Tafakuri ya FaizaFoxy 2: Korosho

Tafakuri ya FaizaFoxy 2: Korosho

Yani serikali itumie fedha ya walipa kodi ili ikanufaishe kabila fulani kwa sababu za kisiasa? Kwanza subiri muone lazima Magufuli aje siku moja atueleze ni kwanini alitumia fedha ya walipa kodi kwenda kununulia korosho kinyume kabisa cha taratibu za kiuongozi. Mambo ya korosho waachiwe wenye korosho zao kama alivyosema Nape. Mbona kabla serikali haijapeleka uchafu wake kule walikuwa wametulia tuli kama maji kwenye mtungi? Yani zitumike fedha za walipa kodi kwa hasara ili kunufaisha kundi fulani kwa sababu za kisiasa? Tutazidai na tutazidai kweli kweli. Mambo ya vita kati ya Manji na Magufuli ndiyo yaliyowaumizeni nyie wamakonde kuanzia mbaazi hadi korosho. Mchawi mnaye nendeni mkamuulize! Tatizo ni nyie mashangazi mnaogopa kupigwa!
Wacha porojo. Weka hizo "taratibu za ki uongozi" tuzione.

Umekurupuka usingizini ukiwa na hangover ya mbege?
 
Kwa nini wawakopeshe bila riba wakati wakianzisha ivyo viwanda watatengeneza faida na kuendelea kujilimbikizia utajiri. Ilo wazo lako ni madudu sana na halina faida wala tija kwa wakulima wa korosho. Ukitaka kuwa tajiri lazima uwe mzulumaji wakulima watazulumika sana.
 
Udini haachagi huyo,ukisoma kiutulivu utagundua udini uliomo kwenye uzi wake huu..msome vizuri
Enzi za alhaj kikwete alikuwa hatoi ushauri,sasa hivi ushauri mwingi implying that things ain't going well wakati jakaya ndo katufikisha hapa
Alhaj ni muumin aliyefika makha kwa lengo la kuhij ili kutekeleza nguzo mojawapo katika nguzo tano ndani ya uislam.
 
Wacha porojo. Weka hizo "taratibu za ki uongozi" tuzione.

Umekurupuka usingizini ukiwa na hangover ya mbege?
Na nakuhakikishia kwa madudu ambayo Magufuli amefanya kwenye zao la korosho "Ama mna muda mrefu ili msimame tena au ndiyo mwanzo wa mkono wa kwaheri kwenye hilo zao" Mtu ni mgeni kwenye mambo mengi ila anajifanya mjuaji hadi anakera. Nyie chezeni naye halafu msimu unaokuja tutakuja kuelezana hapa.

Tararibu za kiuongozi huzijui? Umeona wapi serikali inatumia mali ya umma kijinga vile? Magari ya jeshi, fedha za walipa kodi na muda halafu unaleta hasara mara dufu. Hilo ni sawa?
 
Narudia tena, ilani ya viwanda ni ya ccm, na viwanda vinalipa kuliko udiwani, ubunge na urais. Kwakuwa wanaccm huwa tunaona wanafanya lolote kuhakikisha wanapata madaraka, kwanini wasikope bila riba wafungue hivyo viwanda kisha tuone matokeo ya wanachoamini?

Tena kwa kuanzia mawaziri wajiunge wanne wanne kila kundi lianzishe kiwanda watoe ajira tuone matokeo. Na funga kazi rais ajiunge na mawaziri watatu wa viwanda, wawili aliowatumbua na huyu mpya wajenge kiwanda kisha tuone mfano halisi wa hicho wanachohubiri. Akina Mo, Bakhresa and the likes hawahitaji ushauri wako kwenye viwanda maana tayari wanavyo, hawa wanaohubiri sasa ndio watoe shamba darasa la mahubiri yao.
Nahisi nimekuelewa sana....
 
Ushauri mzuri lkn ccm hakuna tena hata ntu mmoja anaejitambua, bunge ndy limejaa wabunge wasio na mawazo mbadala. Wenye mawazo yenye tafakuli nzuri ndiyo hao hufukuzwa.

Kwanza korosho ni zao linalo endelezwa na Kangomba kumfirisi kangomba ni kuua korosho, ni ujinga wa daraja la juu kumuona kangomba hafai utolewe ushauri na uelimishaji ili kangomba asiwadhurumu wenye mashamba. Na serikali iwalipe pesa zao na kuwaomba radhi.

Pili makangomba wahamasishwe na kukopeshwa mitaji wafungue viwanda vyenye ubora wa kuongeza thamani korosho vingi nasi viwanda vikubwa viwe vidogovidgo vyenye ubora.

Ccm na viongozi wenu mkiona tunatoa ushauri kwa lugha kama hizi mnaamua kudharau au hata kutudhuru au kutuua mmewaweka akina Msiba kutishia wenye mawazo mbadala ni aibu.

Chama hiki na watu wake lazima waondoke ndiyo mawazo yako bibi huenda huko kwenye vyama vingibe wakatokea wenye kutekeleza haya lkn kwa hawa miungu wenye kujua kila jambo ni kupoteza muda. Acha wafanye wanachopenda wao ndiyo wanajua sasa hivi utaonywa na huyo msiba wenu.

Kwanza nakushauri rekebisha makosa hayo. Kiswahili ni lugha yetu ya taifa, kitendee haki.

Una mawazo mema lakini punguza ghadhab, tulizana kaa uandike vizuri. Au unakimbizwa?

Maendeleo hayana chama.
 
Bana Gas waliandamana nahili kimya ina maana hainahaja kwenda kwa bibi ova
 
Juzi Mheshimiwa Rais amesema wanaoona hali ngumu ni wale waliozowea pesa zisizo halali.
Kauli ya rais si 'msahafu', hapo aliongea kwa kudhania tu labda kama angetuwekea na solid proofs za kusimamia kauli yake.
Mfano je hawa wakulima wa korosho walioumizwa na huu utaratibu uliotumia mpaka TPDF katika kuzikusanya korosho zao pia walizoea pesa zisizo halali ndiyo maana wakakutana kadhia hii inayoendelea kuwatia uchungu mpaka sasa?
 
Umelala, kuna njia ya muda mfupi njema zaidi ya kuwapa kilo shillingi 3,400 wakati wanunuzi wa nje walitaka kuwapa shillingi 1,700?

Hivi upo dunia hii kweli? Wewe kweli msukule. Maana umepita kiwango cha kusomea ujinga.
Sasa kama mliuza kilo Tshs 3400 mbona mnalia hadi kujibaraghaza chini? Si muendelee na utaratibu huo?
Hizi siasa za kijinga mnazofanya mnawaumiza hao mnaowaita wanyonge ambao mnasema mpo kwa ajili yao.
 
Na nakuhakikishia kwa madudu ambayo Magufuli amefanya kwenye zao la korosho "Ama mna muda mrefu ili msimame tena au ndiyo mwanzo wa mkono wa kwaheri kwenye hilo zao" Mtu ni mgeni kwenye mambo mengi ila anajifanya mjuaji hadi anakera. Nyie chezeni naye halafu msimu unaokuja tutakuja kuelezana hapa.

Tararibu za kiuongozi huzijui? Umeona wapi serikali inatumia mali ya umma kijinga vile? Magari ya jeshi, fedha za walipa kodi na muda halafu unaleta hasara mara dufu. Hilo ni sawa?
Mali ya umma hutumiwa kusaidia umma.

Ulitaka serikali ikae tu inaona wakulima wanadhulumiwa?

Uamuzi wa haraka aliouchukuwa na Rais ni mwema sana kwa mwenye uelewa, kilichobakia sasa ni kutafuta long term solution. Na uzi huu umelenga hilo la long term solution.

Nafahamu wengi mliotumbuliwa kwa vyeti feki na wizi serikalini saa hizi mnahaha.
 
Sasa kama mliuza kilo Tshs 3400 mbona mnalia hadi kujibaraghaza chini? Si muendelee na utaratibu huo?
Hizi siasa za kijinga mnazofanya mnawaumiza hao mnaowaita wanyonge ambao mnasema mpo kwa ajili yao.
Naona hata mada hujaielewa. Tatizo ni lako siyo letu.
 
Mali ya umma hutumiwa kusaidia umma.

Ulitaka serikali ikaletwa inamna wakulima wanadhulumiwa?

Uamuzi wa haraka aliouchukuwa Rais ni mwema sana kwa mwenye uelewa, kilichobakia sasa ni kutafuta long term solution. Na uzi huu umelenga hilo la long term solution.

Nafahamu wengi mliotumbuliwa kwa vyeti feki na wizi serikalini saa hizi mnahaha.
Wewe utakuwa hujaenda kusini. Upo hapo Ilala umebaki kupiga porojo. Lipi ambalo Magufuli alifanya limewasaidia wadau wa korosho zaidi ya kuzidisha kero na gharama tupu? Halafu wala wewe huhitaji kunifundisha kitu maana nina akili mbele yako zaidi ya maili milioni tano! Wewe kwangu kiakili ni mchanga sana bibi. Yani naweza kuiweka hii nchi mkononi mwangu ikaenea na nikawa naiperuzi kama simu. Nina uelewa mpana.

Halafu Magufuli mwenyewe unayeniambia ninaweza kukupa list ya mambo aliyofeli ambayo ni mara dufu ya aliyofaulu. Kiufupi wewe wakati umelala mimi nilishamu-assess Magufuli hivyo namuelewa sana na akifanya jambo naelewa litaisha vipi. Kwa hayo naomba niheshimu. Huyo wala hataweza eti kunitumbua kwa vyeti feki! Kanizidi tu kwa cheo cha nchi!
 
Naona hata mada hujaielewa. Tatizo ni lako siyo letu.
Hiyo long term solution uliyotoa ni ya kijinga! Kama mliuza kwa faida hivyo si mnaweza kujiendeleza? Sasa mbona unataka tena huruma? Ukishakuwa tatizo huwezi kuelewa lilipo tatizo!
 
Pita pita zangu humu nimekutana na huu uzi na nimesoma mchango wako kuhusu zao la korosho ushahuri wako ni wa ujenzi.

Mimi napita naenda kunywa kahawa na kashata za karanga.


Ahsanta...
Mheshimiwa umepotea sana. Msalimie sana the big boss, sijui kama alisalimika na korosho

Ahsanta
 
Hiyo long term solution uliyotoa ni ya kijinga! Kama mliuza kwa faida hivyo si mnaweza kujiendeleza? Sasa mbona unataka tena huruma? Ukishakuwa tatizo huwezi kuelewa lilipo tatizo!
Tatizo lako kubwa ni muono duni na kukosa ubunifu. Utajiendeleza kwa kuendelea kuuza korosho ghafi?

Kujiendekeza ndiyo huko. Soma post namba moja ikuingie.
 
Back
Top Bottom