Tanzania: Utawala bora vs Rushwa

Tanzania: Utawala bora vs Rushwa

Kingunge asikitishwa na madai ya rushwa ya upinzani.

Serikali imepinga hayo maadai. na aliyepinga ni Kingunge.

Habari zaidi

Staye Tunned!
 
hako kajizee kamezoea propaganda tuu na sijui bado kanafanya nini naona kanataka kufia ofisini...kaache waliotajwa wajitetee wenyewe kama wanaona kuna cha kujitetea,yaani kamenichafua ile mbaya
 
Kingunge amesema.

  • Wapinzani wanaichafua Serikali, Chama na taifa kwa Ujumla.
  • Wao wapinzani waendele kuzunguka kwani hakuna kazi inigne wanayofanya.
  • Wao Wanakazi nyingi za kufanya
Vitu vingine vingi ameweza kuongea, lakini taarifa ya habari ya TVT ndio hicho nilichosikia.
 
Niliwahi kuota ndoto utotoni kwamba kuna watu watakuwa wanapelekwa ofisini kwa machela maana inaonekana kuwa wana akili za dhahabu na maneno ya shaba ila naamini kuwa kabla yao nchi ilikuwepo na itaendelea kuwepo baada ya wao....

Kingunge ameshazeeka na anatakiwa aache siasa na kupumzika kama mwenzake kawawa...
 
Mbona BBC wamemuweka live jioni hii Kingunge.. kachoka hadi sauti!

Kwangu mimi sikuona lolote la maana alilo ongea zaidi ya kupiga debe, tena la kujikanganya kwamba CCM haina rushwa wakati mpaka sasa wanakimbizwa mahakamani kwa tuhuma za rushwa!

Na alipo jikanganya zaidi kwamba kudai katiba mpya ni sera ya chama?? kwamba wapinzani hawapaswi kudai katinba mpya, bali wawaeleze wananchi kwamba mkituchagua tutaleta katiba mpya?

Huyu babu kachoka mbaya.. apumzike tu!

Nilipo furahi ni maoni ya wananchi yanayo rushwa moja kwa moja ambap hawakumkopesha kwa kumwambia kwamba asidhani watanzania bado wamelala, ufisadi tunauona!

Lakini Pia Zitto alivo hojiwa, naye kajieleza kwa umahiri mkubwa na kuweka wazi kwanini wameamua kusema kwa wananchi na kwamba si jukumu lao kupeleka PCCB, bali PCCB ndo wanajukumu la kufatilia tuhuma zinatolewa!
 
Ngoja niwaambie kitu. Baada ya Ofisi ya Waziri Mkuu kukurupuka kujibu hoja ya "kupaa" na baada ya Maelezo kukurupuka na kujibu suala la "kuitwa wasanii" CCM wameamua kutumia njia nyingine kabisa nayo ni kupuuza. Kwa siku za karibuni angalieni na mtaona kuwa hawajibu hoja tena isipokuwa kutoa kauli za "kupuuzia". Hili la kina Dr. Slaa ni mwanzo tu.

Chochote ambacho kitasemwa na wananchi watawala wetu watajibu kwa kejeli na kudharau, hawataenda mahakamani kudai defemation, hawataandika makala kujibu tena, watawatumia kina Kingunge, Makamba na wapambe wao kutoa kauli za kejeli na kupuuzia.. mtasikia kauli kama "hao ni wapinzani hawana jingine la kufanya", "wana haki ya kutoa maoni yao na huo ndio uzuri wa demokrasia" Kitu pekee ambacho hawatafanya ni kujibu hoja kwa hoja.

Now, sisi wakosoaji tunabadili mwelekeo pia, mwelekeo ambao utawalazimisha wajibu hoja.
 
... nakuamini mzee. umeona mbali na aluta continua mpaka kieleweke
 
hako kajizee kamezoea propaganda tuu na sijui bado kanafanya nini naona kanataka kufia ofisini...kaache waliotajwa wajitetee wenyewe kama wanaona kuna cha kujitetea,yaani kamenichafua ile mbaya

Wiki iliyopita Muungwana katika sherehe ya kumuaga Ndejembi alirusha dongo ambalo linadhaniwa alimrushia Malecela kwamba waliokula chumvi nyingi ndani ya CCM wang'atuke. Cha kustaajabisha yeye mwenyewe kampa uwaziri Kingunge wakati hastahili hata ujumbe wa nyumba kumi kumi! Ukistaajabu ya Mussa...

Halafu ameshakuwa msemaji wa siri kali! katika kutetea maovu kwamba kwenye siri kali hakuna rushwa!...waache wachezee shilingi chooni na kutofanya mabadiliko ya kweli yatakayowaridhisha wananchi. Ikifika 2010 kama hakuna mabadiliko ya kweli cha moto watakiona.
 
Mwanakijiji, Nakuunga mkono. lakini hawa watu inabidi kutumia sayansi ya hali ya juu ili wananchi waujue ukweli. na kazi hiyo haitakiwa kuwa ya zima moto maana watanzania husahau haraka, inatakiwa iwe endelevu na yenye thibitisho na hoja madhubuti.

Kazi iliyoanza sasa isilegee. Najua CCM wataanza kuwarubuni Viongozi wetu kwa pesa, nadhani pia wajiandae kwa hilo maana hiyo pia ni moja ya michezo yao. Tuwasupport pia wale wote walio mstari wa mbele kupigania Nchi, kifedha, kimawazo n.k
 
Kingunge is a used politician. He was once useful, at least to Mwalimu, as a staunch party ideologue. We discarded the party ideology but forgot to discard this ideologue as well. We are paying the price of that.

Huku "kupuuza" kunakofanywa na CCM kunatokana na "kuhaha". Hawajui wajibuje hasa. Marmo amejaribu kusema ilibidi wapinzani wapeleke taarifa Polisi. Nani kamwambia Polisi hawana taarifa? Kuna kupeleka taarifa Polisi kunakozidi Waziri wa Mapolisi (Lyatonga) kwenda na Mkuu wa Polisi (Mahundi) na kumwonyesha wakosaji wenyewe Uwanja wa Ndege, na Polisi kuwakuta wakosaji wenyewe wameshika kosa mkononi?

Naona CCM inapata kigugumizi kutokana na kufunuliwa hujuma zinazofanywa na viongozi wake wakuu. Wajue hizo ni rasha rasha tu. Mvua zenyewe bado kabisa!

You can cheat some of the people some of the time, but you cannot cheat all the people all the time! Ngojeni magazeti na redio huru, na magazeti na redio za wapinzani zianzishwe na kuimarishwa zaidi halafu mtaona jinsi hujuma zenu zitakavyoanikwa kwa wananchi.
 
Ngoja niwaambie kitu. Baada ya Ofisi ya Waziri Mkuu kukurupuka kujibu hoja ya "kupaa" na baada ya Maelezo kukurupuka na kujibu suala la "kuitwa wasanii" CCM wameamua kutumia njia nyingine kabisa nayo ni kupuuza. Kwa siku za karibuni angalieni na mtaona kuwa hawajibu hoja tena isipokuwa kutoa kauli za "kupuuzia". Hili la kina Dr. Slaa ni mwanzo tu.

Chochote ambacho kitasemwa na wananchi watawala wetu watajibu kwa kejeli na kudharau, hawataenda mahakamani kudai defemation, hawataandika makala kujibu tena, watawatumia kina Kingunge, Makamba na wapambe wao kutoa kauli za kejeli na kupuuzia.. mtasikia kauli kama "hao ni wapinzani hawana jingine la kufanya", "wana haki ya kutoa maoni yao na huo ndio uzuri wa demokrasia" Kitu pekee ambacho hawatafanya ni kujibu hoja kwa hoja.

Now, sisi wakosoaji tunabadili mwelekeo pia, mwelekeo ambao utawalazimisha wajibu hoja.

Nadhani njia hii ni mbaya zaidi kwao; walichokosea mwanzo ni kukurupuka kujibu kisiasa badala ya kuja na facts za maana. Kwa kuamua kukaa kimya ndipo watakuwa wanajichimbia kaburi zaidi kwa vile wataruhusu wananchi walishwe facts zote kikamilifu ambayo haitawasaidia wao kama viongozi.
 
Mwalimu ni mbaya, lakini wamepiga mahesabu kuwa wakiendelea kutekeleza Ilani (it doesn't matter kwa kiasi gani) basi wanauhakika wakifika 2009 kwenda kwenye uchaguzi basi watauza "mafannikio" against any accusations against them.
 
Jambo moja watakuwa wanasahau ni kuwa ushindi wote unaopatikana kwa CCM siku zote umekuwa hausababishwi na sera au Ilani, ila unasababishwa na kutokuwapo kwa upinzani ambao ni alternative nzuri. Kwa hiyo wakiruhusu upinzani kuwaonyesha wananchi kuwa wanaweza kufanya vizuri zaidi ya CCM kwa kutoa nje makosa ya CCM ambayo yasingefanywa na wapinzani, basi watakuwa wameruhusu upinzani kupiga hatua kubwa sana dhidi ya CCM minus mizengwe ya uchaguzi.

Kumbuka kuwa hili la wizi wa madini linaingia sana akilini mwa wananchi kuliko sera za kujenga sekondari zisizokuwa na waalimu.
 
Jambo moja watakuwa wanasahau ni kuwa ushindi wote unaopatikana kwa CCM siku zote umekuwa hausababishwi na sera au Ilani, ila unasababishwa na kutokuwapo kwa upinzani ambao ni alternative nzuri. Kwa hiyo wakiruhusu upinzani kuwaonyesha wananchi kuwa wanaweza kufanya vizuri zaidi ya CCM kwa kutoa nje makosa ya CCM ambayo yasingefanywa na wapinzani, basi watakuwa wameruhusu upinzani kupiga hatua kubwa sana dhidi ya CCM minus mizengwe ya uchaguzi.

Kumbuka kuwa hili la wizi wa madini linaingia sana akilini mwa wananchi kuliko sera za kujenga sekondari zisizokuwa na waalimu.

Hapo nimekuelewa,tena hilo mie nilikuwa silijui,ccm kuchaguliwa mara zote si kwa sababu ya sera zao au ilani ya chama,ni kwa sababu kulikua hakuna upinzani ulionyesha imani kwa raia.Ilikua rahisi kuwarubuni wapinzani na vipesa,kwa hiyo wananchi waliona wapinzani kama wasaliti,mfano Lamwai,na wenzake wote waliorudi ccm.Ila leo hii upinzani umejiimarisha kuna damu mpya,pia mwamko wa wananchi upo juu sana,mawasiliano yamekua rahisi sana,uozo ukifanyika tunaujua mara moja,wafanyakazi wa serikali wamechoka na mishahara midogo.Huu upuuzi wa huyu mzee Kingunge asiyekuwa na dini,tunamuambia asome alama za nyakati,vinginevyo atakuja kufa kwa pressure pale 2010 huo upinzani anaoudharau ukiwa na viti 50% bungeni,tena vijana wenye damu changa wasiogopa kitu.Angalia sana Kingunge huo utumbo kale mwenyewe,kwanza wamekusamehe kutokukutaja kwenye orodha ya hao matapeli.Mie nachukua nafasi hii kusema,nawe Kingunge unamechangia katika maamuzi kudhoofisha taifa letu,nawe ni mla rushwa.
 
Unajua kuna kitu kimoja ambacho wapinzania wanatakiwa kukua. The battle ground on graft should not only be confined at home, they should go abroad Brussels, London or Washington. By doing so inaweza kuongeza nguvu. Ni kweli watanzania walio wengi wakisikia Kingunge akisema aaaaaahhhhhhhhhh ni uzushi tu, au wakisikia Makamba anasema aahhh wanakichafua chama wanaweza kuamini. Pamoja na kuwa Slaa amesema aliyosema unaweza kushangaa kuwa Slaa anachafuliwa na kuonekana hana maana tena. Nadhani approach ya Seifu ilikuwa nzuri sana, ilifanya crisis ya Zanzibar ijulikane world over na serikali ikalazimika kuanza na talks. Lakini Kama slaa akiishia hapo tu nadhani haitatusaidia sana, lakini it is a good thing that he put things in public, japokuwa kwa watanzania wachache wanaojua it is same old story, may be sasa hatua zitaweza kuchukuliwa.
Lakini kutokana na kuwa sasa hivi serikali imefungwa mikono sidhani kama inaweza kufanya kitu, i do not see JK taking actions against Mramba, Balali, Karamagi, Chenge au Mkono. Sana sana atakachofanya ni kuwaondoa uwaziri lakini hakuna la zaidi atakalofanya. Can he put them behind bars? nadhani aliykuwa anaongea na Condi ni kuwageresha donors tu, and Tanzania has been doing best on that.
 
Bongolander umesoma kweli hiyo list? JK atawaajibishaje watu na wakati yeye ndiye ametajwa kuwa mhujumu wa juu kabisa? Ametajwa kuwa Waziri aliyetumia FFU kuwanyanganya wananchi mali yao LUSU na kuwapa SAMAX (mali ambayo mara ikauzwa kwa US$253 mil.) na kutumia jeshi kupora mali ya wananchi Bulyanhulu na kuwapa Sutton Resources (mali ambayo nayo mara ikauzwa kwa US$ 280 mil.).

Wakiambiana ambaye hana dhambi ndiye atupe jiwe la kwanza, wataondoka kwa aibu wote, wakitangulia wazee.
 
Kingunge is a used politician. He was once useful, at least to Mwalimu, as a staunch party ideologue. We discarded the party ideology but forgot to discard this ideologue as well. We are paying the price of that.

Huku "kupuuza" kunakofanywa na CCM kunatokana na "kuhaha". Hawajui wajibuje hasa. Marmo amejaribu kusema ilibidi wapinzani wapeleke taarifa Polisi. Nani kamwambia Polisi hawana taarifa? Kuna kupeleka taarifa Polisi kunakozidi Waziri wa Mapolisi (Lyatonga) kwenda na Mkuu wa Polisi (Mahundi) na kumwonyesha wakosaji wenyewe Uwanja wa Ndege, na Polisi kuwakuta wakosaji wenyewe wameshika kosa mkononi?

Naona CCM inapata kigugumizi kutokana na kufunuliwa hujuma zinazofanywa na viongozi wake wakuu. Wajue hizo ni rasha rasha tu. Mvua zenyewe bado kabisa!

You can cheat some of the people some of the time, but you cannot cheat all the people all the time! Ngojeni magazeti na redio huru, na magazeti na redio za wapinzani zianzishwe na kuimarishwa zaidi halafu mtaona jinsi hujuma zenu zitakavyoanikwa kwa wananchi.

Maoni haya ni mazuri kweli kweli. Umemalizia kwa kuzungumzia vyombo vya habari hur? Haviwezekani Tz bila kuondoa sheria mbaya zilizopo zinazowashika waandishi mikono na midomo.
 
Unajua kuna kitu kimoja ambacho wapinzania wanatakiwa kukua. The battle ground on graft should not only be confined at home, they should go abroad Brussels, London or Washington. By doing so inaweza kuongeza nguvu. Ni kweli watanzania walio wengi wakisikia Kingunge akisema aaaaaahhhhhhhhhh ni uzushi tu, au wakisikia Makamba anasema aahhh wanakichafua chama wanaweza kuamini. Pamoja na kuwa Slaa amesema aliyosema unaweza kushangaa kuwa Slaa anachafuliwa na kuonekana hana maana tena. Nadhani approach ya Seifu ilikuwa nzuri sana, ilifanya crisis ya Zanzibar ijulikane world over na serikali ikalazimika kuanza na talks. Lakini Kama slaa akiishia hapo tu nadhani haitatusaidia sana, lakini it is a good thing that he put things in public, japokuwa kwa watanzania wachache wanaojua it is same old story, may be sasa hatua zitaweza kuchukuliwa.
Lakini kutokana na kuwa sasa hivi serikali imefungwa mikono sidhani kama inaweza kufanya kitu, i do not see JK taking actions against Mramba, Balali, Karamagi, Chenge au Mkono. Sana sana atakachofanya ni kuwaondoa uwaziri lakini hakuna la zaidi atakalofanya. Can he put them behind bars? nadhani aliykuwa anaongea na Condi ni kuwageresha donors tu, and Tanzania has been doing best on that.

Ushukuriwe kwa tathmini mwafaka kuhusu hatua wanazopaswa kuchukua wapinzani.

Tazama hayo maneno niliyowekea bold. Jk mwenyewe ni mtuhumiwa mwenzao, yuko kundi moja nao, hawezi kuachukua hatua kwa wenzie! kwi kwi kwi
 
Back
Top Bottom