Ipo taarifa imetundikwa katika Blog ya Michuzi ikiainisha idadi ya madaktari idara kwa idara kwa wamerejea kazini na kila kitu kiko shwari, taarifa hii ni ya kweli ni jambo jema katika kuokoa maisha ya watanzania. Hata hivyo kufuatia taarifa za awali za mchana kuwa madaktari bingwa nao wamegoma taarifa hii imeanza kutuchanganya. Itakuwa busara madaktari wenyewe wakatujulisha juu ya ukweli wa taarifa. Najua wengine watadhani uamuzi huu ni sawa na kumsaliti Dr, Ulimboka, sidhani kama mtazamo huo utakuwa sahihi. Ni imani yangu kuwa majadiliano yaliyokuwa yanaendelea kati ya serikali na madaktari yaendelee ili kufikia muafaka ya majadiliano hayo katika awamu time kwa maana ya yale ya muda mfupi yatekelezwe, ya muda wa kati nayo yaendelee na yale ambayo ni muda mrefu yaendelee kutekelezwa kwa awamu.
Ni ukweli uliowazi kuwa ujumbe waliotaka kuufikisha umefika na tena umefika juu kabisa, ninaimani tutaona mabadiliko japokuwa haitasemwa mabadiliko hayo yamesababishwa na msukumu wa madaktari, ukweli utabakia pale pale, this was an eye opener.