MwanajamiiOne
Platinum Member
- Jul 24, 2008
- 10,470
- 6,588
Kwa hapa imenibidi nicheke tu peke yangu- hata mahakamani sijawahi tia Mguu wangu mkuu MUNGU anisaidie.huyu jamaa atakuwa aliwahi kuwa karani wa mahakama!!!!!!!!!!!!
Kwa hapa imenibidi nicheke tu peke yangu- hata mahakamani sijawahi tia Mguu wangu mkuu MUNGU anisaidie.huyu jamaa atakuwa aliwahi kuwa karani wa mahakama!!!!!!!!!!!!
Naamini hayo hayatampata kwa vile wananchi tuko nyuma yake kwa ukaribu zaidi! Muhimu ni hatua hii ya mahakama kufanya kazi yake kwa haki.Wananikumbusha Adam Mwaibabile mie hawa!!
Si hapo sasa! Hebu kwa mara ya kwanza katika mahakama zetu Tanzania tuone ushahidi wa simu unavyoweza kutumika kutoa tafsiri isiyoleta mashaka kwa umma!Hiyo call detail haitasaidia unless iwe na content ya hayo mazungumzo, ambayo sidhani kama kampuni ya simu inayo. Inawezekana huyo bw. mawenge akawa kweli ndiye aliyempigia na wakazungumza. Hiyo sio ishu maana hata mimi nikikupigia sasa hivi japo huijui namba yangu utapokea na tutaongea. Nikidai baadaye kwamba ulinidai rushwa?
Labda watoe call details za mwezi mzima waangalie kama hizo namba zao zimekuwa zikiwasiliana frequently - implying kwamba likely walikuwa wanajuana kwa muda. Maana huwezi kupiga mara moja na kuomba rushwa hapohapo.
Unafikiri tuna jeshi lenye akili ya kufanya investigation kama hizi basi? We acha tu.
JF addict! Masanilo niache, nafanyakazi kwa mhindi ndio maana namuibia muda, kwani naye anaibia nji hii. Utamuonea huruma J Patel wa EPA kweli!
bado masaa tu, naona mwisho wa Kova kuwa mkuu wa Police kanda maalumu ya Dar es salaam ukikaribia, naiona aibu yake haiko mbali....shitaka jepeesi.......Ah hapo mheshimiwa tulipitiwa kidogo ila hata hivyo mheshimiwa tulifanya vizuri kwenda kwani tulimkamata mshtakiwa akiwa na pingu garini
Hakimu: Je pingu hizo zinahusika vipi na mashtaka?
Mashtaka: Mpaka sasa hatujawezakuilink kisawa sawa bwana hakimu lakini mshtakiwa haruhusiwi kumiliki pingu
Hakimu: Sheria inasemaje juu ya hilo?
Mashtaka: Ah........... hebu ngoja kidogo Bwana hakimu tuconsult sheria zetu ila inaonekana kuwa hakuna sheria inayokataza ila tu huwa hatuuzii pingu kwa raia
Hakimu: Jibu swali bwana mashtaka, sheria inaruhusu au hairuhusu?
Je ni kwanini police wamelivalia njuga kiivyo?sipati picha kamili
Ushaidi wa kimazingira ni kama ifuatavyo:
1. Kamera yake ilikuwa na nyumba za jamaa mhasibu anazojenga Morogoro so Jerry alikuwa anamchunguza
2. Walionekana wote na CCTV hotelini ambako Jerry alikana kwenye maelezo yake kuwa hamjui jamaa
3. Mhasibu alisema wazi kuwa ndani ya gari la Jerry kuna nini (pingu, bastola)
4. Miwani ya mhasibu ilikutwa ndani ya gari la Jerry inaonyesha kimazingira walishakutana jambo ambalo jerry alikana.
Jerry alikurupuka, laiti angesema alishamuona mahali au jana yake huyu mhasibu na wakakaa meza mmoja, maana unaweza hotelini kukaa meza moja na mtu usiemjua hasa kama CCTV kamera ikionyesha kulikuwa kumejaa..ANGEKUWA HANA KESI YA KUJIBU KABISA.
Yeye Jerry ndo amekaribisha ushahidi wa kimazingira.
Tatizo alishavimba sana bichwa....linaelekea kupasuka sasa.
Senior Officer wa serikali anayefanyakazi bagamoyo mkoa wa pwani [siyo biharamulo]eti haju tofauti kati ya polisi na takukuru tehe tehe tehe.Mheshimiwa Hakimu: Ndugu Mawenge ukiwa kama shahidi wa kesi hii je unasema kuwa mshitakiwa alikulazimisha umpatie kiasi cha pesa
Mawenge: Ndiyo Mheshimiwa
Hakimu: Je mshitakiwa alitaka kiasi gani? na alijitambulisha kama nani?
Mawenge: Milioni 10 na alisema yeye ni afisa wa Takukuru
Hakimu: je rushwa hiyo ilitakiwa kwa ajili ya nini? Kwa sababu inafahamika kuwa mtu huwa anatoa rushwa pale anapohitaji kupewa huduma flani, je wewe ni huduma gani uliyoitaka kutoka kwa mshtakiwa hadi akuombe rushwa?
Mawenge: Alisema ili asinitoe kwenye vyombo vya habari kama fisadi
Hakimu: Je wewe ni fisadi?
Mawenge: Hapana mimi si fisadi, mwulize hata mke wangu mimi si fisadi kabisa bwana hakimu
Hakimu: Sasa kama wewe si fisadi kwa nini ulikubali kutoa rushwa? kwa nini usimpuuze tu kwa sababu hata akikutoa kwenye vyombo vya habari wewe si fisadi.
Mawenge: Ndio maana mheshimiwa hakimu nikaenda kumripoti polisi
Hakimu: Wewe ulikuwa mtumishi wa uma, je masuala ya rushwa huwa yanaripotiwa polisi au TAKUKURU? na je uliporipoti polisi, walikupatia pesa za moto ambazo ulitakiwa kumpa mshitakiwa?
Mawenge: Ah bwana Hakimu, unajua, kule kwetu Bagamoyo huwa hatujui tofauti kati ya polisi na TAKUKURU tunachojua wote ni polisi tu!! ...................
Ah kumbe naota mchana.!!
lets hope mahakama itatenda haki juu ya tukio hili la aina yake 2010
Hivi ni mahakama ileile iliyomwachia huru yule polisi aliyeamuru wafanya biashara wa madini kuuawa kwa jina la majambazi? Au ni ileile ambayo kwa miaka mitano sasa haijamhukumu hata mmoja wa wale waliokula mabilioni ya EPA? Nikumbushe pliz.
Jerry Muro na Edmund Kapama
walitimiza masharti ya dhamana na kuachiwa.
Mwenza Ngassa amepelekwa rumande.
Anaenuna anune anaecheka acheke bwana Muro kwa namna moja ama nyingine lazima atakua anajihusisha na makundi ya kihalifu.Hata kama inaruhusiwa kisheria mtu yeyote kumiliki pingu mwanahabari na pingu wapi na wapi?alizinunua kwa ajili gani?self defence or what?haiingii akilini,hata panga,kisu,shoka n.k mtu yeyote anaruhusiwa kumiliki lakini nadhani kila mtu atakushangaa ukionekana unatembea na shoka mitaani wakati huonekani kuwa na shughuli yeyote inayohitaji uwe na shoka!!
Senior Officer wa serikali anayefanyakazi bagamoyo mkoa wa pwani [siyo biharamulo]eti haju tofauti kati ya polisi na takukuru tehe tehe tehe.
Kwa vile jamaa ameondolewa hapo ofisini kutokana na ubadhirifu isije ikawa anajihami fulani ili asichunguzwe kwa vile amesaidia******
Lakini mwisho wa siku tutajua chuya ni ipi na mchele ni upi