kuonyesha meno yake na kuwasaidia wananchi.

Inavyoonekana hapa DSTv ni kama vile anaogopwa na Serikali yetu (TCRA), kwanza hawa jamaa bado wanachaji huduma zao kkwa kutumia US $ (japo suala hili limepigiwa sana kelele na wadau wengi, lakini hakuna utekelezaji wowote), leo hii tena tumeingia kwenye digitali wanaonyesha local channel moja TBC, ambayo na yenyewe kuiona ni mpaka ulipe - hii sio bure.

Ushauri kwa TCRA: Weka hawa wauza ving'amuzi na warusha matangazo ya dijitali (Startimes, DStv etc ) kwenye kapu moja (acheni uoga) na wote waonyeshe hizo local channels 5 za kitaifa - asiyetaka afunge virago arudi kwao - kuweni na msimamo ili muweze kuwasaidia wananchi wenu.
Mkuu Ishina, DSTV, ZUKU, Easy TV na wengine watakaokuja hawana vibali vya TCRA ku distribute local contents, the official distributer wanaitwa multiplex operators wako 3. Vituo vya TV vinabaki kuwa content provider hata sisi jf tukiamua kuwa na channel yetu, tunafungua JF TV!.

DSTV wana service licence only lakini hawaruhusiwi kupokea local contents, hata vipindi kama Wanawake live, na lots of Bingo movies kwenye DSTV Swahili, zinarushwa kutokea Afrika Kusini!. Hata hiyo TBC yenyewe kwenye DSTV, iko beamed kwa nchi za Afrika Mashariki tuu, hata ukiwa South Africa, TBC haionekani!.

Hapo ilipo hata hilo la kuonyesha 5 channels bure ni ubabe tosha!, channel ya bure ilipaswa iwe moja tuu, TBC ambayo tunailipia kwa kodi zetu, nyingine zote tulipaswa kulipia!. Kwa msio fahamu TV kama CNN, BBC, Al Jazeera na nyingine za wenzetu zilikwenda digital kitambo kidogo, ukiwa ulaya kuna ma chanell ya CNN kibao suprising, hii tunayoiona huku kwetu kule haionekani!, wakati fulani nikiwa huko ndipo nililiona Tangazo la utalii la Tanzania kwenye CCN masikini Afrika hatulioni!.

Kitendo cha kuilazimisha DSTV ionyeshe hizo chanell tano za bure, ni sawa na kuilazimisha CNN itangaze matangazo ya TBC!. Kwanza huko DSTV hakuna hata chanel moja ya bure, kule inaongea pesa tuu!, na ili kuona mechi zote, lazima kila mwezi ulipie zaidi ya laki!, kama hizi za kulipia elfu 10 kwa mwezi watu wanapiga kelele, DSTV tutaigusa?.

Pasco.
 
Pasco hayo makampuni uliyoyataja sio yote,mpaka sasa najua kuna hao Star-times,ting,zuku na mengine.Sio kweli kuwa hizo zote zimetimiza hiyo requirement ya five local channels.Labda star times tu ambao naona kama vile ndo wanapigiwa upatu na serikali.

Kinacholalamikiwa ni hiki,kwanini serikali haiwabani hawa warusha mtatangazo wawe na hizo free 5 local channel kwenye packages zao?Iliweka hili kama sheria mojawapo ya kupewa leseni ya usambazaji na ikapiga mkwara kuwa bila kutimiza hili takwa mpaka january mosi basi kampuni husika inanyang'anywa leseni.

Sasa mbona hili halijatekelezwa na yenyewe ipo kimya tu na badala yake imejikita tu kuwambia wananchi wasitupe tv zao za migongo kitu ambacho kilishaeleweka?(Raisi pia amelirudia hili la migongo juzi kwenye hotuba yake!)

Mi naona serikali inafanya makusudi tu ili watu wao star times waonekane wana local channels nyingi kuliko wengine na wafanye biashara wao kwanza!Lakini wakumbuke kuwa tupo wananchi ambao hatujaichagua star times nasi tunapenda tuone hizo local channel 5 huku tulipo na ni sheria hiyo ndiyo iliyotupa choice ya kuwa na king'amuzi chochote tunachopenda.Otherwise wangetangaza kuanzia mwanzo kuwa tununue star times kwani wao pekee ndo watakuwa na hizo local channels.

CC😡Selemani
Soma post yangu #49
 
Natumia Startimes; nipo mby city; naona local channel zote 5; ITV, STARTV, EATV, TBC & CHANNEL 10. Ila nitahama vikija ving'amuzi ambayo package zake zina ridhisha, coz ktk startimes kifurushi cha bei rahisi (9,000) channel za ziada nyingi hazina mvuto sana!

mbona DTV,C2C,CAPITAL,ATN , CTN na TRENEET hakuna inamaana nazo cyo local channel
 
Mkuu uko nchi gani wewe?, yaani matangazo yote yale yaliyotolewa na TCRA wewe bado hujaelewa!.
King'amuzi ni kimoja tuu utaona TV zote tano za "free to air" bure!.

Mpaka sasa kuna makampuni matatu ya kurusha matangazo, Star Media, Agape Associets "ting" na kampuni ya Mengi na Dialo ambayo king'amuzi chao bado hakijaingia sokoni, ila kimeanza kutangazwa!.

Ukishanunua king'amuzi chochote, hizo TV tano za bure utaziona bila kulazimika kuzilipia na zitaonekana kwenye ving'amuzi vyote vitatu, hivyo uko huru kuchagua kununua kingamuzi chochote kati ya hivyo!.

Mfano kingamuzi cha Star media hawana chanel ya movie ya HBO, kama wewe ni mpenzi wa HBO, huna jinsi, lazima ununue king'amuzi cha Agape!. Huko pia utaziona bute zile tv tano za bure!.

By choice, kama unataka usipitwe kitu, na unapenda mambo mazuri yote, then utavinu nua ving'amuzi vyote vitatu?.

Mimi nilianza na kingamuzi cha Easy TV, nikaja cha DSTV, Sasa ninacho cha Star Media, my boys wanapenda movies za HBO hivyo soon nitanunua cha Agape!.

Wengi wa Wakazi wa Dar, tunapenda zaidi starehe kuliko kuzijali familia zetu!, mimi nakunywa Sinza, kuna bar 250 na zote zinajaa, kwa nini tushindwa kulipia king'amuzi elfu 10 kwa mwezi?!.
Heri ya Mwaka Mpya.
Pasco.

tutake radhi kwa kauli yako chafu kama unapesa niwewe cyo kuwakejeri wenzako
 
Kuna jinsi ya kurejesha sauti mkuu, bonyeza track kwenye remote yako then click audio track utapewa option 3 select right. kwangu ilisaidia jaribu na wewe. Tatizo lao kubwa ni signal.:rofl:
 
Sioni tofauti ya analoji na dijitali. Picha bado ni zile zile yaani "poor quality".
 
tutake radhi kwa kauli yako chafu kama unapesa niwewe cyo kuwakejeri wenzako
Mkuu Jipu, kuhusu pesa kiukweli ninazo, mimi nalipwa elfu 20,000 kila siku, (zile bahasha zetu huwa zinawekwa 20,000), hivyo kwa wiki natengeneza Sh. 100,000 kwa mwezi natengeneza 400,000?= hizi ni pesa nyingi sana kwa mwandishi wa habari, kwa kifupi kwa fedha hizo, mimi ni miongoni mwa waandishi wa habari matajiri sana, hata nyumba ninayokaa, nimepanga vyumba vitatu!, yaani jiko, chumba na sebule!, usafiri niliokuwa nikiutumia sikuzote ilikuwa ni bodaboda, lakini sasa nimeweza hata kubadili usafiri kutoka boda boda sasa natumia bajaj!.

Huko Sinza tunakokunywa kwenye hizo baa 250, wengi wetu tunakunywa huko kutokana na uwezo, mfano mimi ningependa sana niwe nakunywa Samaki Samaki pale Mlimani City, ila bei yao iko juu, na mimi uwezo wangu ni wa kunywa bia moja kila siku, na siku ya mwisho wa mwezi, huweza hata kuywa bia 3!, hivyo nikijinyima tuu bia 4 kwa mwezi, pesa hiyo inatosha kulipia king'amuzi!.

Siombi msamaha kuwasisitiza kuwa kuna watu wanapenda zaidi kuendekeza starehe kuliko kuzijali familia zao!. Hakuna TV inayouzwa chini ya laki!, kama uliweza kununua TV zaidi ya laki, utashindwaje kununua kingamuzi elfu 30?!.
Kwani wewe "ile starehe" huwa unailipia sh, ngapi?, au unalipwa Sh. ngapi?!. Nunueni vingamuzi, tuko katika ulimwengu wa digitali, lazima na sisi tubadilike tuishi kidigitali!.
P.
 
Kweli taifa hili majanga matupu

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
tutake radhi kwa kauli yako chafu kama unapesa niwewe cyo kuwakejeri wenzako
utakwe radhi vipi? mijitu mingine bana?? mkielezwa ukweli mnaombwa mtakwe radhi
 
Mkuu Ishina, DSTV, ZUKU, Easy TV na wengine watakaokuja hawana vibali vya TCRA ku distribute local contents, the official distributer wanaitwa multiplex operators wako 3. Vituo vya TV vinabaki kuwa content provider hata sisi jf tukiamua kuwa na channel yetu, tunafungua JF TV!.

DSTV wana service licence only lakini hawaruhusiwi kupokea local contents, hata vipindi kama Wanawake live, na lots of Bingo movies kwenye DSTV Swahili, zinarushwa kutokea Afrika Kusini!. Hata hiyo TBC yenyewe kwenye DSTV, iko beamed kwa nchi za Afrika Mashariki tuu, hata ukiwa South Africa, TBC haionekani!.

Hapo ilipo hata hilo la kuonyesha 5 channels bure ni ubabe tosha!, channel ya bure ilipaswa iwe moja tuu, TBC ambayo tunailipia kwa kodi zetu, nyingine zote tulipaswa kulipia!. Kwa msio fahamu TV kama CNN, BBC, Al Jazeera na nyingine za wenzetu zilikwenda digital kitambo kidogo, ukiwa ulaya kuna ma chanell ya CNN kibao suprising, hii tunayoiona huku kwetu kule haionekani!, wakati fulani nikiwa huko ndipo nililiona Tangazo la utalii la Tanzania kwenye CCN masikini Afrika hatulioni!.

Kitendo cha kuilazimisha DSTV ionyeshe hizo chanell tano za bure, ni sawa na kuilazimisha CNN itangaze matangazo ya TBC!. Kwanza huko DSTV hakuna hata chanel moja ya bure, kule inaongea pesa tuu!, na ili kuona mechi zote, lazima kila mwezi ulipie zaidi ya laki!, kama hizi za kulipia elfu 10 kwa mwezi watu wanapiga kelele, DSTV tutaigusa?.

Pasco.

Mkuu Pasco,

Nashukuru saana kwa ufafanuzi wako, ingawa umetumia a lot of technical terminologies zinazotoa picha kuwa kuwa jambo hilo ni gumu sana na haiwezekani kwa hawa jamaa kuingiza hizo 5 local channels kwenye ving'amuzi vyao vya DSTV.

Mimi bado naamini kuwa haijarishi hayo matangazo ya DSTV yanarushwa kutoka wapi, eidha ni South Africa, au Bongo – kikubwa hawa jamaa wanafanya biashara hapa kwetu na and they're making a lot of money, umeifka wakati sasa Serikali isimamie mchakato (ikibid kuwalazimisha) wa hizo local channels kuonekana na kwenye DSTV Decoder, ambapo kwa sasa zaidi ya 99% ni channel za nje (hii kitu utaikuta Tanzania tu)


Hapo kwenye Red: Je pale ambapo wanaporusha hayo matangazo ya TBC kwa kutumia hiyo uliyoiita 'Service licence only', huwa wanakiuka masharti ya leseni yao?!! Anyway, if that the case, TCRA ilitakiwa iwapatie licence (technically sijui inaitwaje ) ambayo itawawezesha kupokea local contents na kuzingiiza kwenye Decoder zao kwa manufaa ya mlaji ambaye ni mtanzania, na hizo local channel ziendelee kuonekana bure hata kama account ya mteja haina hela.

Wakati mwingine kwenye hii biashara huria, Serikali inatakiwa iwe na mkono wake kuweza ku-regulate mambo, kama ambayo Serikali mefanya ubabe wa kulazimisha hizo hizo 5 local channels ziwe za free, kumbe inawezakana kukaa nao meza moja na ku-harmonize hii kitu, kama haiwezekana ni kuwalazimisha na wakishindwa wachape mwendo (japo hii opotion ya mwisho, naamini itakuwa ngumu saana kwani kuna baadhi ya wakubwa wana 10% zao)
 
Back
Top Bottom