Mkuu mkonga umekuja Kuongeza Speed na capacity, mfano Kwa TTCL kabla ya Mkonga walikuwa wakitumia Simu ( Adsl) ila siku hizi wana njia za kisasa zaidi sababu Ya mkonga hivyo wameweza kuunganisha Taasisi nyingi.
Na zamani kabisa mkuu hakukuwa na internet kabisa, enzi za mwalimu. Internet imeingia Africa 1995, na huku kwetu internet za mwanzo zilikuwa ni satelite tena tunaziona ziona tu kwenye mashirika kama World vision ukipita nje ya Ofisi zao unakuta Dishi kubwa.
Then zikafuatia Hizo internet za Simu aka Dial up Connection, speed mwendo wa Kobe, zenyewe TTCL wanakuletea simu ya Mezani nyumbani, kupitia hio simu ndio unapata Internet. Zilikuwa zikitumia zile waya zao za shaba za namna hii
Halafu baadae zikaja hizo fiber ila hazikuwa zikitosheleza, mpaka leo fiber zinaongezeka moja wapo ikiwa ni huo mkonga.