Tanesco mmekubali kutumika kudai kodi ya majengo (TRA) kinyume na mkataba wenu? Kwa hili Tutawashitaki; serikali hamna huruma

dmkali

JF-Expert Member
Nov 17, 2014
11,284
21,403
Hiki ni nini serikali imefanya?

Yaani majukumu ya TRA wameyaingiza TANESCO ili iweje!

Kodi ya jengo, kodi ya ardhi ni miongoni mwa kodi za kizamani sana zilizopitwa na wakati kama ile kodi ya kichwa!

Ni utwana uliopitiliza kuendelea kukusanya kodi hii kibabe!

Sheria ziko wazi kabisa kwamba chombo kinachosimamia masuala ya kodi ni TRA!

Sasa inakuwaje mambo ya TRA yaingizwe TANESCO kama chombo cha kukusanya mapato?

Usahihi wa takwimu za makusanyo umezingatia vigezo gan kuchukua kodi kupitia LUKU?

Nachojua shirika la umeme Tanzania ni la kiserikali lakini pamoja na yote hayo! Bado haiondoi ukweli kwamba TANESCO ni taasisi ya kibiashara inauza na kusimamia umeme kwa wateja wake!

Sasa kama ni taasisi ya kibiashara kwanini ishirikishwe kwenye uzembe wa TRA?

Yaani kama tutaruhusu huu ujinga wa kila taasisi kutumia LUKU wananchi watakuwa na hali gani?

Haya Leo TRA wanakusanya kupitia LUKU, kesho manispaa naowaombe, keshokutwa NHC nao waombe, dawasco nao waombe!
Huyu mwananchi atakuwa na hali gani?

Kwanza kitendo cha TANESCO Kutumika kukusanya kodi TRA ni kutokuzingatia masharti waliyoyaweka kwa wateja wa umeme kupitia mkataba wa maombi;
Ukisoma masharti ya TANESCO kwenye fomu ya maombi ya umeme TANESCO! Hakuna kipengele hata kimoja palipoandikwa kwamba mteja Usipolipa kodi ya Jengo umeme hautanunulika!

Sasa kwanini Leo mteja anyimwe umeme TANESCO kisa anadaiwa kodi ya jengo?
Huku ni kwenda kinyume na mkataba wa biashara! Nashauri Kwa hili TANESCO tuwapeleke mahakama ya kibiashara kwa kutunyima wateja haki ya kupata umeme kinyume na utaratibu!

Napinga sana huu utaratibu wa TRA kukusanya kodi kupitia LUKU!
Kila mtu afanye kazi yake anayolipiwa nayo mshahara!
Kwamba hebu fikilia unyonyaji huu!

1.ukiwa na wapangaji kwenye jengo moja na kiwanja kimoja wote wanafyekwa kodi ya jengo!
2. Inamaana huu utaratibu kwa wanaotumia solar na majenereta hawalipi kodi
3. Wale ambao hawana umeme hawalipi kodi
4. Ukijenga Leo nyumba na kuweka umeme mwezi huu wa tano wanakutoza kodi kama mtu aliyejenga nyumba zamani!
5. Hakuna elimu yoyote iliyotolewa wananchi tunakutana na kodi kama surpplize pasipo kujipanga! (Usipolipa kodi ya TRA huna haki ya kupewa umeme na TANESCO! (Ebu fikilia mtu unadaiwa 180000 au 240000 usiku! Na usipolipa hupati umeme ajabu sana hili)

Haya yanatokea huko EWURA kuna taasisi inayosimamia walaji wa huduma za umeme imesinzia usingizi wa pono kusubilia mshahara wakati walipaswa hili zoezi watusemee wananchi!

Ebu someni hapa chini masharti ya TANESCO kuunganishiwa umeme kama kuna sehemu pameandikwa kwamba mtu asipokuwa na hela ya kodi ya jengo hataki kupata umeme!

Ardhi kaumba mungu bure, majengo yetu tunajenga kwa gharama ambazo kila vifaa tulivyojengea mlikata kodi!
Lakini Bado mnatufuatilia hadi kwenye LUKU ili iweje?

Nchi hii tatizo siyo walipa kodi, Bali tatizo kubwa ni wasimamizi wa kodi, kwasababu pesa zinapotea kwenye mambo yasiyo na tija

Mfano;
Kuna haja gani kuwa na mkuu wa wilaya/ mkoa awe mwenyekiti wa ulinzi na usalama wakati kuna ma OCD na RPC?

Wakuu wa wilaya na mikoa kila mwaka wananunuliwa mashangingi mapya, mishara na huduma ni nyingi kiasi gani?

Kwanini serikali wasingejikita kupitisha katiba ya kufuta hivyo vyeo ili kutuondolea KODI ZA KIPUUZI ambazo hazina tija kama hizi kodi za ardhi na majengo?
202305091544361000.jpg
 
Mkuu baadhi ya majanga yanayoikumba nchi hii ni matokeo ya kuwa na wanasheria vilaza....kuna mambo yangepingwa mahakamani na yakasitishwa bila kumuathiri mwananchi lakini wao wako bize na kuvaa suti na kesi za kusingizia.
 
Mkuu baadhi ya majanga yanayoikumba nchi hii ni matokeo ya kuwa na wanasheria vilaza....kuna mambo yangepingwa mahakamani na yakasitishwa bila kumuathiri mwananchi lakini wao wako bize na kuvaa suti na kesi za kusingizia.
Inaumiza sana kuwa na serikali inayowarundika watu mzigo
 
Hakuna sehemu hata moja kwenye masharti ya TANESCO palipoandikwa mtu asipolipia kodi ya jengo basi asipatiwe umeme!
Mngetujulisha kabla ya kuweka umeme ili tuamue kuacha!

Mmekiuka masharti tuliyosaini
View attachment 2615717
Kizazi Cha kuhoji "Enlightenment age"

Siku Moja nikiwa shule Moja ya vipaji maalum A_level,

Mwanafunzi mwenzetu monitor alipewa adhabu kubwa sana ya kumkomoa na mwalimu wa zamu (T.O.D).
Ilikua ni adhabu ya kumkomoa Kwa sababu alipewa adhabu ya kufyeka eneo la viwanja vitatu vya mpira.................kiasi Kwamba akiangusha sindano ionekane...😊

Eneo lile lilikua na nyasi ngumu sana na isinge kua rahisi mtu kuweza kumaliza Kwa uraisi...maana mwenzetu alikaribu kufika jioni kavimba na kuchanika mikono....

Ilipo fika prepo usiku tuka organize twende kufyeka usiku watu wakaenda kunoa mafyekeo night mida ya saa 4 makamanda Zaid ya hamsini tukaenda kufyeka eneo fasta kumbe mwalimu alitonywa.....

Ilipo fika asbh baada ya assembly mwalimu akaja darasani akiwa na hasira za nyati dume Alie jeruhiwa akaomba majina ya watu wote walienda kufyeka usiku....

Alipo toka ikaanza discussion tupeleke majina mangapi wapo walio SEMA kumi...Mimi nikamwambia majina yasipungue 30 tuka andika tukayapeleka.....

Kesho mchana tukaitwa head office pale mbele watu 30 ivi...tukasomewa mashitaka mbele ya second master na discipline master....

Mwalimu alikua na mwembwe yule.....alianza😊 inasemekana....mnamo tarehe.......
Mbwembwe..

Tukapewa uhuru wa kujitetea watu wakawa wanajitetea..

Mimi nikumbuka nilianza Kwa kuwaambia wakati nasoma join instructions nilisoma kanuni Sheria na taratibu sikuona sehemu yeyote iliyo someka....
"KUMSAIDIA MTU ADHABU SHULENI NI KOSA"

WALIMU wakapaniki wewe ni mwanafunzi mzur unasema sana Sheria za shule😊
Wakaanza kutafuta kama Kuna hiyo adhabu au katazo wasipate....

Unajua nini kilitokea baada ya kusema ivyo.....😊

Ntarudi baadae
 
watunga sheria kwa hati ya dharula kuhalalisha uhuni huu.
Ujinga waliofanya wabunge wetu ni kumruhusu Waziri wa Fedha aweze kutunga kanuni zinazoweka kiwango cha Tozo, badala ya kusema kuwa kiwango kiwekwe bungeni na bunge lenyewe ila waziri atunge kanuni ya namna gani atatumia kukusanya tozo.

Nimesoma mitandaoni, mpaka wabunge wanashangaa kwa kuwa hawakupitisha kiwango. Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge inayohusu nishati anasema wao sio kazi yao kutunga viwango hivyo aulizwe waziri. Yaani aisee nchi hii tunachezewa mno.
 
Ujinga waliofanya wabunge wetu ni kumruhusu Waziri wa Fedha aweze kutunga kanuni zinazoweka kiwango cha Tozo, badala ya kusema kuwa kiwango kiwekwe bungeni na bunge lenyewe ila waziri atunge kanuni ya namna gani atatumia kukusanya tozo.

Nimesoma mitandaoni, mpaka wabunge wanashangaa kwa kuwa hawakupitisha kiwango. Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge inayohusu nishati anasema wao sio kazi yao kutunga viwango hivyo aulizwe waziri. Yaani aisee nchi hii tunachezewa mno.
Shida ya nchi hii siyo ukusanyaji wa kodi Bali ni matumizi mabaya ya kodi .... Ulishawahi kujiuliza kwanini magari ya serikali huwa hayazimwi kwenye mikutano hata kama ni SAA mbili yanaunguruma tu,
 
Shida ya nchi hii siyo ukusanyaji wa kodi Bali ni matumizi mabaya ya kodi .... Ulishawahi kujiuliza kwanini magari ya serikali huwa hayazimwi kwenye mikutano hata kama ni SAA mbili yanaunguruma tu,
Kwa sababu ng'ombe sisi tutanunua tu mafuta kwenye magari yao. Kama wanaweza kununua magari ya milioni 600 bila sababu yoyote ya maana, tutashindwaje kununua mafuta ili dereva apigwe na AC wakati anamsubiri Waziri asaini mikataba ya kimagumashi!!

Viongozi wa serikali wanatuona sisi ni ng'ombe tutafanya wakitakacho.
 
Shida ya nchi hii siyo ukusanyaji wa kodi Bali ni matumizi mabaya ya kodi .... Ulishawahi kujiuliza kwanini magari ya serikali huwa hayazimwi kwenye mikutano hata kama ni SAA mbili yanaunguruma tu,
Jamaa wanadharau za kis*ng* sana na hela za wanainchi wanahisi wao ni untouchables. MUNGU awalinde tu ila siku wanainchi wakisema enough is enough tukasanuka na kutaka kila kitu kisimame hawa mbwa hakuna atakayepona watajikuta wote wapo matatani.

Hiyo siku inakuja
 
Back
Top Bottom