TBC: Huduma hospital Dar zaendelea kuimarika

TBC: Huduma hospital Dar zaendelea kuimarika

[QUOTE/] Stella Manyanya kanitibua nyongo kwa kumuita Dr Ulimboka Hitler, mbele ya bunge! How cruel![/QUOTE]

Kama kasema hivyo kweli anachefua maana hao wapo wengi wanajipendekeza kwa Kikwete ili asiwaondoe madarakani lakini wanajichimbia shimo wenyewe.

Serikali inafanya ubabe kwasababu viongozi wake hawatibiwi hapa, kitu ambacho ni kibaya tena sana. Huwezi ukatetea sehemu ambayo wewe hufaidiki nayo. Hivi kweli inaingia akilini Nchi nzima hakuna CT Scan na viongozi wetu wakaona ni sawa, basi tuna safari ndefu sana. Shule haziwezi kuboreshwa, public transport pia kwasababu haziwahusu wao kabisa. Tutaendelea kuwasema madaktari lakini viongozi wetu ndio wanatuchimbia kaburi.

Dr. Stephen Ulimboka ni mmoja wa watu wachache duniani na wala sio Tanzania, mimi namfananisha na Steve Biko wa SA. Yeye ameamua kupigania maslahi ya mtanzania wa chini ambaye hawezi kwenda nje ya nchi au hospitali binafsi. Hata madaktari wakiongezwa kima cha chini hicho cha 3.5million yeye hakimhusu kwasababu hafanyi kazi serikalini. Kwanini watu hilo hawalioni? Inavyoonekana pia ni kiungo muhimu mno kwa madaktari kiasi cha kwamba kutokuwepo kwake madaktari wanaanza kuyumba. Mungu amsaidie apone na kurudi salama.

Hii ya Serikali kutaka kuingia mkataba na hospitali binafsi kwa ajili ya wananchi kutibiwa huko ni namna nyingine ya kutafuta ulaji. Ubabe hautasaidia, tunaoumia ni sisi wananchi wa kawaida

MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI SEKTA YA AFYA.
 
  • Thanks
Reactions: FJM
TBC wa zushi .Saa ya ukombozi kwenye afya na nchi kwa ujumla imekaribia kuliko tunavyosubiria 2015 .Watanzania tumeteseka mno.hospitali zetu hazina dawa, vifaa na wataalamu wetu hawalipwi vizuri.
 
ritz na wewe ni mtanzania kumbe maana watanzania wengi hawana akili kama yako ubongo wako umedumaa
Tunashukuru Madakatari wetu kwa kurudi kazini kuendelea na kazi kutibu Watanzania wenzetu.
 
madaktari walio kuwa likizo wamerudi kazini na wanachapa mzigo huko sio kuimarika? Acha kuwa kibaraka wa cdm wanaochochea mgomo na kutaka kumuua ulimboka

hebu ni kama sijakuelewa, cdm ndio waliotaka kummua ulimboka?
 
mijitu mingine bana....kwa iyo nyiie mnao wasapot madaktari mna maana ipi sasa..mmeridhika na vifo vya ndugu zetu kisa maslahi binafsi ya madaktari sio
 
ITV saa mbili usiku wametangaza mgomo wa madaktari bingwa Muhimbili. Ni kusema kuwa ITV hawapo Dar es salaa au Tanzania?
 
Huwezi kurekebisha mfumo huu kwa siku moja kama ni madai serikali ilishaanza ya kuyafanyia kazi kama hotuba ilivyojieleza mbona mpaka leo hii jumuiya ya madakatari haijatoa taarifa yao kuipinga yale yaliyosemwa na mh. Raisi? Vifaa wezi wa dawa na vifaa kutoka hospitali za serikali ni waajiriwa wa sekta ya afya wakiwamo madaktari au hilo pia hulijui?

Chama
Gongo la Mboto DSM

Hapo kwenye red: Maana yake serikali imeshindwa kutatua tatizo la wezi? Lakini wala sishangani maana mgeuza kazi za polisi toka kuchunga usalama wa raia na mali na sasa wanakuwa watesaji.
 
Eeee hii ni muhimbili ya wapi?ni hii hii ninayoifahamu au kuna mpya?duh hizi ndo taarifa anazopelekewaga kikwete!na ndizo anazotumia kutoa conclusion ya mambo.sasa nashindwa kuelewa huyu afisa uhusiano kapata psychotic disorder(ana'hallucinate) au ...
 
Usicheze na ajira wewe, watoto wantakula pumba? JK ulitakiwa umwe mkali mapema! Asiyeridhishwa na malipo ya 3.5 M aATAFUTE MUAJIRI ATAKAYEMLIPA PESA HIYO SIO KUGOMA.

Nijuavyo mimi hakuna daktari anayelipwa 'fuba' hilo. Siri kali imeligomea!
 
hongereni sana kwa kurudi kutoa huduma madai yenu yatarudi mezani kwa mazungumzo
 
Msiamini huu waraka. Ni FEKI.
Haya ni madudu ya usalama wa TAIFA.......!!!!
Madaktari wanachezewa akili ili warudi kazini kesho....LOL
Nimewasiliana na watu kadhaa Mhimbili hakuna Daktari Kazini
 
hongereni kwa kuchagua fungu jema....... I can join you to fight the good fight
who needs you?what for?wacha kujikomba kwani walikuandikia barua ya maombi ujiunge nao?
Tell your gvt to stop playing politics with people's lives.
 
Back
Top Bottom