Tanzania: Utawala bora vs Rushwa

Tanzania: Utawala bora vs Rushwa

Wewe unategemea Kingenge aseme nini? Mimi babu yangu mwenye umri sawa na Kingunge kule kwembe akiniona anasema hanifahamu na mim si mjukuu wake, lakini baada ya kunisikia vizuri anakubali kuwa mimi ni mjukuu wake. Nahdani hatuwezi kumlaumu Kingunge kutokana na kuwa umri wake unaweza kumfanya aseme anayosema!
Jaka Mwambi, alisema juzijuzi alikiri kuwa kuna tatizo la rushwa, Ndejembi alikiri, sasa sijui babu anasema nini.
 
Maneno yako Mzee wa Kijijini na Mwalimu Augustino ni ujumbe tosha .Ni kweli huku Tanga na hata kule Dari salama watu wa usalama wa Taifa wame waambia watawala kwamba wakae kimya na kutafuta namna ya kuwatia hatiani wasemao ukweli . Mimi nasema hakuna utawala usio kuwa na mwisho.Hata Waisrael na ubabe wao leo hii wanakaa na kuongea na Wapalestina itakuwa CCM ? Najua wanataka kuzidi kukandamiza lakini naamini wananchi sasa wameamka na wanataka kujua ukweli. Walifanya makosa wakatumia TV yao kuonyesha mambo LIVE wakidhani kwamba wana wapa uhuru wananchi kuujua ukweli sasa wakakosea kubonyeza na sasa wanabanwa mbavu.Tuendelee kuwasaidia akina Zitto kwa njia mbali mbali . Hivi kiwango cha mvuto cha muungwana kiko chini sana na wana haha hovyo wanawatumia akina Manumba nk .
 
Nadhani njia hii ni mbaya zaidi kwao; walichokosea mwanzo ni kukurupuka kujibu kisiasa badala ya kuja na facts za maana. Kwa kuamua kukaa kimya ndipo watakuwa wanajichimbia kaburi zaidi kwa vile wataruhusu wananchi walishwe facts zote kikamilifu ambayo haitawasaidia wao kama viongozi.

ukimya mara nyingi unalipa...uzoefu unaonyesha kuwa kujibu kwao mapigo ndio kunaamshaga hisia za wananchi, inawezekana kuna mmoja wao kafanya assessment nzuri ya hali halisi na kuwapa ushauri huo wa 'kupuuzia' ...na kwa watanzania wa kawaida hoja kama ya Slaa ya juzi ndo itakufa kimya kimya kwenye akili zao ikiwa watuhumiwa wananyamaza kimya ...

..na ukiona kobe kainama ujue anatunga sheria ..na sisi tujipange upya
 
naamini kuwa wanahaha kufunika ukweli ambao unaonekana wazi.....
Namini ktk JF kuna uhuru wa kuchangia na mawazo mengi yanatoka humu ambapo watawala wetu wangeweza kuelewa tuyasemayo na wakatumia as chalenge but wanazidi kuweka shingo ngumu.
Nazidi kuamini kuwa utabiri wa nyerere utatimia tu ktk nyakati zetu...
 
Kingunge awatolea uvivu wapinzani

2007-09-19 08:37:14
Na Raymond Kaminyoge


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Siasa na Uhusiano wa Jamii, Bw. Kingunge Ngombale-Mwiru amesema kashfa zinazotolewa na wapinzani dhidi ya viongozi ni kutapatapa baada ya kushindwa uchaguzi na kulitumia Bunge.

Bw. Kingunge aliyasema hayo jana Ikulu, jijini Dar es Salaam katika mkutano na vyombo vya habari uliomshirikisha pia Waziri wa Habari, Michezo na Utamaduni, Bw. Mohamed Seif Khatib.

Alisema serikali haitachukua hatua yoyote itawaacha waendelee kuzunguka huku ikiendelea kutekeleza ahadi zake kwa wananchi.

Kauli ya Bw. Ngombale-Mwiru, imekuja siku nne baada ya umoja wa vyama vya upinzani unaoundwa na TLP, CHADEMA, CUF na NCCR-Mageuzi, kutangaza majina ya vigogo waliodai kuhusika na ulaji na ubadhirifu wa fedha za umma zikiwemo za ujenzi wa majengo pacha ya Benki Kuu Tanzania (BoT).

`Wameshindwa uchaguzi wa 2005, wameshindwa kulitumia Bunge kumaliza hoja zao, sasa wanapita mitaani kuwachafua viongozi, lakini sisi hatutawafuata Mwembeyanga badala yake tunaendelea kuwaletea wananchi maendeleo,` alisema.

Aliongeza kuwa, Bungeni ndiyo mahali ambapo vyama vya upinzani vinatakiwa kuichachafya serikali, lakini siyo mitaani.

Alisema mafanikio ya serikali ya awamu ya nne, ndiyo yanayowafanya wapinzani kuona njia pekee ya kusikilizwa na wananchi ni kuwapaka matope viongozi wake.

Alisema kutaja majina ya viongozi, hakusaidii badala yake kama kuna ushahidi wa tuhuma zifikishwe mahakamani.

Alisema serikali ya CCM imeweka wazi kuwa, yeyote atakayekuwa na ushahidi wa kiongozi kuhusika na rushwa, atoe taarifa.

Aliwaambia wapinzani kuwa, wamesahau kwamba, demokrasia wanayoitumia ya kuwachafua viongozi ilianzishwa na CCM.

Bw. Ngombale-Mwiru alisema serikali haijazipata nyaraka zinazodaiwa kuwa ndiyo ushahidi wa baadhi ya viongozi kuhusishwa na ufisadi na rushwa na kuongeza kuwa zikiwafikia watatoa taarifa.


SOURCE: Nipashe
 
Kingunge awatolea uvivu wapinzani


Aliwaambia wapinzani kuwa, wamesahau kwamba, demokrasia wanayoitumia ya kuwachafua viongozi ilianzishwa na CCM.

Ukisikia kutolewa uvivu na mzee aliyembioni kufa kwa uzee.... basi tegemea statement za kizembe kama hizi.... kuwa CCM ndiyo ilianzisha demokrasia ..?

of all people.. ccm wanamtuma Ngombale? afadhali mchambuzi angejaribu kidogo kabla ya hajakimbia kurudi magogoni...
 
Bw. Kingunge aliyasema hayo jana Ikulu, jijini Dar es Salaam katika mkutano na vyombo vya habari uliomshirikisha pia Waziri wa Habari, Michezo na Utamaduni, Bw. Mohamed Seif Khatib.


...kwani hana press officer au ofisi yake haina department hii???
 
Mtu wa pwani,

Huo uvivi alioutoa ameupata wapi? hata mtoto mdogo sasa anajua kuwa jamaa ni mafisadi tunachosubiri tu mtu wa kutuanzishia njia ya kuwatoa kama walivyofanya watu wa Romania. Kama baba yako ni moja ya hao mafisadi anza kukimbilia Dubai.

Any way hongera bado kwa kuendelea kuamini hawa mafisadi na kuwatetea umebarikwa lazima uwe na karama furani. Vipi Lucifer mzima?
 
Kwanza na yeye na famili yake wamepewa Tenda ya Parking service kwa Upendeleo, pili naomba wawe na mikataba ya wazi na Staff wao, tatu wawajibike kuziendeleza hizo parking.
Nne hiyo nyumba ya Serekali aliyo uziwa , je Bei yake ni Halali??? kutokana na Valuation???
 
Hapa kuna waliopo madarakani na wanaotaka kuwepo madarakani,nafadhaishwa na mwenendo huu,rejeeni alichofanya The Late Oscar Salathiel Kambona siku aliporejea toka exile,alitamka kwa kinywa kuwa Julius na akina Kawawa,Jamal n.k wana mapesa Switzerland,Mwalimu alimpa rafiki yake Kambona siku 7 kama zilivyokuwa zama zile za Lyatonga kuthibitisha,what happened? Sasa tumewasikia akina Nyepesi na Siraha toka mjengoni na yao,facilitator wa Muafaka naye kasema yake , hatujui na hili nalo lina picha ipi,ila nina kaushauri kadogo kwa wote,kuna kawimbo kazuri sana hasa ktk maharusi na mwaka mpya:ZAENI MATUNDA MEMA.........
Nimemsoma na napenda nimnukuu huyu muungwana;I don't know what your destiny will be, but one thing I know. The only ones among you who will be trully happy are those who sought and found how serve-Albert Schweitzer

"The only thing we have to fear is fear itself." – FDR
 
Mzee Kingunge ni kweli ilikuwa lazima wewe ukaingia katika mapambano haya. Ama unataka kuwakumbusha kuwa wakati wa kukuangalia machoni umepita na sasa waanze kukuanika wewe na familia yako. Mzee vijana wa kupgelea matope haya wapo wengi haina haja ya wewe kuingia humo....

Bado tunatambua umuhimu wa busara zako hata kama zimejiegesha katika kulinda mfumo.

Salamu zikufikie, Vijana wako bado tunaamini Kamarade hazeeki....
 
Mtu wa pwani,

Huo uvivi alioutoa ameupata wapi? hata mtoto mdogo sasa anajua kuwa jamaa ni mafisadi tunachosubiri tu mtu wa kutuanzishia njia ya kuwatoa kama walivyofanya watu wa Romania. Kama baba yako ni moja ya hao mafisadi anza kukimbilia Dubai.

Any way hongera bado kwa kuendelea kuamini hawa mafisadi na kuwatetea umebarikwa lazima uwe na karama furani. Vipi Lucifer mzima?

mazaga zaga mengine...mhhm!
 
Huyu mzee aangalie naona anapiga tik-tak akiwa amevaa msuli. Hivi na ile orodha ya wauza unga iko wapo tuone yeye na familia yake wako wapi?
 
Hawezi kuona alama zimeandikwa ukutani, ni wakati wake sasa kuvaa life jacket na kujitosa kwenye maji ili aokoe maisha yake.
 
saa tunachoamini kuwa vyama vya upinzani wanawaanika waovu? na jee wanao ushahidi au ndio kutafuta mass?

kama wana data kwa nn hawaendi mahakamani na vyombo vyengine vinavyohusika ?

hapo tukajua kweli wana hoja ila hili la kupita na kuhubiri chuki na kuharibiana na kuchafuliana heshima sioni kama lina faida.
 
saa tunachoamini kuwa vyama vya upinzani wanawaanika waovu? na jee wanao ushahidi au ndio kutafuta mass?

kama wana data kwa nn hawaendi mahakamani na vyombo vyengine vinavyohusika ?

hapo tukajua kweli wana hoja ila hili la kupita na kuhubiri chuki na kuharibiana na kuchafuliana heshima sioni kama lina faida.

Mahakamani alipelekwa Dito kesi ikabadilishwa na wasanii kina mkono and the rest..... wewe na hilo kundi lako ndio mnasubiri kesi hii huko mahakani... kwa sasa kesi iko kwa wananchi na wataamua wenyewe kama wanavyoamua kila siku vibaka wakishikwa!
 
aah nimekupata kumbe huna imani na vyombo vya adala Tanzania? basi waambie hao Chadema wasiingie bungeni maana wao ndio wanapita kuwaambia wananchi au na wao wanajali matumbo yao?

kaazi, hata hivyo mambo yamo kwenda jana sio leo tumo tunapiga hatua.
 
Mtu wa Pwani
huko nyuma kuna mahali nimesema ukipeleka kesi ya nyani ka ngedere unategemea nini? wewe unadhani mahakama za Tanzania zina uhuru. Mara ngapi serikali imekiuka uamuzi wa mahakama kuu na mahakama ya rufaa. Kama uko US au Ulaya nadhani uliondoka hapa Bongo zamani sana, hapa bongo Rais na mawaziri wake ni Mungu wa pili, they can do anything in this country isipokuwa kumbadilisha msichana kuwa mvulana au kumfufua mtu. Hii ndio bongo bwana.
 
Back
Top Bottom