TANESCO: Tuna upungufu, siyo mgao wa umeme. Wananchi endeleeni kuvumilia

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Dec 11, 2012
5,897
10,358
Akizungumza leo September 18 katika kipindi cha #Supa Breakfast cha East Africa Radio, Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO ndugu Maharage Chande amedai kuwa Tanzania hakuna kabisa mgao wa umeme bali kuna upungufu

Wateja na wananchi watuvumilie katika kipindi hiki najua ni kigumu kuvumilika na kuelekeweka lakini wafanyakazi wanajitahidi, wizara inajitahidi na serikali inajitahidi kuhakikisha tunatatua changamoto, vile vile uchumi unakua sana kwahiyo ni vizuri na mahitaji ya umeme yanaongezeka, tuko katika kushindana kuzalisha na matumizi ambayo ni mashindano mazuri kwa ustawi wa nchi yetu

Katika mitandao ya umeme hitilafu huwa zinatokea mara kwa mara maeneo mbalimbali huwezi kusema utakuwa na mtandao wa umeme isitokee hitilafu na pale zinapotokea wateja wetu huwa wanafahamishwa lakini pale ambapo tunapata upungufu"

Siyo kwamba nchi nzima hakuna umeme, kuna baadhi ya meeneo yanakosa na pia tunatoa taarifa kwenye hayo maeneo, ni vizuri mwananchi apate taarifa na tumekuwa tukitoa taarifa na tutaendelea kufanya hivyo.


 
Eti hakuna mgawo kuna upungufu. This is bull crap from someone anaeweza kupewa ukurungenzi sehemu nyeti kama hii.

Ukishasema kuna upungufu admit kuwa huo upungufu ndio unasababisha mgawo. Call a spade a spade not a big spoon.

Eti hakuna mgawo kuna upungufu. Like for real, biaaatch.
 
Katika waliofanyiwa" Vetting " bwana Maharage ndio aliibuka namba 1 ndio maana akapewa hiyo nafasi....alisikika mwana JF mmoja ...
 
Akizungumza leo September 18 katika kipindi cha #Supa Breakfast cha East Africa Radio, Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO ndugu Maharage Chande amedai kuwa Tanzania hakuna kabisa mgao wa umeme bali kuna upungufu


Wateja na wananchi watuvumilie katika kipindi hiki najua ni kigumu kuvumilika na kuelekeweka lakini wafanyakazi wanajitahidi, wizara inajitahidi na serikali inajitahidi kuhakikisha tunatatua changamoto, vile vile uchumi unakua sana kwahiyo ni vizuri na mahitaji ya umeme yanaongezeka, tuko katika kushindana kuzalisha na matumizi ambayo ni mashindano mazuri kwa ustawi wa nchi yetu

Katika mitandao ya umeme hitilafu huwa zinatokea mara kwa mara maeneo mbalimbali huwezi kusema utakuwa na mtandao wa umeme isitokee hitilafu na pale zinapotokea wateja wetu huwa wanafahamishwa lakini pale ambapo tunapata upungufu"

Siyo kwamba nchi nzima hakuna umeme, kuna baadhi ya meeneo yanakosa na pia tunatoa taarifa kwenye hayo maeneo, ni vizuri mwananchi apate taarifa na tumekuwa tukitoa taarifa na tutaendelea kufanya hivyo.


View attachment 2753272
Kwani upungufu si ndo hupelekea mgao..!!???
 
Kiufupi, Tanesco inahitaji changamoto kama iliyo tokea kwa TTCL hapo zamani, sasa hv hakuna shida sana ya mawasiliano, hivyo basi Serikali inapaswa kuruhusu na kuingiza mashirika mengine hata matatu manne hivi, ili ikitokea shirika moja linafanya uzembe, swala liwe ni kubadilisha tu mita ukutani kwako kua utumie umeme wa shirika lipi, kwisha habari yao, watajifunza namna ya kuhudumia wateja
 
Kiufupi, Tanesco inahitaji changamoto kama iliyo tokea kwa TTCL hapo zamani, sasa hv hakuna shida sana ya mawasiliano, hivyo basi Serikali inapaswa kuruhusu na kuingiza mashirika mengine hata matatu manne hivi, ili ikitokea shirika moja linafanya uzembe, swala ninkubadilisha tu mitani kwako kua utumie umeme wa shirika lipi, kwisha habari yao, watajifunza namna ya kuhudumia wateja
Halafu kelele za kuuza nchi utazizuia wewe, serikali ikifanya hivyo watakuja akina mbowe waseme watanzania wenyewe tunaweza kujiendeshea mashirika yetu, then Tec nao wataandika waraka!!
 
Mgao upo kwetu unanza jioni tunakaa kwenye giza tunalala tukiamka asubui tunakuta umerudi.
 
Hakuna mgao
Ila Kuna upungufu kwa hivyo watu wanapata umeme kwa zamu.
Hivi tukipata umeme kwa zamu, si ndio mgao wenyewe hhuo?
Nhdugu maharage umekula maharage ya wapi?
Huyu si ndiyo karudishwa na Samia baada ya kuwa haziivi na Magu, tena kwa tuhuma mbofu mbofu au siyo huyu?

Kuna syndicate ya kuhujumu Tanesco Magufuli aliisambaratisha, baadaye mama akairejesha!

Mimi nimeona kinyaa hata kuisikiliza hiyo taka taka.

Hali mbaya sana tuliyonayo ya mgao wa umeme isiyowahi kushuhudiwa kwa awamu yoyote nchini Tanzania, leo anajitokeza kiongozi mwandamizi kama huyo na kuanza kutema hayo matapishi yake alitaka kumfurahisha nani?

Hivi angejikalia kimya kulikuwa naulazima gani kwenda kuwadhihaki waTz kwenye vyombo vya habari?

Rais Samia kama hajui kuendelea kuwakumbatia viongozi mumiani kama hawa wanamchafua sana yeye na Serikali yake na kufanya achukiwe na wananchi.
 
Back
Top Bottom