President of China
JF-Expert Member
- Dec 6, 2018
- 31,546
- 89,514
Tanzania imeunga mkono ajenda zote muhimu zilizojadiliwa katika Mkutano wa Tisa wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR).
Makamu wa Rais, Balozi Dk Emmanuel Nchimbi alisema hayo wakati akimwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan kwenye mkutano huo uliofanyika Kinshasha nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).
Alisema Tanzania inaunga mkono ajenda zote muhimu, ikiwemo ya amani na usalama na kusisitiza kuwa itaendelea kutoa mchango mkubwa kama inavyofanya katika nchi mbalimbali kuhakikisha kuwa amani ya kweli inapatikana kwenye kanda hiyo. Mkutano huo ulitanguliwa na vikao vya wataalamu, wakuu wa vyombo vya ulinzi pamoja na Kamati za Mawaziri wa Kisekta, ikiwemo ulinzi, madini na jinsia.
Mkutano huo umebebwa na Kaulimbiu ya “Uimarishaji wa Amani na Usalama kwa Maendeleo Endelevu katika Eneo la Maziwa Makuu.” Kupitia kaulimbiu hiyo, nchi wanachama zimejadili hali ya usalama katika Ukanda wa Maziwa Makuu na kupendekeza njia za kuimarisha amani na usalama kwenye eneo hilo.
Makamu wa Rais, Balozi Dk Emmanuel Nchimbi alisema hayo wakati akimwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan kwenye mkutano huo uliofanyika Kinshasha nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).
Alisema Tanzania inaunga mkono ajenda zote muhimu, ikiwemo ya amani na usalama na kusisitiza kuwa itaendelea kutoa mchango mkubwa kama inavyofanya katika nchi mbalimbali kuhakikisha kuwa amani ya kweli inapatikana kwenye kanda hiyo. Mkutano huo ulitanguliwa na vikao vya wataalamu, wakuu wa vyombo vya ulinzi pamoja na Kamati za Mawaziri wa Kisekta, ikiwemo ulinzi, madini na jinsia.
Mkutano huo umebebwa na Kaulimbiu ya “Uimarishaji wa Amani na Usalama kwa Maendeleo Endelevu katika Eneo la Maziwa Makuu.” Kupitia kaulimbiu hiyo, nchi wanachama zimejadili hali ya usalama katika Ukanda wa Maziwa Makuu na kupendekeza njia za kuimarisha amani na usalama kwenye eneo hilo.