Tamko la CHADEMA - Aprili 14, 2013

Tamko la CHADEMA - Aprili 14, 2013

Status
Not open for further replies.
Kwa muda mrefu kuna tabia imezuka ya Watanzania wengi kupenda kulalamika kuhusu mwenendo mzima wa serikali na kumekiwa na malalamiko mengi kuhusu udhaifu wa serikali ilioko madarakani na ni kweli serikali hii ina madhifu mengi lakini tatizo ni kwamba hao wanaolalamika wakiongozwa na Chadema hawatoi masuluhisho ya matatizo hayo Je mbona hao chadema sijaona sera zao zaidi ya malalamiko na ukosoaji Chadema wasidhani tutawapa nchi kwa kelele zao za kuikosoa CCM majukwaani Tunataka sera madhubuti za kuziba makovu ya CCM na si kelele tu Nyie wapinzani tupeni na nyie sera zeno tuzipitie na si kukosoa za chama tawala tu lasivyo tutaishia kuwa mabingwa wa malalamiko yasio na masuluisho Mungu ibariki Tanzania!
 
Mtoi,

Ni¨lifikiri na wewe ni wale wanaoheshimu ustaarabu wa kutokuzungumzia mambo yaliyo mahakamani.

Nakumbuka jana ulikuwa pamoja na wale wanaounga mkono kesi kufutwa kwa sababu imeongelewa kwenye Bunge. najua Marando akijibiwa mtawalaumu walomjibu.

Lakini kesi iko mahakamani na Tundu Lissu alisema atashinda kesi hiyo kwa nusu saa. Sasa nashangaa Marando anasema ataongeza wanasheria wengine! Hao wanini tena wakati Tundu Lissu alisema within half an hour atakuwa kashamaliza kesi?

Mbona unahangaika mkuu...?
 
Duh! Duru za ukweli. Tunaomba mahakimu wote wanaoshuhulikia kesi hii waache BIA kwa kipindi hiki kigumu! maana kweli CDM kimekamilika kuliko kina Mtella wanavyofikiria kijuujuu.
 
Duh! Hii ni hatari.....Chadema ni noma. Maskini CCM....mbinu zote zinabumbuluka.
 
Asante mkuu hapo mahali nilishapaona kwa nje tu! Marafiki zangu wote wa system nilio skuli nao sitaki hata kuwaona siku hizi. Nikikumbuka jinsi vijana wanavyotumika miaka ya hivi karibuni kufanikisha mambo maovu nasikia hofu na hasira ndani ya moyo wangu.
Vijana niliowafahamu leo wameajiriwa sehemu zinazonuka damu ya wanyonge kweli? Hivi usalama wa taifa wanatupeleka wapi Pasco?

Hii ni dhahiri kabisa usalama wa taifa sasa ni vipande vipande. Na hata nguvu tunazoaminishwa kwamba wanazo hadi kufikia uwezo wa kumkaripia rais wa nchi ni mambo ya kusadikika. Usalama wa taifa yaani imegeuka genge la wahuni kweli hii ni haki?
Yaani wanaacha kushughulikia mambo magumu yanayoliumiza taifa, kama vile mambo ya EPA, DOWANS, MEREMETA, KIWIRA kutatua vitendawili hivi lakini wao wanageuka wauwaji. Tena vifo vya kikatili kwa kung'oa watu kucha na meno hadi kuwatoboa macho jamani hii ni haki kweli? Kisa cha yote haya ni kufanikisha interest za kisiasa kwa makundi fulani.
Mkuu Investa, zile number zote zilizotajwa ni za vijana tuu wa kazi, wao wakishamaliza ndio wanakuja kuripoti kwetu!, ofisi yangu iko pale nyuma ya St. Peter lile jengo jipya mithili ya meli, karibu unitembelee, pale ila usiniulizie kwa jina hili la jf, pale natumia jina la kazini, naitwa chifu!, ukifika tuu getini, ukisema wewe ni mgeni wa chifu, hutaulizwa chochote, utapitishwa ndani, ndipo nitaitwa na nitakutembeza tembeza sehemu mbalimbali!, hadi desk la jf, nitakuonyesha majina halisi ya vimbelembele wote hadi locations na ip address zao!. Karibu sana!.
Pasco.
 
Mkuu Investa, zile number zote zilizotajwa ni za vijana tuu wa kazi, wao wakishamaliza ndio wanakuja kuripoti kwetu!, ofisi yangu iko pale nyuma ya St. Peter lile jengo jipya mithili ya meli, karibu unitembelee, pale ila usiniulizie kwa jina hili la jf, pale natumia jina la kazini, naitwa chifu!, ukifika tuu getini, ukisema wewe ni mgeni wa chifu, hutaulizwa chochote, utapitishwa ndani, ndipo nitaitwa na nitakutembeza tembeza sehemu mbalimbali!, hadi desk la jf, nitakuonyesha majina halisi ya vimbelembele wote hadi locations na ip address zao!. Karibu sana!.
Pasco.


hahahahahahahaha Pasco
 
Last edited by a moderator:
"BONAFIDE GENUINE", "BONafide genUINE",
"bonafide genuine" "bonafIDE GENUINE"
"BONAFIDE GENUINE", "BONafide genUINE",
"bonafide genuine" "bonafIDE GENUINE"
"BONAFIDE GENUINE", "BONafide genUINE",
"bonafide genuine" "bonafIDE GENUINE"
"BONAFIDE GENUINE", "BONafide genUINE",
"bonafide genuine" "bonafIDE GENUINE"

"BONAFIDE GENUINE","BONafide genUINE",
"bonafide genuine" "bonafIDE GENUINE"

Pasco.


Uje utunge wimbo au shairi la bonafide genuine make hilo neno umekariri kama vtoto vya form1 vnavokariri maneno ya sayansi
 
I'm Speechless!.
Ila pia tumepiga hatua kubwa sana za kimaendeleo ya kimawasiliano na kisheria, ambapo mawasiliano ya simu binafsi za watu ambayo ni siri, na yamepatikana kinyume cha sheria, yanapowekwa wazi kwa waandishi wa habari pamoja na namba za simu!, haya ni maendeleo makubwa sana kimawasiliano!.

Pia kwa kawaida, maombi huwasilishwa kwanza mahakamani ndipo umma ukatangaziwa ni maombi gani yamewasilishwa, lakini sasa kumbe unaweza kuwasilisha maombi kwa kuwatangazia wanahabari, hadi clasified information ulizonazo, ambazo zimepatikana kinyume cha sheria, kwa kutangaza details za hizo info, na ndipo kuziombea rasmi kibali cha mahakama ili ziwe releazed legally, haya pia ni maendeleo makubwa katika tasnia ya sheria!.

Kiukweli hii ni very high profile case, nadhani kwa kumbukumbu zangu, it the highest kwa hapa nchini, kwa mshatakiwa mmoja, kutetewa na mawakili 7!, wakati mshtakiwa mwenza bado hana wakili hata mmoja!.

Please watch out kwa twists and turns za hii kesi hapo mahakamani hiyo kesho!, mambo matatu haya yanaweza kutokea.

  1. Kesi inaweza kufutwa na kufunguliwa upya, washtakiwa wakaongezeka au kupunguzwa ukiwemo uwezekano mkubwa sana wa Ludo kuondolewa mashtaka na kugeuzwa shahidi No.1 wa serikali!.
  2. Kesi inaweza kufutwa na kufunguliwa upya ikijumlisha kosa la utekaji wa Kibanda.
  3. Kesi mpya ya shitaka la Kibanda inaweza kufunguliwa au hivyo kuzifanya hizi kesi kuwa ni kesi mbili tofauti.
  4. Kesi inaweza kuendelea kutajwa kama kawaida bali kwa kuongeza mshakiwa yule "Bukoba Boy!".
  5. Lolote kati ya hayo linaweza likafanyi, au yote yakafanyika au yote yasifanyike!.

Pasco.

Pasco
Kujua namba ya simu ya mtu ni classified inf? Sijaona mahali walipotoa nini wameongea au text to each other or one another. Mpaka sasa mpewa tu nani aliongea na nani na lini hii si classified info. Tutaitaka mahakama iombe kwa makampuni ya simu mawasiliano ya hizi namba tarehe tajwa. Ukumbuke huwezi kutetea kesi bila kuifanyia uchunguzi.

Usiweweseke subiria mechi halafu mbeep bosi.
 
usilolijua kama usiku wa giza, tuombe mumgu ukweli wa watesaji wa kibanda wapatikane maana kila binadamu anaupeo wake wa kufikiri, roho zimetofautiana na shetani ananguvu, siku moja tutashangaa ukweli ukipatinana tuombe mungu
 
Katika andiko looooote hilo la Marando, wewe umeamua kuandika vitu visivyosurface kwenye hilo andiko. Ni kwamba hujaona cha kuandika kinachohusu hilo andiko au hujaelewa au ndo nyie wapanga mauaji???? Unaeleweka kwa shida sana kwa kukosa hoja ya kuongea kuhusu hili sakata lililopo mbele yetu. Wewe wapi panakutatiza kulielewa uulize tukueleweshe??? Mbona unatoka nje ya mada????

Hayo yote unayoyataja hapo juu yanayofanywa genuinely na cdm ni kuwa yanadhihirisha uhai wa chama (achilia mbali tuhuma za kupikwa). Ukiona chama cha siasa kipo dormant had wakat wa uchaguzi jua hicho ni chama cha msimu. CDM imeshavuka state hiyo, CDM ni chama kilichobeba matumaini ya watanzania. Hivyo ni muhimu sana kuwapa wananchi feedback ya hali ya mambo mbalimbali yanayoendelea na ndo mana kila kinachotokea wananchi wanauliza msimamo wa chama wakimaanisha CHADEMA na sio TLP au UPDP wala ccm.

Kuhusu suala la kutoa hoja mbadala, nadhan ww ni mgeni wa siasa za nchi hii, ni vyema ukajua tu kuwa sasa hivi nchi hii inaendeshwa kwa remote control na CDM. Angalia bungeni, angalia katika mambo mengine mengi sana. Utajua ni CDM ndiyo inayofanya mambo ya happen, bila cdm hii imara, nchi hii ingekuwa ishauzwa.

Kaka uko sahihi kabisa. Wasnaotaka kudivert kutoka katika hili tamko ni walio na hofu nna wanatapatapa kujua cha kuandika. For sure ni ifike mahali hata kama mtu ni mjinga nkiasi gani akubaliane na reality na sio kupindisha. Kila uendapo Tanzania hii na nje CHADEMA imekuwa gumzo kwa jinsi inavyoipeleka puta CCM na machache yanayoonekana kufanywa na hii serikali currupt na dhaifu ni kwa kuogopa kunyukwa na wananchi wanapopata taarrifa. ni vyema CCM kijiondoe katika kashfa hii kwa kuwatosa hawa wote waliohusika na mipango hii michafu. Chama kitanuka kwa matukio haya na hasa yalivyokuwa revealed. Jamii inajua nna hii taarifa itakuwa cemented na tamko la Chadema. Mwigulu is nothing to CCM rather than trouble maker as ZITTO KABWe and their allies.Ni vyema CCM ijiepushe na kwa kuwaosha wote hawa la sivyo jamii imeshawashtukia na itawagarimu sana. Mpango huu mlokuja nao mliingia chaka na ni lazima mrudi, uonevu, udhalimu na vitisho vitawaangamiza.Makamanda tutafanya kazi na watafanikiwa kwa kuwa Mungu tunayemwabudu ni mwema na atawaangamiza watesi hawa wote.
 
Unajua watu wengi sana wanajua wanaopinga dhurma inayofanywa nchini ni lazma uwe wanachama wa chadema uliye front line. Wanasahau kuwa wapo wanachama damu wa chadema ndani ya Ikulu, ndani ya ccm, ndani ya serikali na wizara zake na ndani ya vodacom, tigo etc ambao wala hawajitokezi wala kutambuliaka.

Watu wengi wanajua pia wenye uchungu na nchi hii wapo kwenye vyama vya siasa tu, wanasahau pia kuwa wapo wananchi wasiowanachama wa chama chochote na ambao ndugu zao wamekuwa wakiteswa na kudhurumiwa na serikali kila kona ya nchi hii.

Lakin la msing wanasahau kuwa siku zote watu wakishachoka na utawala dharimu, watashirikiana kwa kila njia kuutokomeza utawala huo. Katika hali hiyo, huwezi kushangaa kwann cdm inapata information toka kila kona ya nchi hii hata zile ambazo ni classified documents. Wananchi wamechoka, hawataki kukiona ccm kinaendelea kutuibia na kutudhalilisha na sera ya sisi masikini.

Aidha, ni iman yangu pia wakati wanachunguza hizo nani kumpigia/kamtumia nan sms, waliweza kupata pia ujumbe gani ulikuwa umebebwa katika hizo intensive communications. Sisi tupo pembeni tunasubiria kuona hii movie ya ukombozi.

hii ishu ya kutunga kwani malando hamumjui kuwa anataka u makamu mweyekiti ndo antafuta sifa kwa migongo ya watu kweli dunia tambala bovu hata wazee waongo.
 
Hahahaah kwa hao mawakili basi tena labda jaji awe mwigulu mwana wa nchemba

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
When the hunter become the hunted!!!...someone should write a book about ccm going from being the hunt to being the hunted!!
 
Wadau, siamini kama tamko hili limetolewa na mwanasheria ambaye si tu amebobea katika fani yake bali pia ni mtu ambaye aliwahi kufanya kazi katika idara ya usalama wa taifa kutokana na ushahidi wa tamko lake hili. Cha kusikitisha zaidi, ameongea mambo ambayo anajua kuwa anayo fursa kupitia mahakama kueleza yote hayo ambako ninaamini ndiko kwenye msaada mkubwa kuliko kuongea na waandishi wa habari ambao wataishia kuandika tu. ninajua kwa sasa chadema wanatafuta huruma za wananchi kupitia matamko yao hayo kwa vile wamechungulia na kuona kuwa hawawezi kushinda kesi ya lwakatare.

Mmetumwa na bado mengi yatajulikana
 
Pasco
Kujua namba ya simu ya mtu ni classified inf? Sijaona mahali walipotoa nini wameongea au text to each other or one another. Mpaka sasa mpewa tu nani aliongea na nani na lini hii si classified info. Tutaitaka mahakama iombe kwa makampuni ya simu mawasiliano ya hizi namba tarehe tajwa. Ukumbuke huwezi kutetea kesi bila kuifanyia uchunguzi.

Usiweweseke subiria mechi halafu mbeep bosi.

jipange tena huo muhanga utajitoa mwenyewe kwa kutojua matakwa ya wanasiasa unao watetea hivi unalipwa sh ngapi kwa hii kazi ya kutetea magaid
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom