Tanzania tunanunulia wapi/nchi gani Internet?

Tanzania tunanunulia wapi/nchi gani Internet?

Emmet

Member
Joined
Jan 18, 2019
Posts
83
Reaction score
169
Habari za mda huu waungwana,

Leo nimetamani nijifunze jambo jipya! Naomba nifahamishwe Internet Service Provider (ISP) wetu ni nani na njia gani imetumika mpaka internet ikatufikia hapa nchini?
 
watu wa kwanza kabisa kutumia hii kitu duniani ni wamarekani wapi tunakoitoa sisi tusubiri wajuvi waje
 
Habari za mda huu waungwana,

leo nimetamani nijifunze jambo jipya! Naomba nifahamishwe Internet Service Provider (ISP) wetu ni nani na njia gani imetumika mpaka internet ikatufikia hapa nchini?
Wanaweza tumia njia kama
1. Satelite Internet, sema hii haitumiki sana ni kama backup tu.

2. Cable za Chini ya Bahari ama Nchi kavu, angalia hii picha kwa list ya provider

cable_map51_EN-1.png

Ukisikia mkonga wa Taifa ndio hizo cable, zinakuwa na bandwidth za maana, zaidi ya Terabyte kwa sekunde, kuna moja hapo inaenda hadi terabit 100.

Hizo cable ndio Internet Servoce Provider wanatumia kuunganisha na nje ya Bara la Africa.
 
Wanaweza tumia njia kama
1. Satelite Internet, sema hii haitumiki sana ni kama backup tu.

2. Cable za Chini ya Bahari ama Nchi kavu, angalia hii picha kwa list ya provider
View attachment 1523682
Ukisikia mkonga wa Taifa ndio hizo cable, zinakuwa na bandwidth za maana, zaidi ya Terabyte kwa sekunde, kuna moja hapo inaenda hadi terabit 100. Hizo cable ndio isp wanatumia kuunganisha na nje ya Bara la Africa.
Kumbe duniani Bado sana! Bado tunatumia mi waya!
 
Waya unaspeed sana tena sana sana sana compare na wireless,

Kuna kipindi fulani miaka kama 8 ama 9 iliopita meli iligonga hizo waya network ya internet ikakata nchi nzima, na baadhi ya mitandao kama voda wakaswitch kwenda satelite, ilikuwa slow balaa.
So tupo kwenye right position..?

Mi naona ni mbinu tu za wafanyabiashara wa hiyo miwaya!.. itachukua muda kuja kubadili mwenendo..
 
Wanaweza tumia njia kama
1. Satelite Internet, sema hii haitumiki sana ni kama backup tu.

2. Cable za Chini ya Bahari ama Nchi kavu, angalia hii picha kwa list ya provider
View attachment 1523682
Ukisikia mkonga wa Taifa ndio hizo cable, zinakuwa na bandwidth za maana, zaidi ya Terabyte kwa sekunde, kuna moja hapo inaenda hadi terabit 100. Hizo cable ndio isp wanatumia kuunganisha na nje ya Bara la Africa.
Very informative Salute kiongoz
 
Hapana Aisee, na waya Ndio rahisi zaidi kuliko wireless, zikitandazwa hizo kila eneo internet inakuwa bei ya maandazi,
Chief hapa unamaanisha wireless ni expensive ukilimganisha na wire? Au nimeelewa tofauti?
 
Waya unaspeed sana tena sana sana sana compare na wireless,

Kuna kipindi fulani miaka kama 8 ama 9 iliopita meli iligonga hizo waya network ya internet ikakata nchi nzima, na baadhi ya mitandao kama voda wakaswitch kwenda satelite, ilikuwa slow balaa.
Wambie hawaoni tu Television signal za sattelite zinavyosumbua hata yakiwepo mawingu kidogo. Same sattelite internet lazima iathiriwe na hali ya Hewa
 
ndio mkuu wireless ni expensive, sababu wireless haina bandwidth kubwa kushinda waya. unaweza ukapitishwa waya mmoja tu mtaani wa 10gbps na mtaa mzima mkawa na internet ya maana.
Hivi huu mkonga wa taifa si ulishaanza kazi tz?
Mbona speed ileile, bei zinazidi kupanda nk

Wakati tuliambiwa mkonga ukianza kazi soeed itapaa na bei itashuka
 
Wanaweza tumia njia kama
1. Satelite Internet, sema hii haitumiki sana ni kama backup tu.

2. Cable za Chini ya Bahari ama Nchi kavu, angalia hii picha kwa list ya provider
View attachment 1523682
Ukisikia mkonga wa Taifa ndio hizo cable, zinakuwa na bandwidth za maana, zaidi ya Terabyte kwa sekunde, kuna moja hapo inaenda hadi terabit 100. Hizo cable ndio isp wanatumia kuunganisha na nje ya Bara la Africa.
Kwanini service inaletwa kwa cable halafu tunakuja kusambaziwa kwa wireless?
 
Wanaweza tumia njia kama
1. Satelite Internet, sema hii haitumiki sana ni kama backup tu.

2. Cable za Chini ya Bahari ama Nchi kavu, angalia hii picha kwa list ya provider
View attachment 1523682
Ukisikia mkonga wa Taifa ndio hizo cable, zinakuwa na bandwidth za maana, zaidi ya Terabyte kwa sekunde, kuna moja hapo inaenda hadi terabit 100. Hizo cable ndio isp wanatumia kuunganisha na nje ya Bara la Africa.
Hizo cable zinachukua Internet kutoka wapi?
 
Hivi huu mkonga wa taifa si ulishaanza kazi tz?
Mbona speed ileile, bei zinazidi kupanda nk

Wakati tuliambiwa mkonga ukianza kazi soeed itapaa na bei itashuka
mkuu kusema kweli huku mijini wameitandaza sana internet na speed si haba, sasa hivi ukienda Kariakoo maduka mengi yana fiber, hata mitandao yetu kama Halotel na Voda speed zao za 4g ni zaidi ya average speed ya dunia.

tatizo ni kwamba ipo katikati ya majiji tu ukitoka nje kidogo tu hakuna fiber na hata hizo 4g zinaanza kupotea, hivyo wanaofaidika wanakuwa ni wachache.
 
Kwanini service inaletwa kwa cable halafu tunakuja kusambaziwa kwa wireless?
sababu ni rahisi wireless kufikia watu kuliko cable, mfano imagine uswahilini utatandaza vipi cable? ama magari yanayotembea, watu wanaotembea etc, hivyo cable zinaleta mpaka mahala fulani halafu wireless inamalizia ili kuhakikisha kila mtu anafikiwa.
 
Hizo cable zinachukua Internet kutoka wapi?
hakuna eneo maalumu maana kazi yake ni kuzungusha tu hizo data kwenda maeneo mbalimbali, mfano

- unaangalia youtube, umesearch video ya kiba, ile request yako itapelekwa na waya hadi server za youtube marekani, kisha kule marekani itachukuliwa ile video na huo waya na kuletwa hadi Tanzania.

-unachat na rafiki yako china kwa snapchat, inamaana waya utapeleka msg yako kwenye server za snapchat marekani, kisha waya mwengine utachukua na kumpelekea msg yule rafiki yako wa china

hivyo kazi za hizo waya ni kusafirisha tu taarifa baina ya watumiaji na servers mbalimbali duniani, internet inazunguka dunia nzima hakuna aneimiliki ni kama vile barabara, Tanzania tuna miundo mbinu yetu, Kenya wana yao, Usa wana yao, China wana yao etc then kuna makampuni ya kimataifa yanaunganisha miundo mbinu ya nchi mbalimbali pamoja
 
hakuna eneo maalumu maana kazi yake ni kuzungusha tu hizo data kwenda maeneo mbalimbali, mfano

- unaangalia youtube, umesearch video ya kiba, ile request yako itapelekwa na waya hadi server za youtube marekani, kisha kule marekani itachukuliwa ile video na huo waya na kuletwa hadi Tanzania.

-unachat na rafiki yako china kwa snapchat, inamaana waya utapeleka msg yako kwenye server za snapchat marekani, kisha waya mwengine utachukua na kumpelekea msg yule rafiki yako wa china

hivyo kazi za hizo waya ni kusafirisha tu taarifa baina ya watumiaji na servers mbalimbali duniani, internet inazunguka dunia nzima hakuna aneimiliki ni kama vile barabara, Tanzania tuna miundo mbinu yetu, Kenya wana yao, Usa wana yao, China wana yao etc then kuna makampuni ya kimataifa yanaunganisha miundo mbinu ya nchi mbalimbali pamoja
Nimekupata mkuu.
 
Back
Top Bottom