East African Eagle
JF-Expert Member
- Jul 26, 2013
- 3,759
- 2,209
Jana nilimsikia Museveni akiongea kwa tahadhari kubwa kuwa Tanzania haijatengwa bali kwa sasa wanashughulikia Northern Corridor yaani Mombasa - Kampala - Kigali! Baadaye watashughulikia Southern Corridor yaani Dar - Tabora-Kigoma - Mwanza!
Ni kweli MUSEVENI alikuwa makini mno.Hata alipoulizwa na mwandishi wa habari kuwa Kuna kiongozi wa Tanzania alisema kile kikao chao kilikuwa illegal kulingana na makubaliano ya EAC alijibu kuwa hafanyi kazi kupitia waandishi wa habari hadi atakapopata barua rasmi kutoka kwa huyo kiongozi ndio atajibu kwani waandishi wa habari mara nyingi waongo.
Kwa ujumla MUSEVENI alikuwa makini mno kuepuka maswali mtego yaliyoilenga Tanzania.
Nafikiri anakumbuka wema nchi iliomfanyia.Mzee Kawawa alimkabidhi dola 50,000 zimsaidie kuanza vita Uganda ashike nchi.Pale alionekana ndiye kinara wa kujibu maswali na alikuwa katulia mno.Yale maswali yangeenda kwa Kagame au Kenyatta sijui wangejibuje?