Tanzania haijaolewa EAC - Samwel Sitta

Tanzania haijaolewa EAC - Samwel Sitta

Hatupendwi kwa sababu ya uropokaji na shallow mind ya viongozi wetu
 
3:50:45 AM Yaliyopita Pekua Tovuti
Sitta: Hatujaolewa EAC
• ASEMA WATAWAMWAGA KAGAME,
MUSEVENI, KENYATA
na Salehe Mohamed, Dodoma
WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Samuel Sitta, amesema Tanzania itatoa talaka
kwa nchi za Rwanda, Kenya na Uganda ambazo
zimeamua kuanzisha Jumuiya ya hiari nje ya
Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Sitta alisema kutokana na nchi hizo kuonekana
kuitenga Tanzania na Burundi ambazo ni
wanachama wa jumuiya hiyo, wameshaanza
mazungumzo ya kushirikiana kiuchumi, kisiasa
na nchi za Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia
ya Watu wa Congo (DRC).
Kauli hiyo ya Sitta inatokana na mikutano ya
mara kwa mara inayofanywa na marais Uhuru
Kenyata wa Kenya, Paul Kagame (Rwanda) na
Yoweri Museveni (Uganda) kuzungumzia
masuala mbalimbali ya kushirikiana nje ya
Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Waziri Sitta alibainisha msimamo wa Tanzania
kutengwa na nchi hizo tatu jana bungeni,
alipokuwa akijibu maswali ya wabunge
mbalimbali waliokuwa wakitaka kujua kauli ya
serikali juu ya vikao vinavyofanywa na marais
hao watatu.
Mbunge wa Viti Maalumu Rukia Ahmed (CCM),
aliitaka serikali ipeleke pendekezo bungeni la
kujitoa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki
kabla haijapewa talaka kutoka kwa Rwanda,
Uganda na Kenya ambazo zimekuwa zikifanya
mikutano inayojadili masuala ya jumuiya bila
kuihusisha serikali ya Tanzania.
Akijibu hoja hiyo Sitta, alisema ni mapema kwa
Tanzania kupeleka bungeni hoja ya kujitoa
katika jumuiya hiyo kwa kuwa kinachofanywa
na nchi hizo kimeshafikishwa kwa Mwenyekiti
wa Baraza la Mawaziri wa nchi wanachama
ambaye atakitolea ufafanuzi katika kikao
kitakachofanyika wiki mbili zijazo.
Sitta alifafanua kauli ya Waziri mwenzake wa
Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,
Bernard Membe, hivi karibuni ya kwamba
Tanzania inasubiri talaka akisema yenyewe
ndiyo yenye uwezo wa kutoa talaka kwa
jumuiya hiyo kwa kuwa inamiliki asilimia 52 ya
eneo lote huku nchi zilizobakia zikigawana
asilimia 48 iliyobakia.
“Hawa wenzetu wanafanya utoto wa
kutuzunguka, sisi tunatumia hekima za mzee
Mwinyi aliyesema ‘mwongo, mwongoze’. Kama
wao wana hila zozote juu yetu, siku si nyingi
tutazibaini, kama ni ndoa kwenye jumuiya basi
sisi ndio tutakuwa tumeoa…hivyo tutatoa talaka
wakati wowote,” alisema.
Naye Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango
Malecela (CCM), aliitaka serikali isiendelee na
hatua zozote kwenye jumuiya hiyo ambayo
inaonekana kuelekea kuvunjika.
Akijibu swali hilo, Sitta alisema serikali haijakaa
kimya bali imeamua kutoshiriki vikao vyote
ambavyo nchi za Kenya, Rwanda na Uganda
zitakuwa zimeshayazungumzia masuala husika
na kuamua kuwa na msimamo wa pamoja nje
ya jumuiya.
Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed
(CUF), alihoji serikali inangoja utafiti gani juu
ya kutengwa kwao kiuchumi na nchi hizo tatu
wakati Kenya wameshaingia makubaliano ya
kibiashara na Ethiopia na Sudan.
Katika jibu lake, Sitta alisema Tanzania
imeshafanya mazungumzo na nchi za DRC na
Burundi kushirikiana katika nyanja mbalimbali.
Alisema kuwa DRC ndiyo yenye manufaa
makubwa kiuchumi kwa Tanzania kuliko
Rwanda, Uganda, Kenya na Burundi kwa sababu
mizigo mingi hutegemea bandari ya Dar es
Salaam.
“Burundi nao wanatengwa kama
tunavyofanyiwa sisi, lakini tumeamua
kushirikiana kikamilifu na DRC pamoja na
Burundi ambao tuna imani wana manufaa
makubwa kwetu,” alisema.
Hivi karibuni Tanzania iliingia kwenye mgogoro
na Rwanda baada ya Rais Jakaya Kikwete kutoa
ushauri kwa Rais wa Rwanda, Kagame kuketi
chini na waasi wa nchi hiyo ili kuzungumzia
masuala ya amani kwa nchi yao.
 
WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Samuel Sitta, amesema Tanzania itatoa talaka
kwa nchi za Rwanda, Kenya na Uganda ambazo
zimeamua kuanzisha Jumuiya ya hiari nje ya
Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Sitta alisema kutokana na nchi hizo kuonekana
kuitenga Tanzania na Burundi ambazo ni
wanachama wa jumuiya hiyo, wameshaanza
mazungumzo ya kushirikiana kiuchumi, kisiasa
na nchi za Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia
ya Watu wa Congo (DRC).
Kauli hiyo ya Sitta inatokana na mikutano ya
mara kwa mara inayofanywa na marais Uhuru
Kenyata wa Kenya, Paul Kagame (Rwanda) na
Yoweri Museveni (Uganda) kuzungumzia
masuala mbalimbali ya kushirikiana nje ya
Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Waziri Sitta alibainisha msimamo wa Tanzania
kutengwa na nchi hizo tatu jana bungeni,
alipokuwa akijibu maswali ya wabunge
mbalimbali waliokuwa wakitaka kujua kauli ya
serikali juu ya vikao vinavyofanywa na marais
hao watatu.
Mbunge wa Viti Maalumu Rukia Ahmed (CCM),
aliitaka serikali ipeleke pendekezo bungeni la
kujitoa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki
kabla haijapewa talaka kutoka kwa Rwanda,
Uganda na Kenya ambazo zimekuwa zikifanya
mikutano inayojadili masuala ya jumuiya bila
kuihusisha serikali ya Tanzania.
Akijibu hoja hiyo Sitta, alisema ni mapema kwa
Tanzania kupeleka bungeni hoja ya kujitoa
katika jumuiya hiyo kwa kuwa kinachofanywa
na nchi hizo kimeshafikishwa kwa Mwenyekiti
wa Baraza la Mawaziri wa nchi wanachama
ambaye atakitolea ufafanuzi katika kikao
kitakachofanyika wiki mbili zijazo.
Sitta alifafanua kauli ya Waziri mwenzake wa
Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,
Bernard Membe, hivi karibuni ya kwamba
Tanzania inasubiri talaka akisema yenyewe
ndiyo yenye uwezo wa kutoa talaka kwa
jumuiya hiyo kwa kuwa inamiliki asilimia 52 ya
eneo lote huku nchi zilizobakia zikigawana
asilimia 48 iliyobakia.
“Hawa wenzetu wanafanya utoto wa
kutuzunguka, sisi tunatumia hekima za mzee
Mwinyi aliyesema ‘mwongo, mwongoze’. Kama
wao wana hila zozote juu yetu, siku si nyingi
tutazibaini, kama ni ndoa kwenye jumuiya basi
sisi ndio tutakuwa tumeoa…hivyo tutatoa talaka
wakati wowote,” alisema.
Naye Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango
Malecela (CCM), aliitaka serikali isiendelee na
hatua zozote kwenye jumuiya hiyo ambayo
inaonekana kuelekea kuvunjika.
Akijibu swali hilo, Sitta alisema serikali haijakaa
kimya bali imeamua kutoshiriki vikao vyote
ambavyo nchi za Kenya, Rwanda na Uganda
zitakuwa zimeshayazungumzia masuala husika
na kuamua kuwa na msimamo wa pamoja nje
ya jumuiya.
Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed
(CUF), alihoji serikali inangoja utafiti gani juu
ya kutengwa kwao kiuchumi na nchi hizo tatu
wakati Kenya wameshaingia makubaliano ya
kibiashara na Ethiopia na Sudan.
Katika jibu lake, Sitta alisema Tanzania
imeshafanya mazungumzo na nchi za DRC na
Burundi kushirikiana katika nyanja mbalimbali.
Alisema kuwa DRC ndiyo yenye manufaa
makubwa kiuchumi kwa Tanzania kuliko
Rwanda, Uganda, Kenya na Burundi kwa sababu
mizigo mingi hutegemea bandari ya Dar es
Salaam.
“Burundi nao wanatengwa kama
tunavyofanyiwa sisi, lakini tumeamua
kushirikiana kikamilifu na DRC pamoja na
Burundi ambao tuna imani wana manufaa
makubwa kwetu,” alisema.
Hivi karibuni Tanzania iliingia kwenye mgogoro
na Rwanda baada ya Rais Jakaya Kikwete kutoa
ushauri kwa Rais wa Rwanda, Kagame kuketi
chini na waasi wa nchi hiyo ili kuzungumzia
masuala ya amani kwa nchi yao.

source: tanzania daima
 
Ninavyoona mimi nikuwa! Hakuna haja kuwa kwenye shirikisho na nchi ambazo hazikutaki! Kama wao wameamua kujiunga nchi tatu, namaanisha, Kenya, Rwanda na Uganda wakati shirikisho lina nchi zaidi ya hizo! Mi naona TZ iungane na nchi zilizobaki na maisha ya endelee! Hizi ni nchi ambazo ni wapinzani wakubwa kiuchumi! Na wangependa waendelee kuwa juu ya TZ! Na sababu hizi hizi nakumbuka ndizo zilizoua EAC,1977! Na sababu ilikuwa ni nchi ya kenya kwa hiyo hawa jamaa asili yao ni wabinafsi! Na wanajifanya wana akili sana, mi naona tuachane nayo! Tujipange kivyetu!

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Hatutaki kukaa eda siku 30 tunasubiri kama atatoa rejea, tumemchoka, hatumtaki tena huyu bwana Kenya na wake wenza wanne.
 
Sita na Membe wanalenga kitu kimoja hapa sema tu Sita kaliweka kimajungu ili kumkosoa mwenzake, cha msingi ni kwamba EAC ilishavunjika tukaachiwa majengo tu Arusha kwa sasa tusimame kwenye maamuzi yetu tu kama Watanzania...tunayo SADC and we are very active there.
 
Msimamo wa serikali yetu ni mzuri na mahususi. Hakuna haja ya kulialia bali ni kuangali DRC na BURUNDI na kuunda umoja wetu wa Africa mashariki nyingine imara. Pia, Malawi na Zambia tuwajongelee zaidi na zaidi kwa kuimarisha mashirikiano yetu nao.
 
President Jakaya Kikwete of Tanzania and Pierre Nkurunziza of Burundi stayed out of the loop of the third infrastructure summit in Kigali, Rwanda but their absence loomed large in the conference room.



President Museveni told journalists in a brief press conference on Monday that talk of a "coalition of the willing" involving Uganda, Rwanda and Kenya was inaccurate since the three countries were only discussing infrastructure projects along the northern corridor and would involve Tanzania once discussions moved to the southern corridor.



However, the final communiqué read out after the meeting of the three heads of state did not include an update on efforts to fast-track the East African political federation, a matter whose discussion outside the East African Community Tanzanian officials have expressed concern over.



At the last infrastructure summit in Mombasa Uganda was tasked to spearhead efforts to fast-track the political federation and a committee headed by the country's Internal Affairs Minister Gen. Aronda Nyakairima met in Kampala this month to kick-start the writing of a draft constitution. They had been expected to provide an update to the summit on Monday.



Gen. Nyakairima on Monday declined to comment on the exercise while Kenya's East African Affairs, Commerce and Tourism minister Phyllis Kandie said talk of a political federation was a "side-show" which had not been discussed by the ministers or the heads of state in Kigali.



Tanzania's ministry of East African Cooperation recently issued a statement warning that the tri-lateral talks among Kenya, Rwanda and Uganda are against the EAC protocol.



The statement argued that all EAC member states had to endorse the regional infrastructure deals signed by Presidents Kenyatta, Museveni and Kagame otherwise they contravene Article 7(1) (e) of the EAC protocol.



"Even though this Article allows member countries to enter bi-lateral or Tri-lateral agreements, it is a must that issues under consideration for implementation under this arrangement are fully discussed and agreed upon by all member countries," the statement from the ministry said.



However President Museveni said yesterday he was unaware of complaints from Tanzania about the trilateral agreements.



"Unless I get an official letter from the state, I consider what I see in the press as lies," he said in response to a journalist's question.



Tanzanian diplomats are understood to have expressed their concerns about being left out of the regional plans through the Council of Ministers. Officials in Dar es Salaam say they have not been invited to participate in the Coalition of the Willing and are expected to raise the matter more directly at the next EAC Heads of State Summit in Kampala in late November.



Burundi sent a ministerial delegation to the last summit in Mombasa and President Nkurunziza visited with President Kenyatta a few days later on what was said to be a private visit. We were unable to confirm whether Bujumbura or Dar es Salaam had been invited to Monday's summit.
 
Bungeni leo kwenye kipindi cha maswali na majibu akijubu swali la Mbunge John Komba kuhusu EAC Waziri wa wizara ya Afrika mashariki Mh. Samweli Sitta amesema hakubaliani na kauli ya kusema Tanzania inasubiri talaka kutoka Nchi za Afrika mashariki zinazoonekana kuizunguka EAC.

Waziri Samwel Sitta amesema Tanzania inaeneo la 52% katika eac na nchi zinazobaki zina 48% hivyo akasema katika EAC Tanzania ni muoaji kama litatokea jambo baya Tanzania ndio itatoa Talaka.

Ila Imechumbiwa na kama pia haijachumbiwa basi ndio type ile ya changudoa anayeliwa na kila mtu ili mradi pesa yako tu.
 
Dhana ya kutoa au kupokea talaka,

Membe aliijenga katika mantiki ya kuwa kama mwanandoa unampenda lakini yeye yuko busy na watu wengine ambao hata wewe mwenyewe unawafahamu, ina maana amekuchoka na anachokifanya amedhamiria hivyo haitakuwa ajabu kukupa talaka. Wewe huwezi kumuomba talaka vile unatarajia labda atarudi kwenye akili zake na pia unampemda sana.

Sitta amejenga mantiki yake kuwa kwa vile yeye ndiye mwenye mali nyingi katika ndoa basi yeye ndiye mwenye haki ya kutoa talaka bila kujali kama mwenzie anampenda au la. Kwake kumiiliki mali ndio kete yake ya kufanya maamuzi.

Katika muktadha wa siasa za Bongo kuelekea 2015, hii kauli ya Sitta ina uzito wake katika kutathmini alliances za kisiasa kuelekea 2015
 
haya ni maneno ya ajabu kabisa hawa ndo viongozi wetu na kauli zao za uongo uongo poor ccm
 
Mkuu ime-exclude Kenya hapo? je kwenye GDP ya TZ wote tunazalisha au kwa mawazo yako kwa kuwa tuna population kubwa basi ni soko zuri? how much are we selling to those market achana na wao wanatuuzia nini?Mind you Sitta ameongelea habari za ukubwa wa eneo na wala si faida au hasara tutakayopata kwa ukubwa wa eneo letu, na wewe pia naona unaelekea huko

Nilijibu swali 'what are we benefiting...' Je, una hoja ya kupinga huo kweli au una maswali?
 
Kwa dharau wanakutana kwa bendera ya Africa Masahariki abayobozi_bakuru_uganda_kenya_n_u_rda.jpg
 
Bungeni leo kwenye kipindi cha maswali na majibu akijubu swali la Mbunge John Komba kuhusu EAC Waziri wa wizara ya Afrika mashariki Mh. Samweli Sitta amesema hakubaliani na kauli ya kusema Tanzania inasubiri talaka kutoka Nchi za Afrika mashariki zinazoonekana kuizunguka EAC.

Waziri Samwel Sitta amesema Tanzania inaeneo la 52% katika eac na nchi zinazobaki zina 48% hivyo akasema katika EAC Tanzania ni muoaji kama litatokea jambo baya Tanzania ndio itatoa Talaka.

vilevile by simple logic kwenye polygamous marriage wanawake ndo wengi hatutegemei kwamba Tanzanzania awe ndo mke wakati wao wapo watatu
 
Bungeni leo kwenye kipindi cha maswali na majibu akijubu swali la Mbunge John Komba kuhusu EAC Waziri wa wizara ya Afrika mashariki Mh. Samweli Sitta amesema hakubaliani na kauli ya kusema Tanzania inasubiri talaka kutoka Nchi za Afrika mashariki zinazoonekana kuizunguka EAC.

Waziri Samwel Sitta amesema Tanzania inaeneo la 52% katika eac na nchi zinazobaki zina 48% hivyo akasema katika EAC Tanzania ni muoaji kama litatokea jambo baya Tanzania ndio itatoa Talaka.
Kwani ajabu kabwana kadogo kuoa jimama nene?
 
vilevile by simple logic kwenye polygamous marriage wanawake ndo wengi hatutegemei kwamba Tanzanzania awe ndo mke wakati wao wapo watatu
Lakini mwana mke mmoja anaweza kua na wanaume wengi pia.
 
Siwachukii wala kuwabagua watutsi. Nachukia tabia zao za kishetani. Hivi wanachofanya huko DRC wewe unaona ni sawa? Unajua plans walizonazo ku distabilize nchi ya Tanzania?.. anyway, let me not waste my time with you. Huenda ni mmoja wapo. Na kama sio utakapoamka usingizini ndo utajua nina maana gani

no research no rights to speak..! huenda walishakuchukulia mke? huenda walisha kuibia mali zako! owkei am sorry am just reasons by analogy...sawa mkuu bhana hata mimi nisipoteze muda wangu hapa! huenda we unawajua sana coz nyote ni wale wale tu wahaya na watutsi majigambo na kujiona nyie ni ndugu, mi wa kaskazini ntawajulia wapi?
 
no research no rights to speak..! huenda walishakuchukulia mke? huenda walisha kuibia mali zako! owkei am sorry am just reasons by analogy...sawa mkuu bhana hata mimi nisipoteze muda wangu hapa! huenda we unawajua sana coz nyote ni wale wale tu wahaya na watutsi majigambo na kujiona nyie ni ndugu, mi wa kaskazini ntawajulia wapi?
hahaaaa,,,,,hata mimi wa Kaskazini ndugu, ila hawa watu nawajua vizuri sana kwani nimekaa nao sana na hadi sasa nakaa nao. Pia kwa ajili ya usalama wa nchi hii sisi tunawajua sana..
 
Back
Top Bottom