Tanzia: Mwana JF Straton Mushi aaga dunia

Tanzia: Mwana JF Straton Mushi aaga dunia

RIP, siku nikifa taarifa haitafika humu, hakuna anayenijua humu
 
Haya majina haya,nilifikiri ni Stratton Munish ,ex Dakawa stdnt!
 
RIP, siku nikifa taarifa haitafika humu, hakuna anayenijua humu
Ahahahah.
Hata mm nikizima huku itakuwa kimya kimya..Hatar..
Ila nadhan ndio maana ya fake id ili hata uki fake death inakua ngoma droo tu wanajua umekufa kumbe umechange id..as no one knows u.
 
RIP, siku nikifa taarifa haitafika humu, hakuna anayenijua humu
Ahahahah.
Hata mm nikizima huku itakuwa kimya kimya..Hatar..
Ila nadhan ndio maana ya fake id ila hata uki fake death inakua ngoma droo tu wanajua umekufa kumbe umechange id..as no one knows u.
 
Kwa masikitiko makubwa ninapenda kuwataarifu msiba wa mwana JF mwenzetu bwana Straton Mushi aliyefariki mapema wiki hii baada ya kuugua muda mfupi. Mwili wa marehemu uliagwa Jana nyumbani kwake Salasala Dar Es salaam na badae kusafirishwa kuelekea Moshi- Uru Mawela kanisani kwa ajili ya mazishi yatakayofanyika kesho jumamosi hapo hapo Mawela.

Marehemu atakumbukwa kwa upendo wake na harakati za kupigania haki bila kuogopa.

Poleni wana JF, wafanyakazi wote wa airtel na wanafamilia.

Kwa watakaoweza kwenda msibani Kama upo Moshi mjini Nenda stendi kuu panda magari yanaoenda uru halafu Shuka mawela kanisani hapo hapo kushoto kwako Ndio penye msiba. Kama unatumia usafiri binafsi basi ukifika Mawela kanisani ukiulizia kwenye msiba utaoneshwa bila wasiwasi.

Bwana alitoa na Bwana alitwaa jina lake lihimidiwe.

View attachment 1269118
Apumzike kwa amani
 
Kuna umuhimu mkuu. Kuna umuhimu kwa sababu ametoa Jina lake halisi na sehemu ya mazishi. Walio karibu watajua huyu ni member mwenzetu. Na walio mbali watatoa salam za rambirambi hapa hapa jukwaani. Kama mtu hakutaka kujianika akiwa hai basi anapofariki siyo vizuri kum'expose
Ukifa sisi tulio hai ndio tutakuamulia kwasababu wewe aunauwezo tena wa kufanya chochote
 
Sisi humu tunamjua kwa ID wewe unatuletea jina halisi taarifa inakosa mashiko na uzito kabsa

Kweli bhana! Statesmann na sisi wengine hatumjui kabisa huyo Straton Mushi.

Taarifa za kifo cha Straton Mushi ziende kule anakotambulika kwa jina hilo na hapa ziletwe taarifa za kutwaliwa kwa mwana JF ID so and so!
 
Angesema member mwenzetu... ametuacha akataja Id yake.. basi!
 
Poleni kwa msiba. Ila kwasisi wadau wa siasani tungejua ID yake bana ...tafadhali kwa anayejua...
 
Km mtoa mada kazingua, basi hata lugha zilizotumika kumwelekeza ni kali...
Na yy akashindwa kujizuia akapaaa.....

Ngoja niulize kitu kimoja....
Hivi sheria za jf zinaruhusu kutangaza kifo cha member/ID bila uthibitisho kwao?

Maan km ni hivyo humu alooo tutatiana nuksi.....
Umelala zako unaamka una comment kila mtu anakukimbia kucheki unakutana na tag zimejaa R.I.P,
aloo sijui utaanzia wapi kuwashawishi watu that you're not a ghost....

M nahisi kuwe na uthibitisho flan hv,
na binafsi naona
njia bora ya kumuenzi kama member ni kufahamu ID yake....
Na njia bora ya kumuenzi km ndugu ktk jamii ni kufahamu uhalisi wake....

Hii ya kutajiwa Jina halisi wakat hapa tunamjua kwa ID halaf unaomboleza,
ndio naweza sema ni sawa kwa sbb ya ubinadamu...

Ila ni sawa na mmeenda kwenye mashindano live,
washindani wanatambulika kwa namba.......
Na umekariri namba na sura
Halaf baadae unasikiliza redio mtangaza ushindi anataja majina....

Si utahisi kuna kuzungukana...?
Amini utakakanyaga ka redio....
 
"COMRADE" apumzike salama, ameumaliza mwendo. Wafikishie salamu kina "Mw. Nyerere" na "Baba Karume" yale waliotukataza ya kuchagua vingozi wasiofaa ndio imekua mila/ibada ya CCM. Ila tutaendelea kusukuma bendera JF mpaka tutakapofikia kilele cha demokrasia.

Swali fikirishi, sisi tusiojulikana kwa ndugu/jamaa/marafiki kama tunatumia JamiiForums, siku tukivuta taarifa za vifo sijui vipi itawafikia humu wana harakati wa JF.

Tafuta member humu mjuane ili siku ikifika kati yenu mmoja akavuta basi anaebaki anakuja kuweka thread humu
 
Hakuna sababu ya kutupa taarifa ya kifo chake kama hutaki kuitaja ID yake, na kama target yako kupata mchango hapa hupati kitu.
Kuna mahali ametaja kuchangiwa? Kama huna hela kaa kimya kama siai wenzako. Wenye nazo wataenda msibani na watamchangia na si kupitia mtoa tangazo.
 
Wengi wanataka jina alilokuwa analitumia humu kuna member mmoja anaitwa same body nani ngoja niangalie jina lake last see ni tarehe ngapi niunge dots....

tatizo moja mkitajiwa jina lake la Jf mnafukua makaburi
 
Back
Top Bottom