TCRA, Tunaomba ufafanuzi

TCRA, Tunaomba ufafanuzi

Mjadala ni mmoja tu ambao mpaka sasa sijaona aliyejibu....je mtanzania wa kisarawe anunue kinga'muzi gani aweze kujipatia habari 'bure' tena kutoka kwenye hizi local channels?

Kama hili 'dili' ni la star times tuwekane wazi.

Hivi ofisi za serikali zitatumia kinga'muzi gani....labda nirahisishe swali kwa namna hii.
Mkuu, authorized multiplex operators mpaka sasa ni watatu tuu, Star Media, Agape Associets na Mengi na Dialo, mpaka sasa ving,amuzi vilivyopo sokoni ni cha Star Media kinachoitwa Star Tmes, na cha Agape kinaitwa Ting, cha Mengi na Dialo kinatangazwa tuu ila bado hakijaingia sokoni!. DSTV, ZUKU na Easy TV wao hawapo kwenye mpango huu!.

Sasa ili kuzipata hizo tv tano za bure, unahitaji kununua king'amuzi kimoja tuu kati ya hivyo!.

Kingamuzi cha ofisi za serikali ni kile king'amuzi cha waserikali!.

TV zinazoonekana ZUKU na DSTV zote ni za kulipia!, hakuna bure kule!.

Kwa kuongezea tuu, signal niliokuwa naipata ITV direct ikiwa free to air ni strong kuliko ITV inayoonekana kwenye kingamuzi cha Star Time, sababu, matangazo yanayorushwa na ITV kwenda Star Time, ni matangazo ya analogia ila yatangwa kwenye mfumo wa Digitali!. King'amuzi cha ITV na Star TV kikitoka, kitarusha digital kwenye HD, hivyo ITV na Star TV, picha zitakuwa clear kama DSTV.
Pasco.
 
Mkuu, authorized multiplex operators mpaka sasa ni watatu tuu, Star Media, Agape Associets na Mengi na Dialo, mpaka sasa ving,amuzi vilivyopo sokoni ni cha Star Media kinachoitwa Star Tmes, na cha Agape kinaitwa Ting, cha Mengi na Dialo kinatangazwa tuu ila bado hakijaingia sokoni!. DSTV, ZUKU na Easy TV wao hawapo kwenye mpango huu!.

Sasa ili kuzipata hizo tv tano za bure, unahitaji kununua king'amuzi kimoja tuu kati ya hivyo!.

Kingamuzi cha ofisi za serikali ni kile king'amuzi cha waserikali!.

TV zinazoonekana ZUKU na DSTV zote ni za kulipia!, hakuna bure kule!.

Kwa kuongezea tuu, signal niliokuwa naipata ITV direct ikiwa free to air ni strong kuliko ITV inayoonekana kwenye kingamuzi cha Star Time, sababu, matangazo yanayorushwa na ITV kwenda Star Time, ni matangazo ya analogia ila yatangwa kwenye mfumo wa Digitali!. King'amuzi cha ITV na Star TV kikitoka, kitarusha digital kwenye HD, hivyo ITV na Star TV, picha zitakuwa clear kama DSTV.
Pasco.

tararaa traarar!movie inaanza!
Kwa hiyo ndugu pasco unakubali kuna ukurupukaji katika jambo hili!

Kumbe mbwembwe zote za kuingia digitali hakukuwa na maandalizi both kwa service providers na pengine wananchi.vinga'muzi viwili viko sokoni vingine vinategemewa kuingia (itv na star tv)

hivi DSTV ZUKU na Easy tv sio ving'amuzi?kwa nini wao ni exception katika mchakato huu ?

Unaposema star times wanachukua matangazo ya analogia na kuyapeleka kwenye digitali unapingana na maneno ya TCRA kwamba tunahama toka analog kwenda digitali....mbona mchanganyo?analogia itaendelea kuwepo au entirely tumehamia digitali?

Unaposema ving'amuzi vya itv na star tv vitakuwa na ubora zaidi mwenyewe waita HD unazidi kunichanganya kwani walivyotuambia TCRA ni kuwa sasa matangazo ya kidigitali yatakuwa na ubora zaidi,ina maana baada ya muda mfupi tutatakiwa kuhamia ''HD'' na mitambo kama ile ya star times ''itazimwa'' !!

Naomba ufafanue je hizi Tv zetu za ofisi za serikali zitatumia kinga'amuzi gani?
 
hakuna lolote hao startme baadhi ya sehemu hazshik, hizo antena wanataka zifike juu ya mawingu ndo tushike. shame on u TCRA
 
hakuna lolote hao startme baadhi ya sehemu hazshik, hizo antena wanataka zifike juu ya mawingu ndo tushike. shame on u TCRA
watakwambia unaishi kwenye 'dark spots' maana yake ni bondeni sana au mlimani sana!
 
kupata habari sio basic need kwa mtanzania!
Ni mtanzania huyuhuyu aliyeshindwa kulipia ada ya shule lakini leo anaambiwa anunue kinga'muzi kwa elfu 80.ni mtanzania huyu huyu aneyeambiwa huduma za watoto ,wajawazito na vizee ni bure lakini ananyimwa haki ya kupata tangazo la uzazi wa mpango.
Hivi mtanzania ni mtu wa namna gani?
 
me mbona nina cha startimes na local chaneli zote tano nazipata though bado nasubiri vingine nihame.elfu kumi na nane then chaneli zenyewe za kizushi tu.kwa anayetumia zuku anaweza tupa data zake?

Nina STAR Time ATN sipati nazani kwa kuwa nao wanakingamuzi chao....
 
Kwa mujibu wa Baraza la Kiswahjili la Taifa (BAKITA) kisimbuzi ndiyo kiswahili sahihi kwa 'Decorder'. King'amuzi ni kiswahili sahihi kwa 'detector'

kwa hiyo Makamba na wizara nzima hawakuliona hili. Vilaza wengi sana nchi hii
 
Hii kitu itatufanya tuanze kuwa na ving'amuzi zaidi ya kimoja kama line za simu
 
tararaa traarar!movie inaanza!
Kwa hiyo ndugu pasco unakubali kuna ukurupukaji katika jambo hili!

Kumbe mbwembwe zote za kuingia digitali hakukuwa na maandalizi both kwa service providers na pengine wananchi.vinga'muzi viwili viko sokoni vingine vinategemewa kuingia (itv na star tv)

hivi DSTV ZUKU na Easy tv sio ving'amuzi?kwa nini wao ni exception katika mchakato huu ?

Unaposema star times wanachukua matangazo ya analogia na kuyapeleka kwenye digitali unapingana na maneno ya TCRA kwamba tunahama toka analog kwenda digitali....mbona mchanganyo?analogia itaendelea kuwepo au entirely tumehamia digitali?

Unaposema ving'amuzi vya itv na star tv vitakuwa na ubora zaidi mwenyewe waita HD unazidi kunichanganya kwani walivyotuambia TCRA ni kuwa sasa matangazo ya kidigitali yatakuwa na ubora zaidi,ina maana baada ya muda mfupi tutatakiwa kuhamia ''HD'' na mitambo kama ile ya star times ''itazimwa'' !!

Naomba ufafanue je hizi Tv zetu za ofisi za serikali zitatumia kinga'amuzi gani?
Kwanza naomba ku declare mimi sio mtu wa TCRA, ila nimekuwa nikimsikiliza meneja mawasiliano wa TCRA Bw. Inocent Mungy, hivyo kujikuta ninauelewa wa kutosha tuu kwa kuanzia!.

Hili la kusema TCRA wamekurupuka sii kweli, matangazo walianza miaka miwili kabla!. Kingamuzi kimoja, kinaweza kubeba chaneli mpaka 500!, hivyo hata ingekuwa ni Star Times pekeyake, kingetosha, hivyo ving'amuzi vingine vyote ni ziada tuu!.

Hapa Tanzania, hatuna hata kituo kimoja kilichokuwa kinarusha Digital Signal za TV, japo TV zote zinafanya digital production lakini transmitter zote, zinarusha analogy. Kinachofanyika sasa, TV zote badala ya kuirusha ile analogy signal free to air hivyo TV kuzinasa bure, signal hiyo sasa inapelekwa Star Media, na star media ndio wanairusha kidigitali. Ili uweze kuelewa hii lazima kwanza uwe na DSTV na Star Times, ukitazama quality ya picha ndipo utanielewa!.

Sasa ITV na Star TV wao wanakuja na kingamuzi cha cha kidigitali na wanajitapa watarusha signal kwenye HD!, ili walitimize hili, inamaana wao ITV na Star TV wataachana na zile transmiters za analogia na watafunga za digitali!. Picha zao zitakuwa kama za DSTV!.
TV za ofisi za serikali, zinatumia king'amuzi chao!.
Pasco.
 
Tatizo kubwa ni ITV, star tv na channel 10. TBC ni uchuro tu
 
Mkuu Jipu, kuhusu pesa kiukweli ninazo, mimi nalipwa elfu 20,000 kila siku, (zile bahasha zetu huwa zinawekwa 20,000), hivyo kwa wiki natengeneza Sh. 100,000 kwa mwezi natengeneza 400,000?= hizi ni pesa nyingi sana kwa mwandishi wa habari, kwa kifupi kwa fedha hizo, mimi ni miongoni mwa waandishi wa habari matajiri sana, hata nyumba ninayokaa, nimepanga vyumba vitatu!, yaani jiko, chumba na sebule!, usafiri niliokuwa nikiutumia sikuzote ilikuwa ni bodaboda, lakini sasa nimeweza hata kubadili usafiri kutoka boda boda sasa natumia bajaj!.

Huko Sinza tunakokunywa kwenye hizo baa 250, wengi wetu tunakunywa huko kutokana na uwezo, mfano mimi ningependa sana niwe nakunywa Samaki Samaki pale Mlimani City, ila bei yao iko juu, na mimi uwezo wangu ni wa kunywa bia moja kila siku, na siku ya mwisho wa mwezi, huweza hata kuywa bia 3!, hivyo nikijinyima tuu bia 4 kwa mwezi, pesa hiyo inatosha kulipia king'amuzi!.

Siombi msamaha kuwasisitiza kuwa kuna watu wanapenda zaidi kuendekeza starehe kuliko kuzijali familia zao!. Hakuna TV inayouzwa chini ya laki!, kama uliweza kununua TV zaidi ya laki, utashindwaje kununua kingamuzi elfu 30?!.
Kwani wewe "ile starehe" huwa unailipia sh, ngapi?, au unalipwa Sh. ngapi?!. Nunueni vingamuzi, tuko katika ulimwengu wa digitali, lazima na sisi tubadilike tuishi kidigitali!.
P.

kumbe maskini akipata......hulia
 
Hapa Tanzania, hatuna hata kituo kimoja kilichokuwa kinarusha Digital Signal za TV, japo TV zote zinafanya digital production lakini transmitter zote, zinarusha analogy. Kinachofanyika sasa, TV zote badala ya kuirusha ile analogy signal free to air hivyo TV kuzinasa bure, signal hiyo sasa inapelekwa Star Media, na star media ndio wanairusha kidigitali.

Sasa ITV na Star TV wao wanakuja na kingamuzi cha cha kidigitali na wanajitapa watarusha signal kwenye HD!, ili walitimize hili, inamaana wao ITV na Star TV wataachana na zile transmiters za analogia na watafunga za digitali!. Picha zao zitakuwa kama za DSTV!.
Pasco.

ama!kumbe tunaohamishiwa ni wananchi tu tunaopokea huduma!kweli tanzania ni zaidi ya tuijuavyo.

KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA
 
kumbe maskini akipata......hulia
Nikweli kabisa, ndio maana nimeweka hadharani mijihela ninayopokea!.
Nimekulia katika familia ambayo kula wali kuku ni mpaka siku ya sikukuu, na soda ni mpaka wakija wageni, wakishakunywa sisi ndio tunamalizia vile vitone vinavyobaki chini!.
P.
 
Kwanza naomba ku declare mimi sio mtu wa TCRA, ila nimekuwa nikimsikiliza meneja mawasiliano wa TCRA Bw. Inocent Mungy, hivyo kujikuta ninauelewa wa kutosha tuu kwa kuanzia!.

Hili la kusema TCRA wamekurupuka sii kweli, matangazo walianza miaka miwili kabla!. Kingamuzi kimoja, kinaweza kubeba chaneli mpaka 500!, hivyo hata ingekuwa ni Star Times pekeyake, kingetosha, hivyo ving'amuzi vingine vyote ni ziada tuu!.

Hapa Tanzania, hatuna hata kituo kimoja kilichokuwa kinarusha Digital Signal za TV, japo TV zote zinafanya digital production lakini transmitter zote, zinarusha analogy. Kinachofanyika sasa, TV zote badala ya kuirusha ile analogy signal free to air hivyo TV kuzinasa bure, signal hiyo sasa inapelekwa Star Media, na star media ndio wanairusha kidigitali. Ili uweze kuelewa hii lazima kwanza uwe na DSTV na Star Times, ukitazama quality ya picha ndipo utanielewa!.

Sasa ITV na Star TV wao wanakuja na kingamuzi cha cha kidigitali na wanajitapa watarusha signal kwenye HD!, ili walitimize hili, inamaana wao ITV na Star TV wataachana na zile transmiters za analogia na watafunga za digitali!. Picha zao zitakuwa kama za DSTV!.
TV za ofisi za serikali, zinatumia king'amuzi chao!.
Pasco.

mkuu Pasco nakufahamu vizuri sana kwamba hausiki na TCRA lakini wewe ni mdau nyeti katika tasnia ya habari!nakuheshimu katika hili.

TCRA wamekurupuka kwani hata wewe umekiri kuwa hakuna station inayoweza kurusha matangazo yake kidigitali.ni upuuzi na kukurupuka kumkomalia mwananchi wa kawaida ahamie digitali huku ukijua hata taasisi za utangazaji nchini hazijaanza kufanya hivyo.
Kutoa matangazo kwa miaka miwili haimaanishi kuwa tumefanya utafiti wa madhara na mazuri ya tukio hili kwa mwananchi wa kawaida na maskini wa nchi hii!

Kuhusu kinga'amuzi cha serikali ningependa nikijue kwani nahisi kitakuwa 'perfect'
 
Last edited by a moderator:
Pasco nimesoma maelezo yako na kuona huu uhamaji wa kutoka analogy kwenda dijitali ni kumuumiza muangaliaji TV tu na siyo kuheshimu teknolojia.
Unasema TV zilikuwa zinarusha signal za analogy na sasa zitaendelea kurusha signal za analogy na kwamba tofauti iliyopo ni kwamba signal hiyo ya analogy sasa itapelekwa kwa star media ili waibadilishe na kuwa digital. Sasa kama TV zinaendelea kurusha analogy signal ambayo inaweza kukamatwa na TV bila malipo wala usumbufu, kwanini mwananchi huyo alazimishwe kununua king'amuzi?
Je, kitendo cha kuipeleka analogy signal kwa star media ili waibadilishe kuwa digital inaongeza thamani gani kwa muangaliaji wa televisheni? Je, iwapo tungeendelea na utaratibu uliokuwepo ni madhara gani yangetokea?
 
Last edited by a moderator:
Bei sh 39000/- kumbe chanel nyingi tu wamebania. Tulionunua ving'amuzi kitambo tuna ahueni
 
nimejiuliza hili swali sana then nahic tcra walipaswa kuwa makini kabla ya kuzima hiyo mitambo,kwani ilikuwa lazima kuwahi kwenda uko kabla ya makampuni kujipanga?dah! yaani wabongo kuwa kimbelembele.ss startime channel zingine hazioneshi.
 
Back
Top Bottom