Tafakuri ya FaizaFoxy 2: Korosho

Mimi najiuliza swali moja Yale maghala makuu yamejaa korosho zilizokosa mnunuzi, na msimu mwingine unakuja, sijui wataziweka wapi. Ni dhahiri wanunuzi wanaweza wakarudi nyuma msimu ujao kwa hawajui wataingiliwa namna gani. Mkuu anaweza akamuru kama wanataka kununua korosho tz lazima wanunue Kwanza za kwenye maghala. Hapo ndo utakuwa mwisho marketability ya zao la korosho tz. Kaburi li wazi.
 
"Se non sta andando bene, chiama tua nonna." Hiyo ni methali maarufu ya Kitaliano ambayo nimepata tabu kidogo kutafuta ya Kiswahili inayofanana-nayo, sijafanikiwa kuipata. Kwa tafsiri isiyo rasmi inasema "ikiwa hakuna linalokwenda sawa, muone bibi".

Nafahamu Kitanzania ukisema "kumuona bibi" au "babu" wengi wengine huhusisha na kuwaona mabibi na mababu ili waongee na mizimu mambo yaende sawa. Wataliano kwa msemo wao huo hawamaanishi kama Watanzania, Wataliano wanamaanisha umuone bibi kwa hekima na busara zake. Labda niifananishe na methali yetu ya "uzee ni dawa".

Binafsi kama bibi, leo nimedhamiria kutoa tafakuri yangu kwenye zao la korosho na ufumbuzi wa "matatizo" ya zao hilo.

Kwanza napenda ku "declare interest" kuwa binafsi ni mdau wa korosho kwa kuwa na mikorosho, mingi tu, tiliyoirithi toka mashamba ya mabibi zetu ile mbegu ya asili ya kizamani mpaka tumejaribu kuiendeleza na kupanda ya kisasa na tunaliona tija nzuri tu.

Ushauri: Serikali ijitowe kimasomaso kuwakopesha bila riba wafanya biashara wakubwa wenye uzoefu wa viwanda kama vile akina Bakhresa na Mo kufunguwa viwanda vikubwa vya kisasa vya kubangua, kusindika na kufungasha korosho kwa kiwango cha Kimataifa na kuwasaidia kushindana na masoko ya Kimataifa.

Hiyo ni badala ya serikali kuingilia zao hilo.

Sababu kuu ni kuwa wafanya biashara hao tayari wana uzoefu mpana wa viwanda vya "food processing" na tayari wana mitaji katika nchi kadhaa za SADC na Afrika Mashariki.

Ni tafakuri tu ya FaizaFoxy .

Thank you. A very good Idea....Mo simuamini sana mana muhindi kwao kulee atatugeuka tu
 
Narudia tena, ilani ya viwanda ni ya ccm, na viwanda vinalipa kuliko udiwani, ubunge na urais. Kwakuwa wanaccm huwa tunaona wanafanya lolote kuhakikisha wanapata madaraka, kwanini wasikope bila riba wafungue hivyo viwanda kisha tuone matokeo ya wanachoamini?

Tena kwa kuanzia mawaziri wajiunge wanne wanne kila kundi lianzishe kiwanda watoe ajira tuone matokeo. Na funga kazi rais ajiunge na mawaziri watatu wa viwanda, wawili aliowatumbua na huyu mpya wajenge kiwanda kisha tuone mfano halisi wa hicho wanachohubiri. Akina Mo, Bakhresa and the likes hawahitaji ushauri wako kwenye viwanda maana tayari wanavyo, hawa wanaohubiri sasa ndio watoe shamba darasa la mahubiri yao.
Wana CCM wengi sana ni wafanya biashara. Fatilia utaona. Hata wale wakubwa. Pia wabunge na madiwani wengi wa CCM (Kama si wote) ni wafanya biashara mbali mbali.

Huo ushauri wako hauna maana yoyote kwa CCM. Been there done that.
 
Usemayo ni mawazo duni sana. Mbona kuna Watanzania wengi sana wamefanikiwa? Bakhresa ni mfano mzuri sana, alikuwa ana kiduka tu cha kushona makubadhi pale mtaa wa Uhuru.

Kila unapoona matatizo ufahamu kuwa kuna fursa, nnakushangaa sana wewe unashindwa kuziona fursa na unayaona makaburi tu.

Pamoja na mawazo yangu duni, unafikiri hilo ni wewe wakwanza kushauri?? Ndio maana nikakwambia katika taifa ambalo limeshawahi kupewa kila aina ya ushauri basi tanzania ni namba moja, TUMESHAJIULIZA KWANINI KILA USHAURI MZURI HAUFANYIWI KAZI?? - TAMBUA HII SIO BAHATI MBAYA BALI WANATAMBUA KILA WAFANYALO..

Kila kukicha toka enzi za Nyerere watu walishauri juu ya kuweka nguvu sekta binafsi na kuifanya iwe strong kiasi pia ya kuwekeza kila mahala kuanzia kwenye muhogo mpaka Korosho..Sekta binafsi sio tu kilimo kila mahala hata viwandani, transportation, majini na kwenye elimu nk but who cares??.

Tanzania imebalikiwa kila mahala lakini Tanzania pia ndio yenye shida kila mahala..tunashindwa wapi? Kama tuna nguvu kazi ya watu zaidi ya milioni 50???. Kwanini tusiseme kipo chanzo cha matatizo yote ya Tanzania ambacho ni CCM..
 
Poleni sana...

Kwani mfumo wa zamani wa ukusanyaji na ubanguaji ulikua na kasoro zipi?

Tatizo ujuaji mwingi ndiyo umepelekea haya yote..


Cc: mahondaw
 
Pamoja na mawazo yangu duni, unafikiri hilo ni wewe wakwanza kushauri?? Ndio maana nikakwambia katika taifa ambalo limeshawahi kupewa kila aina ya ushauri basi tanzania ni namba moja, TUMESHAJIULIZA KWANINI KILA USHAURI MZURI HAUFANYIWI KAZI?? - TAMBUA HII SIO BAHATI MBAYA BALI WANATAMBUA KILA WAFANYALO..

Kila kukicha toka enzi za Nyerere watu walishauri juu ya kuweka nguvu sekta binafsi na kuifanya iwe strong kiasi pia ya kuwekeza kila mahala kuanzia kwenye muhogo mpaka Korosho..Sekta binafsi sio tu kilimo kila mahala hata viwandani, transportation, majini na kwenye elimu nk but who cares??.

Tanzania imebalikiwa kila mahala lakini Tanzania pia ndio yenye shida kila mahala..tunashindwa wapi? Kama tuna nguvu kazi ya watu zaidi ya milioni 50???. Kwanini tusiseme kipo chanzo cha matatizo yote ya Tanzania ambacho ni CCM..
Kila zama na kitabu chake.

CCM wanashaurika sana tena sana, ingekuwa hawashauriki usingeona Rais anaitisha mikutano na vikundi tofauti tofauti ili kusikiliza maoni yao.

Ukisoma huelewi basi hata picha huoni?
 
Poleni sana...

Kwani mfumo wa zamani wa ukusanyaji na unanguaji ulikua na kasoro zipi?

Tatizo ujuaji mwingi ndiyo umepelekea haya yote..


Cc: mahondaw
Hakuna kasoro bali biashara ni ubunifu, ushauri umelenga katika kuzidisha thamani ya zao la korosho.
 
Wana CCM wengi sana ni wafanya biashara. Fatilia utaona. Hata wale wakubwa. Pia wabunge na madiwani wengi wa CCM (Kama si wote) ni wafanya biashara mbali mbali.

Huo ushauri wako hauna maana yoyote kwa CCM. Been there done that.

Waache ubunge wajikite kwenye biashara maana huko kwenye siasa ndio wameharibu kwa kutoa rushwa, kufanya ukatili nk ili washinde. Kama unaweza kunisaidia unaweza kuniambia Profesa Kabudi kiwanda chake kiko wapi? Ukiweza nitajie na kiwanda cha Makonda kilipo nikaombe ajira.
 
Naona udini umeweka pembeni kwa muda, hongera
Udini haachagi huyo,ukisoma kiutulivu utagundua udini uliomo kwenye uzi wake huu..msome vizuri
Enzi za alhaj kikwete alikuwa hatoi ushauri,sasa hivi ushauri mwingi implying that things ain't going well wakati jakaya ndo katufikisha hapa
 
Hakuna kasoro bali biashara ni ubunifu, ushauri umelenga katika kuzidisha thamani ya zao la korosho.

Na umetaja serikali ijaribu kukopesha wafanyabiashara wakubwa wenye uzoefu na biashara ili waweze kuboresha zao la korosho...

Hilo linawezekana, ila hao wafanyabishara wanakwepa masharti magumu yaliyopo kwenye hilo zao...


Cc: mahondaw
 
Mimi huwa sielewi hoja hii ya mheshimiwa, maana najua wafanyakazi sekta ya umma na binafsi Tanzania wote wanalia mishahara yao haikidhi kujikimu kwa mambo muhimu kama chakula, malazi na mavazi.

Madili ni lazima yawepo mpaka hapo mishahara ya wavuja jasho itapotosha kwa masuala ya msingi chakula na mavazi ndipo wawabeze 'wamezoea Madili ili hali mishahara inatosha kujikimu.

Nchi zingine hakuna hata rushwa ndogo ndogo au kuombwa pesa ya chai kwa vile mishahara inatosha kujikimu chakula, mavazi na malazi.
Tafakuri imelenga ku add value, kama hatuja add value ya mazao yetu vipi kipato cha wafanyakazi kitaongezeka?
 
Kila zama na kitabu chake.

CCM wanashaurika sana tena sana, ingekuwa hawashauriki usingeona Rais anaitisha mikutano na vikundi tofauti tofauti ili kusikiliza maoni yao.

Ukisoma huelewi basi hata picha huoni?

Kuna hivi vitu bibi.
preventive maintenance = fix before failure.
Breakdown maintenance = fix after failure.
Kikao =breakdown maintenance..
Tunataka kurekebisha baada ya tatizo wakati watu walishauri kabla ya tatizo na sio hili tu yapo mengi sana..

Athari za kutengeneza baada ya tatizo ni kubwa na wanaozibeba wananchi kila siku na hakuna wakuwafidia na bado tunaendelea kuishi kwa majaribio mwaka wa 50 sasa huku wanaoumia na kuendelea kuwa masikini ni watanzania..

CCM hawakuwahi kushaurika na hawatashaurika maana kwasasa Tanzania ni mali yao na watanzania ni misukule yao hivyo tutaendelea kuishi sana kwa majaribio..
 
Na umetaja serikali ijaribu kukopesha wafanyabiashara wakubwa wenye uzoefu na biashara ili waweze kuboresha zao la korosho...

Hilo linawezekana, ila hao wafanyabishara wanakwepa masharti magumu yaliyopo kwenye hilo zao...


Cc: mahondaw
Masharti siyo misahafu ya Mungu, yanabadilika.
 
Kuna hivi vitu bibi.
preventive maintenance = fix before failure.
Breakdown maintenance = fix after failure.
Kikao =breakdown maintenance..
Tunataka kurekebisha baada ya tatizo wakati watu walishauri kabla ya tatizo na sio hili tu yapo mengi sana..

Athari za kutengeneza baada ya tatizo ni kubwa na wanaozibeba wananchi kila siku na hakuna wakuwafidia na bado tunaendelea kuishi kwa majaribio mwaka wa 50 sasa huku wanaoumia na kuendelea kuwa masikini ni watanzania..

CCM hawakuwahi kushaurika na hawatashaurika maana kwasasa Tanzania ni mali yao na watanzania ni misukule yao hivyo tutaendelea kuishi sana kwa majaribio..
Hayo maisha ya kila siku, uamuzi mmoja unaweza ukaharibu lakini kuharibu ndiyo kujifunza. Hutarudia na inabidi utafute njia mbadala.
 
Udini haachagi huyo,ukisoma kiutulivu utagundua udini uliomo kwenye uzi wake huu..msome vizuri
Enzi za alhaj kikwete alikuwa hatoi ushauri,sasa hivi ushauri mwingi implying that things ain't going well wakati jakaya ndo katufikisha hapa
CCM ni ile ileee.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom