TRA na TANESCO, Kuzifungua mita za umeme kisa kodi ya majengo ni wizi na uonevu

sajo

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
3,022
5,254
Jana usiku umeme uliisha kwenye mita yangu. Nikanunua wa shilingi elfu 9 kwa tigopesa, nashangaa muamala unasitishwa kila naponunua. (Ninatumia tarrif ya chini ile) umeme wa elfu 9 unanitosha kwa mwezi mzima.

Ikabidi nipige simu tigo, wakaniambia kuwa mita inadaiwa shilingi laki 1 deni ya kodi ya majengo kwa mwaka 2022/23, kwa hiyo ninunue umeme wa kuanzia Tshs. 100,000/= ndio itakubali.

Kwa kweli nikashangaa na kusikitika sana. Nyumba ni andagraundi, imehesabika kuwa ni ghorofa, na muda wote nilikuwa nalipa elfu 1 kila naponunua umeme. Kama ni limbikizo, sio mimi niliyelizalisha bali ni TRA wenyewe kwa kutonichaji kwa wakati. Ile elfu 1 wanasema waliikata kimakosa, ilipaswa nilipe elfu 5 kwa mwezi kwa kila sakafu

Sasa hii ya kufungia mita ili ninunue umeme wa laki kwa kweli ni uonevu, hapa ndio nimeelewa kwa nini wafanyabiashara wa Kariakoo waliandamana. Yaani usiku umeme umeisha halafu unaambiwa ili upate umeme, nunua wa kuanzia Tshs. 100,000/=, itoke wapi??

Halafu mwaka wa fedha 2022/23 unaisha mwezi huu, Juni 30, maana yake ikifika mwezi wa 7 watanifungia tena ili nilipe wanaloliita deni la mwaka 2023/24 la kodi ya majengo..vyumba viwili vya andagraundi nachajiwa laki na ishirini.. TRA Tanzania hapa mnazingua, mnachofanya ni wizi. Mnashirikiana na TANESCO kutufanyia wizi huo.

Kodi ya majengo kwanza ni kodi kandamizi ya kizamani, badala ya kupeleka majeshi DRC huko walete madini hapa tuuze nyie mnawaza kutukamua sisi wananchi. Yaani mnapowaza mapato chanzo pekee kwenu ni wananchi wenu, hamuwazi kuwapa huduma bora bali mnawaza kuwakamua kodi.

Cha ajabu bunge nalo linakuwa zembe, linatunga sheria halafu linaacha waziri wa fedha ndio awe na jukumu la kupanga kiwango cha Tozo, hili ni jambo la aibu.

Fedha yoyote ya kodi, inapaswa kupitishwa na bunge na sio na waziri. Viwango vipitishwe bungeni, sio kwenye kanuni za waziri. Waziri mwenyewe hajali chochote, yeye ashasema tuhamie Burundi, mtu wa hivi mnapaje mamlaka ya kutamka viwango yeye peke yake??

Hapa nilipo nawaza laki ya ghafla naipata wapi ili ninunue umeme. Japo najua kwa kununua umeme huo nitakuwa nabariki wizi wenu, ila inabidi ninunue ili nisiingie hasara ya vyakula kuharibika na kazi kushindwa kufanyika. Floor za ghorofa si mngezichaji tu kama nyumba mbili, hela iwe ni ya nyumba mbili, kila moja elfu 1.
 
Hii nchi ngumu sana.

Ukiwa nacho unaongezewa zaidi na yule asiyenacho hata hicho kidogo chake kinakwapuliwa.
Yaani nchi ina ufala sana. Yaani hata msingi wa kodi ya jengo haieleweki ni nini, maana kodi lazima iwe na sababu. Yaani kuweka flat rate kwa majengo yote wanaona wanateseka sana?? Halafu unapishana na RC tu anatembelea LC 300 series, ndio unajua kuwa tunapewa lundo la makodi sio kwa faida yetu bali kwa faida yao hawa michwa wachache.
 
Hii nchi kuna siku watu watachoka wataingia barabarani liwalo na liwe.
Yaani ni utitiri wa kodi pasipo matokeo. Yaani serikali wao kazi yao ni kuwaza wampe mzigo gani mwananchi, hata hiyo mwezi wa 6 wanapopitisha bajeti ya nchi, lazima Mwigulu atatambulisha kodi mpya kadhaa za kutuumiza na wabunge watazipitisha. Kwa kweli hii liwalo na liwe inabidi ije mapema sana
 
Kuna wanufaikaji wa hiyo kodi watakuja kusema eti tuwe wazalendo kila kitu kiko sawa na hata hiyo tozo ni ndogo inapaswa kuongezwa.
 
Kuna wanufaikaji wa hiyo kodi watakuja kusema eti tuwe wazalendo kila kitu kiko sawa na hata hiyo tozo ni ndogo inapaswa kuongezwa.
Na siku hizi wakiona kelele, utaona hao fasta wanakuja kutoa ufafanuzi. Mwigulu amefanya kazi ya bunge, alipaswa kuwajibishwa. Viwango vya tozo/ kodi havipaswi kupangwa na waziri,vinapaswa kupitishwa na bunge.

Neno Uzalendo linatumika vibaya kutukandamiza.
 
Jana usiku umeme uliisha kwenye mita yangu. Nikanunua wa shilingi elfu 9 kwa tigopesa, nashangaa muamala unasitishwa kila naponunua. (Ninatumia tarrif ya chini ile) umeme wa elfu 9 unanitosha kwa mwezi mzima.

Ikabidi nipige simu tigo, wakaniambia kuwa mita inadaiwa shilingi laki 1 deni ya kodi ya majengo kwa mwaka 2022/23, kwa hiyo ninunue umeme wa kuanzia Tshs. 100,000/= ndio itakubali.

Kwa kweli nikashangaa na kusikitika sana. Nyumba ni andagraundi, imehesabika kuwa ni ghorofa, na muda wote nilikuwa nalipa elfu 1 kila naponunua umeme. Kama ni limbikizo, sio mimi niliyelizalisha bali ni TRA wenyewe kwa kutonichaji kwa wakati. Ile elfu 1 wanasema waliikata kimakosa, ilipaswa nilipe elfu 5 kwa mwezi kwa kila sakafu

Sasa hii ya kufungia mita ili ninunue umeme wa laki kwa kweli ni uonevu, hapa ndio nimeelewa kwa nini wafanyabiashara wa Kariakoo waliandamana. Yaani usiku umeme umeisha halafu unaambiwa ili upate umeme, nunua wa kuanzia Tshs. 100,000/=, itoke wapi??

Halafu mwaka wa fedha 2022/23 unaisha mwezi huu, Juni 30, maana yake ikifika mwezi wa 7 watanifungia tena ili nilipe wanaloliita deni la mwaka 2023/24 la kodi ya majengo..vyumba viwili vya andagraundi nachajiwa laki na ishirini.. TRA Tanzania hapa mnazingua, mnachofanya ni wizi. Mnashirikiana na TANESCO kutufanyia wizi huo.

Kodi ya majengo kwanza ni kodi kandamizi ya kizamani, badala ya kupeleka majeshi DRC huko walete madini hapa tuuze nyie mnawaza kutukamua sisi wananchi. Yaani mnapowaza mapato chanzo pekee kwenu ni wananchi wenu, hamuwazi kuwapa huduma bora bali mnawaza kuwakamua kodi.

Cha ajabu bunge nalo linakuwa zembe, linatunga sheria halafu linaacha waziri wa fedha ndio awe na jukumu la kupanga kiwango cha Tozo, hili ni jambo la aibu.

Fedha yoyote ya kodi, inapaswa kupitishwa na bunge na sio na waziri. Viwango vipitishwe bungeni, sio kwenye kanuni za waziri. Waziri mwenyewe hajali chochote, yeye ashasema tuhamie Burundi, mtu wa hivi mnapaje mamlaka ya kutamka viwango yeye peke yake??

Hapa nilipo nawaza laki ya ghafla naipata wapi ili ninunue umeme. Japo najua kwa kununua umeme huo nitakuwa nabariki wizi wenu, ila inabidi ninunue ili nisiingie hasara ya vyakula kuharibika na kazi kushindwa kufanyika. Floor za ghorofa si mngezichaji tu kama nyumba mbili, hela iwe ni ya nyumba mbili, kila moja elfu 1.
Nimekutana na jambo kama hili wiki iliyopita nanunua umeme napewa maelezo nadaiwa 100k kupiga simu Tanesco ndio wanasema nina deni la laki 20 so ninunue umeme umaozidi laki moja, yani nyumba wanyosema ni ghorofa sasa!! Ni chumba kimoja kiko juu basi! Hakuna usawa kwa kweli!
 
Back
Top Bottom