Mleta mada nitakujibu hapa hapa baadhi ya hoja zako muhimu.
Ni kosa kubwa sana kumlinganisha Tundu Lissu na Mzee Jiwe. Wakati Tundu Lissu anatumia hoja zake kama nguzo yake ya kuwashawishi watu na dunia nzima iweze kuelewa kile kinachoendelea Tanzania, Mzee Jiwe yeye kajifungia ndani ya nchi, anakwepa kutoka ndani ya nchi, anatumia kick, mamlaka, nguvu na ubabe ili watanzania wote tuamini na tumuunge mkono, na yoyote atakayempinga au kumkosoa anageuzwa kuwa adui yake na adui wa taifa la nzima.
Tundu Lissu amekuwa makini na mstahimilivu katika kupigia kelele hoja zake, mwanzoni alionekana kama kupuuzwa(wakati aliposema Tz imepata dikteta uchwara), leo hii kila mtu duniani anayetaka kujua kinachoendelea kisiasa tanzania anatamani kusikia kila kinachosemwa na Tundu Lissu. Lissu anavutia kumsikiliza, anashawishi na anaaminika sana kwa sasa.
Hayo ni mafanikio makubwa sana kwake. Tunaelezwa zaidi ya vyombo vya habari 22 vikubwa katika nchi za ulaya na Marekani vimeomba kufanya mahojiano na Lissu. Kumbuka Lissu bado ni mgonjwa anayetibiwa nje ya nchi. Shauku yote hiyo ya hao watu inatoka wapi? Nadhani hoja zake zimeiva, zinalika.
Tukija kwa mzee Jiwe hali ni tofauti sana. Mpaka sasa watanzania hatujui tunapelekwa wapi. Wafanyakazi, wafanyabiashara, wakulima, wanafunzi, wachimba madini, wawekezaji nk. wote tupo njia panda. Kila analolifanya linageuka kuwa mwiba wa kumchoma yeye mwenyewe. Mambo ya sukari yakamshinda, Tanzania ya viwanda imegeuka kuwa hadithi ya kiuwendawazi(Charles Mwijage anayajua haya), Makinikia imegeuka hadithi ya simanzi(Kwa sasa hata Kabudi anaogopa kuliongelea), Ndege nacho kitendawili chenye maumivu(Mheshimiwa ameshanusa ATCL hawawezi, ni hasara tupu), Korosho imekuwa hadithi ya uchungu(Hadi jeshi limesalimu amri), Ukusanyi wa kodi nao hali ni mbaya(Dr.Mpango kichwa kinamuuma), Kikotoa chake alichokitengeza yeye mwenyewe amekuja kukikana(Mama mhagama anajua hayo..), Ufisadi nao ndio umemea kama magugu(Sakata la Trilioni 1.5 linamnyima raha, hana wa kumtwika, Dr.Assad anatafutiwa sababu ya kutolewa kafara) Kipi tena? Kuna jipya?