Tamko la Wapiganaji CCM Feb 10, 2010

Tamko limekuja wakati muafaka?

  • Ndiyo

    Votes: 8 57.1%
  • Hapana

    Votes: 5 35.7%
  • Sijui

    Votes: 1 7.1%

  • Total voters
    14
  • Poll closed .
moto umewashwa.. tofauti imewekwa wapo wapiganaji na wapo wapiganaji wa kweli; wapiganaji wameonekana wakiunga mkono wizi na uporaji wa raslimali zetu.. wapiganaji wa kweli.. wamekana kuwa sehemu ya maamuzi yaliyofikiwa jana usiku Dodoma. Anayefikiri kuwa suala la Richmond limefikia mwisho anaota njozi.. subirini mtaamini kuna tofauti kati ya maembe na machungwa japo yote ni matunda.

- Ndio tunaita Great Thinking by great thinker, saafi sana mapambano bado yanaendelea waliokata tamaa tunawaacha kwenye mataa, tunasonga mbele!

Respect.

FMEs!
 
Kuna wanachama wa CCM ambao labda hata majina yake watu hawajawahi kuyasikia (which means.. hata kama wangeweka majina yatu wangeuliza "who are these people" kama ilivyokuwa CCJ.

Watu labda wanatarajia kuona majina ya Mwakyembe, Seleliii na wengine wanaojitambulisha kama "wapiganaji"... ndio waridhike. CCM ni zaidi ya majina ya watu; na wenye chama wamecharuka sasa.. watch..
 
ngoja sisi wajinga tuwe na subira, maana hata mtoto azaliwapo hatoki miguu, mikono pamoja na kichwa kwa pamoja, pengine wameanza nsa kichwa na miguu baadae........waelevu endeleeni kujibu kwa jazba
 
Sidhani kwamba kuna makosa sana kwa wao kutotaja majina yao. Tunafahamu mambo mengine yaliyokwisha kuwatokea hata wanafunzi wa vyuo walipopinga serikali katika maamuzi fulani fulani. Hakuna haja ya kuharakisha maana hatutaki kupoteza hata kiungo kimoja kwa sasa. Ni hasira za mkisi zitakuwa. Wana-JF tukubali kuwa kila mtu anajiuliza kuwa yale meno ya serikali yameenda wapi? Mara kimya kabisaa! huyu simba mjeruhiwa anatakiwa kuzungukwa kwa uangalifu na taratibu kidogo. Wengine hapa wanasema tu lakini wakiitwa kuweka sahihi na majina yao kwenye dokumenti kama hii, sijui ni wangapi watakuwa tayari.
Ila nimeipenda, imeandikwa kwa ustadi mkubwa na imewakilisha mawazo yetu wote tulio wapenzi wa nchi yetu. Na kama yalishasemwa hapa siyo dhambi sasa kuwekwa sawa zaidi, tena ni ushuhuda kuwa JF iko mwelekeo sahihi.
Mimi nawapongeza sana na nawatakia kazi njema.
 
Mwenzenu nilishasema hawa jamaa ajenda yao ni kulindana fikiria kashfa zote hizo lakini jamaa wanasimama kutuomba kura hata aibu hawana. WANYONGWE TU!

Me nadhani bora vibaka wa Manzese kuliko hawa jamaa wa bungeni hakuna uzalendo wala nini WANYONGWE TU!

Kwanza hiyo orodha nimeona jamaa wawili ambao kila wakioneshwa kweny TV mwenzenu nakumbuka misiba tu. Lowasa na KARAMAGI. Hawa nadhani anapaswa kutumika kama kamba ya kunyongea wenzao. jamani mi nalia na wanao jiita WAZALENDO WA CCM na wanalinda na kutetea Ufisadi, hawa nao WANYONGWE TU.
Kazi nzuri WAPIGANAJI WA CCM nadhani hamtaishia kweye maneno tu bali mtatenda pia. Kazi ipo!
icon8.gif
 
Watu wanataka kuwajua walioleta hii message, wanataka kujua ni nani wako nyuma ya hii; kama vile walivyotaka kujua nani wako nyuma ya CCJ na nani wako nyuma ya JF.. hawataki kuongelea hoja zinazotolewa wanataka kujua nani katoa hoja! Na watu wanaopenda "mepesi mepesi" wameng'ang'ania "tunataka majina"..

Binafsi nimependa kilichochukuliwa yaani msimamo! wakati wabunge wa CCM wameamua kuwa kitu kimoja katika umoja wa ufisadi Bungeni ili kujilinda wao na chama, kuna kikundi cha wana CCM ambao kimekataa moja kwa moja kuwa na ushirika na mafisadi hata kama ni kwa ajili ya kukisaidia chama.

Siku mkiona Mwakyembe na Rostam wamekumbatiana basi mjue kweli hakuna wapiganaji wenye msimamo

Siku mkiona kina Selelii wanawapigia kampeni kina Lowassa basi mjue mambo yamekwisha.

DO NOT read too much into what happened 2day Bungeni kuhusu Richmond. In warfare.. as long as you can win the war, you can afford to lose some battles.. Ushindi wa wapiganaji wa kweli (that is a functional word ambalo watu hawajalisoma hapo mwanzoni, wamesoma neno "wapiganaji" tu..) hauwezi kuhesabiwa kwenye suala la Richmond.. as a matter of fact.. wapiganaji wameshinda zaidi (in total) kuliko kushindwa!
 
Binafsi napongeza hatua ya hawa wapambanaji (kama wapo sio wa kufikirika) kwa kauli zifuatazo: "Wahusika wakuu katika kashfa zifuatazo washughulikiwe kichama na kiserikali ikiwa ni pamoja na kufikishwa mahakamani chini yha sheria ya mitandao ya kihalifu na uhujumu wa uchumi ya 1984. Tunatambua baadhi yao ni wale ambao tumependekeza hapo juu wawajibike wenyewe kwa kuachilia nafasi za uongozi ndani ya chama (hapa kashfa zooote zimetajwa).

Kashfa hizo zote zimetutia aibu kama watanzania na zaidi pia kama wana CCM ambao chama chetu ndiyo kimeunda serikali inayotawala. Hatuwezi kamwe kukubali kwa namna yoyote ile kuendelea kukaa na wahusika wa kashfa hizo kwa kisingizio au sababu yoyote ile. Endapo chama chetu kitaamua kuwavumilia na kuwasafisha wahukia wa kashfa hizi mbalimbali kwa kisingizio cha kutafuta "umoja, mshikamano, na utulivu" basi watakuwa wamepiga kura ya kukimega chama.

Kwa kauli hizi naona wako katika nafasi nzuri ya kukisafisha chama chao. Kwa kujitangaza ingekuwa ni kama kuomba huruma za wananchi na hasa wapigakura wao. Mapambano hufanyika msituni na sio mjini kwa hiyo kujificha ni mbinu na silaha muhimu sana bila kusahau propaganda kama hii walioitoa, mimi nasema safi sana kwa kuwa kuendelea kuelewana kwa wezi ni hatari kwa hatma ya taifa letu.

Aluta continua mapambano bado yanaendelea.
 
Watu wanataka kuwajua walioleta hii message, wanataka kujua ni nani wako nyuma ya hii; kama vile walivyotaka kujua nani wako nyuma ya CCJ na nani wako nyuma ya JF.. hawataki kuongelea hoja zinazotolewa wanataka kujua nani katoa hoja! Na watu wanaopenda "mepesi mepesi" wameng'ang'ania "tunataka majina"..

Binafsi nimependa kilichochukuliwa yaani msimamo! wakati wabunge wa CCM wameamua kuwa kitu kimoja katika umoja wa ufisadi Bungeni ili kujilinda wao na chama, kuna kikundi cha wana CCM ambao kimekataa moja kwa moja kuwa na ushirika na mafisadi hata kama ni kwa ajili ya kukisaidia chama.

Siku mkiona Mwakyembe na Rostam wamekumbatiana basi mjue kweli hakuna wapiganaji wenye msimamo

Siku mkiona kina Selelii wanawapigia kampeni kina Lowassa basi mjue mambo yamekwisha.

DO NOT read too much into what happened 2day Bungeni kuhusu Richmond. In warfare.. as long as you can win the war, you can afford to lose some battles.. Ushindi wa wapiganaji wa kweli (that is a functional word ambalo watu hawajalisoma hapo mwanzoni, wamesoma neno "wapiganaji" tu..) hauwezi kuhesabiwa kwenye suala la Richmond.. as a matter of fact.. wapiganaji wameshinda zaidi (in total) kuliko kushindwa!
hilo ndiyo tatizo la uchoyo wa mawazo, hivi sasa we una njaa, mtu kakuletea msosi then unauliza nani kamtuma, badala ya kupokea n a kuufanyia kazi, kwa nini hatubadiliki?
 
Tatizo moja la siasa za Tanzania yetu, pengine tofauti na nchi zingine hapa Afrika, ni kukosa watu wenye ujasiri wa kisiasa, ambao wapo tayari kuhesabiwa, sio kwa maneno yao bali kwa matendo yao. Pengine hii inachangiwa kwa kiasi fulani na ukweli kwamba ni wanasiasa wachache sana wanaoweza kusurvive bila mkono wa serikali. Wanasiasa wetu wengi wanaishi ama kwa kuitegemea serikali moja kwa moja, kwa kuajiriwa, kwa pensheni wanazopata au kwa kuwa wafanyabishara wakifanya biashara ambazo ufanisi wake kwa kiasi kikubwa unategemea short cut kama vile kukwepa kodi, etc., kiasi kwamba serikali ikiamua kuziba mianya sawasawa hawezi kukatiza siku mbili.

Ni kwa sababu hii wengine hatukashangazwa kwa waanzilishi wa CCJ kujificha wakipima upepo, na ndio maana na leo wanatoa nyaraka kwa kujificha. Kama unaamini unachokiongea kwa nini ufiche jina lako? Woga ni adui mkubwa sana wa maendeleo ya kisiasa katika nchi hii.
 
Nadhani kuna watu wanamiss pointi kubwa sana ya ujumbe huu; ndani ya CCM kuna wapiganaji wa kweli na wapiganaji uchwara; wapiganaji wa kweli hawajali wabunge wa CCM wanafanya nini Bungeni au wanachama wengine wanafanya nini; wao wanapigana.

Ninavyoelewa ni kuwa mstari umechorwa ardhini sasa kati ya wale wanaCCM walioweka Chama kwanza kwamujibu wa ibara ya 14:1 na wana CCM ambao wameamua kujitenga 'nao'. Ukiniuliza mimi I'll stand with these people than their opponents. CCM has been put on notice.

Nimemuuliza mmoja wao leo anasema mambo ya Ngoswe mwachie Ngoswe, wanajua wanachofanya na tamko hili ni kuwapa notice JK na uongozi wa juu wa CCM. Ati wamefunika kombwe mwana haramu apite.. lakini "haendi kokote"!

MM
Kwa yaliyotokea leo huko Dodoma, napenda sana kuamini hiki unachokisema.
Lakini notice yanini? Hawabadiriki hao, hivi kweli ukimwangalia Mkuu unadhani kuna nini hapo.. kwao ni furaha Yameisha salama.
kama hukubaliani unasubiri nini??
 
MM
Kwa yaliyotokea leo huko Dodoma, napenda sana kuamini hiki unachokisema.
Lakini notice yanini? Hawabadiriki hao, hivi kweli ukimwangalia Mkuu unadhani kuna nini hapo.. kwao ni furaha Yameisha salama.
kama hukubaliani unasubiri nini??


Kiraka.. msimwangalie Kikwete kama sehemu ya suluhisho; he like the rest of the bunch of his supporters need to be stopped. Kwangu kwa mabadiliko ya kweli Kikwete hawezi kuwa sehemu yake.. kama atachaguliwa tena.. tutasubiri nafasi nyingine.
 
Nitayainua macho yangu, nitazame milima...msaada wangu utatoka wapi?

Utatoka kwa bwana aliyeziumba mbingu na nchi

Mungu wa mabondeni ni Mungu huyo huyo wa mlimani, na
Mungu wa wakati mzuri ni Mungu huyo huyo wa wakati mbaya
Na mungu wa mchana ni huyo huyo inapokuwa usiku

.... lakini vitu vinapokwenda vubaya ana uwezo wa kuviweka sawa
 
It is surprising the way skepticism is built kwenye hii habari. Well, people behave as if they knew the names of those who exposed EPA SCANDALS before they turned into reality.

Wakuu like others walivyosema sometimes names are just unimportant, get the message of which you have the right to believe or dis it. In short hii inatuonyesha pia tatizo kubwa tulilonalo kama Taifa............... People are much more concerned on personalities kuliko issues!
 
Nadhani kuna watu wanamiss pointi kubwa sana ya ujumbe huu; ndani ya CCM kuna wapiganaji wa kweli na wapiganaji uchwara; wapiganaji wa kweli hawajali wabunge wa CCM wanafanya nini Bungeni au wanachama wengine wanafanya nini; wao wanapigana.

Ninavyoelewa ni kuwa mstari umechorwa ardhini sasa kati ya wale wanaCCM walioweka Chama kwanza kwamujibu wa ibara ya 14:1 na wana CCM ambao wameamua kujitenga 'nao'. Ukiniuliza mimi I'll stand with these people than their opponents. CCM has been put on notice.

Nimemuuliza mmoja wao leo anasema mambo ya Ngoswe mwachie Ngoswe, wanajua wanachofanya na tamko hili ni kuwapa notice JK na uongozi wa juu wa CCM. Ati wamefunika kombwe mwana haramu apite.. lakini "haendi kokote"!

Mzee Mwanakijiji,

Naheshimu sana mchango wako.Lakini katika hili naomba kutofautiana nawe hasa kuhusu hao unaowaita "wapambanaji wa kweli".Kwanza,kama ni wapambanaji wanapambana na nani?Mafisadi au mfumo wa kifisadi?Pili,kama wanapambana,je ni kwa ajili yetu au wanatetea maslahi yao ya kisiasa?

Mwandishi mahiri wa makala,Padre Privatus Karugendo alishawahi kuwakosoa hao wanaoitwa "wapiganaji dhidi ya ufisadi".Alitoa mfano wa padre anayetangaza kupinga mafundisho ya kanisa lakini bado anamsujudia Papa (or something like that).Nilivyomuelewa,alikuwa akiwakemea baadhi ya wabunge wa CCM wanaojitambulisha kama wapambanaji wakati wao ni sehemu ya mfumo dhalimu unaodumishwa na CCM hiyohiyo.Kwa wanaofahamu masuala ya vita,watakubaliana nami kwamba vita ya ndani inaweza kuwa ngumu zaidi kuliko ya nje.Kinachowafanya hao "wapambanaji wa kweli" waendelee kuwa ndani ya CCM hadi leo ni nini kama si ubinafsi wao?Hata kwenye Maandiko Matakatifu tunausiwa umuhimu wa kujikana sisi wenyewe kama tunahitaji kuuona ufalme wa mbingu

Hata hizi nyaraka wanazokuja nazo wakati huu zinapaswa kuangaliwa kwa mashaka.Walikuwa wapi siku zote hizi wakati taifa linateketea?Kwani iwe sasa miezi michache kabla ya uchaguzi?Hivi hawa hawajitengenezei mazingira kuwa wakibwagwa huko CCM waje na hadithi kuwa "siku zote tulikuwa nanyi kiroho japo kimwili tulikuwa na CCM". Wanachofanya ni sawa na kupuuza afya ya mgonjwa hadi inakuwa mahututi na kuanza "kutangaza severity ya ugonjwa husika".Kwanini tusihisi kuwa hawa ni matapeli wa kisiasa wanaojaribu kujitengenezea mazingira mazuri pande zote mbili?Hapa namaanisha kuwa wanaonekana wana-CCM waaminifu kwa kushiriki kuunga mkono hoja za kifisadi kama hiyo ya Richmond lakini pia wanatuzuga huku pembeni kwa kutoa nyaraka za kukemea kilekile wanachokitumikia!

Lazima tufahamu kuwa si lazima kwa wao kuendeleza mapambano dhidi ya ufisadi (if we were to believe them) wakiwa ndani ya CCM.By the way,Mtanzania halazimiki kuwa mwanasiasa,let alone mbunge wa CCM,kuweza kushiriki mapambano ya kuleta "ukombozi wa pili".Wewe Mwanakijiji ni mfano sahihi kabisa katika hili.Wewe si mbunge au mwanachama wa CCM lakini harakati zako zinaonekana kuwatikisa CCM hadi wanakuchukia.Kwani tuwaamini wanafikia hawa wanaoogopa "lawama" au "kuchukiwa"?Askari anayefaa kuwamo vitani ni yule tu aliye tayari kumwaga damu kwa ajili ya taifa lake.Sasa kwa hawa "wazushi" kuendeleza mapambano yao nje ya CCM wala hakutapeleka umwagaji damu as such hasa kwa vile wamekuwa sehemu ya adui kwa muda mrefu.

Historia inatukumbusha pia kuwa hata baadhi ya waliopigania uhuru wetu hawakuwa ndani ya bunge la mkoloni.Na kwa wale walioingizwa serikalini au katika bunge la mkoloni waliendelea kujitoa mhanga kuhakikisha uhuru unapatikana.

Mbona Mrema aliweza kujitoa ndani ya CCM na ku-mount upinzani nje ya mfumo huo (licha ya ukweli kwamba mafanikio yake in long run yamekuwa disappointing)?Sasa kwanini hao "wapambanaji wa kweli" wasijiondoe CCM na kuanzisha mapambano ya dhati nje ya mfumo dhalimu?

Tunawatenganishaje na maamuzi kama hayo ya jana huko Dodoma hata wakijitetea kuwa "kusapoti kwao ni sehemu ya mkakati wa harakati zao"?Na kwanini tuwaamini ilhali hakuna ushahidi japo kidogo wa kututhibitishia kuwa kauli zao za "chuki" dhidi ya ufisadi ni za dhati kweli,na sio kutupumbaza?Actions speak louder than words.Na kwa hapa,matendo yao ndio yanapaswa yawahukumu badala ya vijinyaraka vya kutupumbaza kuwa ni 'notice kwa CCM na JK.Unatoaje notice kwa mwenye nyumba kama huna dhamira ya kuhama?

Let's imagine wangekataa KATAKATA kuunga mkono azimio hilo,nini kingetokea?Wangefukuzwa uanachama wa CCM?I don't think so kwa vile CCM inafahamu vizuri sana kuwa laiti ingewafukuza wangeivua nguo hadharani kuwa wamefukuzwa ili azimio la kuwalinda mafisadi lipite.

Mwanakijiji,wababishaji hawa hawana excuse hata moja ya kutoonyesha upinzani dhidi ya azimio hilo la kifisadi.Wameshiriki kurefusha mjadala wa Richmond only for them to give in dakika ya mwisho.Si bora wangekubali yaishe mapema tu!

Walichofanya ni sawa na kumbaka mtoto kisha kujitetea mahakamani kuwa ubakaji huo ulikuwa sehemu ya tambiko la kumsafishia mafanikio mtoto huyo.
 
Si walisema Tanzania ina wenyewe. Wenyewe watajitokeza, ngumi za usoni tena hakuna aibu. Hivi waliotajwa hapo kwa ufisadi wanajisikiaje nafsi zao na familia zao. Mfano watoto wakienda shule wanaambiwa na watoto wenzao ya kwamba tumesikia baba yako ni fisadi anataafuna pesa ya walipa kodi, je ni kweli?
 
Najua hapa watu wengi hadi wasaidiwe kutafuna tafuna..

Ni adui yupi hatari na wa kumwogopa sana? yule unayemjua au yule usiyemjua? Wakati mwingine wale wanaojulikana kwa majina yao siyo maadui!!!!
 
Well, nilikuwa mbishi, but it would appear this thing is really, coming from really people, not mysterious at all!!
 
Back
Top Bottom