Ushaidi wa kimazingira ni kama ifuatavyo:
1. Kamera yake ilikuwa na nyumba za jamaa mhasibu anazojenga Morogoro so Jerry alikuwa anamchunguza
siyo kosa; tumepiga picha nyumba ya Gavana, Ikulu, n.k!
2. Walionekana wote na CCTV hotelini ambako Jerry alikana kwenye maelezo yake kuwa hamjui jamaa
maelezo ya wapi? Maelezo yote ambayo Jerry na Polisi wameyatoa nje ya kiapo cha mahakama hayana nafasi katika ushahidi. Polisi hawawezi kusema mahakamani ati "jerry alipozungumza global publishers alisema x,y"; mahakama itawapiga stop.. inadmissible!
3. Mhasibu alisema wazi kuwa ndani ya gari la Jerry kuna nini (pingu, bastola)
Itakuwaje mtu mwingine alimpa hizo information? Polisi ni lazima watatakiwa waoneshe the chain of possession kuthibitisha hilo.
4. Miwani ya mhasibu ilikutwa ndani ya gari la Jerry inaonyesha kimazingira walishakutana jambo ambalo jerry alikana.
Polisi watatakiwa kuthibitisha walikuta miwani ndani ya gari la Muro; Ni jukumu la Polisi kuthibitisha kuwa walikuta miwani humo. Je, kabla ya kulipekua hilo gari walimuonesha Muro kuwa wao hawakuwa na kitu mikononi mwao? Je walikuwa na waranti ya kulipekua hilo gari?
Jerry alikurupuka, laiti angesema alishamuona mahali au jana yake huyu mhasibu na wakakaa meza mmoja, maana unaweza hotelini kukaa meza moja na mtu usiemjua hasa kama CCTV kamera ikionyesha kulikuwa kumejaa..ANGEKUWA HANA KESI YA KUJIBU KABISA.
NI jukumu la Polisi kuthibitisha hilo.
Yeye Jerry ndo amekaribisha ushahidi wa kimazingira.
Tatizo alishavimba sana bichwa....linaelekea kupasuka sasa.
Ushahidi wa kimazingira unaonesha kuwa polisi walijaribu kumtegea mtego Muro ili akamatwe na rushwa lakini walishindwa.
a. Hakuna CCTV inayoonesha Muro akipokea fedha yoyote
b. Hakuna mtu yeyote aliyejitokeza kudai kuwa amempa fedha za rushwa Muro
c. Hakuna mahali popote ambapo panaonesha kuwa Muro alimtishia mtu yeyote. Alikuwa kwenye gari peke yake, unless alikuwa anamtishia mlalamikaji kwa kutumia njia za osmosis!
d. Hakuna mahali popote ambapo Muro amekataa kumiliki Pingu au Bunduki; vitu ambavyo vyote ameonesha kuwa anavimiliki kihalali.
e. Humo hotelini kulikuwa na watu wengine wengi; kwanini na hao watu wasiitwe (wanaonekana kwenye CCTV siyo) kuja kutoa ushahidi kama walimuona Muro humo ndani na kama kulikuwa na jaribio lolote la kutoa rushwa.
f. Muro (kama alikuwa hotelini) inaonekana aliamua kutoka na kwenda kwenye gari yake. Hii ni dalili kuwa hakutaka kuwa sehemu ya jaribio la kutoa rushwa.